Magehema,
Sijui kama umenielewa, kama unaifuatilia Maisha Plus show inajaribu kuonyesha uhalisia wa maisha ya ki-tz. Katika show hii maadili ambayo nimezungumzia ni mwenendo mzima unaoonyeshwa na washiriki pale kijijini. Hakuna vitendo vya aibu kama kufanya mapenzi hadharani, kutembea nusu uchi, kutumia lugha zisizostahili dhidi ya mshiriki mwenzake, hakuna uvivu kila mshiriki anajumuika na wenzake katika kuendesha maisha ya pale kijijini. Tofauti na show ya big brother ambayo ishara za ngono za wazi au pengine kufanya ngono ni sehemu ya show, kutembea uchi ni jambo la kawaida, ugomvi na matusi kwao kawaida. Vitu kama hivyo hutavikuta katika show ya maisha plus. Kuthamini utamaduni wetu ni pamoja na kufahamu tulikotoka, wazee wetu walivaa mavazi ya magome ya miti hili likionyeshwa pale maisha plus linawafundisha vijana wetu tulikotoka. hakuna anayetembea uchi kama ulivyosema. Najua tuko pamoja Mkuu Magehema
Operationalisation, that's it. That is what I was looking for. Nimekuelewa Mkuu, nashukuru sana kwa kutoa ufafanuzi wa maadili ya ki-tz.