Maisha mema yanapatikana kijijini

Maisha mema yanapatikana kijijini

Tangu niamie huku kijijini, sizeeki kihasara hasara
  • Napata maji safi,
  • Hewa safi,
  • Kelele nzuri za ndege,
  • Hakuna msongo wa mawazo,
  • Napata mayai, nyama, maziwa muda wowote ninaotaka,
  • Napata vitu vingi bustanini,
  • Matumizi ya hela ni madogo sana kutokana na vitu vingi kupatikana shambani na kwenye mifugo,
  • Ngozi ya mwili inang'aa haina mabakamabaka,
  • Hakuna uchafuzi wa hewa unaosababishwa na msongamano wa watu,
  • Na mika 73 lakini naonekana kama kijana wa miaka 20,
  • Koti la suti limenikaa vizuri halijanizidi mwili kama wa huko mjini,
Kweli maisha mema, yanapatikana huku kijijini

View attachment 3659541
Hongera mkuu! halafu kijijini hakuna joto!
 
Kila sehemu ina uzuri na ubaya wake lakini pia inategemea aina ya kijiji ulichopo.
1. Unapofurahia sauti za ndege tambua kuna nyoka pia. Huku kufungua mlango asubuhi na kukutana na nyoka anakatiza uwanja sio jambo la ajabu
2. Maji safi ni uongo - sehemu nyingi ambazo serikali au wadau hawajapeleka huduma ya maji wanatumia maji ya mto. Watu wanafua humo, wanaoga, mifugo inakunywa humo na watu wanachota maji ya kutumia majumbani
3. Vyakula unapata fresh sawa lakini kwa msimu. Sehemu za miji au majiji vyakula vinapatikana muda wote...mfano Dar ukitaka kula mhogo hakuna siku utaenda sokoni ukose mhogo maana mihogo inatoka kila upande, kama upande wa kusini sio msimu wa viazi vitaletwa kutoka kaskazini.
 
Kijijini ni nguvu zako tu, utapata nyama toka bandani, utapata matunda toka bustani n.k kama utaishi kijijini na kuleta uvivu wa mjini ata mchicha ushindwe kuotesha, itabidi upambane upate hela ili uweze kununua mahitaji yako kwa watu wengine.​
Mimi sizungumzii hela ya kula maana kijijini vyakula ni vingi na ni nafuu. Nazungumzia pesa za kukuletea maendeleo mengine kando na chakula, malazi na mavazi. Hiyo ni ngumu kuipata unless ubase kote kote mjini na kijijini.
 
Kila sehemu ina uzuri na ubaya wake lakini pia inategemea aina ya kijiji ulichopo.
1. Unapofurahia sauti za ndege tambua kuna nyoka pia. Huku kufungua mlango asubuhi na kukutana na nyoka anakatiza uwanja sio jambo la ajabu
2. Maji safi ni uongo - sehemu nyingi ambazo serikali au wadau hawajapeleka huduma ya maji wanatumia maji ya mto. Watu wanafua humo, wanaoga, mifugo inakunywa humo na watu wanachota maji ya kutumia majumbani
3. Vyakula unapata fresh sawa lakini kwa msimu. Sehemu za miji au majiji vyakula vinapatikana muda wote...mfano Dar ukitaka kula mhogo hakuna siku utaenda sokoni ukose mhogo maana mihogo inatoka kila upande, kama upande wa kusini sio msimu wa viazi vitaletwa kutoka kaskazini.
Maji ya chemchem tunayanywa bila kuchemsha, mchicha tunajichumia tu mashambani, tunaokota mayai tunakula, hakuna magonjwa ya akili n.k
 
Mimi sizungumzii hela ya kula maana kijijini vyakula ni vingi na ni nafuu. Nazungumzia pesa za kukuletea maendeleo mengine kando na chakula, malazi na mavazi. Hiyo ni ngumu kuipata unless ubase kote kote mjini na kijijini.
Uko sahihi, mfano sasa hivi unafanya kazi mjini; pato lako unaliwekeza kijijini, baada ya miaka 5 au 10, unarejea kijijini kula matunda ya kile ulichokianzisha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom