Mahakama ya kadhi hii hapa!

Mahakama ya kadhi hii hapa!

Hahahaah mimi nakuwa mkorofi nikichokozwa ndugu!:A S thumbs_up:
Aaaah! Mbona wakati mwingine unavua shati makusudi, na kulitupa barabarani... watu wakiliganya tu ugomvi... Nasikia uliwahi kumpiga kwenzi mtoto wa jirani kwa kukanyaga kivuli chako... :A S thumbs_up:
 
Aaaah! Mbona wakati mwingine unavua shati makusudi, na kulitupa barabarani... watu wakiliganya tu ugomvi... Nasikia uliwahi kumpiga kwenzi mtoto wa jirani kwa kukanyaga kivuli chako... :A S thumbs_up:

Hahahaahah ukisoma matundiko ya Malaria Sugu lazima uvue shati na kuanza mtafuta umpe makonzi yake! :A S thumbs_down:
 
Kwa mara ya kwanza hujanitukana wala kunikashfu! Nadhani hakuna haja ya serikali kujali hata wale minority ambao population yao haiko significant.

Mapumziko ya kitaifa tarehe hizi January 14, 2011, na February 3, 2011. Ni muhimu sana pia iundwe wizara ya kushughulikia walemavu, maana mahakama ya kadhi na sharia wengi watakatwa mikono, miguu na kupondwa mawe.Hongereni sana waislam sauti yenu imesikika.



Kwa mujibu wa Islamic Sharia kila mtu atakayehukumiwa kwa wizi na kukatwa mkono, jamii anayoishi inatakiwa imtunze na kuhakikisha huduma zote za msingi anapatiwa.Hivyo suala la kuwa na vilema wengi kwa hofu ya kuwa tegemezi haitakuwepo.
 
Hivi Mahakama ya Kadhi itatuletea tija gani kama waTZ??
 
Kweli sasa Kikwete sasa umetuchoka............. naona SASA UMEAMUA KUTUTENGENEZEA BOMU...

Sidhani kama MUISLAMU WA "utandawazi" ( namaanisha hawa tunaokunywa nao MIBIA, MAJIKITIMOTO, TWANGA PEPETA kwa sana, Kona SANA, HAWAGUSI MISIKITINI, namaanisha waisilamu wanaoishi katika misingi ya KIMAISHA na sio kidini saaaana) kama watakubali kupelekwa kesi zao huko.

Ninauhakika wale waliokulia katika kipindi hii mahakama haipo, ambao hawaijui WATAKUWA WANAONA WANAONEWA......... then kesi ikiisha huko WATAKATA RUFAA mahakama ya KISUTU.

Hakyamungu SIPATI picha akitoka kikwete, alafu aje mwingine HAONDOE KABISA HILO WAZo sipati picha.

Kweli Mwl. Nyerere aliona mbali, kutokukupa Urais 1995, sijui ungekuwa umetufikisha wapi, Maana umekuja KUIBOMOA CCM na WATANZANIA kabisa......

Eeeh mungu tuondolee huyu MTU KWA JINSI YEYOTE
 
Wana JF hebu mnielimishe: zile mahakama za nchi za kiislam zinazokata watu mikono na hii ya kadhi kuna tofauti??????
Kama hazina tofauti, je waswahili vibaka wa hapa bongo si wataogopa na kuhamia dini zingine, na upagani???????????????!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Ndugu zangu Waislam aliyewaambia kuwa 01.01 ni mwaka mpy wa wakristo ni nani. Mwaka mpya wa katoliki ni week ya kwanza ya MAJIRIO mwishoni mwa NOVEMBER. Je na wakatoliki wadai iwe siku ya mapumziko?
 
Ndugu zangu Waislam aliyewaambia kuwa 01.01 ni mwaka mpy wa wakristo ni nani. Mwaka mpya wa katoliki ni week ya kwanza ya MAJIRIO mwishoni mwa NOVEMBER. Je na wakatoliki wadai iwe siku ya mapumziko?

Hivi tangu mjadala huu uanze kuna mtu amesema tarehe 1 january ni mwaka mpya wa Wakristo?
 
kwani mahakama si zipo kibao kuna tofauti gani kati ya mahakama ya kadhi na mahakama za kawaida

Mahakama ya kadhi ni maalumu kwa ajiri ya kutatua migogoro ya miradhi,ndoa na mambo mengine yanayowahusu waamini wa dini ya kiislamu,na hutoa maamuzi yake kwa kutumia sheria na miongozo ya kiislamu.Wakati mahakama za kawaida husuluhisha migogoro mbalimbali kwa kutumia katiba mama na sheria mabalimbali zinazotoa miongozo ya namna ya kuongoza nchi na raia wake bila kujali dini zao.[/QUOTE]

Kuhusu mambo ya ndoa chukulia mfano Bw John amekamatwa ugoni na mke wa Abdallah Je Je hapo kadhi hatoweza kutoa hukumu?
Makanisa yanawatumia Mapadre na wachungaji kama mahakimu kwa hiyo kama Kadhi atalipwa mshahara na serikali basi mapadre wote na wachungaji nao walipwe mshahara na serikali na gharama itakuwa kubwa sana! waislam anzisheni hiyo mahakama nje ya utaratibu wa serikali kuepusha migogoro na gharama kwa serikali.
 
kwa jinsi mambo yanavyoenda tutashindwa kuiongoza nchi hii vizuri kama kila mtu atapewa atakacho!
Siku zote tumeishi bila huo mwaka mpya na mambo yalikuwa mazuri tu. Tafadhali busara itumike.
 


Kwa mujibu wa Islamic Sharia kila mtu atakayehukumiwa kwa wizi na kukatwa mkono, jamii anayoishi inatakiwa imtunze na kuhakikisha huduma zote za msingi anapatiwa.Hivyo suala la kuwa na vilema wengi kwa hofu ya kuwa tegemezi haitakuwepo.
Acha jokes wewe jamii inashindwa hudumia watoto yatima Ije kuwa walemavu wezi?
 
Hapa ndipo udini unapoanzia,
kuanzia hapo hakutakuwa na kuoana kwa dini tofauti tena,
ule umoja ulioanzishwa na Waasisi wa Taifa hili utakuwa umevunjwa rasmi,
na hapa pia tukumbuke ukabila utarudi upya,
matabaka ya kitaifa yataanza kuonekana kwa Wakristo na Waislamu
migongano, mitafaruku na kutengana baina yetu kutaanza rasmi polepole kwa kadri ya kizazi kitakavyoendele

Am still WAITING, keep in MIND this WORDS!
 
Mimi nina maswali kadhaa ya jinsi gani hizi mahakama za kadhi. Siulizi kwa ubaya lakini ni katika kujuzana tu:

1. Je kama sharia ita kuwa ina contradict sheria mama ya Jamhuri ipi ina take precedent? Kwa mfano sharia iseme kosa "X" lina stahili adhabu "Y" lakini sheria ya Jamhuri ina sema ina stahili adhabu "Z" hapa katiba ipi itaangaliwa? Kama sheria za Jamhuri zita take precedent haitafanya mahakama ya kadhi zisiwe na nguvu? Maana hata katiba ina sheria za ndoa, mirathi nk.

2. Kuna wanaosema katiba mpya ita shughulikia mambo ya mirathi, ndoa nk. Je kwa mfano mimi "John" nimuoe "Amina" je sheria ipi ta chukua mkondo? Au hata tuki badilisha kibao na kusema "Abdalah" kamuoa "Jane". Je likitokea swala la mirathi au migogoro ya ndoa mahakama ipi ita husika? Hapa ni under the assumption Muislamu na Mkristo wameoana bila hata mmoja kubadilisha dini. Na je hii haita fanya ndoa kati ya Mkristo na Muislamu zionekane kuwa mwisho wake ni matatizo tu na kuincourage watu kuto kuoa nje ya dini zao?

3. Je hizi sheria za mahakama ya kadhi zita apply kwa kila Muislamu hata ambae hazi taki na hazi kubali? Mfano ni kwamba mimi ni Muislamu nime fanya kosa ndiyo lakini sitaki kuhukumia chini ya mahakama za kadhi bali mahakama za kawaida je ita kuaje hapa? Je haoa Muislamu ata lazimishwa kuhukumia chini ya sheria za kadhi? Kama aki lazimishwa hili halita wakwaza Waislamu ambao hawa amini katika hukumu za sharia? Na kwa upande mwingine isipo kuwa lazima si itaondoa maana nzima ya hizi mahakama?

4. Je zikianzishwa hizi mahakama zita fuata sharia law down to the book ama zita chaguliwa vipengele hadi vipengele? Haoa tujumbuke kwamba maswala ya makosa na hukumu gani iendane na kosa ni la kijamii pia. Ji kama sharia law inasema kitu fulani lakini kwa asilimia kubwa watu (Waislamu) hawata amini hiyo ni hukumu stahiki ita kuaje?

5. Je mtu akiamua kubadilisha dini kwa kuogopa hukumu za sharia itakuaje? Kwa mfano "Omari" kashtakia mahakama ya kadhi akaona kwamba hukumu itakua nzito na akaamua kubadilisha dini kukwepa hukumu ita kuaje?

Nina maswali mengi zaidi ila kwa post hii nadhani ina tosha. Maswali yote haya ni katika kuelimishana tu na natumai yata jibiwa na wataalamu wa hizi mahakama au sharia law.
 


Kwa mujibu wa Islamic Sharia kila mtu atakayehukumiwa kwa wizi na kukatwa mkono, jamii anayoishi inatakiwa imtunze na kuhakikisha huduma zote za msingi anapatiwa.Hivyo suala la kuwa na vilema wengi kwa hofu ya kuwa tegemezi haitakuwepo.

Mkuu hapa unaongea under the assumption kwamba jamii itakua tayari kufanya hivyo. Kwa vile jamii kuwa hudumia haipo kwenye sheria ina maana hii ita tegemea na utashi wa jamii yenyewe specifically Waislamu wenyewe. Je Waislamu mta kuwa tayari kuwa hudumia hao watu? Au ndiyo lita kua jukumu la serikali tena?
 
Hivi TZ inaelekea wapi??? sasa hivi mtasikia Ijumaa nayo ni off day, waislam wanaenda kuswali.

Please tusiendeshe nchi kama mchezo wa kujipikilisha......
 
Na wale Coptic Orthodox Christians amabo Christmas yao ni 7th of January, nayo hiwe siku ya mapumziko...!

Na wakatoliki wanasikukuu yao ya mwaka mpya wa kikatoliki unaoanza jumapili ya mwisho ya mwezi wa kumi na moja nao pia wapewe!
 
Mimi nina maswali kadhaa ya jinsi gani hizi mahakama za kadhi. Siulizi kwa ubaya lakini ni katika kujuzana tu:

1. Je kama sharia ita kuwa ina contradict sheria mama ya Jamhuri ipi ina take precedent? Kwa mfano sharia iseme kosa "X" lina stahili adhabu "Y" lakini sheria ya Jamhuri ina sema ina stahili adhabu "Z" hapa katiba ipi itaangaliwa? Kama sheria za Jamhuri zita take precedent haitafanya mahakama ya kadhi zisiwe na nguvu? Maana hata katiba ina sheria za ndoa, mirathi nk.

Hizo ni hoja za msingi ambazo ni vema zikajadiliwa kwa utulivu na mantiki bila kuchukua mwelekeo wa ushabiki na kubezana ambako kunaweza kubadilisha sura nzima ya hoja iliyopo.

Sheria za Kiislamu ni moja miongoni mwa vyanzo vya sheria nchini Tanzania, mwaka 1964, Bunge la Tanganyika kwa wakati huo lilipitisha “Sharia ya Kiislamu (Sheria ndogo)” iliyompa madaraka Waziri aliyehusika na mambo ya Sheria kuandaa na kuchapisha kipengele cha Sharia ya Kiislamu baada ya kushauriana na wanachuoni wa Sharia za Madh-hebu za Kiislamu. Na hatimae Katibu Mkuu wa Bunge wakati huo, alikamilisha kuandika Mswada wa ndoa wenye sehemu 4 (kwa msaada wa masheikh wa madh-hebu za Kiislamu).

Mswada huu uliotolewa kama Sharia ndogo chini ya kifungu kidogo cha Sharia ya Kiislamu (Na: 56 ya mwaka 1964) ikiwa ni sehemu ndogo ya Gazeti la Serikali na Na: 34 la tarehe 27, Juni, 1967.

Ilifahamika kuwa sehemu zilizosalia, kuhusiana na kuwalea watoto na talaka n.k. zingechapishwa mapema. Lakini zoezi hili lilisitishwa na badala yake serikali ilitunga sheria ya ‘Ndoa’ kupitia Mswada wa Ndoa wa mwaka 1971.

Hata hivyo, kwa mujibu wa kumbukumbu zangu, kanuni ya Sheria ya Kiislamu 1964 bado haijafutwa na bado ni sehemu ya Kitabu cha Bunge.

Hoja ya msingi hapa ni kuwa sheria hizo zilikuwepo, pamoja na kutokuwepo kwa Mahakama ya Kadhi, aidha sheria husika katika mswada jadiliwa zinahusiana tu na yale mambo ya Ndoa, Talaka, Mirathi, na malezi ya watoto kwa Waislamu na hazigusi kabisa uhuru wa raia wengine katika kuabudu dini zao.


2. Kuna wanaosema katiba mpya ita shughulikia mambo ya mirathi, ndoa nk. Je kwa mfano mimi "John" nimuoe "Amina" je sheria ipi ta chukua mkondo? Au hata tuki badilisha kibao na kusema "Abdalah" kamuoa "Jane". Je likitokea swala la mirathi au migogoro ya ndoa mahakama ipi ita husika? Hapa ni under the assumption Muislamu na Mkristo wameoana bila hata mmoja kubadilisha dini. Na je hii haita fanya ndoa kati ya Mkristo na Muislamu zionekane kuwa mwisho wake ni matatizo tu na kuincourage watu kuto kuoa nje ya dini zao?

3. Je hizi sheria za mahakama ya kadhi zita apply kwa kila Muislamu hata ambae hazi taki na hazi kubali? Mfano ni kwamba mimi ni Muislamu nime fanya kosa ndiyo lakini sitaki kuhukumia chini ya mahakama za kadhi bali mahakama za kawaida je ita kuaje hapa? Je haoa Muislamu ata lazimishwa kuhukumia chini ya sheria za kadhi? Kama aki lazimishwa hili halita wakwaza Waislamu ambao hawa amini katika hukumu za sharia? Na kwa upande mwingine isipo kuwa lazima si itaondoa maana nzima ya hizi mahakama?

4. Je zikianzishwa hizi mahakama zita fuata sharia law down to the book ama zita chaguliwa vipengele hadi vipengele? Haoa tujumbuke kwamba maswala ya makosa na hukumu gani iendane na kosa ni la kijamii pia. Ji kama sharia law inasema kitu fulani lakini kwa asilimia kubwa watu (Waislamu) hawata amini hiyo ni hukumu stahiki ita kuaje?

5. Je mtu akiamua kubadilisha dini kwa kuogopa hukumu za sharia itakuaje? Kwa mfano "Omari" kashtakia mahakama ya kadhi akaona kwamba hukumu itakua nzito na akaamua kubadilisha dini kukwepa hukumu ita kuaje?

Nina maswali mengi zaidi ila kwa post hii nadhani ina tosha. Maswali yote haya ni katika kuelimishana tu na natumai yata jibiwa na wataalamu wa hizi mahakama au sharia law.

Kwenye sheria ya ndoa ya Tanzania, kuna ndoa za aina tatu zinazo tambuliwa na serikali.

A: Ndoa ya serikali, ambao inafungwa Bomani.
B: Ndoa za Kidini, Ambazo ni za Kiislam na Kikristo
C: Ndoa za Kimila.

Wanaotaka kuingia kwenye ndoa ni hiyari yao kuchaguwa kati ya mafungu hayo matatu. Ikitokea kuwa ni watu wa Imani na dini tofauti, wengi wao uelekea kwenye ndoa ya kiserikali, yaani wanafunga ndoa yao Bomani na kukiwa na tatizo litatatuliwa uko uko bomani.

Kama ni ndoa ya Kiislam hapo sasa ndipo Kadhi atakapo husushwa, na kama wana ndoa hawataki kutambua mahamuzi ya kadhi, hiyo pia ni hiyari yao wanaweza kwenda kwenye mahakama za kawaida.
 
Back
Top Bottom