Makamba Ayataka Makampuni ya BIMA Nchini Kutumia Fursa Katika Sekta ya Nishati

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,903
945
MAKAMBA AYATAKA MAKAMPUNI YA BIMA NCHINI KUTUMIA FURSA KATIKA SEKTA YA NISHATI

Makampuni ya Bima nchini, yametakiwa kuhakikisha kwamba yanazitumia fursa zilizopo katika Sekta ya Nishati, kuzitambua na kufahamu kuwa wana nafasi ya kuzifikia na kuzipata.

Wito huo umetolewa tarehe 15 Julai, 2023 na Waziri wa Nishati, January Makamba wakati wa ufunguzi wa Semina ya kujadili ushiriki wa Kampuni za Bima nchini kwenye miradi ya Nishati.

Waziri Makamba ametoa wito kwa wadau, wahusika makampuni ya Bima na wadau wengine, kufahamu kuwa, kwa upande wa Wizara ya Nishati, mlango uko wazi kuendelea kushirikiana nao, na kuwasiliana kwa karibu lakini pia kuna uwekezaji kwa upande wao wa ujuzi, maarifa ya mahitaji mahsusi ya Sekta ya Nishati ikiwemo upanuzi wa mtaji kutokana na ukubwa wa uwekezaji katika Sekta ya Nishati.

Akizungumzia kuhusu madhumuni ya mkutano huo, Waziri Makamba ameeleza kuwa, umelenga kujadiliana kati ya makampuni ya Bima ambayo yametengeneza umoja wao ambao unataka kujishughulisha na fursa zilizoko katika Sekta ya Nishati hasa Miradi ya Gesi na Mafuta, Miradi ya Umeme na miradi mingineyo katika Sekta ya Nishati.

“Kama mnavyofahamu, tunaelekea katika utekelezaji wa miradi mikubwa sana ya kimkakati ya Nishati ikiwemo Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) kutoka Hoima-Uganda hadi Chongoleani Tanga, Mradi wa kuchakata na kusindika Gesi Asilia kule Lindi. Moja ya fursa zilizopo katika Miradi hiyo mikubwa ya kimkakati ya Nishati ni Bima.” Alisema Waziri Makamba.

Waziri Makamba alifafanua zaidi kuwa, Bima ni sehemu ya huduma ya fedha, ni Biashara kubwa na kuwa yapo makampuni 22 ambayo yametengeneza umoja wao hapa nchini na yameialika Wizara ya Nishati ili kufanya mazungumzo nao kueleza ni fursa zipi zilizopo za Bima katika Miradi ya Nishati na wanaweza kuzifikia vipi fursa hizo, ushirikiano ambao unaweza kuwepo kati ya Serikali, kati ya Wizara ya Nishati na Taasisi na kampuni hizi.

Amesema, mazungumzo ya kutengeneza Mradi wa Kusindika na Kuchakata Gesi kule Lindi Mradi yamemalizika na kulikuwa na mazungumzo na vipengele vinavyohusu Bima.
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2023-07-16 at 18.47.07.jpeg
    WhatsApp Image 2023-07-16 at 18.47.07.jpeg
    35.7 KB · Views: 4
  • F1JqjGfaEAYVF_J.jpg
    F1JqjGfaEAYVF_J.jpg
    54.6 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2023-07-16 at 18.47.07.jpeg
    WhatsApp Image 2023-07-16 at 18.47.07.jpeg
    35.7 KB · Views: 2
Back
Top Bottom