Mahakama ya Kadhi "Ruksa" - Pinda

Mahakama ya Kadhi "Ruksa" - Pinda

Status
Not open for further replies.
Mimi ni Mkristo, lakini nakuunga mkono, na pia naunga mkono kuanzishwa kwa mahakama hii. Hivi tatizo liko wapi? Mbona haya ni mambo private kabisa ya imani ya mtu? Na kama ni suala la wakristo kugharimia mambo ya kiislamu, mbona hatujiulizi yafuatayo: (1) Ijumaa, waislamu wanatakiwa msikitini, lakini na kazini pia (2) Jumamosi, wakristo (wasabato) wanatakiwa waende kanisani na KUPUMZIKA (3)Jumapili, wakristo wengine wote wanatakiwa waende kanisani na KUPUMZIKA. Hapo hatuoni kama kodi za watanzania wote, bila kujali imani ya mtu zinalipia mambo ambayo ni ya wakristo? Hivi ni kwa nini hatuangalii ni kwa kiasi gani uchumi wa nchi unaathirika kwa kutofanya kazi siku 2 katika wiki? Nani anagharimia au kufidia mapato yanayokosekana katika siku hizo 2, kama si mwananchi kupitia VAT na kodi zingine, hasa katika nchi kama hii ambapo wawekezaji wasio weusi wameachwa wafanye biashara zao bila kulipa kodi inavyostahili? No, tukae chini tukubaliane kupingana bila kupigana, lakini pia hatimaye tuwe fair. Mahakama ya Kadhi ianzishwe, na iwezeshwe kufanya kazi zake. Nchi hii ni yetu sote!!
 
kama wanashindwa kuendesha hata shule ya msingi,wataweza kuendesha mahakama na kulipa wafanyakazi wa mahakamani?...wanajitwisha mzigo wa mawe tu hadi nawaonea huruma.

wasaidie basi
 
kuna mtu anaitwa shardkole, namwambia kwamba.kama waislam wanafadhiliwa na watoa kafara,BASI WAKRISTO WANAFADHILIWA NA FREEMASON NA UKRISTO NI FREEMASON
 
Hii mada naiona kama haina faida yoyote! Udini na upuuzi mtupu unaongelewa hapa. Bora kuendelea mbele... kwaherini.
 
kama wanashindwa kuendesha hata shule ya msingi,wataweza kuendesha mahakama na kulipa wafanyakazi wa mahakamani?...wanajitwisha mzigo wa mawe tu hadi nawaonea huruma.

Hujui mwanafunzi bora wa Tanzania katokea shule gani mwaka huu? uliza!
 
Sideeq ulitaka kwenye Mikataba ya MOU waislamu washirikishwe alafu iweje? jengeni zenu nanyie ili msamehewe kodi nafasi ipo siyo kulalamika tu.Serikali hii bila hospital za makanisa khali ya uduma za afya itakuwa mbovu sana zaidi ya hii.wewe Thread yenyewe hapa ni Mahakama ya kadhi, lkn kwa chuki zako dhidi ya WAkristo ukabidi uingize MOU, mkijadili maswala yenu bila kuwataja wakristo mambo yenu ayaendi? Mwende mkatibiwe wote Aghakhani sasa na wao siwanapewa misamaha?

MoU haihusishi kusamehewa kodi, usipoteze maana.

Kwanza ngoja nitafute mawakili tulipeleke hili swala la MoU mahakamani.
 
Mlipa kodi mkubwa Tanzania ni TBL hawa jamaa wanafanya kila liwezekanalo fedha hii ya TBL iende ikaendeshe mahakama ya Kadhi,.

TBL, Salama condom, riba za mabenki yote, mabucha ya nguruwe,....pesa haramu haziwezi kulipa mishara na vifaa vya mahakama hii ambayo ni sehemu ya IBADA ya watukufu waislam! Sisi wasio na dini yetu macho.
 
Si kitu, tutapata njia ya kuziendesha tena kwa ufanisi mkubwa sana. Bakhresa kisha jitolea budget ya miaka 5 kwa mahakama moja kila mkoa, hapo sasa!

Oilcom anasema atajenga mahakama 30 kwa fedha yake.

Hao wawili tu, mambo ndio hayo, ngoja wafumke na wengine.

Tunamsubiri Lowassa kwa kutaka kura za Waislaam 2015 sijui atatoa ngapi. Kwi kwi kwi teh teh teh!


....Tatizo kubwa ni Hilo! Mnapenda sana kufanyiwa na kupewa tu bila nyinyi wenyewe kutoka jasho. Hao watu uliotaja inatakiwa waongezee tu katika kile ambacho mmeishafanya, sio watumie pesa zao huku nyi mmejibweteka tu mkingoja kufanyiwa...Shauri lenu. Mjini hapa!
 
Mimi ni Mkristo, lakini nakuunga mkono, na pia naunga mkono kuanzishwa kwa mahakama hii. Hivi tatizo liko wapi? Mbona haya ni mambo private kabisa ya imani ya mtu? Na kama ni suala la wakristo kugharimia mambo ya kiislamu, mbona hatujiulizi yafuatayo: (1) Ijumaa, waislamu wanatakiwa msikitini, lakini na kazini pia (2) Jumamosi, wakristo (wasabato) wanatakiwa waende kanisani na KUPUMZIKA (3)Jumapili, wakristo wengine wote wanatakiwa waende kanisani na KUPUMZIKA. Hapo hatuoni kama kodi za watanzania wote, bila kujali imani ya mtu zinalipia mambo ambayo ni ya wakristo? Hivi ni kwa nini hatuangalii ni kwa kiasi gani uchumi wa nchi unaathirika kwa kutofanya kazi siku 2 katika wiki? Nani anagharimia au kufidia mapato yanayokosekana katika siku hizo 2, kama si mwananchi kupitia VAT na kodi zingine, hasa katika nchi kama hii ambapo wawekezaji wasio weusi wameachwa wafanye biashara zao bila kulipa kodi inavyostahili? No, tukae chini tukubaliane kupingana bila kupigana, lakini pia hatimaye tuwe fair. Mahakama ya Kadhi ianzishwe, na iwezeshwe kufanya kazi zake. Nchi hii ni yetu sote!!
Hakuna Mkristo mwenye kichwa chepesi kama cha kwako.
 
Sideeq ulitaka kwenye Mikataba ya MOU waislamu washirikishwe alafu iweje? jengeni zenu nanyie ili msamehewe kodi nafasi ipo siyo kulalamika tu.Serikali hii bila hospital za makanisa khali ya uduma za afya itakuwa mbovu sana zaidi ya hii.wewe Thread yenyewe hapa ni Mahakama ya kadhi, lkn kwa chuki zako dhidi ya WAkristo ukabidi uingize MOU, mkijadili maswala yenu bila kuwataja wakristo mambo yenu ayaendi? Mwende mkatibiwe wote Aghakhani sasa na wao siwanapewa misamaha?

Kama makanisa yanategemewa ktk afya mbona hawatoi huduma bure na mbona bado watu wenye hela wanakimbilia India?Hapana tuwe na fursa ya kuangalia pande zote mbili bila kujipendelea upande wako.Angalia hapa JF uone jinsi gani wakristo wanavoupiga vita uisilamu na mpaka wanatumilia propaganda za ugaidi na maneno mengi ya kashfa na sio kama hufahamu unajua fika.Uisilamu hautaki kumdhulumu mtu lakini vilevile hauruhusiwi kudhulumiwa mtu kwani dhulma ndio chanzo cha matatizo.
 
Si kitu, tutapata njia ya kuziendesha tena kwa ufanisi mkubwa sana. Bakhresa kisha jitolea budget ya miaka 5 kwa mahakama moja kila mkoa, hapo sasa!

Oilcom anasema atajenga mahakama 30 kwa fedha yake.

Hao wawili tu, mambo ndio hayo, ngoja wafumke na wengine.

Tunamsubiri Lowassa kwa kutaka kura za Waislaam 2015 sijui atatoa ngapi. Kwi kwi kwi teh teh teh!
Wapi shule, wapi vyuo, wapi hospitali? Bakhresa and co wanafadhili ujenzi wa misikiti na mahakama ya kadhi tu?
 
Magdalena, hawa watu wa ajabu, hivi watapata faida gani kwa kuwa na hizo mahakama. I am trying to imagine having a catholic court, of what benefit will it be to me as a catholic anyway!!! Labda sina ufahamu wa hizo mahakama za kadhi with regard to faida zake. naomba kueleweshwa!
Mnapojadili jambo matusi na dsharau hazifai hata kidogo. kama unataka kuuliza swali uliza na sio kuikashiifu dini ya mtu maana hujui ulisemalo. Mahakama ya kadhi ni kutoa HAKI kwa waumini wa kiislaam hivyo hakuna HAKI inayopimwa kwa thamani ya fedha kama mnavyofikiria Wakatoliki...

Ni haki ya Waislaam kikatiba maana inasema wazi kabisa kwamba tuna fuata sheria mbili nchini, Secular na Cultural nd ndio maana tunazitambua ndoa za kiislaam, Kiasili na dini nyinginezo sii kwa maslahi ya kifedha ama kumfurahisha mtu bali ujenzi wa familia hizo ktk maadili ya imani zao. Na itakuwa ujinga mkubwa sana kufikiria waislaam wafanye kama wakristu walkati wewe hukuwa Muislaam kwa sababu kama hizi. What made U not being a muslim ni pamoja na sababu kama hizi hivyo hivyo muislaam pia hakuwa mkristu kwa sababu ndoa yake hataki iamuliwe na serikali.

Catholic hawawezi kuwa na mahakama ya kadhi kwa sababu ndani ya Ukatoliki hakuna sheria ya Talaka wala mirathi..Hivyo unachojaribu kufikiria ni sawa na mwanamke anayetaka kujua kwa nini mwanamme hufuga ndevu..Hivyo unapopinga mahakama ya kadhi jaribu kuwa upande huu halafu bishana kwa kutazama na kuujua Uislaam wenyewe..
 
Mimi ni Mkristo, lakini nakuunga mkono, na pia naunga mkono kuanzishwa kwa mahakama hii. Hivi tatizo liko wapi? Mbona haya ni mambo private kabisa ya imani ya mtu? Na kama ni suala la wakristo kugharimia mambo ya kiislamu, mbona hatujiulizi yafuatayo: (1) Ijumaa, waislamu wanatakiwa msikitini, lakini na kazini pia (2) Jumamosi, wakristo (wasabato) wanatakiwa waende kanisani na KUPUMZIKA (3)Jumapili, wakristo wengine wote wanatakiwa waende kanisani na KUPUMZIKA. Hapo hatuoni kama kodi za watanzania wote, bila kujali imani ya mtu zinalipia mambo ambayo ni ya wakristo? Hivi ni kwa nini hatuangalii ni kwa kiasi gani uchumi wa nchi unaathirika kwa kutofanya kazi siku 2 katika wiki? Nani anagharimia au kufidia mapato yanayokosekana katika siku hizo 2, kama si mwananchi kupitia VAT na kodi zingine, hasa katika nchi kama hii ambapo wawekezaji wasio weusi wameachwa wafanye biashara zao bila kulipa kodi inavyostahili? No, tukae chini tukubaliane kupingana bila kupigana, lakini pia hatimaye tuwe fair. Mahakama ya Kadhi ianzishwe, na iwezeshwe kufanya kazi zake. Nchi hii ni yetu sote!!

...Huna haja ya kujipachika ukristo ili hoja zako zikubalike. Suala la kupumzika siku ya Jumamosi halina usabato wala ukristo. Ni watawala wetu dhaifu ndio waliamua Jumamosi kuwa siku ya mapumziko kwa baadhi ya ofisi za kiserikali, kama sio zote.
Maamuzi ya kufanya siku ya Jumapili kuwa ya mapumziko hayakulenga zaidi Ukristo bali kanuni tu ya kwamba siku moja katika saba za wiki ni siku ya Mapumziko. Na ndio maana katika siku hiyo hata wewe Muislamu unaPumzika na huendi kazini na pia hukatazwi kuendelea na ibada zako Tano kama Uislamu unavyotaka.
Mkuu, hii haina tofauti sana na Nchi za Uarabuni ambako siku ya Ijumaa ndio ya mapumziko na jumapili ni siku ya kawaida ya kudunda mzigo hata kwa Wakristo!
Ama unataka kusema kuwa Uarabuni walivyochagua siku ya kupumzika kuwa Ijumaa na Jumapili kuwa siku ya Kazi ni Haki ila sisi tulivyochagua Siku ya kupumzika kuwa Jumapili (ambayo inakubalika na nchi nyingi duniani bila kujali Imani za watu wake) na Ijumaa kuwa ya Kazi ni Kosa?????
 
Mnapojadili jambo matusi na dsharau hazifai hata kidogo. kama unataka kuuliza swali uliza na sio kuikashiifu dini ya mtu maana hujui ulisemalo. Mahakama ya kadhi ni kutoa HAKI kwa waumini wa kiislaam hivyo hakuna HAKI inayopimwa kwa thamani ya fedha kama mnavyofikiria Wakatoliki...

Ni haki ya Waislaam kikatiba maana inasema wazi kabisa kwamba tuna fuata sheria mbili nchini, Secular na Cultural nd ndio maana tunazitambua ndoa za kiislaam, Kiasili na dini nyinginezo sii kwa maslahi ya kifedha ama kumfurahisha mtu bali ujenzi wa familia hizo ktk maadili ya imani zao. Na itakuwa ujinga mkubwa sana kufikiria waislaam wafanye kama wakristu walkati wewe hukuwa Muislaam kwa sababu kama hizi. What made U not being a muslim ni pamoja na sababu kama hizi hivyo hivyo muislaam pia hakuwa mkristu kwa sababu ndoa yake hataki iamuliwe na serikali.

Catholic hawawezi kuwa na mahakama ya kadhi kwa sababu ndani ya Ukatoliki hakuna sheria ya Talaka wala mirathi..Hivyo unachojaribu kufikiria ni sawa na mwanamke anayetaka kujua kwa nini mwanamme hufuga ndevu..Hivyo unapopinga mahakama ya kadhi jaribu kuwa upande huu halafu bishana kwa kutazama na kuujua Uislaam wenyewe..


...So, in short, what you are saying ni kwamba Mahakama ya Kadhi inaazishwa kwa ajili tu ya 'Sheria ya Talaka na Miradhi' kwa Waislamu....
 
Utatufundisha nini wewe kuhusu amani?! fanya research kuhusu Mtume SAW jinsi alivyofunga makataba wa amani na Makafiri huko Hudaybiyah, uone kuwa sisi ni watu tunaomaliza matatizo kwa amani kabla ya vita, kubakieni kwenu nyinyi Wakristo miaka yote hii huku mkifanya kila aina ya uvunjaji wa amani(kutoka mwembechai mpaka MOU) bila ya kuguswa ni ushahidi tosha kuwa Waislamu ni watu wa amani.

Wala hujakosea nchi nyingi za kiislamu zinatoa ushuhuda huu wa amani,Libya,misri,iraq,irani,syria,indonesia, zipo so peaceful na nyingi za kikristu vurugu kibao....hands down kwa amani ktk nchi nilizozitaja...lol
 
Mnapojadili jambo matusi na dsharau hazifai hata kidogo. kama unataka kuuliza swali uliza na sio kuikashiifu dini ya mtu maana hujui ulisemalo. Mahakama ya kadhi ni kutoa HAKI kwa waumini wa kiislaam hivyo hakuna HAKI inayopimwa kwa thamani ya fedha kama mnavyofikiria Wakatoliki...

Ni haki ya Waislaam kikatiba maana inasema wazi kabisa kwamba tuna fuata sheria mbili nchini, Secular na Cultural nd ndio maana tunazitambua ndoa za kiislaam, Kiasili na dini nyinginezo sii kwa maslahi ya kifedha ama kumfurahisha mtu bali ujenzi wa familia hizo ktk maadili ya imani zao. Na itakuwa ujinga mkubwa sana kufikiria waislaam wafanye kama wakristu walkati wewe hukuwa Muislaam kwa sababu kama hizi. What made U not being a muslim ni pamoja na sababu kama hizi hivyo hivyo muislaam pia hakuwa mkristu kwa sababu ndoa yake hataki iamuliwe na serikali.

Catholic hawawezi kuwa na mahakama ya kadhi kwa sababu ndani ya Ukatoliki hakuna sheria ya Talaka wala mirathi..Hivyo unachojaribu kufikiria ni sawa na mwanamke anayetaka kujua kwa nini mwanamme hufuga ndevu..Hivyo unapopinga mahakama ya kadhi jaribu kuwa upande huu halafu bishana kwa kutazama na kuujua Uislaam wenyewe..

Hujanielewa, sipingi mahakama ya kadhi maana hainihusu, just for curiosity!!!! hapana. Nawaheshimu sana na maamuzi yenu!!Ila najiuliza faida zake ni zipi kuliko secular laws? Ndio maana nimeomba nieleweshwe. Sina dharau na dini yoyote. hata kama wakatoliki wangelikuwa na mahakama, sidhani kama zingelinisaidia sana katika maisha ya humu mudunia kuliko sheria za serikali. Pole kama nimekukwaza. Na kweli ndevu zina faida gani, usumbufu wa kunyoa tu!! ukiacha kuwa Mtume SAW anawataka mzifuge!!
 
Alaah! kumbe ulikuwa hujui lakini unabisha tu.. sasa wewe ulitaka iwe kwa ajili gani?


.....Sio Kubisha Comrade. Zaidi ni kushangaa kwamba Surely Mahakama ilipaswa kuliliwa kuanzishwa kwa ajili ya Mambo makubwa zaidi na Muhimu ya Kimaendeleo na sio kwa ajili tu ya kusimamia minor things kama Taratibu za jinsi ya Watu Kuachana na Nani achukue nini katika Kuachana huko ama katika Vifo ....?:wacko:
 
Msidanganyane! mlipa kodi mkubwa wa nchi hii ni Waislamu kutokana na idadi ya uwingi wao (wekeni kipengele cha dini kwenye sensa) na ufanyabiashara.



tusidanganyane ndugu yangu siseeq, waislam sisi hat kama ni asilimia 90 ya watanzania hatuna lolote zaidi ya kulalama tuuu!!
wenzetu wanasoma kwa bidii sisi tunalalama ati tunabaniwa kwenye matoke!
wenzetu wana weka investments za kweli tena nyingi sisi tunabaki kulalama ati wanapendelewa,
tusiwe wanafiki wala kuendeshwa kwa imani kali zisizokua na faida kijamii wala kiuchumi.....tuangalie tulichelewa wpi na tujifunze toka kwa wenzetu tuweze kubadilika!! otherwise tutabaki ng'ang'ania kadhi isokua na tija kiuchumi tukija kushtuka wako maili 1000 mbele ya hapo walipo
 
Si kitu, tutapata njia ya kuziendesha tena kwa ufanisi mkubwa sana. Bakhresa kisha jitolea budget ya miaka 5 kwa mahakama moja kila mkoa, hapo sasa!

Oilcom anasema atajenga mahakama 30 kwa fedha yake.

Hao wawili tu, mambo ndio hayo, ngoja wafumke na wengine.

Tunamsubiri Lowassa kwa kutaka kura za Waislaam 2015 sijui atatoa ngapi. Kwi kwi kwi teh teh teh!


I guess it doesn't matter how unclean is the money!
Matajiri wengine huwa mnawasifia sana (kwa vile tu wana majina ya kiislaam) lakini beneath their wealth, lies uncleanness, extortion and other crimes!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom