Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,817
- 4,566
Sambamba na amri hiyo iliyotolewa na Naibu Msajili wa Mahakama hiyo, Mary Mrio, pia imemteua dalali wa kutekeleza amri hiyo, Jesca Massawe kutoka kampuni ya udalali ya MM Auctioneer & Debt Collectors.
Mahakama hiyo imefikia uamuzi huo kufuatia maombi yaliyowasilishwa na waandishi hao, Maregesi Paul na wenzake tisa ili kutekeleza tuzo yao waliyopewa na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), katika shauri la mgogoro wa kikazi walilolifungua dhidi ya mwajiri wao huyo.
Akizungumza na Mwananchi, Paul amesema wakati amri hiyo inatolewa, Dudley ambaye ni mtoto wa Freeman Mbowe, mwenyekiti wa Chadema, hakuwepo mahakamani licha ya kwamba alikuwa ameahidi kuwa angefika na fedha za kuwalipa.