Cha kusikitisha zaidi ni kuwa hawa Wasabato ambao ni wachache sana ukilinganisha na Waislamu nao wamepewa siku yao ya kupumzika (Jumamosi) kwa heshima tu ya Ukristo wao, upande wa pili Muislamu anaambiwa ni upuuzi kudai siku ya Ijumaa kuwa ni siku ya mapumziko.......tugawaneni tu hii nchi ili upuuzi huu uishe!
Sideeq,
..watu wakianza kulipwa kwa masaa, na siku za kazi zikianza kuzingatia mahitaji ya kibiashara, basi hayo yote yatafutika. watakaobakia kupumzika jumamosi na jumapili watakuwa ni watumishi wa serikali tu ambao hata hivyo watakuwa ni segment ndogo sana ya wafanya kazi.
..kwenye nchi za wenzetu kazi ni masaa 24 na siku 7 kwa wiki. kama mtu anataka kufanya ibada basi anaomba ruksa maalum asipangiwe kazi say ijumaa,jumamosi,au jumapili. kuna wengine wanapenda kufanya kazi hizo siku za weekend ili kujiepusha na anasa manaake anasa nyingi pia zinafanyika siku hizo 3.