Kama sio Muislam sio rahisi kujua faida zake, kwa vile you will view the whole issue negatively. Lakini itoshe kwako kuwa kesi nyingi za Ndoa na Mirathi za Waislamu hazitakuwa katika Mahakama hizi za kawaida hivyo itapinguza workload kwa Mahakimu wachache waliopo ambao anyway wako overloaded. Wajane wengi wa Kiislamu wanadhulumiwa na ndugu za waume zao waliofariki, wanatelekezwa na mayatima, kwa sababu tu Mahakimu wengi hawako compatible na sheria za ndoa na mirathi za Kiislamu ingawa zinatambuliwa rasmi na sheria za nchi, hivyo wajane hao wanachelewa sana kupata haki zao (eg nina Shemeji yangu alifiwa na Mume sasa ni 12yrs anafuatilia mahakamani na hajapata haki, huenda mpaka atakufa na asiipate) Mahakama ya Kadhi inarahisisha sana upatikanaji wa haki hizo, na masuala ya ndoa ni kadhalika. Mkoloni hakuwa mpumbavu kuientertain Mahakama hii, hata nchi zenye Waislam Wachache kama Kenya wameiestablish siku nyingi, sijui kwanini Tanzania waliiondoa, sijui ni kwa interests za nani hasa, kama ni gharama, Waislam katika nchi hii ni significant portion ya Tax paying population, tax ambayo Billions zinaenda kufinance miradi ya Makanisa ambayo huduma zake ni very expensive kwa mlipa kodi mdogo wa kawaida (eg Shule na Hospitali za Mission) Walipa kodi wa Kiislam wanavumilia, ni vyema basi Wakristo nao wakavumilia wananchi wenzao wa Kiislam wakirekebishiwa masuala yao, tutaenda vizuri as a Unified Nation, la sivyo, kama kuna agenda ya siri, au Kama dini moja itajiona ni superior na inastahili mgao wa keki ya taifa na nyingine haistahili.... basi..!! Bila haki hapawezi kuwa na amani.