Mahakama yathibitisha Stella Moses aliyepoteza maisha akiwa Kituo cha Polisi Mburahati alijinyonga

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,989
Mahakama ya Korona Kinondoni Jijini Dar es Salaam, imetoa hukumu hiyo Ijumaa Septemba 22, 2023 imetoa uamuzi wa uchunguzi ilioufanya kuhusu mazingira ya kifo cha Stella Moses ambaye alifariki akiwa mahabusu katika Kituo cha Polisi Mburahati, Desemba 20, 2020, ambapo imesema kifo chake kilisababishwa na mtuhumia kujinyonga.

Katika uamuzi huo Mahakama imesema kujinyonga kulifanyika licha ya mwili wake kukutwa na majeraha kichwani na shingoni.

Stella Moses akiwa na umri wa miaka 30, alijisalimisha kituoni hapo baada ya kupata taarifa kuwa alikuwa anahitajika, baadaye ikatangazwa kuwa amefariki, tukio ambalo lilizua mvutano mkubwa baina ya Polisi na ndugu wa marehemu kwa kile wanachodai kuna mazingira tata ya kifo hicho.

Ndugu wa marehemu waliamua kufungua kesi Mahakamani dhidi ya Jeshi la Polisi na Hospitali ya Taifa Muhimbili wakitaka uchunguzi wa kina kuhusu tukio hilo.

Walifungua shauri hilo baada ya kutoridhika na upelelezi, mwenendo wa uchunguzi wa tukio na sababu za kifo hicho, hivyo wakitaka ufanyike uchunguzi huru.

Shauri hilo lilifunguliwa na shemeji wa marehemu, Emmanuel Kagongo kwa niaba ya familia ya marehemu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Dar es Salaam, Kivukoni (Kinondoni) kupitia kwa wakili Peter Madeleka.

Itakumbukuwa naada ya kifo cha Stella, Jeshi la Polisi kupitia aliyekuwa Kamanda wa Polisi Wilaya ya Kinondoni, Ramadhani Kingai, lilitoa taarifa kuwa Stella, mama wa Watoto wawili amefariki Dunia baada ya kujinyonga akiwa mahabusu kwa kutumia nguo yake.

Kingai ambaye kwa saa ni Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) alisema inaonekana mwanamke huyo alikuwa na madeni mengi na kwamba baada ya kuchunguza waliona kifo hicho hakikusababishwa na uzembe wa askari, kwa kuwa wakati mtuhumiwa anaingizwa mahabusu taratibu zote, ukiwemo ukaguzi, zilifuatwa.

Hata hivyo kufuatia uamuzi huo Wakili wa upande wa wafungua shauri, Peter Madeleka amesema hawajalizika na uamuzi huo wanakusudia kukata rufaa Mahakama Kuu.
 
Hivi mtuhumiwa akijinyonga anakuwa na majeraha kichwani na sehemu nyingine za mwili? Waseme tu walimpa kipondo akafariki ndiyo wakaona Bora wamvishe kitanzi ili kuficha ushahidi. Poleni Sana Yatima mmebaki bila mama na haki hamtakaa muipate na mama hatarudi tena milele duniani huku
 
Hivi mtuhumiwa akijinyonga anakuwa na majeraha kichwani na sehemu nyingine za mwili? Waseme tu walimpa kipondo akafariki ndiyo wakaona Bora wamvishe kitanzi ili kuficha ushahidi. Poleni Sana Yatima mmebaki bila mama na haki hamtakaa muipate na mama hatarudi tena milele duniani huku
It's very sad, indeed!
 
inawezekana alipigwa na wanao mdai ndiyo akaamuwa kujisalimisha polisi akiwa tayari ana majeraha.

Tusubiri "details" zaidi za kesi na rufaa.
Sawa, mahakama imethibitisha alijinyonga, je vitu / vifaa alivyotumia kujinyonga vilipitaje wakati mtuhumiwa kabla ya kuingizwa mahabusu anatolewa vitu vyote vinavyoweza kuleta au kuharibu amani humo ndani?

Wakati anajiua alikuwa selo ya peke yake? Inawezekanaje mtuhumiwa kujinyonga mpaka kufikia mauti wenzie wakiwa wanamtazama?

Alifika na majeraha, je hatuna utaratibu wa kuwafikisha hospital watuhumiwa wakiwa chini ya ulinzi tunawashikilia hivo hivo wakiwa wagonjwa / mahututi?

Anyway apumzike kwa amani.
 
Nilipoona tuu jina kingai akili imeniambia kuna udanganyifu hapo, kwa tabia ya askari wa uswahilini huyo mdada walimpiga hadi akafariki wakaziba noma kwa kumnyonga ili ionekane alijinyonga, kwa sababu swali la kujiuliza hayo majeraha ya kichwani na sehemu zingine mwilini yalitoka wapi 🤔🤔 yule kingai na askari wake watachomwa moto kabla hawajafika jehanamu,

hua nikisia askari amepigwa au ameuliwa hua nafarijika moyoni kwa madhira waliyo nipatia wale washenzi,😡😡😡 hata nikipita sehemu nikute askari anafanyiwa jambo lolote baya hakika nitapita kama naaga maiti😡😡😡
 
Mahakama ya Korona Kinondoni Jijini Dar es Salaam, imetoa hukumu hiyo Ijumaa Septemba 22, 2023 imetoa uamuzi wa uchunguzi ilioufanya kuhusu mazingira ya kifo cha Stella Moses ambaye alifariki akiwa mahabusu katika Kituo cha Polisi Mburahati, Desemba 20, 2020, ambapo imesema kifo chake kilisababishwa na mtuhumia kujinyonga.

Katika uamuzi huo Mahakama imesema kujinyonga kulifanyika licha ya mwili wake kukutwa na majeraha kichwani na shingoni.

Stella Moses akiwa na umri wa miaka 30, alijisalimisha kituoni hapo baada ya kupata taarifa kuwa alikuwa anahitajika, baadaye ikatangazwa kuwa amefariki, tukio ambalo lilizua mvutano mkubwa baina ya Polisi na ndugu wa marehemu kwa kile wanachodai kuna mazingira tata ya kifo hicho.

Ndugu wa marehemu waliamua kufungua kesi Mahakamani dhidi ya Jeshi la Polisi na Hospitali ya Taifa Muhimbili wakitaka uchunguzi wa kina kuhusu tukio hilo.

Walifungua shauri hilo baada ya kutoridhika na upelelezi, mwenendo wa uchunguzi wa tukio na sababu za kifo hicho, hivyo wakitaka ufanyike uchunguzi huru.

Shauri hilo lilifunguliwa na shemeji wa marehemu, Emmanuel Kagongo kwa niaba ya familia ya marehemu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Dar es Salaam, Kivukoni (Kinondoni) kupitia kwa wakili Peter Madeleka.

Itakumbukuwa naada ya kifo cha Stella, Jeshi la Polisi kupitia aliyekuwa Kamanda wa Polisi Wilaya ya Kinondoni, Ramadhani Kingai, lilitoa taarifa kuwa Stella, mama wa Watoto wawili amefariki Dunia baada ya kujinyonga akiwa mahabusu kwa kutumia nguo yake.

Kingai ambaye kwa saa ni Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) alisema inaonekana mwanamke huyo alikuwa na madeni mengi na kwamba baada ya kuchunguza waliona kifo hicho hakikusababishwa na uzembe wa askari, kwa kuwa wakati mtuhumiwa anaingizwa mahabusu taratibu zote, ukiwemo ukaguzi, zilifuatwa.

Hata hivyo kufuatia uamuzi huo Wakili wa upande wa wafungua shauri, Peter Madeleka amesema hawajalizika na uamuzi huo wanakusudia kukata rufaa Mahakama Kuu.
kule kituo cha polisi huwa wanaweka vitu vya kujinyongea? au alikuwa chumba tofauti na mahabusu zile.
 
Sawa, mahakama imethibitisha alijinyonga, je vitu / vifaa alivyotumia kujinyonga vilipitaje wakati mtuhumiwa kabla ya kuingizwa mahabusu anatolewa vitu vyote vinavyoweza kuleta au kuharibu amani humo ndani?

Wakati anajiua alikuwa selo ya peke yake? Inawezekanaje mtuhumiwa kujinyonga mpaka kufikia mauti wenzie wakiwa wanamtazama?

Alifika na majeraha, je hatuna utaratibu wa kuwafikisha hospital watuhumiwa wakiwa chini ya ulinzi tunawashikilia hivo hivo wakiwa wagonjwa / mahututi?

Anyway apumzike kwa amani.
Mahakama imeonesha dhahiri kuamua kutetea wauaji ili kuficha uovu na kuiokoa serikali na aibu.Ila,kwa kila aliyeshiriki uovu huo,atapata tu malipo yake.Kuna watu wajinga sana.Unaletewa mtuhumiwa wa madeni na si jambazi anayetishia amani katika jamii,halafu kwa vijirushwa njiwa wanashirikiana kuhujumu uhai wa mtuhumiwa?🤔
 
Back
Top Bottom