Mufti mkuu wa waislamu muadhama sheikh simba ametangaza kuwa mahakama ya kadhi kwa ajili ya waislamu itaanza kazi zake hivi karibuni baada ya serikali kukubali kuirudisha tena mahakama hiyo iliyokuweko enzi za nyuma na pia kuiomba serikali kufanya siku kama ya jana tarehe 7 kuwa siku ya mapumziko kwa kuwa ni mwaka mpya wa waislamu!
Source: Gazeti la mwananchi 08.12.10
kama serikali imekubali mahakama hiyo basi naipongeza kwa uamuzi huo wa busara wa kuwapa waislamu kile wanachotaka kwa mujibu wa sheria na kusisitiza hoja ya mufti kufanywa siku ya mapumziko kwa kuingia mwaka mpya wa kiislamu kwa sababu hata dini zingine huwa wanamapumziko siku za mwaka mpya wa tarehe 1.1 kila mwaka hivyo waislamu nao wana haki ya kusherehekea mwaka wao mpya na ifanywe kuwa ni siku ya holliday!!
kwa kweli inaonyesha kwamba watu wengi hawajui wanachokisema!
wakristo wana amri na mfumo wao wa kimahakama unaojulikana kama
"canons laws " na hapa kuna takribani sheria kama 4300 ambazo zinahusu mirathi,talaka, ndoa, na mahusihano kati ya mtu na mtu na kati ya Mungu na mtu. waislamu pia wana mfumo wao wa kimahakama unatunga sheria za aina mbili yaani
"IBADAT NA MUAMALAT" sasa kwa nchi za kidini kama
saudia Arabia sheria za kidini ndio zainatwala nchi hiyo yaani mfumo wa kiislamu kwa madhehebu ya suni na sio suni tu bali "wahabiyya" na pia kama Vatican ni nchi ambayo wakazi wake wanafuata canons laws!
kwa Tanzania katiba iliamua sheria zisiwe za kidini na masuala ya dini yasiingie katika mifumo ya nchi bali suala la dini liwe la mtu binafsi!
sasa leo waislamu wakikubaliwa mahakama ya kadhi na sheria Zao katika mfumo wa nchi kesho wakristo wakiomba nao mfumo wao kisheria utambuliwe na serekali hapo hatuna nchi tena!
nchi yetu ni ya "kisekula" yaani isiyofuata sheria ya dini yoyote bali katiba huru na kama tunataka tuuingize Tanzania katika muundo wa kidini amani iliyopo itatoweka kabisa!
kama waislamu wanataka kadhi fine but ifanyike katika misikiti yao na kama wakristo wanataka canons laws sawa lakini ifanyike katika makanisa yao LAKINI TANZANIA ISIINGILIWE NA DINI YOYOTE!
LEO serikali ikiwakubalia waislamu mahakama ya kadhi kesho haitaweza kuwazuia wakristo kuwa na mahakama za "canons" na pia haitawazuia wahindu kuwa na mahakama za kihundu na isiwazuie wapagani na waabudu mashetani kuwa na mahakama zao!
wanaoshabikia mambo ya dini kuingizwa katika serikali "hawajui hasa madhara ya kitu wanachodai"