Matatizo ya ndoa kusuluhishwa ndani ya ndoa haliwezi likawa jibu la taasisi ya ndoa kuwa taasisi iliyo jaaa unafiki! Pengine hukuelewa vyema uzi hule.
Sikuona sababu ya wewe kuanzisha uzi huu ulitakiwa kujibu kulekule.
Kwangu mimi sioni ulicho jibu kabisa
Nimelazikimika kuisaka comment hii baada ya lara 1 kusema nimeikwepa na mimi ng`wana ong`wa kulwa si mtu wa kukwepa wala kuogopa sasa nitaijibu tufuatane.
...Anaanza kudai matatizo ya ndoa kusuluhishwa ndani ya ndoa haiwezi kuwa jibu la taasisi kuwa ni taasisi iliyojaa unafiki,jibu linabaki lilelile matatizo ya ndoa yatatuliwa na wanandoa wenyewe labuda wewe unajibu zuri liweke hapa wadau waona na wapime.
...Anadai haoni sababu ya kuanzisha uzi nilitakiwa nijibu kulekule,swahili hili ulitakiwa kumuuliza lara 1 kwanza kwa nini hakujibu kulekule kwa Mgiriki badala yake akaanzisha uzi wake ndo uje uniulize na mimi.
....Kwa manufaa ya wengine ni kuwa nilianzisha uzi huu ili kupanua mjadala wa kuonyesha kuwa ndoa si taasisi ya kinafiki heri ya mtu anaye kaa single na kujirusha kwa raha zake.
Nazidi kusisitiza kama kuna maisha ambayo mtu akiyakosa duniani atakuwa amekosa kitu muhimu ni ndoa.
...Unakuwa na mtu unayemwamini sana kwa kila kitu na yeye anakuamini sana,yeye ni kila kitu na wewe ni kila kitu kwake.
....Anaujua ukweli kuwa msingi wa ndoa si pesa ila ni upendo,pesa zinaweza kwisha lakini upendo utadumu daima.
.....Mtu amabaye pamoja na kuwa amesoma na ana kazi nzuri,ni mzuri,lakini hii haimfanyi asimuheshimu mmewe anaona mume ni baba kwake na mume anaona yeye ni mama kwake.
....Mtu ambaye siri za moyo wako zoooote unazibwaga kwake na huna hofu hata kidogo kwamba atazitoa nje.
....unakuwa na mtu ambaye yuko available wakati wote kwa shida yoyote ikiwa utahitaji tunda unapewa tena bila kusutwa na dhamiri/nafsi.
.....Mtu ambaye mmeweka malengo yenu yote mezani na mishahara yenu mezani mnatazama kilicho mbele kwa pamoja,siyo yule anadai mwanaume hagusi mshahara wangu kwani kanisomesha.
.....Mtu ambaye akitoa hoja ikikataliwa anakubaliana na hoja ya mwingine kwa amani si kununa kisa hajasikilizwa.
....Mtu ambaye unaamka tu unakuta chai tayari,nguo tayari unaambiwa karibu baba mezani hamuuachii house girl majukumu labuda awe kazini.
....Mtu ambaye haongozi ndoa yake kwa kutegemea muongozo wa wazazi wake.
....Mtu ambaye anajua miongoni mwamajukumu yake ni kumpikia chakula akipendacho mmewe si kila siku baby twende tukale hotel.
....Mtu anayesimamia mtoto katika maadili mema.
,..Mtu ambaye amekuwa ndugu na rafiki kwako wakati mwingine full utani mnakimbizana kama watoto mnacheka anakuangukia,anajilaza miguuni mwako we acha tu.nk.
Huyu ndiye mke ninayeishi naye ukiniambia ndoa ni unafiki wewe ndiyo utakuwa mnafiki.
...umesema hakuona nilichojibu sawa wewe hukuona wengine wameona nilichojibu otherwise kama ulitegemea nijibu kama unavyopenda hilo siwezi acha ukweli ujitetee kuwa ndoa na iheshimiwe na watu wote.