Majibu kwa lara 1

Majibu kwa lara 1

Ile mada ilikua ni Hamna cha Maana kabisa kinachoongelewa Zaidi ya kurundikana tu kule hoja za ajabuajabu! Nilipita mapema tu nikaiangalia lkn sikutaka kutia neno Coz niliona Hamna kitu pale!

Ulitakiwa ushushe nondo mkuu hata moja mbili.
 
Matatizo ya ndoa kusuluhishwa ndani ya ndoa haliwezi likawa jibu la taasisi ya ndoa kuwa taasisi iliyo jaaa unafiki! Pengine hukuelewa vyema uzi hule.

Sikuona sababu ya wewe kuanzisha uzi huu ulitakiwa kujibu kulekule.

Kwangu mimi sioni ulicho jibu kabisa


Nimelazikimika kuisaka comment hii baada ya lara 1 kusema nimeikwepa na mimi ng`wana ong`wa kulwa si mtu wa kukwepa wala kuogopa sasa nitaijibu tufuatane.
...Anaanza kudai matatizo ya ndoa kusuluhishwa ndani ya ndoa haiwezi kuwa jibu la taasisi kuwa ni taasisi iliyojaa unafiki,jibu linabaki lilelile matatizo ya ndoa yatatuliwa na wanandoa wenyewe labuda wewe unajibu zuri liweke hapa wadau waona na wapime.

...Anadai haoni sababu ya kuanzisha uzi nilitakiwa nijibu kulekule,swahili hili ulitakiwa kumuuliza lara 1 kwanza kwa nini hakujibu kulekule kwa Mgiriki badala yake akaanzisha uzi wake ndo uje uniulize na mimi.

....Kwa manufaa ya wengine ni kuwa nilianzisha uzi huu ili kupanua mjadala wa kuonyesha kuwa ndoa si taasisi ya kinafiki heri ya mtu anaye kaa single na kujirusha kwa raha zake.

Nazidi kusisitiza kama kuna maisha ambayo mtu akiyakosa duniani atakuwa amekosa kitu muhimu ni ndoa.
...Unakuwa na mtu unayemwamini sana kwa kila kitu na yeye anakuamini sana,yeye ni kila kitu na wewe ni kila kitu kwake.
....Anaujua ukweli kuwa msingi wa ndoa si pesa ila ni upendo,pesa zinaweza kwisha lakini upendo utadumu daima.
.....Mtu amabaye pamoja na kuwa amesoma na ana kazi nzuri,ni mzuri,lakini hii haimfanyi asimuheshimu mmewe anaona mume ni baba kwake na mume anaona yeye ni mama kwake.
....Mtu ambaye siri za moyo wako zoooote unazibwaga kwake na huna hofu hata kidogo kwamba atazitoa nje.
....unakuwa na mtu ambaye yuko available wakati wote kwa shida yoyote ikiwa utahitaji tunda unapewa tena bila kusutwa na dhamiri/nafsi.
.....Mtu ambaye mmeweka malengo yenu yote mezani na mishahara yenu mezani mnatazama kilicho mbele kwa pamoja,siyo yule anadai mwanaume hagusi mshahara wangu kwani kanisomesha.
.....Mtu ambaye akitoa hoja ikikataliwa anakubaliana na hoja ya mwingine kwa amani si kununa kisa hajasikilizwa.
....Mtu ambaye unaamka tu unakuta chai tayari,nguo tayari unaambiwa karibu baba mezani hamuuachii house girl majukumu labuda awe kazini.

....Mtu ambaye haongozi ndoa yake kwa kutegemea muongozo wa wazazi wake.
....Mtu ambaye anajua miongoni mwamajukumu yake ni kumpikia chakula akipendacho mmewe si kila siku baby twende tukale hotel.
....Mtu anayesimamia mtoto katika maadili mema.
,..Mtu ambaye amekuwa ndugu na rafiki kwako wakati mwingine full utani mnakimbizana kama watoto mnacheka anakuangukia,anajilaza miguuni mwako we acha tu.nk.
Huyu ndiye mke ninayeishi naye ukiniambia ndoa ni unafiki wewe ndiyo utakuwa mnafiki.

...umesema hakuona nilichojibu sawa wewe hukuona wengine wameona nilichojibu otherwise kama ulitegemea nijibu kama unavyopenda hilo siwezi acha ukweli ujitetee kuwa ndoa na iheshimiwe na watu wote.
 
Asante na wewe kwa maneno yako umekubali kuwa ndoa ni moja ya taasisi zilizo jaa unafiki ili kulinda desturi!
Ni heri tufe na yetu ya chumbani ili kulinda desturi na si sheria.

Na hapo katika kuchagua ya kusema huwa yanasemwa mazuri tuu!

Sioni wapi UNAFIKI unakuja katika swala zima la kuwa na PRIVACY ya ndoa yangu. Labda sielewi nini maana ya UNAFIKI.
...Kutoelewana kupo baina ya watu wawili wakiishi pamoja, iwe ndugu au wanandoa. Kutoa mambo ya ndani ni moja ya weakness katika taasisi hii, that's how we've been taught-to keep our issues inside us, and that's what makes us stronger.
..Labda nikuulize, wewe kila linalokusibu (as a bachelor) unalitoa kwa watu? Si unatafuta suluhu na watu wako wa karibu, kwa nini usiseme kwa kila mtu kuwa una matatizo? Mbona usiende kila nyumba kusema shida zako---kumbe huo sio unafiki...!!!
..Anways, marriage wasn't meant for everyone to exercise.
 
Sioni wapi UNAFIKI unakuja katika swala zima la kuwa na PRIVACY ya ndoa yangu. Labda sielewi nini maana ya UNAFIKI.
...Kutoelewana kupo baina ya watu wawili wakiishi pamoja, iwe ndugu au wanandoa. Kutoa mambo ya ndani ni moja ya weakness katika taasisi hii, that's how we've been taught-to keep our issues inside us, and that's what makes us stronger.
..Labda nikuulize, wewe kila linalokusibu (as a bachelor) unalitoa kwa watu? Si unatafuta suluhu na watu wako wa karibu, kwa nini usiseme kwa kila mtu kuwa una matatizo? Mbona usiende kila nyumba kusema shida zako---kumbe huo sio unafiki...!!!
..Anways, marriage wasn't meant for everyone to exercise.

Loh mkuu umekuja na point muhimu sana kumbe kila siri tunayotunza iwe ya kazini,nyumbani ni unafiki? .....
 
Ile mada ilikua ni Hamna cha Maana kabisa kinachoongelewa Zaidi ya kurundikana tu kule hoja za ajabuajabu! Nilipita mapema tu nikaiangalia lkn sikutaka kutia neno Coz niliona Hamna kitu pale!

kweli Ntuzu wanataka kuamisha jamii maisha ya kujirusha kuigiziwa mitulinga ya kila namna wanaachwa wanagugumia maumivu,kutoa mimba,kulamba viatu vya wenye pesa wakiogopa kuachana nao maana picha zao za utupu wataziona kwenye mitandao,kutumiwa na mijamaa hali wanajua hayana future nayo eti ndiyo maisha ulinganishe na ndoa?
 
Mwenyewe ingawa sijaolewa kiukweli ndoa na iheshimiwe na watu wote siwazi kuiongelea vibaya wakati sijaingia wala sina experience matatizo yako kila.mahali tu ku learn kwa watu walioshindwa lazima ukate tamaa changamoto zipo kila mahali ndoa na iheshimiwe na watu wote

price sayuni ni kweli kabisa. mbona maisha ya kusaka mkate! watu wanapambana nayo kila siku hawajawahi kukata tamaa kila siku wamo kwa nini kwenye ndoa ikitokea changamoto na wanandoa wanapojaribu kuitatua wao wenyewe iitwe unafiki?
 
Ulitakiwa ushushe nondo mkuu hata moja mbili.


Vema!

Kuna nondo Unaweza kushusha iwapo kuna watu wapo tayari kuzipokea! Lkn km tayari kuna msimamo hasi unafikiri hizo nondo zitapokelewa? Ni sawa Na kumpigia Mbuzi Gita!

BTW, huwezi kuja kudai ndoa ni unafiki BILA KUTUAMBIA KUA NDOA NI NINI? sasa km hujatuambia ndoa ni nini iweje uite ni UNAFIKI?

Nimeona Mkuu Eli79 Ktk post yake moja hapo Juu akimjibu Ruta, ameleeza vichache Na vzr! Nafikiri wengi huingia Ktk mahusiano ACHILIA NDOA KINAFIKI NA NDIO MAANA NDOA ZINAONEKA ni km UNAFIKI! Lkn UNAFIKI mkubwa ni huu Wa Kua ETI NA VUMAHUSIANO VYA UBOYFRIEND NA UGIRLFRIEND! Huko ndio kuna UNAFIKI mkubwa Na utapeli Na ngono zembe kutokua waaminifu Na ni kinyume Na KANUNI ZA MUNGU PIA KUA KTK MAHUSIANO KABLA YA NDOA!
 
Last edited by a moderator:
Hujanielewaa! Ndoa naipa nafasi nyingi SEMA ULE UZI ULIKUWA MAALUMU KWA SIFA HII YA HYPOCRICY!

Hapo ndiyo kwenye tatizo huwezi chukua hata jema moja kwenye ndoa ila hilo ulilobumba siyo?,unapoona ndoa ni unafiki inamaana wazazi wetu kukaa paomoja ni wanafiki? ni kweli sisi na vielimu vyetu hivyi vya .com tumekuwa werevu kuliko wazee wetu hata kuita ndoa ni taasisi ya unafiki heri kujirusha?

Je watoto tunaozaa,dada zetu ni maneno ya kuwaambia haya ndoa ni unafiki wajirushe kwa raha zao?

NDOA NA IHESHIMIWE NA WATU WOTE.
 
Sioni wapi UNAFIKI unakuja katika swala zima la kuwa na PRIVACY ya ndoa yangu. Labda sielewi nini maana ya UNAFIKI.
...Kutoelewana kupo baina ya watu wawili wakiishi pamoja, iwe ndugu au wanandoa. Kutoa mambo ya ndani ni moja ya weakness katika taasisi hii, that's how we've been taught-to keep our issues inside us, and that's what makes us stronger.
..Labda nikuulize, wewe kila linalokusibu (as a bachelor) unalitoa kwa watu? Si unatafuta suluhu na watu wako wa karibu, kwa nini usiseme kwa kila mtu kuwa una matatizo? Mbona usiende kila nyumba kusema shida zako---kumbe huo sio unafiki...!!!
..Anways, marriage wasn't meant for everyone to exercise.



Mkuu Eli79 umeongea vitu vichache lkn vinagusa baadhi ya Maana ya ndoa! Sio mtu aje hapa aseme ndoa ni UNAFIKI bila KUTUAMBIA ni Maana ya ndoa!

Mimi ambae napenda mambo ya Kiroho nionapo haya Naona ni muendelezo Wa Kauli za kishetani kupingana Na Mungu! Maana Mungu ametuagiza wanadamu tuoane lkn leo tunapoita ndoa ni UNAFIKI tunahararisha UZINZI NA UASHERATI NJE YA NDOA! Sasa hii MACHUKIZO MBELE ZA MUNGU!
 
Last edited by a moderator:
Achana nao. Baki na msimamo wako

Sita waacha nakaba mpaka
penati uongo ukisemwa sana utaonekana ndiyo ukweli wapo dada zetu hawajaolewa hii kauli inaweza wavunja moyo na kuanza maisha ya ufuksa ambayo hayana tija hata kidogo.

Ndoa na iheshimiwe na watu wote.
 
Mie sikumwelewa Lara maana niliona mkanganyiko,kimombo mara kiswahili!mbwembwe tu nikapita!

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
kweli Ntuzu wanataka kuamisha jamii maisha ya kujirusha kuigiziwa mitulinga ya kila namna wanaachwa wanagugumia maumivu,kutoa mimba,kulamba viatu vya wenye pesa wakiogopa kuachana nao maana picha zao za utupu wataziona kwenye mitandao,kutumiwa na mijamaa hali wanajua hayana future nayo eti ndiyo maisha ulinganishe na ndoa?


Mkuu, mi Ktk hiyo mada nilikaa pembeni tu Na Kua mtizamaji tu!

HAKUNA KITU KIZURI NA KITAMU NA CHENYE FURAHA HAPA DUNIANI KM NDOA! Na ndio MAANA SISI TUMEFUNGA NDOA NA BWANA YESU KRISTO! NA NDOA YETU NA KRISTO HAINA UCHAKACHUAJI WA AINA YOYOTE ILE NA SISI NDOA ZETU ZATUPASA KUA SAFI!

Ukitizama MAANA YA UPENDO KIROHO BASI NDOA ITAKUA POUWA!

Wengi wanaingia Ktk mahusiano KINAFIKI Na hawana upendo Wa kweli wamefata vitu au wanakua Na sababu zao Na ndio Maana huzaa ndoa za KINAFIKI LUKUKI!
 
Ndoa ni nzuri na ni tamu sana asemae ndoa mbaya huyo haijui ndoa achiliambali ndoa zakukurupuka watu wamekutana bar,wamimbishana,wamefumaniwa au mtu kamuona dada/kaka anapesa na kigari cha mkopo hiyo sio ndoa ila ndoana , Ndoa hasa inapangwa na Mungu na ndio maana ukaambiwa upo wakati wakuoa/kuolewa lakini hakuna umri wakuoa /kuolewa hata mtu afikishe 40 sio issue bado anaweza kuwa na ndoa bora na tamu. Kikubwa ni wanandoa wenyewe kuiheshimu hiyo ndoa.


Kweli mkuu mke mwenye busara mtu hupewa na Bwana.
 
Ndio maana nimekwambia ndoa hazifanani... Kila watu na style yao. kama ndugu/ shosti wako anawaamsha matisa ya usiku, ana emoro, kaharibu wtt sijui, ni ndoa yao, siyo zetu. You cannot generalize huo mfano wako kwa kila ndoa.

and, there is nothing wrong with being 40 and single.. as long as you are emotionally and mentally satisfied with your choice

Hata huyo shosti anayeomba ushauri wa lara 1 kwenye ndoa atakuwa ana matatizo anataka ushauri kwa mtu anayefurahia akiona walioko kwenye ndoa wanagombana?na kuita ni wanafiki kama ni shosti yake atakuwa na tabia kama ya rafiki yake ni ngumu kuimudu ndoa.
 
Vema!

Kuna nondo Unaweza kushusha iwapo kuna watu wapo tayari kuzipokea! Lkn km tayari kuna msimamo hasi unafikiri hizo nondo zitapokelewa? Ni sawa Na kumpigia Mbuzi Gita!

BTW, huwezi kuja kudai ndoa ni unafiki BILA KUTUAMBIA KUA NDOA NI NINI? sasa km hujatuambia ndoa ni nini iweje uite ni UNAFIKI?

Nimeona Mkuu Eli79 Ktk post yake moja hapo Juu akimjibu Ruta, ameleeza vichache Na vzr! Nafikiri wengi huingia Ktk mahusiano ACHILIA NDOA KINAFIKI NA NDIO MAANA NDOA ZINAONEKA ni km UNAFIKI! Lkn UNAFIKI mkubwa ni huu Wa Kua ETI NA VUMAHUSIANO VYA UBOYFRIEND NA UGIRLFRIEND! Huko ndio kuna UNAFIKI mkubwa Na utapeli Na ngono zembe kutokua waaminifu Na ni kinyume Na KANUNI ZA MUNGU PIA KUA KTK MAHUSIANO KABLA YA NDOA!
Exactly my point mkuu...!
...Sijui wenye hoja ya kuhusisha NDOA--->UNAFIKI wanaliangalia vipi swala la URAFIKI(NGONO)--->UNAFIKI? Au huo ni unafiki wa waziwazi, mimi sijui. Lakini katika mahusiano yasiyo rasmi kuna UNAFIKI mwingi sana, kutatishana tamaa kwingi sana, kupotezeana mda na malengo. Au kwa vile watu wamejichokea, wametafuta MR/MISS RIGHT na hapatikani ndio maana wameona kurusha mawe kwenye taasisi iliyobarikiwa na MUNGU ndio UNAFIKI.

Lakini pia mkuu Ntuzu, tuangalie na hisia kwa nyakati tofauti. The same people who criticise marriage leo, wiki/mwezi/mwaka iliyopita walihitaji sana kuwa ndani ya hii taasisi, lakini uwezekano kuwa mambo hayakwenda walivyotarajia kumewakatisha tamaa na wanaona bora wakatishe wenzao tamaa.

"Hata hivyo, ndoa haikuwekwa kwa ajili ya watu wote, wengine watabaki hivyo''
 
Last edited by a moderator:
Hii ni sawa na hadithi ya nyani 'Sizitaki mbichi hizo'
Nyani aliziona ndizi mbivu zilizomvutia zikining'ing'inia juu ya mgomba wake. Akatamani azipatte kwa kuzirukia ili azichume ale. Aliruka mara ya kwanza. Ikabakia kidogo kuzifikia. Akajaribu mara ya pili huku akiongeza nguvu zaidi, lakini kwa bahati mbaya hakuzifikia tena. Akajaribu mara ya tatu, uwezo wake wa kuzifikia uliendela kupungua kuliko hata alivyoanza. Kwa kukata tamaa ndipo akasema 'SIZITAKI MBICHI HIZI' Wenye kujua fasihi wanaweza sasa kumwelewa lara 1 kuandika alivyoandika. Mara nyingi huyu lara 1 huandika juu ya ndoa au wanaume. Mimi nadhani hayo ndiyo anayowazana hulazimika kutumia njia ya kuandika ili kupunguza msongo wa mawazo. Tiba mojawapo ya kukabiliana na msongo wa mawazo ni kuandika.


tehetehe great thinker
 
SASA MNACHOLIA LIA GENERALISATION IHESHIMIWE NA WATU WOTE NINI??? Au WOTE manake nini? Tulizeni ball kabisaaaaa! Usipoheshimu yako mimi hio watu wote tukuheshimu kama mazombi wakti mwenyewe mufilisiiii mtanisamehe!

Ndoa ya wenzio lazima uiheshimu wacha waishi maisha waliyoyachagua wao eti yule mama anateseka kwenye ndoa inakuhusu nini? wewe mbona hutuambii wanaume wanaokutenda?.Ndoa na iheshimiwe na watu waote.
 
Back
Top Bottom