Maisha Plus Tv Show ya Masoud Kipanya

Maisha Plus Tv Show ya Masoud Kipanya

Mimi naona ni Bigbrother ya Bongo! Vijana wako 18 na wanajaribu kuishi maisha ya kijima!

Wakati wa usaili wa vijana hawa nilijifunza kitu kimoja. Watanzania wengi tu wajinga wa kutupa (labda wengine kati yetu tu wapumbavu)! Kuna vijana waliulizwa waoneshe IQ au Black box zao ziko sehemu gani ya mwini na kweli wakawa wanazitafuta hata kwenye vidole vya miguu. Na kuna mwingine alisema voice box yake iko karibia na magoti! Nadhani hizo tapes wampelekee JK na Timu yake

Kuhusu vijana wenyewe sitaki kusema mengi. Jaribu kufuatilia mwenyewe!

Kama waliwalenga vijana wa vijijini au wale ambao kiwango chao cha elimu hakikuwa kigezo katika usaili huo, nadhani ilikuwa ni makosa kuyahusisha maneno kama IQ au Black box katika huo usaili . Hasa ukizingatia kuwa lugha ya taifa si Kiingereza, na lugha ya kufundishia bado ni ugonjwa wa taifa.
 
KP ni kijana anayejitahidi sana,angekuwa ni mwekezaji wa nje kaandaa Maisha Plus tungemsifia,lakini kwa kuwa ni Mtanzania mwenzetu tunamponda...
Ndio kuna mapungufu mengi katika Maisha Plus lakini tumtie moyo... Na sio kumbeza..
MASOUD KIPANYA BIG UP!!!!

Jambo la maana kubwa ni kumsaidia na kumshauri Masoud katika kuendesha kipindi chake. Kumbeza hakutasaidia kwani tayari jamaa yupo hewani.

Napatwa na wasiwasi na wandugu wengine hasa wale mlioangalia kile kipindi.... nadhani kingekuwa cha Kizungu/kiingereza kingekuwa ni bora zaidi kwao!

Sijui hapa tatizo ni Masoud au lugha au...?

Tumsaidie ili aboreshe kipindi chake. Kwanza amejitahidi sana kwa namna moja au nyingine hadi kufikia pale. Big up Masoud.

Jama wa JF, Masoud anahiji kupongezwa kwa ubunifu aliounonesha. Ni kweli kuna mapungufu mengi tu lakini tukumbuke ndo kwanza ameanza next time atakapoandaa tena nafikiri atafanya vizuri kuanzia jinsi ya kuwatafuata hadi huku kijijini. Tuchukilie mfano wa Bongo Star search ya madam Rita ilivyoanza, ilianza ikiwa na mapungufu lakini ilivyokuja kwa mara ya pili angalau ilionesha kubadilika ukikompare na ile ya kwanza, naamin hata Masoud ataimprove huko mbeleni.

Ila nashauri wangetoa maybe email address au namba ya simu kwa ajili ya kupokea maoni ya watazamaji.

Keep it up KP!!!!!!!

Hapo umenena mkuu, kwanza kama yupo mhudumu karibu hebu pewa kamoja baridi. Nadhani ni athari za utumwa na ukoloni watu kuona vya kitanzania ni vibaya kushupalia kuponda tuuu!!Kijana wa kitanzania kaanzisha kitu hakina hata muda mfupi badala kuangalia ni jinsi gani anaweza kurekebisha hayo mapungufu watu wanaanza kumpambanisha na big brother, acheni hizo toeni mawazo jenzi sio bomozi. Kwa tasnia ya runinga bado changa na bado tuna safari ndefu, akina masoud wamefungua njia na sisi tu fuate au kama hatuwezi ni bora tukawasaidia badala kukimbilia kumfananisha na big brother. Ungekuwa unajua gharama za kuandaa show ya big brother ana gharama anazotumia masoud ungempongeza KP.

Kama waliwalenga vijana wa vijijini au wale ambao kiwango chao cha elimu hakikuwa kigezo katika usaili huo, nadhani ilikuwa ni makosa kuyahusisha maneno kama IQ au Black box katika huo usaili . Hasa ukizingatia kuwa lugha ya taifa si Kiingereza, na lugha ya kufundishia bado ni ugonjwa wa taifa.

Haraka haraka, kuna watu wamegusia mfumo wa elimu na tunakolipeleka taifa! kijana wa sasa ni tofauti sana na vijana wa zamani , tunajua utandawazi unavyodumaza ubongo! kama mwendesha kipindi ana tatizo, na wahusika wana matatizo zaidi, then this is starting point ya kujua taifa liko wapi.

Anyway nampongeza huyu kijana , japo naye anataka shule, he is doing right things though.
 
Big up masoud wa kipanya, wasikudiscourage wala nini. Komaa we just fanya marekebisho. Kuna sehemu za kutolea maoni jamani, kama vile mail ambayo wanadisplay kila kipindi kinapokuwa hewani
 
Me nadhani tukimsifia tutakuwa tunampa kichwa bure ukiangalia hiyo show anaiga karibu kila kitu kutoka big brother, ajaribu kuwa creative na sisi tutamuunga mkono.
 
Me nadhani tukimsifia tutakuwa tunampa kichwa bure ukiangalia hiyo show anaiga karibu kila kitu kutoka big brother, ajaribu kuwa creative na sisi tutamuunga mkono.

Wewe umecreate nini?
 
Haraka haraka, kuna watu wamegusia mfumo wa elimu na tunakolipeleka taifa! kijana wa sasa ni tofauti sana na vijana wa zamani , tunajua utandawazi unavyodumaza ubongo! kama mwendesha kipindi ana tatizo, na wahusika wana matatizo zaidi, then this is starting point ya kujua taifa liko wapi.

Anyway nampongeza huyu kijana , japo naye anataka shule, he is doing right things though.

Ni show ya Masoud imetupa firsa ya kuchanganua hapa. Tunachanganua kuhusu swala la elimu etc and we got this from that show... Hatuwezi kusema ni useless. Ni msingi wa kitu cha msingi na cha muhimu siku zijazo baada ya masahihisho muhimu toka kwa wadau.

Ukiangalia Maisha plus ina ladha ya ki_JKT... which i know it can activate some domant potentials..zinazo dumazwa na utandawazi etc... na ni kweli trough the whole thing tunagundua umakini usiokuwepo kwa masood na vijana wake kwenye swala zima la elimu na integrity.... vimaswali wanavyoulizana ...na Vimajibu.... vinavyotolewa.... na main theme...na ..nini hasa kinatakiwa kuwa achived pale ..kuna namna hakijitokezi vizuri...kimechwa loose ...!! Ni kama panatakiwa mtu meenye qualification zaidi kidogo ku smoothen the program!!

Lakini hakuna sababu ya msingi ya kutokumpongeza kijana wetu...
 
Kusema kweli jamaa anajitaidi sana,Nina uhakika kabisa wote tulikuwa nauhakika kwamba kutakuwa na mapungufu,hasa kwa kuwa tayari tuna reference.

kama katika show ya jana,ilikuwa bomba sana.Kama kweli jamaa walilala na njaa na kushindia ugali na mlenda,itawafanya washiriki waanze kuactivate potential zao ili waweze kuishi.pia jana niligundua kuna kitu tunaweza kujifunza kutoka maisha plus.Cha kufanya ni kumpa moyo na kumuelekeza nini kifanyike kwa mtazamo wako ili show izidi kupendeza.

Kusema ile kweli,mwanzo mzuri tena sana hasa ukizingatia na uwezo wa kiuchumi na kiteknolojia tulionao.
 
Yep, mimi nimetazama kile kipindi mara tatu, wala sikujua kinataka kufundisha nini. Kina sound so fake sioni originality ya watu wenyewe. bora big brother kwani inaweza kumfanya mtu awe au afanye kama angekuwa kwingineko. Kwanza hiyo maisha plus sio eti kun hidden camera hivyo kumfanya mtu awe not very original since anajua kamera inakuwa inamchukua. Vitu vyenyewe wanavyo fanya kwenye kijiji wala havieleweki vinamjenga nini mtu pale ili awe nini! probably am wrong kwa kuwa sijafuatilia kiundani. Masood mwenyewe is so much involved to the extent i feel inabore sana.... dont know. but to me i dont get anything out of it rather than waste of time!



Tuwape muda wajameni. Mambo hayawezi kuanza na kuwa bomba muda huo huo. Bila shaka mwakani au next time watafanya improvement
 
Masudi kwa ujumla pamoja na mapungufu kiasi anahitaji pongezi tena sana tuu! ameonyesha ubunifu wake na nadhani pia tunatakiwa kumpa ushauri pale tunapoona amekwenda kombo kidogo! wengi huwa tuko kimya na hata tuna wazo kichwani hatulitoi ila wazo linapotolewa na mtu mwingine ndipo tunatafuta makosa, ni kama mpira ukiwa nje unaona makosa kibao ukiingia wewe unaweza kufanya madudu zaidi ya uliyokuwa unayaona..Kijana anastahili pongezi
nimeangalia kipindi cha jana na kimenipa mvuto mno...natamani jioni ifike nione hatma ya wali walume waliolala njaa
 
Mimi maisha plus imenifunza mengi maisha plus, hasa kipindi cha usaili. Inasikitisha sana, elimu ya vijana wetu sasa ni almost zero. Vijana hawana hata ufahamu wa kawaida tu, yaani kweli kabisa zile tape apelekewe jk aone taifa lake linapoelekea, kama ataweza ajitahidi kufanya mapinduzi makubwa sana kwenye elimu, hasa shule za serikali ambako watoto wetu wengi wanasoma. Maoni yangu akiboresha mapato ya walimu wake (serikalini) bila shaka tutasonga mbele, otherwise kazi ipo, hatujui taifa lijalo litakuwaje.
 
Ukiangalia Maisha plus ina ladha ya ki_JKT... which i know it can activate some domant potentials..zinazo dumazwa na utandawazi etc... na ni kweli trough the whole thing tunagundua umakini usiokuwepo kwa masood na vijana wake kwenye swala zima la elimu na integrity.... vimaswali wanavyoulizana ...na Vimajibu.... vinavyotolewa.... na main theme...na ..nini hasa kinatakiwa kuwa achived pale ..kuna namna hakijitokezi vizuri...kimechwa loose ...!! Ni kama panatakiwa mtu meenye qualification zaidi kidogo ku smoothen the program!!

Lakini hakuna sababu ya msingi ya kutokumpongeza kijana wetu...


Heshima mbele mkuu, ila huo uchanganyaji wa lugha ukizidi sana hata maana ya ujumbe wako inapotea, na imani ulilotaka kutueleza ungetumia mojawapo ya hizo lugha mbili ulizozitumia ungeeleweka zaidi.
 
At least kijana anaonyesha ubunifu flani ambao tunatakiwa kumpongeza na kutakiwa kumsaidia kwa mawazo ili aboreshe vizuri.Huu ni mwanzo tu, nakumbuka siku za nyuma watu wengi walikuwa wakiwaponda waigizaji wa filamu za kibongo lakini hivi sasa asilimia kubwa ya watu wanazikubali filam za vijana wetu. (kanumba/ray na wengine wengi).
 
Mtazamo wangu Serikali ya Tanzania sasa imefika wakati wa kuacha kufanya Masikhara na mfumo wa elimu hususan kwa vijana ambao ndio nguvukazi na tegemeo kubwa kwa maendeleo ya Taifa. Ni ukweli usiopingika vijana wamepoteza dira ya kielimu, morali wa kujifunza umepungua sana among vijana, wengi wetu hatuna ufahamu wa kina kuhusu mambo mbalimbali ya msingi yanayoiathiri dunia na jamii kwa ujumla, wengi huishia kusoma vichwa vya habari magazetini na kuridhika bila kupata habari kwa undani, wakati taarifa ya habari kwenye luninga si ajabu kumkuta kijana akibadilisha channel kutafuta channel yenye maigizo ama bongo fleva. Ni nadra sana kumkuta kijana wa kisasa kama wengi wanavyojiita (hususan age btn 7 - 28) ana ratiba ya kwenda Library kujisomea na kujifunza ama kupata ufahamu katika nyanja mbalimbali.
Serikali kama Serikali ina uwezo mkubwa na wakutosha kuweza kujenga mazingira na motisha kwa namna ambayo itawafanya vijana wajijengee tabia ya kupenda kujifunza.
Nadhani pia Magazeti ya udaku yangeongezewa kodi hata kwa asilimia 600% zaidi ili ku-discourage manunuzi ya magazeti hayo among vijana ambao wengi huishia kutafuta na kusoma habari za udaku zaidi kuliko kusoma vitabu na majarida yenye kujenga kwowledge.
Bei ya vitabu vya kujenga knowledge na tafiti ipunguzwe kwa asilimia kubwa ili kuwapa vijana uwezo wa kuvi-afford.
Naomba niishie hapa kwa sasa, ila bado nna mengi ya kuchangi kuhusu hili suala.

Tunavuna tulichopanda..uvivu wa kujisomea ni matokeo ya ile mikakati tuliyoipa msukumo mkubwa wa vijana kufanya tuition zaidi.
Library ni msaada mkubwa wa vijana kuongeza knowledge lakini hazitumiki ipasavyo sasa hivi. Na hata hizo library zilizopo karibu nchi nzima, mpaka za vyuo vikuu, hazina vitabu vya kutosha au ni zina vitabu vya muda mrefu sana.
Inatisha hii hali ya kuwa wavivu wa kujisomea.Masihala masihala haya, Inaweza kuja muda hapa tukawakaribisha investors wa kuja kutusomea somea vitu vyetu mana wenyewe hatuna muda wa kusoma. Kazi kwelikweli
 
Kwanini mara nyingi huwa tunapenda kukosoa tu miradi inayoanzishwa na wajasiliamali wa kitanzania bila hata kutoa maoni ya namna miradi hiyo ingepaswa kuboreshwa? Hivi ni wivu au ni sababu ya utumwa wa tulionao kwa mambo tunayofikiri mazuri ya nchi za wenzetu walikoendelea?

Tunakosoa show za kwenye TV, tunakosoa Movie za kibongo, tunakosoa wasanii wetu (bongo favouvers), sasa tutaanzia wapi kuendelea? kwani hao walioendelea si walianzia huku tuliko sisi ndugu zangu?

Si vibaya kukosoa, lakini tufanye hivyo na kutoa ushauri namna ya kuboresha ili kuwapa nguvu wajasilimali wetu kuendelea zaidi na zaidi!
 
MTM;392175]Dark City... Thanks!
Kweli kuna viazi mule hadi basi lakini Nadhani sio fair kulinganisha vijana wa maisha plus na ku-conclude kwamba majority wa vijana wako hivyo, kimtazamo naona sio wengi ambao ni mambumbu, tunaowaona mambumbu kwenye maisha plus ni wale wasio na alternatives you can just tell from their looks wako na background gani...

Mkuu MTM, mimi ni miongoni mwa wafuatiliaji na mdau wa elimu hapa TZ. Pia nimefuatilia Maisha Plus toka kwenye usaili. Hawa unaowaona ndio wamefanya vizuri, yaani ni ndio vipanga walioweza kuvuliwa katika ziwa la vijana wa Tz. Amini usiamini hali ni mbaya sana.

kumbuka showbiz bongo bado hailipi na ni alternative ya walioshindwa mainstream life tofauti na developed world where elimu inaweza kuwa alterantive ya walioshindwa sports and entertainment.

Kuna ukweli ndani yake ila kiwango cha kutoelewa kwa hawa vijana, wengine wakisema wamemaliza kidato cha sita ni cha chini sana. Hii imenigusa sana na ikanikumbusha mtoto mmoja ambaye tulimfanyia tathmini baada ya kumaliza darasa la saba na kukuta uelewa wake ni sawa na darasa la 4. Tulimfundisha kuanzia kiwango hicho na sasa yuko Chuo kikuu. Hawa vijana si wapumbavu bali ni wajinga. Kwa maana hiyo wanaweza kufundishwa wakafanya maajabu!

Jaribu kuangalia debates programs hapohapo TBC kwa watoto wa sekondari wapo wanaojitahidi sana tofauti na maisha plus

Ndugu yangu, vijana ambao wanachapa mjadala kwa pointi za nguvu siku hizi wanahesabika. Hata kwenye hiyo mijadala ya TBC1 ambako naamini wanachua wakali tu bado vijana wanapwaya!
Kwa uelwa wangu, tabia zote za binadamu na viumbe wengine zinatengeneza kitu kinaitwa normal distribution. Kwa hili la elimu, ina maana unakuwa na 75% ya watu wakiwa na upeo mzuri tu (average scores) na 12.5% wakiwa wajinga sana wakati 12.5% nyingine wanakuwa vipanga (super genius). Sasa hapa kwetu inakaribia 60-75% wako hoi. Kama ni mfuatiliaji utakuwa umesikia mfano wa mwanafunzi wa chuo kikuu kimoja hapa nchini aliyebadilishiwa kozi (yeye alitaka kusoma wildlife management) akaandika barua ambayo ni kituko sana; akisema kuwa hakubaliani na uamuzi wa kuhamishwa kozi kwa sababu malengo yake ni kuwa wild animal (mnyama wa mwitu) akishamaliza shule. Hali kwa hao vijana wengi unaoona ni bora, ambao wako elimu ya juu ni kama ya huyo ndugu yetu anayetamani kuwa wild animal.
 
Kwanini mara nyingi huwa tunapenda kukosoa tu miradi inayoanzishwa na wajasiliamali wa kitanzania bila hata kutoa maoni ya namna miradi hiyo ingepaswa kuboreshwa? Hivi ni wivu au ni sababu ya utumwa wa tulionao kwa mambo tunayofikiri mazuri ya nchi za wenzetu walikoendelea?

Tunakosoa show za kwenye TV, tunakosoa Movie za kibongo, tunakosoa wasanii wetu (bongo favouvers), sasa tutaanzia wapi kuendelea? kwani hao walioendelea si walianzia huku tuliko sisi ndugu zangu?

Si vibaya kukosoa, lakini tufanye hivyo na kutoa ushauri namna ya kuboresha ili kuwapa nguvu wajasilimali wetu kuendelea zaidi na zaidi!

Hii tabia ni mbaya sana kwa sababu inaua vipaji, kwa sababu watu wengi wanashindwa kujaribu kwa kuogopa kutupiwa madongo. KP ni mbunifu kwa mambo mengi na hili mojawapo (hata kama kaiga kwa sababu yeye si wa kwanza).

Naamini atakuwa na nafasi ya kupokea maoni au washikaji wanaopita humu wataweza kumpa baadhi ya maoni mazuri mnayotoa. Itakuwa vizuri pia wenye ushauri wampatie. Ila hata wale ambao wana maoni tofauti wayatoe ili kama yanaweza kusaidia yaonekane kwa wadau. Ujamaa ulishaisha na sasa watu wanatakiwa kujitafutia jinsi ya kuishi bia kuiba au kufisadi. Na hapa ndipo suala la ubunifu linapokuwa la muhimu sana.

Mwenye namba yake ya simu atuwekee hapa tumtwangie. Nitakuwa wa kwanza kumtia moyo. Ila kama ningekuwa mjanja basi hii kwangu ingekuwa fursa ya kutegeneza mradi kwani wateja wapo (vijana wajinga walio na kiu ya kujiendeleza). Kazi nzuri KP
 
Me nadhani tukimsifia tutakuwa tunampa kichwa bure ukiangalia hiyo show anaiga karibu kila kitu kutoka big brother, ajaribu kuwa creative na sisi tutamuunga mkono.

mzeee umesahau siku hizi ni mwendo wa copy, paste and edit! ukija na jipya kila mtu atalichukua na kuliboresha zaidi...na ukisubiri uwe na jipya utasubiri hadi uzeeke bila kutoa mchango wowote humu duniani..sana sana labda mbolea
 
Yep, mimi nimetazama kile kipindi mara tatu, wala sikujua kinataka kufundisha nini. Kina sound so fake sioni originality ya watu wenyewe. bora big brother kwani inaweza kumfanya mtu awe au afanye kama angekuwa kwingineko. Kwanza hiyo maisha plus sio eti kun hidden camera hivyo kumfanya mtu awe not very original since anajua kamera inakuwa inamchukua. Vitu vyenyewe wanavyo fanya kwenye kijiji wala havieleweki vinamjenga nini mtu pale ili awe nini! probably am wrong kwa kuwa sijafuatilia kiundani. Masood mwenyewe is so much involved to the extent i feel inabore sana.... dont know. but to me i dont get anything out of it rather than waste of time!

Mkuu,

Mtu unatakiwa kuwa mbunifu uanza sehemu furani, masoud kipanya nayekawa mbunifu huo ni mwanza. Watanzania wenzetu si vema kumponda kiasi hicho, wewe kinaku-bore kuna watu wengi tu wanakifurahia.

Binafsi naona kama umeangalia na kuona mapungufu toa "positive criticism" kwa ajiri ya kuki-improve kipindi wanavyoendelea. Kumbuka leo unamfurahia kupanda ndege lakini mtu wa kwanza wakati anaanza na idea yake kuna watu kama wewe walimpnda kwa kumwoma kama punguani, kuna wale walitoa positive challenge na kufanya improvement kila wakati mpaka leo. Ulizia story ya SUN CITY South Africa utashangaa.

Pia si sahii kufananisha maishaplus na big brother maana hiyo iko tayari level ya juu sana na capital invested ni kubwa sana. Leo hii Masoud Kipanya akipata hela ya kutosha utashangaa, lakini akija hata kwako waafrika wengi walivyo na idea ya ku-improve imeandikwa safi utamwambia humwamini na hauta mpa hela.

Kimsingi wazo la masoud ni zuri linatakiwa kuungwa mkono kimawazo na kipesa ili tuwe na kitu cha kwetu kizuri nchi nyingine za africa na ulaya wawe nao wanafuatilia
 
Wana JF
Leo nilikuwa naangalia TBC1 TV nikakutana na inayosemekana kuwa ni reality TV show inayoongozwa na aliyekuwa mtangazaji wa power breakfast show ya Clouds FM Masooud Kipanya. Show hii inafahamika kama MaishaPlus na ina vijana kama 15 wake kwa waume walioko camp huko kijijini sasa nauliza je hii show madhumini yake nini?
Natumai kuuliza sio ujinga!
ebwana weee! sisi tuliopo nje ya tz kumbe tunakosa mambo huko, enhee...! hebu tujuvyeni vizuri mshaiga nini , baada ile BSS?
 
Back
Top Bottom