Mahakama ya kadhi hii hapa!

Mahakama ya kadhi hii hapa!

Kwani bila hiyo mahakama hayo masuala yanashughulikiwa vipi?[Originally posted by SAFARI NI SAFARI]

Kwa kawaida yangeshughulikiwa na mahakama hizi za kawaida na kwa muda mrefu yamekuwa yakishughulikiwa na mahakama hizihizi za kawaida.Kwa mfano kwa suala la miradhi ili kutambua uwepo wao serikali ilizigawanya sheria katika makundi matatu nayo ni sheria za kimila,sheria za kiislamu na sheria za kiserikali.Katika kutoa hukumu sheria za kiislamu za mirathi zimekuwa zikitumika ikibainika mhusika alikua muislamu na alikuwa anaishi maisha yake kwa kuzingatia sheria za kiislamu.Mimi sijui hawa jamaa wanatafuta nini?nafikiri lengo lao nchi hii iwe ya kiislamu!

Kenya ina mahakama ya Kadhi, je ni ya kiislam?
 
Mahakama ya kadhi ni maalumu kwa ajiri ya kutatua migogoro ya miradhi,ndoa na mambo mengine yanayowahusu waamini wa dini ya kiislamu,na hutoa maamuzi yake kwa kutumia sheria na miongozo ya kiislamu.Wakati mahakama za kawaida husuluhisha migogoro mbalimbali kwa kutumia katiba mama na sheria mabalimbali zinazotoa miongozo ya namna ya kuongoza nchi na raia wake bila kujali dini zao.

Kwani bila hiyo mahakama hayo masuala yanashughulikiwa vipi?
kuuliza si ujinga...zaidi ya kuchapwa mboko na mengineyo kama hayo, ndugu huyu akifungwa anaenda jela ipi? Ile ya wote ama special, je ndugu hawa wasiporidhika na qadhi wanakata rufaa wapi? Je katika kuamua maamuzi yao hayo yakagusa wanadini wengine tunaisort out vipi? Mfano hizi kesi lukuki za haki ya kuzika kikristu ama kiislam..
 
ITAENDESHWA KWA GHARAMA ZA NANI ? KAMA NI KWA GHARAMA ZA SERIKALI WATAKUWA NA UPUNGUFU WA AKILI KICHWANI. :mod:
Buchu, mambo mangapi ya kidini yanafanyika kwa gharama za serikali, Unajua chochote kuhusu MoU kati ya serikali na wakristo?, inamaana kwa serikali kufinance projects za makanisa wamekuwa na upungufu wa akili?, it seems you didint think properly
 
ITAENDESHWA KWA GHARAMA ZA NANI ? KAMA NI KWA GHARAMA ZA SERIKALI WATAKUWA NA UPUNGUFU WA AKILI KICHWANI. :mod:

kwani wewe unadhani serikali hii ina viongozi wazima wa akili!haijulikani kwa vipi wameruhusu mjadala huu uendelee!
 
Mkuu tufanye hesabu ya haraka ni shule ngapi za kanisa zimefunguliwa tangia mwaka 1985 halafu tucompare na shule zengine za waislamu, wapagani, mabuddha nadhani utajua nini nazungumza. Pili tuje katika hospitali ngapi zimefunguliwa za kikristo tangia mwaka 1990 mpaka leo ukishajijibu haya ndio utaona kaka nini nachokizungumza.

Waislamu hawakunyimwa kufungua vyuo vyao, shule nyingi za kikristo zimerudi serikalini kama Pugu,Ashira,Mazengo ila kali kuliko yote ni chuo cha TANESCO kupewa waislamu tena kwa amri ya kutochukua hata samani moja...thinking abt it, and being in recruitment for over 20yrs I am yet to recruit a single candidate from there..no hatin just thinkin was it worth it????
 
Mkuu tufanye hesabu ya haraka ni shule ngapi za kanisa zimefunguliwa tangia mwaka 1985 halafu tucompare na shule zengine za waislamu, wapagani, mabuddha nadhani utajua nini nazungumza. Pili tuje katika hospitali ngapi zimefunguliwa za kikristo tangia mwaka 1990 mpaka leo ukishajijibu haya ndio utaona kaka nini nachokizungumza.

Huzungumzii shule za BAKWATA ama unakuwa kipofu wa mawazo na fikra?

Mpaka mwaka 2005 BAKWATA ilikuwa na shule 17 na chuo kimoja! na walikuwa na mpango wa kuongeza nchi nzima.

Msome Muadhama Mufti Shekhe Issa Shamban Simba alipokuwa akihutubia maulidi Kibaha

Bakwata owned and managed 17 secondary schools and one college, and was planning to build a secondary school in each district all over the country.

Zaidi soma hapa

Mufti underscores peace
 
Mie napendekeza ili kusiwe na manung'uniko, basi:

1. Ijumaa iwe siku ya Mapumziko - Waislaam.
2. Jumamosi iwe ni siku ya Mapumko - Wasabato
3. Jumapili iwe ni siku ya Mapumziko - Wakristo wengine.

Kama ikipatikana na siku nyingine ya watu gani sijui na yenyewe ikawa siku ya mapumziko, itakuwa safi sana.

Au tufuate wimbo wa Ebo Masaai ambaye anataka Wiki iwe na siku tatu yaani Ijumaa, Jumamosi na Jumapili.
Wapagani iwe siku ya mapumziko ALHAMISI weeeeeee ila patamu!
 
waislamu ni miongoni mwa watanzania wanaolipa kodi hivyo serikali inawajibika kuchangia gharama za uendeshaji wa mahakama za kadhi kama inavyochangia gharama za uendeshaji wa huduma mbali mbali zinazotolewa na makanisa baada ya kusaini memorundum of understanding mwaka 1992.

Kaka kwa waislam kuwa miongoni mwa walipa kodi si kigezo cha kufanya serikali iwalipie gharama/malipo ya kadhi, hiyo ni hoja dhaifu kabisa kuwahi kutokea. Kodi wanayolipa pamoja na wakristu wa nchi hii inafanya shughuli nyingi tu za kimaendeleo ambazo waislam na wakristu wote hunufaika nazo.

Labda miye sielewi, Naomba utaje huduma za makanisa ambazo kodi ya serikali inayochangiwa na waislam na wakristu hutumiaka kuhudumua makanisa. KAKUNA KODI ya serikali inayotumika kuhudumia viongozi wa makanisa hapa Tanzania. Jamani tuwe wakweli kwa kujenga hoja.

Unajua ukijenga hoja ikawa na mashiko, hata iwe imetolewa na mtu ambaye humpendi utaipenda tu na utaona ukweli ndani yake.

Miye binafsi sipingi mahakama ya kadhi hata siku moja, ila kadhi mlipeni nyie wenyewe waislam, Kadhi hashughulikii mambo ya wakristu kwa nini alipwe na Serkali ya wakristu na waislam wakati yeye anahudumia upande mmoja- hapo haitakuwa halari.

Kaka nikuulize swali, Rafiki yako anaweza akaoa mke wewe ndo ukawa unatoa matumizi kwa ajili ya mke wa rafiki yako? wakati huyo mke wa rafiki yako hata siku moja hatakupikia chakula wala kukuandalia maji ya kuoga?
 
Kinachohitajika ni elimu kuhusu mahakama ya kadhi na utendaji wake wa kazi. waislamu ni asilimia 35 ya watanzania, Asilimia 65 iliyo bakiinamaswali mengi ambayo mpaka sasa hayajapatiwa majibu yanayojitosheleza. Itolewe elimu ya kutosha kabla ya kuanzishwa kwa hii mahakama ili kuondoa hofu ya udini inayojengeka.

Mkuu,

Na mimi naomba source ya Takwimu zako.
Ninavyojuwa hakuna kipengele cha uainisho wa dini kwenye sensa hapa Tanzania. Utanisaidia sana, tafadhali ninaihitaji.

Natanguliza shukrani zangu kwako.
 
mi nina swali kwa waislam na wengine wote mnaolipamba hili la mahakama ya kadhi.
1. Ni nini kinafanya mpaka muishinikize serikali?
2. Kwa nini hamtaki kuianzisha wenyewe bila kupitia serikalini?
Natumai ,tajibu maswali haya!
 
Hili swala ni kama kawizara kengine, hakuna cha maslahi wala nini....kwa nini kawe chini ya Serikali????? watu wanataka KULA.....
 
Mie ninavyofahamu wanazungumzia kurudishwa kwa mahakama ya kadhi.

Mahakama hiyo ilikuwepo hapo awali kwa miaka mingi.

Uwepo wake haukukwaza waumini wa dini nyengine zisizokuwa uislam kuendelea na itikadi zao, bali iliwezesha waumini wa kiislam kutekeleza itikadi zao kwa mujibu wa dini yao.

Tanzania ni nchi isiyo na dini, ila wananchi wake wana dini.

Katiba ya tanzania inampa uhuru raia yoyote kufanya ibada bila kubughudhiwa.

Mahakama ya kadhi itawapa uhuru waislamu kufanya ibada zao, na haitomuingilia asiyekuwa muislamu kufanya ibada zake.

Kuhusu gharama za uendeshaji.

Mahakama itaendeshwa kwa kutumia fedha za waislamu na sio fedha inayokusanywa na kaisari, ya kaisari atapewa kaisari.
 
...mwanamume wa kiislamu kaoa mke wa kikristo (ameishi nae kwa miaka 20 na kuzaa nae watoto 3). wamejaaliwa kuwa na mali kadhaa (nyumba 3, gari 2, duka 1 na mashamba 2). kwa sababu za manyanyaso yaliyo dhahiri ya mume huyu kwa mkewe na uzinzi dhahiri, mke huyu anadai talaka. Mume anapeleka shauri mahakama ya kadhi, itakuwaje?
 
Mie ninavyofahamu wanazungumzia kurudishwa kwa mahakama ya kadhi.

Mahakama hiyo ilikuwepo hapo awali kwa miaka mingi.

Uwepo wake haukukwaza waumini wa dini nyengine zisizokuwa uislam kuendelea na itikadi zao, bali iliwezesha waumini wa kiislam kutekeleza itikadi zao kwa mujibu wa dini yao.

Tanzania ni nchi isiyo na dini, ila wananchi wake wana dini.

Katiba ya tanzania inampa uhuru raia yoyote kufanya ibada bila kubughudhiwa.

Mahakama ya kadhi itawapa uhuru waislamu kufanya ibada zao, na haitomuingilia asiyekuwa muislamu kufanya ibada zake.

Kuhusu gharama za uendeshaji.

Mahakama itaendeshwa kwa kutumia fedha za waislamu na sio fedha inayokusanywa na kaisari, ya kaisari atapewa kaisari.
hujajibu swali kwa nini mnaishinikiza serikali ihusike? Kwani iliwanyima uhuru kuianzisha bila kelele za kuihusisha serikali? Waislam mnaodai jambo hili kiserikali mnaboa.
 
Mie ninavyofahamu wanazungumzia kurudishwa kwa mahakama ya kadhi.

Mahakama hiyo ilikuwepo hapo awali kwa miaka mingi.

Uwepo wake haukukwaza waumini wa dini nyengine zisizokuwa uislam kuendelea na itikadi zao, bali iliwezesha waumini wa kiislam kutekeleza itikadi zao kwa mujibu wa dini yao.

Tanzania ni nchi isiyo na dini, ila wananchi wake wana dini.

Katiba ya tanzania inampa uhuru raia yoyote kufanya ibada bila kubughudhiwa.

Mahakama ya kadhi itawapa uhuru waislamu kufanya ibada zao, na haitomuingilia asiyekuwa muislamu kufanya ibada zake.

Kuhusu gharama za uendeshaji.

Mahakama itaendeshwa kwa kutumia fedha za waislamu na sio fedha inayokusanywa na kaisari, ya kaisari atapewa kaisari.


Hivi Mahakama ya Kadhi ipo kwenye zile Nguzo tano za Kiislam?

1. Shahada ya Imani
2. Swalah
3. Kutoa Zakaah (Kuwakunjulia Wenye Dhiki)
4.
Kufunga katika Mwezi wa Ramadhaan Kila mwaka (Swaumu)
5.
Kuhiji Makkah

Hii Mahakama Ya Kadhi inaingia wapi? Msaada tafadhali
 
Mahakama ya kadhi haitahitaji polisi wala magereza, kwa sababu itashughulika na mirathi na mambo ya ndoa tu, na haitamlazimisha kila muislam aende akatafute haki yake huko, ni kwa wale tu watakao kuwa tayari kurithia maamuzi ya mahakama hiyo. So kama wewe ni muislam na una imani na mahakama za kawaida you proceed na kufungua malalamiko yako huko, na kama una imani na mahakama ya kadhi waenda huko, so hakuna kulazimishana!
Kuna tofauti gani kati ya sheria za mirathi zinazotumika sasa na hizi za Kiislamu?
 
...mwanamume wa kiislamu kaoa mke wa kikristo (ameishi nae kwa miaka 20 na kuzaa nae watoto 3). wamejaaliwa kuwa na mali kadhaa (nyumba 3, gari 2, duka 1 na mashamba 2). kwa sababu za manyanyaso yaliyo dhahiri ya mume huyu kwa mkewe na uzinzi dhahiri, mke huyu anadai talaka. Mume anapeleka shauri mahakama ya kadhi, itakuwaje?
Atapelekaje kesi yake mahakama ya kadhi, kwani wameona kwa mujibu wa sharia ya Kiislam!? We vipi!?
 
Back
Top Bottom