Majibu ya Dr. Slaa kwa maswali ya watanzania, Julai 2011

Jenifa,

Mkuu nadhani hutakuwa unawatendea haki Watanzania ikiwa sababu unazotumia ni kile kinachomtokea Nape au viongozi wa CCM. Haiwezekanai watu wakimzomea mtu wako basi nawe unaanzisha zomea zomea bila sababu nyingine isipokuwa Uchama utafikiri tupo uwanja wa Taifa. Nape mara zote anakuja hapa kuzunguzia kazi yake, na amejikita ktk kuondoa nguvu ya Upinzani kiitikadi ktk kukisafisha chama..

Hii sii kazi ndogo hasa ikiwa chama kimefanya machafu mengi na Nape anakuwa bangusilo wa lawama za wananchi.. yeye kama mwanasiasa ni lazima azichukue hizi lawama kwa kufuta matusi hayo akilini na kuchukua mzizi wa fitna hizi kuwa kigezo cha kupambana na maadui wa chama ktk kusimamisha maadili..

Hivyo basi mashambilizi mengi ya wana JF kwa Nape yanatokana na uchafu wa viongozi wake ambao yeye amekuwa wakili kuwasafisha. Kazi ambayo sii rahisi kabisa isipokuwa unyenyekevu, kubali makosa na kuonyesha insanity ndio solution zaidi ya kurudisha matusi.. Na kama umemfuatilia Nape muda wote amekuwa wakili wa chama ktk kujivua Magamba akionyesha uwezekano wa kurudisha hadhi ya chama hata kama anazomewa..Pia ni jukumu lake kuonyesha mapungufu ya upande wa pili wa Upinzani ktk kuijenga imani ya watu dhidi ya vyama hivyo.

Mkuu wangu kama ndugu yako ameua ni lazima utakutana na watu watakao wazomea nyote watetezi wa mauaji hayo lakini itakuwa ujinga familia ya muuaji ikaanza nayo kuzomea watu kwa sababu tu wanazomewa wakitumia mifano ya - Mkuki kwa nguruwe!. Hii inaonyesha wazi wewe hufahamu uzito wa makosa yaliyotendeka na nachelea kusema kwamba wanaCCM wengi hawafahamu kiwango cha madhara ya utawala wa CCM kiuchumi isipokuwa wanatazama mavuno ya Ufisadi..

Dr. Slaa anakuja hapa kutujuza hali halisi ya kisiasa ndani ya chama chake na nje. Hakuna mahala popote Dr.Slaa amefikia kiwango cha kuzungumzia personal life ya Nape au viongozi wa CCM na wala sidhani kama kuna sehemu Nape kashambuliwa maisha yake binafsi na wanaJF..Hivyo jifunze sana kuwa mvumilivu kwa sababu Dr.Slaa yupo hapa kwa faida yetu sote bila kujali tofauti zetu za chama. Na kama sikosei maswali mengi yaliyowekwa hapa yametolewa na watu ambao sii wanachama wa CDM wala CCM..
 
Kuna mtu juzujuzi (FF) alitimiza miaka 30 ktk ndoa. Sijui kama ni kweli maana nina mashaka kwa jinsi ninavyomwona asivyojiheshimu anapokuwa kwenye mijadala mbali mbali hasa huu ambao Dk Slaa ameombwa na wanaJF. Nadhani ndio maana hata sikuweza kumpongeza maana najua sio mama anayejiheshimu. Na ni hivyo hivyo pia asivyoiheshimu ndoa yake.

Si majibu ya kumtukana mtu kama Dk Slaa kusema hajui Kiswahili. Swali: Kiswahili ni lugha ya kabila gani hapa Tanzania? Je, ni nani anayeijua kiswahili kilivyo? Sasa hili alilolileta huyu mama limetoka wapi?

Sasa naona Dk Slaa haendelei kutujibia maswali yetu sijui ni kwa sababu ya huyu au kitu kingine; sijui. Tafadhali Dk endnelea kutupa mwanga.

Asante.
Hivi kweli mna-trip kwakuwa FF amebeza matumizi ya lugha?....mimi sioni big deal,Dr alisema atajibu mambo ya CDM,ambayo sasa hivi muhimu sana ni Arusha,igunga na shibuda.Nadhani mengine ataachia wabunge na serikali.
 
Wakuu,



Kwa Dr Slaa,

Mwisho naomba kumwuliza Dr Slaa juu ya msimamo wa Chadema kuhusiana na Suala la mgawanyo wa madaraka kati ya serikali na bunge. Kama alivyosema Mzee Warioba hivi karibuni, kuna mgongano ambapo wakati mwingine bunge limeonekana kufanya kazi za serikali. Wabunge wameanza kufanya hata kazi za kidiplomasia. Kwa mfano kuna wabunge walienda London ku negotiate change ya radar wakati waziri mhusika na balozi yupo. Pia wapo wabunge walioenda Malaysia kutembelea ile kampuni iliyopewa mkataba wa kutengeneza vitambulisho. Haya yote yalifanywa wakati vikao vya bajeti vinaendelea Dodoma.

Ukiangalia ile video ya kamati ya bunge la Uingereza likiwahoji maafisa wa BAE System kuhusiana na suala la change ya radar umwona mbunge wetu mmoja nae alikuwepo kwenye room. Alikuwa anafanya nini pale wakati alitakiwa kuwa bungeni Dodoma ku-scrutinise bajeti za wizara mbalimbali? Chadema haioni kama kuna tatizo hapa la wabunge wetu kufanya shughuli za kidiplomasia, n.k? Mzee Warioba ameghusia pia suala la Kamati za Bunge kutoa maelekezo kwa taasisi za serikali. Najua Tanzania tuna tatizo kubwa kwenye Separation of Powers kati ya bunge na serikali, lakini hili la wabunge kufikia kuwa wanadiplomasia, Chadema hamuoni kama tunavuka mipaka?

Asante.

Umesahau juu ya conflict moja ya majukumu ya serikali na bunge.

Kuna huu mfuko wa maendeleo wa jimbo CDF . Binaffsi naona si sahihi sijui Dr slaa anasemaje. Pili sababu CDF io tayari basi Tumwombe Dr slaa awaagize wabunge wote wa CDM wawe wanachapisha matumizi ya pesa zile za majimbo yao kwenye magazeti kila baada ya miezi mitatu au sita. Hii itasaidia kuonyesha uwajibikaji wa wabunge wa CDM kwa wnanchi tofauti na wa CCM
 
Dr. Slaa,

Kwanza niseme pole na majukumu yako na asante kwa kuingia humu ili kuinteract na members wa JF. Itikadi za kisiasa pembeni mimi nafurahia sana huu utaratibu wa wewe kuweza kuingia JF na kujibu hoja kama zinavyoletwa badala ya kuanzisha tu thread kisha kuachia wengine wajibu kama baadhi ya viongozi wanavyo fanya humu.

Turudi kwenye mada husika....


Pamoja na kuwa sina tatizo kutoa mchango wangu kama mkereketwa wa maendeleo ya Taifa letu, na kuchukizwa sana giza totoro linaloikimba nchi yetu, ni maoni yangu kuwa hoja nyingi zilizoko zinahitaji majibu ya Serikali na Chama Tawala.

Binafsi mimi naona kazi kuu ya chama cha upinzani siyo tu kuonyesha maovu ya serikali bali na wao kuonyesha ni jinsi gani wange deal na swala fulani tofauti yani kuonyesh umbadala. Ili watu washawishike kukuchagua ni lazima uonyeshe ni jinsi gani ungefanya mambo tofauti endapo ungepewa nafasi.

Kwa maana hiyo basi sioni tatizo la wewe kama katibu mkuu wa Chadema na mgombea uraisi wa chama chako kwa mwaka 2010 ukatueleza ni nini chama chako kingefanya na ni nini wewe binafsi ungeanya kama ungekua raisi kwa wakati huu. Kazi ya kulalamika tuachieni sisi wananchi wa kawaida nyie tuambieni tu Chadema ingefanya a,b,c badala ya d,e,f iliyofanywa na chama tawala.


Kwa vile wako wa Chama tawala humu, ninashauri maswali hayo waelekezewe hao tuliowapa dhamana na wanakusanya kodi zetu. Niko tayari kuchangia pale yatakapohitajika maoni yangu kuhusu jambo lolote lile kama maoni hayo yanaweza kusaidia tusonge mbele. Swala la Madiwani wa Arusha nimekuwa nikilitolea ufafanuzi wa mara kwa mara kwenye vyombo vya habari.

Mkuu hata kama jambo umeshalitolea ufafanuzi mara mia siyo vibaya ukalitolea ufafanuzi tena pindi unapo ulizwa na kama kiongozi hutakiwi kuchoka kujirudia rudia. Kwa sababu kwa kutolea ufafanuzi mara nyingi kwanza tutaangalia consistency ya majibu unayotoa kwa maana leo unaweza ukajibu hivi na kesho swali hilo ukajibu kivingine. Lakini pia utawapa fursa ya watu ambao hawakuwahi kusikia ufafanuzi huo wakapata kufahamu.

Natumai mkienda kufanya maandamano au kampeni maeneo mbali mbali ukiulizwa maswali hausemi nisha litolea ufafanuzi hilo. Siku zote kutakua na watu ambao hawa kusikia mara ya kwanza. Kwa hiyo mkuu hata kama umesha toa ufafanuzi tena na tena naomba usichoke kuendelea kutoa ufafanuzi. Binafsi mimi sijasikia maelezo yako kuhusu madiwani wa Arusha.
 
Sasa wewe si unataka umeme, hata ukiwashwa kwa kutumia mavi ya ng'ombe si umeme? Wabongo bana.
Omr, Sisi wakerewe tumeanza zamani toka mkoloni kutumia mavi kuzalisha umeme. Na kama unataka nikwambie tunafanya vipi niko radhi kukufahamisha..

Lakini hii sio hoja, ulichoandika hapa ni ufinyu wa kuelewa mahitaji yetu ktk kukuza uchumi..kwani unachosema hapa ni sawa na kusema hatuna sababu ya kujenga reli, barabara ikiwa Punda wanaweza kubeba mizigo yetu..Nguvu kazi kwa matumizi ya jembe la mkono ktk kilimo haiwezi kuwa suluhisho la upungufu wa chakula nchini - Think big!
Sijui kama umenielewa.
 
Asante sana Dr Slaa kwa kutupatia fursa ya kukuuliza maswali.

Madiwani Arusha;

Kamati kuu ya chadema imetishia kuwafukuza au kuwachukulia hatua madiwani wa arusha kwa muafaka waliofikia; je hatua hii si kugandamiza demokrasia? Je hii haileti tafsiri kuwa makao makuu wanataka kuwa na monopoly ya mawazo yao? Mh lema anasema hatambui muafaka, je hii haionyeshi kuwa mbunge huyu hajui mambo yanayoendelea kufanywa na madiwani wake (maendeleo au shughuli za siku kwa siku za halmashauri)?

Shibuda;

Shibuda si waziri kivuli,ni mbunge wa kawaida tuu ndani ya chadema; je hatua ya Lissu kumlima barua si ukandamizwaji wa demokrasia? je si kumnyima mbunge haki yake ya kutoa maoni na kuwa huru? Je tutawatafautishaje chadema na ccm, kama kuna tabia ya kuziba maoni ya watu binafsi? Naona apeweuhuru ajibiwe kwa hoja.

Wabunge viti maalum;

Upatikanaji wa wabunge vitimaalum umeacha maswali mengi; je ni kweli chadema inashindwa kusimamia uchaguzi wa wabunge hawa mpaka kuwa na uteuzi? Pili huu uchaguzi umetia giza sana kwenye chama, haukuwa wazi. Je hili unaliongeleaje? Je waliohusika kuharibu uchaguzi wa viti maluum walichukuliwa hatua gani? Je utakubali kuwa asilimia 70% walioharibu huo uchaguzi leo hii ni wabunge?

Sababu ya kuwa na vitimaalum ni kuwawezesha wanawake. Nimefurahishwa sana Halima mdee(naomba umpee hizi pongezi) swali kwanini kuna wabunge wa vitimaaluuum waliokaa mda mrefu na hawataki kuachia wengine? Je nini hasa hawa wamefanya ambacho wanachama na watanzania wanaweza kujivunia nao?

Uwakili;

Chadema imejipatia halmashauri kadhaa na wabunge katika maeneo muhimu, tukiweka siasa pembeni je wabunge wanashiriki katika shughuli za maendeleo ipasavyo ( sio maandamano au shughuli za kujenga chama, na popularity syndrome inayowatafuna badhii ya viongozi wachadema wanotaka kuwa kwenye frontpage za magazeti, na kuwa na watu wanao wapepea.. .na kujitafutia ushabiki)

Napenda kutumia fursa hii kukupongeza kwa kuwa ulianza kazi ya kuwafunda madiwani (ni muhimu sana na Mungu akubariki). Swali langu inaonekana chadema makao makuu imetawaliwa sana wabunge, je mnatamba mchango wa madiwani na kuwapa moyo katika shughuli zao za siku kwa siku?

Wizara na bunge

Mwanasheria mkuu alimshtumu mh lisuu kuwa anongea bungeni ili aonekane kwenye tv, hii kauli inaudhi; je kuna ukweli katika hili?

Je unaonaeje madhara ya mbunge kuongea ili aonekane kwenye tv? Je hakuna chembe ya wabunge wetu wachadema wenye nia hiii ndani ya mioyo yao? Je inadhari gani katika maendelo ya chama chetu na nchi kwa ujumla?

Mawaziri kivuli wa chadema wameonekana kupwaya nafasi zao; je hili ndio baraza ambalo chadema ikishika hatamu leo litamaliza kiu ya watanzania? Je chadema ina mkakati gani wa kuziba hii mianya iliyoko sasa hivi?

Pendekezo, naomba uwafunde wabunge namna kupanga hoja zao italeta ufanisi; ukweli ni kuwa wakiendelea hivi itakula kwetu chadema (leo na kesho mashabiki watashabikia , kesho kutwa watazomea; chonde chonde chonde chadema isikubali kupelekwa na ushabiki wa wanachama; tulieni, jipangeni, maendelo yatakuja)

Wabunge wa chadema hasa viti maalum naona wengi hawajui majukumu yao, mchango wao ni kidogo sana..nilitegemea hawa ndio wangeziba mapengo (mfano ni uwazri vivuli).

Tunaomba wabunge wa chadema ambao hawaruki majimboni mwao wachukuliwe hatua, nampongeza mzee ndesamburo kwa kuishi jimboni kwake; wengine vp? Wanazungukia mno mako makuu (je mmesahua sera yenu ya majimbo?) ianzisheni kwanza ndani ya chadema
 
Swala la uvunjifu wa kanunu za chadema ccm wanaingiaje? Serikali ifanye hili ifanye hili nauliza lile la madiwani kuvunja kanuni ama katiba ya chadema yanahitaji serikali ya ccm? Unajua mazoe mabaya tusipoangalia kuna siku kiongozi utaambiwa mke wako mjamzito then useme this must be CCM
 
Asante Dr kwa kuja jf kutibu haja zetu watanzania juu ya mambo mbalimbali yanayolisibu taifa leo, pia na yale yahusuyo CDM hasa suala la ARUSHA.

Pamoja na majibu yako mazuri tunaomba pia uzungumzie kidogo suala la kutofautiana kauli kwa wabunge wa CDM kwenye issue ya posho na hatma ya Mh SHIBUDA.

Nawakilisha
 

Dk Slaa,
Awali, kukushukuruni sana kwa offer ya muda wako kujumuika nasi na kutushirikisha mawazo na fikra zako zenye elimu, busara na hekima na ndivyo tulivyotegemea.

Binafsi napongeza sana jitihada za viongozi wa chadema kuonyesha dalili za kukomaa kiuongozi, kuwa na busara katika maamuzi kwa kutumia kigezo cha subira bila papara, maama Mt. Benedicto wa Nursia huko Italia aliwaambia wanafunzi wake, unapofanya masahihisho ya mwenendo wa mtu angalia tabia kwanza, maana vyombo vingine vina kutu ukiviparuza zaidi vitaboka.

Nawaomba viongozi kitaifa jitahidini sana kuwafunza waandamizi ndani ya chama na katika mabaraza ya uwakilishi kuwa wepesi wa kusoma upepo wa yanayoendelea, kuwa waangalifu katika sheria na taratibu pamoja na uvumilivu ili kasoro ndogo ndogo zisitumiwe na watawala kama kigezo cha kukandamiza hoja kali za upinzani katika uwakilishi wao wa wananchi, kwani sasa hivi hoja zitolewazo zinaonekana wembe wenye makali pande zote kila wanakogeukia ni hatari tu. Na mikutano yo yote ikiwa ni pamoja na maandamano hard copy lazima muwe nayo kama kielelezo, msikubali ruhusu ya mdomo tu.

Jarida la Chama ni muhimu kwa vile ndio njia ambayo sera za chama zitawafikia wengi, na gharama za kuanzisha kijarida si ghali kama uanzishwaji wa TV au Radio. Hii mitandao ni ya wachache sana ambao nafasi zinawaruhusu.

Hayo ni maoni yangu kama mpenda maendeleo na si mwanachama wa chama cho chote ila tu mpenzi wa chama chenye sera za kujali taifa letu.
 
Mkuu Nadhani Sheria za nchi haziruhusu vyama vya Siasa kumiliki Radio au Television unless CDM wangeshafungua tayari
<br />
<br />
radio uhuru na uhurupublications ni mali ya ccm, si kweli hoja yako.
 
redio uhuru inamilikiwa na nani?

Hiyo ipo kwa sababu tu wameshika hatamu...

Ata CDM wakiingia madarakani wataweza kuanzisha redio/television zao bila kikwazo kama wakiamua, lakini sio sasa, na wakati huo ukifika ndipo utakaposikia redio Uhuru imefungiwa kwa kuvunja masharti hayo utadhani TCRA walikuwa hawawaoni muda wote huu, ndo nchi zetu hizi, tutafika tu...
 
Saint Ivuga,

Igunga kimsingi ni ya wana Igunga. Wao ndio wanaofahamu mwana Igunga mwenye kuijua vizuri Igunga, na mwenye Uchungu nayo. Si amini katika kugombea kwa lengo la kupata Ubunge.

Naamini Mbunge kuwa mwakilishi wa watu wake. Mimi nimerwawakilisha wananchi wa Karatu kwa miaka kumi na tano. Sasa nina jukumu la kujenga chama, ambacho nacho kikiwa imara kitawanufaisha wana Igunga. Ni mgawanyo wa majukumu. Ndicho tunachoamini ndani ya Chadema, nani anaweza kufanya vizuri nini na wapi na kwa wakati gani.

Ninawashauri na kuwashawishi sana Wana Igunga wenye sifa popote walipo wajitokeze ili tuweze kuijenga Igunga.
Dr W Slaa,
nimependezwa na majibu yako yote.Na hili pia,isipokuwa hapo kwenye red ndiyo ungedelete.Nadhani inaweza kutafsirika na wengine ama kutumiwa vibaya, kwamba wewe kama kiongozi wa kitaifa huna uchungu na Igunga.
Ni ushauri tu,otherwise it is an excellent answer.
 
Dr. Suala la Arusha unalipotosha sana! Ukweli unaujua fika ila ulitaka uyafanye kama yale mliyoyafanya Hai ilimuichukue hiyo Manispaa lakini Dr. Ukweli ni kwamba CCM wanamadiwani wengi kuliko ninyi. Nasuala la muafaka kulisimamia ninyi makao makuu ya Chadema mnachokitaka ni kwamba CCM iingie kwenye mazungumzo ili kesi yenu inayohusu maandamano ifutwe. Kwa sisi tunaofuatilia siasa zenu kwa karibu tunalijua hili na wala usitumie kivuli hicho kuficha ubinafsi wako kwenye hili. Uliwapeleka Watanzania barabarani wakauwawa ili wewe unufaike kisiasa nani unadhani katika mazingira haya anapaswa kutoa pole kwa wafiwa kama siyo wewe Dr?
 
There are currently 219 users browsing this thread. (67 members and 152 guests)


nadhani hapo kwenye 152 wapo viongozi wengi tu wa CCM, sijui nikwanini wanaogopa kuja kujibu hoja humu? au ndo kikao cha CC kimekolea!!
ningependa washiriki kwenye huu mjadala.
 
Dr. Suala la Arusha unalipotosha sana! Ukweli unaujua fika ila ulitaka uyafanye kama yale mliyoyafanya Hai ilimuichukue hiyo Manispaa lakini Dr. Ukweli ni kwamba CCM wanamadiwani wengi kuliko ninyi. Nasuala la muafaka kulisimamia ninyi makao makuu ya Chadema mnachokitaka ni kwamba CCM iingie kwenye mazungumzo ili kesi yenu inayohusu maandamano ifutwe. Kwa sisi tunaofuatilia siasa zenu kwa karibu tunalijua hili na wala usitumie kivuli hicho kuficha ubinafsi wako kwenye hili. Uliwapeleka Watanzania barabarani wakauwawa ili wewe unufaike kisiasa nani unadhani katika mazingira haya anapaswa kutoa pole kwa wafiwa kama siyo wewe Dr?

unaweza ukatuwekea idadi ya madiwani wa CCM na wa CDM? pia kwani issue ni idadi ya madiwani au ni upindishwaji wa sheria zilizomuweka meya madarakani? soma vizuri majibu ya Dr. Slaa juu.
 
Nguruvi3,

Ahsante kwa maswali yako. Naomba niyajibu kwa pamoja ifuatavyo:-

1) Msingi wa mgogoro wa Madiwani Arusha ni Uvunjifu wa Kanuni, Taratibu na Sheria zinazoongoza uchaguzi wa U meya katika Manispa ya Arusha. Kamati ya Marando imebaini kuwa "mchakato na utaratibu mzima wa uchaguzi wa Naibu Meya haikuzingatia Kanuni na Taratibu za Chama na Halmashauri" (Marando Kif.4.2). Hivyo, kama Chadema ilipinga ukiukwaji katika uchaguzi wa Meya, haiwezi kamwe kuidhinisha ukiukwaji ambao kwa bahati mbaya ni maradufu zaidi katika uchaguzi wa Naibu Meya.

2) Ni kweli mazungumzo husika yalijulikana kwa ngazi ya Taifa. Mara ya kwanza Makao Makuu yalifahamu document ya mwafaka ya 15/4/2011, kwa kuona document tarehe 29/4/2011 katika Mkutano baina ya viongozi wa Madiwani akiwemo Mwenyekiti wao Mhe. Mallah na Mnadhimu Mkuu wa Kamati ya Madiwani Mhe. John Bayo. Kikao kilifanyika New Safari Hotel, Arusha chini ya uenyekiti wa Katibu Mkuu. Miniti za Kikao hicho zinaonyesha mambo 5 ambayo Katibu Mkuu alibainisha kama msingi wa mazungumzo yeyote kama yatakuwepo. Nayo ni:-

i)Serikali ikiri kosa kuwa kanuni na mwongozo wa uchaguzi wa Meya Arusha mjini zilikiukwa.
ii)Uchaguzi wa Umeya urudiwe kwa vile haukufuata kanuni na Taratibu.
iii)Serikali itoe pole kwa wahangaa tukio la tarehe 5 Januari 2011
iv) Serikali ipitie madai ya msingi ya Chadema ikiwa ni ni kuwawajibisha Mkurugenzi wa Manispaa (kwa sababu ndiye alivunja kanuni) na OCD wa Arusha mjini
v) Kesi ya ya Viongozi wa chama na baadhi ya wananchi haina msingi hivyo ifutwe.

Kisha kikao kilijadili document ya 15/4 na kuona ina mapungufu makubwa. Iliazimiwa ifuatavyo:-
1) Miniti hii ina hila na ni ya unafiki na hivyo isitumike katika kufikia muafaka wa suala la Umeya hapa Arusha mjini.
2) Mwenyekiti wa Madiwani Estomih Mallah na Mnadhimu wa Madiwani Mhe. John Bayo wawajulishe madiwani na Mkuu wa Wilaya kuwa muafaka huu kwa mujibu wa chama una mapungufu ambayo chama hakitaweza kuyaafiki na hivyo usitumike kwa kufikia muafaka wowote.
3) Kwa kutambua kuwa CCM wapo tayari kwa mazungumzo, Mhe. Katibu Mkuu atayapeleka mapendekezo ya muafaka huu kwa wanasheria wa chama ili kuyafanyia marekebisho na mapendekezo hayo yatakuwa ni sehemu ya mazungumzo kati ya Mwenyekiti wa Chama Mhe. Freeman Mbowe (MB, KUB na Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda.

Kwa bahati mbaya, tarehe 20/6/2011 Madiwani waliridhia mwafaka wao kama ulivyokuwa kwenye Hati yao ya tarehe 15/4/2011, na kuendelea na uchaguzi, bila kujali mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea kati ya Mhe. Mbowe na Waziri Mkuu. Isitoshe utaratibu wa kisheria wa uchaguzi wa Naibu Meya nayo ilikiukwa (kwa mujibu wa Taarifa ya Marando kukiwa na kugushiwa kwa saini ya Katibu wa Wilaya wakati pia hakuna kikao chochote cha Kamati Tendaji kilichojadili na kuteua mgombea wa Chadema). Hiki ndicho kilichofikisha Kamati Kuu kuelekeza Madiwani waliochaguana kinyume na Kanuni wajiuzulu ndani ya siku 3.

Baada ya hapo Madiwani 6 wakiongozwa na Mallah walikata rufaa, kwa bahati mbaya kwa mujibu wa Katiba na Kanuni za Chama rufaa zao hazikukidhi mahitaji ya Kikatiba na Kanuni. Maswala yote hayo sasa yanarudi mikononi mwa Kamati Kuu ambayo hivi Karibuni itatolea ufumbuzi swala la Madiwani kwa mujibu wa Katiba ya Chadema.


Hapo sasa ndio naamini kuwa kweli kulikuwa kuna kikao baina ya Pinda na Mbowe na sasa ndio naamini aliyosema Mallah kwenye mahojiano na TBC kuwa uongozi wajuu unajua kuhusu hatua za muafaka wa madiwani Arusha, kitu ambacho wewe mwenyewe Dokta Slaa ulikipinga ulipoulizwa na muandishi wa TBC.

Na wana chadema wengi hapa JF walikuwa wakipinga kuwa kulikuwa na muafaka baina ya Pinda na Mbowe. Sasa kwa nini bado mnachakachuwa? si mseme kweli tu?
 
Dr wa kweli na Dr wa heshima tofauti inajitokeza dhahiri.
Majibu aliyotoa Dr Slaa hapa nimesoma kitu fulani kinachonipa jibu ya kiwango cha elimu, busara na hekima aliyo nayo. Majibu haya yanaonyesha dhahiri kwamba
elimu ya rhetoric haikumchenga, si kama mtu aliyekuwa mpiga tebe bingwa pale bus terminal na kupewa jukwa kuanza kuvua tu watu nguo bila kujali kama kuna wakwe, wazazi, au dada zake.
 
FaizaFoxy unamatatizo makubwa,nakuomba uende kuombewa kama magamba wenzako wanavyoenda kwa nabii Joshua.

Halafu nimeshakufahamu,ukicheza nitareveal identity yako sasa hivi kama utaendelea kuleta dharau kwa kiongozi wetu ambaye kama sio uchakachuaji wa magamba angekua kiongozi wa nchi.
 
Back
Top Bottom