Mahakama ya kadhi hii hapa!

Mahakama ya kadhi hii hapa!

Mkuu, X-Paster,

Kwanza asante kwa ufafanuzi. Na ni kweli mjadala lazima uwe wa kwa upole na bila ushabiki. Naona leo kwa kiwango kikubwa watu wame jitahidi kutoa hoja zao binafis bila malumbano au matusi yasiyo ya lazima.

Mkuu mengi ya hapo juu uliyo sema nime yaelewa ila nina swali moja kwenye moja ya vipengele vyako na nanukuu


Kama ni ndoa ya Kiislam hapo sasa ndipo Kadhi atakapo husushwa, na kama wana ndoa hawataki kutambua mahamuzi ya kadhi, hiyo pia ni hiyari yao wanaweza kwenda kwenye mahakama za kawaida.

Mkuu hapa ndiyo haswa wasi wasi wangu. Swali langu hapa ni hivi. Tuchukulie kwamba wote mimi na wewe ni Waislamu. Mkuu X-Paster unaamua kunishtaki mimi MF1 kwa sababu a, b na c kwa mujibu wa dini yetu. Je mimi MF1 kama sitaki kushitakiwa kwenye mahakama ya kadhi inakuaje? Maana si siwezi kulazimishwa kama siamini sharia hata kama si Muislamu? Na je ikiwa hivi si kila mtu anaye shtakiwa kwenye mahakama ya kadhi ata taka ashitakiwe mahakama ya kawaida? Je hii haitafanya uwepo wa hizi mahakama zisiwe za lazima?

Mimi pendekezo langu lingikua kama ifuatavyo. Tungeangalia vipengele vya sharia law ambazo zinaendana na jamii yetu. Tuangalie na hata sheria za Wakristo ambazo zinaendana na jamii yetu. Hizi tuzi incorparate kwenye sheria za nchi zetu. Kwa sababu naamini kabisa kama jamii iliyo jichanganya lazima tuwe tayari kucompromise na siyo kila mtu kupata kila anacho kitaka kwa wakati anao utaka.

Kwa sababu ukiangalia sehemu nyingi ambazo sharia law zina tumika ni zile sehemu ambazo jamii kiujumla imezikubali sheria hizo. Ndiyo maana hata ukitoa mfano wa nchi kama Kenya Na Nigeria mahakama za kadhi haziko sehemu zote bali zile sehemu tu ambazo Waislamu wapo concenrated na jamii hizo zime kubali hizo sharia law. Ndiyo maana sehemu kama Zanzibar kuwa na mahakama za kadhi sishangai kwa sababu 99% ni Waislamu na jamii yao kiujumla wame kubali hizo sharia.

Kwa hiyo tuki sema tuwe na mahakama za kadhi nchi nzima naona kama ni makosa kwa sababu hatuangalii jamii husika. Pia nitakuuliza swali ila usijibu wewe kama wewe ila angalia mtazamo wa Waislamu wote. Je wapo tayari kuhukumiwa chini ya sharia law? Je wengi wana zielewa au wana advocate mahakama ya kadhi kwa sababu tu wanaona hili swala ni kama vile Waislamu dhidi ya Wakristo?

Kwa hiyo mimi naona pia kabla ya yote ni muhimu nyie Waislamu kama Waislamu mukae halafu mtafakari. Muangalie kama kweli wengi wenu mnazielewa fika hizo sharia na mahakama ya kadhi. Kwa sababu nina wasi wasi kuna Waislamu hawajui sharia law zina fanya kazi vipi au mahakama za kadhi zina fanya kazi vipi. Hawa ndiyo naogopa kwamba kwao hili swala ni la ushabiki tu lakini wao wenyewe hawana uhakika na wanacho kitetea.

Yote haya nasema kwa sababu na naomba uni kosoe nikikosea. Sharia laws kwa asilimia kubwa ni sheria ambazo zilikua zinaendana na jamii za watu husika kwa wakati huo. Je kwetu sisi jamii yetu inaendana vipi na hizo sheria? Nasema hivi kwa sababu japo kuna sheria ambazo ni universal kama vile mtu akiua kufungwa maisha au kuuliwa pia kuna sheria ambazo zinaangalia jamii. Kwamba kosa "X" kwa sisi Watanzania tunaweza ona lina stahili adhabu "Y" lakini jamii nyingine wakaona ina stahili adhabu "Z". Kwa hiyo naomba sana tujiangalie sisi kama jamii na tukubali kwamba it is possible kwamba kuna baadhi ya vipengele vya sharia ambazo hata Waislamu wenyewe wa Tanzania wanaweza wasi kubaliane navyo. Na ndiyo maana hapo juu nika sisitiza kuchambua kutoka dini zote kuu mbili sheria zinazoendana na jamii yetu.
 
Mi nawatakia kila la heri ktk kufanikisha hili la mahakama ya kadhi kwa ndugu zetu waislam.nadhani mahakama hiyo ikitumiwa vizuri itawanufaisha waislamu wote na wala haitagusa maslahi ya wakristo.
Ila msije mkataka nchi hii ijiunge na jumuiya ya kiislam oic.hapo ndipo hatutakubali kwani itakuwa sawa na kutusilimisha watanzania wote wakati idadi ya wakristo ni kubwa zaidi hapa tz.
All ze best.

Wewe kilaza una data za hizo pumba unazoongea? Unajua census ya mwisho iliyokusanya idadi ya watu kwa imani ya dini ilikuwa mwaka gani na ni watu gani walikuwa wengi na kwa kiasi gani?
acha kupotosha na data zenu za kupika, tuna ofisi hapa bongo inashughulikia masuala ya taarifa mbalimbali za kijamii, kiuchumi, nk. Tembelea sio unato quote zisizokuwa na ukweli. Aliyelala usimuamshe, utalala wewe!!!!!!!!!!!!!
 
All the best to them.. tuwaachie waendeshe mahakama yao ili mradi isiingilie maisha ya wengine,
hivi hii mahakama wataiendeshaje? mishahara ya hao majaji au qadis na gharama zingine za uendeshaji hili ndio la muhimu zaidi BAKWATA wanajiweza kuendesha hizo mahakama zitakazoanzishwa?
 
Mkuu, X-Paster,

Kwanza asante kwa ufafanuzi. Na ni kweli mjadala lazima uwe wa kwa upole na bila ushabiki. Naona leo kwa kiwango kikubwa watu wame jitahidi kutoa hoja zao binafis bila malumbano au matusi yasiyo ya lazima.

Mkuu mengi ya hapo juu uliyo sema nime yaelewa ila nina swali moja kwenye moja ya vipengele vyako na nanukuu




Mkuu hapa ndiyo haswa wasi wasi wangu. Swali langu hapa ni hivi. Tuchukulie kwamba wote mimi na wewe ni Waislamu. Mkuu X-Paster unaamua kunishtaki mimi MF1 kwa sababu a, b na c kwa mujibu wa dini yetu. Je mimi MF1 kama sitaki kushitakiwa kwenye mahakama ya kadhi inakuaje? Maana si siwezi kulazimishwa kama siamini sharia hata kama si Muislamu? Na je ikiwa hivi si kila mtu anaye shtakiwa kwenye mahakama ya kadhi ata taka ashitakiwe mahakama ya kawaida? Je hii haitafanya uwepo wa hizi mahakama zisiwe za lazima?

Mimi pendekezo langu lingikua kama ifuatavyo. Tungeangalia vipengele vya sharia law ambazo zinaendana na jamii yetu. Tuangalie na hata sheria za Wakristo ambazo zinaendana na jamii yetu. Hizi tuzi incorparate kwenye sheria za nchi zetu. Kwa sababu naamini kabisa kama jamii iliyo jichanganya lazima tuwe tayari kucompromise na siyo kila mtu kupata kila anacho kitaka kwa wakati anao utaka.

Kwa sababu ukiangalia sehemu nyingi ambazo sharia law zina tumika ni zile sehemu ambazo jamii kiujumla imezikubali sheria hizo. Ndiyo maana hata ukitoa mfano wa nchi kama Kenya Na Nigeria mahakama za kadhi haziko sehemu zote bali zile sehemu tu ambazo Waislamu wapo concenrated na jamii hizo zime kubali hizo sharia law. Ndiyo maana sehemu kama Zanzibar kuwa na mahakama za kadhi sishangai kwa sababu 99% ni Waislamu na jamii yao kiujumla wame kubali hizo sharia.

Kwa hiyo tuki sema tuwe na mahakama za kadhi nchi nzima naona kama ni makosa kwa sababu hatuangalii jamii husika. Pia nitakuuliza swali ila usijibu wewe kama wewe ila angalia mtazamo wa Waislamu wote. Je wapo tayari kuhukumiwa chini ya sharia law? Je wengi wana zielewa au wana advocate mahakama ya kadhi kwa sababu tu wanaona hili swala ni kama vile Waislamu dhidi ya Wakristo?

Kwa hiyo mimi naona pia kabla ya yote ni muhimu nyie Waislamu kama Waislamu mukae halafu mtafakari. Muangalie kama kweli wengi wenu mnazielewa fika hizo sharia na mahakama ya kadhi. Kwa sababu nina wasi wasi kuna Waislamu hawajui sharia law zina fanya kazi vipi au mahakama za kadhi zina fanya kazi vipi. Hawa ndiyo naogopa kwamba kwao hili swala ni la ushabiki tu lakini wao wenyewe hawana uhakika na wanacho kitetea.

Yote haya nasema kwa sababu na naomba uni kosoe nikikosea. Sharia laws kwa asilimia kubwa ni sheria ambazo zilikua zinaendana na jamii za watu husika kwa wakati huo. Je kwetu sisi jamii yetu inaendana vipi na hizo sheria? Nasema hivi kwa sababu japo kuna sheria ambazo ni universal kama vile mtu akiua kufungwa maisha au kuuliwa pia kuna sheria ambazo zinaangalia jamii. Kwamba kosa "X" kwa sisi Watanzania tunaweza ona lina stahili adhabu "Y" lakini jamii nyingine wakaona ina stahili adhabu "Z". Kwa hiyo naomba sana tujiangalie sisi kama jamii na tukubali kwamba it is possible kwamba kuna baadhi ya vipengele vya sharia ambazo hata Waislamu wenyewe wa Tanzania wanaweza wasi kubaliane navyo. Na ndiyo maana hapo juu nika sisitiza kuchambua kutoka dini zote kuu mbili sheria zinazoendana na jamii yetu.
Mkuu nikuulize swali dogo tu, unapo kubali kuwa ndoa yako ni ya kikristo... Kisha kukatokea tatizo kwenye ndoa yako... Ukaona kuwa wewe kama wewe labda huta faidika na hukumu ile, je unaweza kukataa na kusema kuwa wewe si mkristo tena!?

Jaribu kuelewa kile nilicho ainisha hapo juu, suhala la kuwepo kwa mahakama ya kadhi si kila Muislam anaelewa, ilo kwanza ufahamu, pili hiyo mahakama itakuwa inashughulika na mambo ya ustawi wa tu wa jamii ya Kiislam na ni pale tu wewe utakapo kubaliana na hizo sheria...

Mahakama hii inatarajiwa kushughurikia mambo haya kwa uchache:

1. Ndoa na Talaka
2. Matunzo ya watoto
3. Mirathi
4. Kuitanguliza ndoa
5. Ugawaji wa mali za marehemu

Sasa ikitokea kuwa uridhiki (na si wote wenye kuridhika) basi utakata rufaa kwenda mahakama itakayo hainishwa ambayo itakuwa juu ya mahakama ya Kadhi. Mimi sioni tatizo hapo.
 
Mimi ni kafiri,nailipa kodi serikali yangu,vyanzo vyangu vya mapato ni kama ufugaji na uuzaji wa nyama ya nguruwe,nalipwa riba na mabenki mbalimbali ambapo nakatwa kodi kwa kipato hiki,pia natengeneza na kuuza pombe za kienyeji ambazo pia hutozwa kodi.Mahakama ya kadhi ianzishwe,lakini sitarajii kadhi awe analipwa mshahara kwa kutumia fedha za mimi kafiri.Naamini serikali yangu ni secular government(is not bias in favour of any religion),hivyo sitarajii ijiingize kwenye mambo ya kidini,ikifanya hivyo itakuwa ni kichekesho na itakuwa ni serikali ya kiislamu na itapaswa kuondoka au kuondolewa madarakani mara moja.Mimi ni mfia dini na nipo teyari kufa kwa ajiri ya kutetea dini yangu.

T


TANZANIA BILA MAHAKAMA YA KADHI INAWEZEKANA HATA KAMA RAIS NA MAKAMU WAKE WOTE NI WAISLAMU :llama::llama::llama:

Tuko pamoja, come rain or sunshine; I have no share in someone's else religion; wasituchanganye hawa maana ahadi za Jk kwa waislamu, aatimize kwa pesa zake na za faimilia yake, sio kwa kutumia kodi zetu....we are not going to let them have it the easy way...why? Pesa za Watanzania zake? Waislamu hawajashindwa kujiendeshea mambo yao kwa pesa zako, na hakina anayewazuiia wasifanye mambo yao ya kidini, but they shoild not load it unto us.....
 
Hii mahakama ni moja ya blunder kubwa ambazo CCM itakuja kujutia sana sababu italeta mgwanyiko mkubwa kwa jamii zetu.

Kama kuifanya hii blunder CCM walitakiw waifanye in a smart way.

  • Nyerere alikuwa na uwezo wa kumualika papa lakini hakufanya hivyo kwa sababu alikuwa ni smart asipelke ujumbe mbaya. Papa John Paul alikuja wakati wa kipindi cha Ali Mwinyi
  • Waislam walipewa majengo Mrorogoro kujenga chuo kikuu lakini aliyefanya hivyo Alikuwa ni mkristu .Na hii ni njia smart ya kufanya mambo ya dini
Ukisoma hiyo mifano yangu miwili utaona kwa kitendo cha rais ambaye yuko madarakani kuwa muislam na kushikia kidedea na kukubali hoja hiyo sio njia smart ya kufanya blunder.Kama CCM wanaona umuhimu wa kufanya hii blunder wasuribi atakapokuja rais mkristo ili wafanyahivyo kupunguza mkwaruzo

Lakini tukiweka ushabiki pembeni Hii mahakama ya kadhi haitakiwi kuanzishwa au kuhudumiwa na pesa za walipa kodi.
 
MZALENDO MKUU,

Mkuu unapoongea weka na mifano kidogo au ukubali kuwa hujapata habari za kutosha kuhusu mahakama ya Kadhi. Mimi nimelifuatilia kidogo hili la mahakama ya kadhi kwa nia ya kutaka kujuwa mahakama ya kadhi ni nini, kazi zake na kwa nini ni muhimu kwa waislamu.


Katika tafuta tafuta hizo habari, Nimejuwa kuwa kwanza hii mahakama ipo Zanzibar, ipo Kenya pia. Huko Kenya baada ya katiba mpya kulikuwa na tofauti ya mawazo kuwa jee ibaki kuendelea kuwepo au la. Lakini tokea Kenya kupata uhuru imekuwepo.


Kazi kubwa za mahakama hii ni kushughulikia migogoro ya ndoa za kiislamu na urithi kwa utaratibu wa dini ya kiislamu na siyo kuendesha kesi za madai na makosa ya jinai kama ambavyo mahakama za kiserikali zinafanya. kwa hiyo hilo la kukatwa mikono au miguu halipo, ni hofu tu uliyojijengea, pengine kwa kutokujuwa nini mahakama ya kadhi na kazi zake, au kwa sababu nyengine unazozijuwa wewe.


kwa kifupi, mahakama ya kadhi itakuwa inatoa usuluhishi katika mambo ya ndoa na talaka za kiislamu, na kuelekeza mgao wa urithi kwa waislamu watakaotaka kufuata viwango vilivyoekwa katika uislamu. Walio na matatizo kama wote ni waislamu wanakuwa wana-option ya kuitumia hii mahakama ya kadhi, ila hawalazimiki kufanya hivyo, wanaweza kutumia mahakama za kawaida wakiamua hivyo.


Ama kama ni lazima, serikali iridhie na iruhusu hii mahakama iwepo au wenyewe tu waislamu waianzishe, hapo nafikiri ndio penye mjadala.

Pengine ni vizuri kutofautisha mahakama za kiislamu kwa maana ya mahakama katika nchi za kiislamu kama Saudi Arabia, Iran, na mahakama ya kadhi katika nchi ambayo misingi yake ya sheria si Islamic laws (sharia).


Mahakama ya kadhi katika Tanzania Bara(Tanganyika) haitakuwa na uweza wa kutoa hukumu ya kukatwa mtu mkono, kunyongwa au kufungwa jela. Nimetumia , Tanzania bara ili kutofautisha na Zanzibar kwani Zanzibar ambayo ni m-bia katika Tanzania wanayo mahakama ya kadhi na wala hakuna aliyekatwa mkono kupitia mahakama hii,wala kupelekwa jela kupitia hukumu ya mahakama hii. Ni vivyo hivyo huko Kenya, vilema hawajaongezeka kutokana na kuwepo kwa mahakama ya kadhi.
Wala si katika kazi zake mahakama ya kadhi kusilimisha mtu au nchi.


Tujielimishe kwanza kabla ya kukurupuka kufanya ubishani na malumbano ambayo hayazingatii facts.

kwani cku zote talaka za kiislam zilikuwa zinashughulikiwa na mahakama gni?
 
Mimi ni kafiri,nailipa kodi serikali yangu,vyanzo vyangu vya mapato ni kama ufugaji na uuzaji wa nyama ya nguruwe,nalipwa riba na mabenki mbalimbali ambapo nakatwa kodi kwa kipato hiki,pia natengeneza na kuuza pombe za kienyeji ambazo pia hutozwa kodi.Mahakama ya kadhi ianzishwe,lakini sitarajii kadhi awe analipwa mshahara kwa kutumia fedha za mimi kafiri.Naamini serikali yangu ni secular government(is not bias in favour of any religion),hivyo sitarajii ijiingize kwenye mambo ya kidini,ikifanya hivyo itakuwa ni kichekesho na itakuwa ni serikali ya kiislamu na itapaswa kuondoka au kuondolewa madarakani mara moja.Mimi ni mfia dini na nipo teyari kufa kwa ajiri ya kutetea dini yangu.
TANZANIA BILA MAHAKAMA YA KADHI INAWEZEKANA HATA KAMA RAIS NA MAKAMU WAKE WOTE NI WAISLAMU :llama::llama::llama:
:whoo::whoo:so ver guuuuuuuuuuuuuuuud:whoo:
 
Tanzania bila mahakama ya kadhi inawezekana hata kama rais na makamu wake wote ni waislamu .lakini tanzania bila ya ubalozi wa vatican haiwezekani maana nchi hii ni ya dini moja tu


Wewe bwana weeeee-nchi huwa haina roho, so haiwezi kuwa na dini;
 
ikiwa mtuhumiwa siyo muislamu inakuwaje?

Mahakama ya kadhi ni ya waislam na kwaajili ya waislam tu. Sio mahakama ya kusikiliza kesi za wizi wa kuku ila kwa maswala yahusuyo mambo ya ndoa za "kiislam" na mirathi. Hakuna hata sehemu moja itakayomgusa asie muislam.
 
MZALENDO MKUU,

Mkuu unapoongea weka na mifano kidogo au ukubali kuwa hujapata habari za kutosha kuhusu mahakama ya Kadhi. Mimi nimelifuatilia kidogo hili la mahakama ya kadhi kwa nia ya kutaka kujuwa mahakama ya kadhi ni nini, kazi zake na kwa nini ni muhimu kwa waislamu.


Katika tafuta tafuta hizo habari, Nimejuwa kuwa kwanza hii mahakama ipo Zanzibar, ipo Kenya pia. Huko Kenya baada ya katiba mpya kulikuwa na tofauti ya mawazo kuwa jee ibaki kuendelea kuwepo au la. Lakini tokea Kenya kupata uhuru imekuwepo.


Kazi kubwa za mahakama hii ni kushughulikia migogoro ya ndoa za kiislamu na urithi kwa utaratibu wa dini ya kiislamu na siyo kuendesha kesi za madai na makosa ya jinai kama ambavyo mahakama za kiserikali zinafanya. kwa hiyo hilo la kukatwa mikono au miguu halipo, ni hofu tu uliyojijengea, pengine kwa kutokujuwa nini mahakama ya kadhi na kazi zake, au kwa sababu nyengine unazozijuwa wewe.


kwa kifupi, mahakama ya kadhi itakuwa inatoa usuluhishi katika mambo ya ndoa na talaka za kiislamu, na kuelekeza mgao wa urithi kwa waislamu watakaotaka kufuata viwango vilivyoekwa katika uislamu. Walio na matatizo kama wote ni waislamu wanakuwa wana-option ya kuitumia hii mahakama ya kadhi, ila hawalazimiki kufanya hivyo, wanaweza kutumia mahakama za kawaida wakiamua hivyo.


Ama kama ni lazima, serikali iridhie na iruhusu hii mahakama iwepo au wenyewe tu waislamu waianzishe, hapo nafikiri ndio penye mjadala.

Pengine ni vizuri kutofautisha mahakama za kiislamu kwa maana ya mahakama katika nchi za kiislamu kama Saudi Arabia, Iran, na mahakama ya kadhi katika nchi ambayo misingi yake ya sheria si Islamic laws (sharia).


Mahakama ya kadhi katika Tanzania Bara(Tanganyika) haitakuwa na uweza wa kutoa hukumu ya kukatwa mtu mkono, kunyongwa au kufungwa jela. Nimetumia , Tanzania bara ili kutofautisha na Zanzibar kwani Zanzibar ambayo ni m-bia katika Tanzania wanayo mahakama ya kadhi na wala hakuna aliyekatwa mkono kupitia mahakama hii,wala kupelekwa jela kupitia hukumu ya mahakama hii. Ni vivyo hivyo huko Kenya, vilema hawajaongezeka kutokana na kuwepo kwa mahakama ya kadhi.
Wala si katika kazi zake mahakama ya kadhi kusilimisha mtu au nchi.


Tujielimishe kwanza kabla ya kukurupuka kufanya ubishani na malumbano ambayo hayazingatii facts.

Kaka nakushukuru sana kwa maelezo mazuri umenifumbua macho kwa hilo, swala ambalo linanitatiza kuhusu hii mahakama ya kadhi ni kwamba, Hao Kadhi watalipwa na nani? serikali au michango ya waisilam?

Kama inashughulikia mambo ya waislam tu kwa nini wanataka kadhi alipwe na serikali? Kwa kuwa inataka kushughulikia mambo ya waislam, hata mimi naunga mkono iwepo lakini, Kadhi asilipwe kutokana na kodi zinazotokana na Matanzania wote yaani wakristu na waislam.

Kuna jamaa humu kasema hata waislam wanalipa kodi,

Ukweli ni kwamba, watanzania wote wanalipa kodi na kodi hiyo huwasaidia wote katika kutekeleza huduma mbalimbali kama barabara, maji, shule, Hospotalini kununua dawa nk.
Huo ujanja wa kutaka kodi za watanzania wote kwa kiasi fulani zilipe viongozi wa dini ambayo haitashughulikia dini zote huoni hapo ni kunyonyana.

Kwa ujumla sisi wote humu JF hatuwezi kuipitisha kwa hizi bra bra, kila mmoja hapa anatoa hisia zake tu wenye uwezo ni wabunge wetu tuliowachagua mwaka huu.

Wito wangu kwa wabunge wetu, kama hili swala likirudi mjengoni, Tunawaomba mtafakari kwa kina KODI isitumike kulipa kadhi ambaye atashughulikia dini moja tu. MAhakama wacha ije lakini KODI wamchangie waumini wa dini hiyo.

Wenye ufahamu tunaomba muweke wazi zaidi, kwani hicho kitabu kitukufu kimesema kadhi alipwe na serikali ambayo haina dini ila inatambua dini za raia wake?

Nawakilisha.
 
Kinachohitajika ni elimu kuhusu mahakama ya kadhi na utendaji wake wa kazi. waislamu ni asilimia 35 ya watanzania, Asilimia 65 iliyo bakiinamaswali mengi ambayo mpaka sasa hayajapatiwa majibu yanayojitosheleza. Itolewe elimu ya kutosha kabla ya kuanzishwa kwa hii mahakama ili kuondoa hofu ya udini inayojengeka.
 
Wewe kilaza una data za hizo pumba unazoongea? Unajua census ya mwisho iliyokusanya idadi ya watu kwa imani ya dini ilikuwa mwaka gani na ni watu gani walikuwa wengi na kwa kiasi gani?
acha kupotosha na data zenu za kupika, tuna ofisi hapa bongo inashughulikia masuala ya taarifa mbalimbali za kijamii, kiuchumi, nk. Tembelea sio unato quote zisizokuwa na ukweli. Aliyelala usimuamshe, utalala wewe!!!!!!!!!!!!!



cheki huyu nae .
 
Kaka nakushukuru sana kwa maelezo mazuri umenifumbua macho kwa hilo, swala ambalo linanitatiza kuhusu hii mahakama ya kadhi ni kwamba, Hao Kadhi watalipwa na nani? serikali au michango ya waisilam?

Kama inashughulikia mambo ya waislam tu kwa nini wanataka kadhi alipwe na serikali? Kwa kuwa inataka kushughulikia mambo ya waislam, hata mimi naunga mkono iwepo lakini, Kadhi asilipwe kutokana na kodi zinazotokana na Matanzania wote yaani wakristu na waislam.

Kuna jamaa humu kasema hata waislam wanalipa kodi,

Ukweli ni kwamba, watanzania wote wanalipa kodi na kodi hiyo huwasaidia wote katika kutekeleza huduma mbalimbali kama barabara, maji, shule, Hospotalini kununua dawa nk.
Huo ujanja wa kutaka kodi za watanzania wote kwa kiasi fulani zilipe viongozi wa dini ambayo haitashughulikia dini zote huoni hapo ni kunyonyana.

Kwa ujumla sisi wote humu JF hatuwezi kuipitisha kwa hizi bra bra, kila mmoja hapa anatoa hisia zake tu wenye uwezo ni wabunge wetu tuliowachagua mwaka huu.

Wito wangu kwa wabunge wetu, kama hili swala likirudi mjengoni, Tunawaomba mtafakari kwa kina KODI isitumike kulipa kadhi ambaye atashughulikia dini moja tu. MAhakama wacha ije lakini KODI wamchangie waumini wa dini hiyo.

Wenye ufahamu tunaomba muweke wazi zaidi, kwani hicho kitabu kitukufu kimesema kadhi alipwe na serikali ambayo haina dini ila inatambua dini za raia wake?

Nawakilisha.
Cassava,

Mimi sijui nani atamlipa kadhi, Lakini kwa mantiki uliyoitumia ya mlipa kodi .Mimi pia sikubaliani ,nisingependa kodi ninayolipa na wengine wengi wanaolipa, kutumia fedha hizo kutoa ruzuku kwa vyama vya siasa, kwani mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa. Lakini nitafanya nini ikiwa serikali imeweka utaratibu wa kutoa ruzuku kwa vyama vya siasa?

Hayo maswali yako yatapata jawabu sahihi kutoka serikalini au kwa vyombo vya waislamu itakapokuwa hiyo issue yao inaingia katika utekelezaji. sasa hivi ni vuta nikuvute tu. Sioni kama limeshatolewa maamuzi.Watakapokubaliana watatujulisha nini wamekubaliana na utekelezaji wake utakuwaje na nani atakuwa mlipia gharama za uendeshaji.
ninachokiona mimi ni kubadilika badilika kwa kauli kutoka kila upande ,sijui usahihi wa kinachojiri au kipi kinapotoshwa.
So let us wait and see how it turns out!
 
kaka nakushukuru sana kwa maelezo mazuri umenifumbua macho kwa hilo, swala ambalo linanitatiza kuhusu hii mahakama ya kadhi ni kwamba, hao kadhi watalipwa na nani? Serikali au michango ya waisilam?

Kama inashughulikia mambo ya waislam tu kwa nini wanataka kadhi alipwe na serikali? Kwa kuwa inataka kushughulikia mambo ya waislam, hata mimi naunga mkono iwepo lakini, kadhi asilipwe kutokana na kodi zinazotokana na matanzania wote yaani wakristu na waislam.

Kuna jamaa humu kasema hata waislam wanalipa kodi,

ukweli ni kwamba, watanzania wote wanalipa kodi na kodi hiyo huwasaidia wote katika kutekeleza huduma mbalimbali kama barabara, maji, shule, hospotalini kununua dawa nk.
Huo ujanja wa kutaka kodi za watanzania wote kwa kiasi fulani zilipe viongozi wa dini ambayo haitashughulikia dini zote huoni hapo ni kunyonyana.

Kwa ujumla sisi wote humu jf hatuwezi kuipitisha kwa hizi bra bra, kila mmoja hapa anatoa hisia zake tu wenye uwezo ni wabunge wetu tuliowachagua mwaka huu.

Wito wangu kwa wabunge wetu, kama hili swala likirudi mjengoni, tunawaomba mtafakari kwa kina kodi isitumike kulipa kadhi ambaye atashughulikia dini moja tu. Mahakama wacha ije lakini kodi wamchangie waumini wa dini hiyo.

Wenye ufahamu tunaomba muweke wazi zaidi, kwani hicho kitabu kitukufu kimesema kadhi alipwe na serikali ambayo haina dini ila inatambua dini za raia wake?

Nawakilisha.

waislamu ni miongoni mwa watanzania wanaolipa kodi hivyo serikali inawajibika kuchangia gharama za uendeshaji wa mahakama za kadhi kama inavyochangia gharama za uendeshaji wa huduma mbali mbali zinazotolewa na makanisa baada ya kusaini memorundum of understanding mwaka 1992.
 
Recipe ya serikali ya mazuzu..hiki ndicho kilichotarajiwa.

Huku inasema haina hela, huku inasema haina dini, huku inasema inashirikiana na kundi fulani la dini ili 'kutekeleza ibada yao'. Nonsensical.

Kwamba haina hela ya kujenga mashule kupata wataalamu wa kesho ambao ndio nguzo ya maendeleo ya kesho, kwamba haina hela ya kununua dawa na kuwakinga wajawazito na wachanga dhidi ya maradhi yanayoepukika, kwamba haina hela ya kujenga walau barabara za vumbi ili wakulima na wafanyabiashara wauze kwa faida...inapeleka bakuli dunia nzima kusema haina hela, lakini inayo hela ya kushughulikia utekelezaji wa ibada za dini fu kikundi fulani..which has nothing to do with maendeleo..this is classic of mazuzu society.

Hii pandora box serkali inayoifungua, inatoa mwanya kwa makundi mbalimbali kuwa na mentality kwamba 'ukiishinikiza serikali mwishoe itakubali matakwa yetu' ..huu ndio mwanzo wa kuigawa jamii...na kila mtu ataanza kueka demands zake, kesho utasikia demands nyingine and so on.

Heko mazuzu wote.
 
TANZANIA BILA MAHAKAMA YA KADHI INAWEZEKANA HATA KAMA RAIS NA MAKAMU WAKE WOTE NI WAISLAMU :llama::llama::llama:

kwani mahakama si zipo kibao kuna tofauti gani kati ya mahakama ya kadhi na mahakama za kawaida[/QUOTE]

Do we really need this crap? Who are gonna be the judges? We are heading fro Sharia, ya'll watch out!
 
Mahakama ya kadhi ni ya waislam na kwaajili ya waislam tu. Sio mahakama ya kusikiliza kesi za wizi wa kuku ila kwa maswala yahusuyo mambo ya ndoa za "kiislam" na mirathi. Hakuna hata sehemu moja itakayomgusa asie muislam.

Natumaini itakuwa hiyo, iwe ni ya kwa waislam tu. Sasa kwa nini serikani inaingilia na inajadili mambo ya dini?
 
Kwani bila hiyo mahakama hayo masuala yanashughulikiwa vipi?[Originally posted by SAFARI NI SAFARI]

Kwa kawaida yangeshughulikiwa na mahakama hizi za kawaida na kwa muda mrefu yamekuwa yakishughulikiwa na mahakama hizihizi za kawaida.Kwa mfano kwa suala la miradhi ili kutambua uwepo wao serikali ilizigawanya sheria katika makundi matatu nayo ni sheria za kimila,sheria za kiislamu na sheria za kiserikali.Katika kutoa hukumu sheria za kiislamu za mirathi zimekuwa zikitumika ikibainika mhusika alikua muislamu na alikuwa anaishi maisha yake kwa kuzingatia sheria za kiislamu.Mimi sijui hawa jamaa wanatafuta nini?nafikiri lengo lao nchi hii iwe ya kiislamu!

Manufaa mojawapo ni ajira kwa mahakimu na majaji watakaoajiriwa na mahakama hiyo. Lakini pia itabidi tuwe na wawakilishi maalumu bungeni kwa ajili ya kupitisha miswaada ya sheria na taratibu zitakazotumiwa na mahakama hii. Mimi nasubiri kwa hamu ianzishwe kwani tutaanzisha madai ya mahakama ya kimila ya kabila letu ambayo itaendeshwa kwa kufuata mila na desturi za kabila letu. Na mahakimu na majaji wa mahakama hii ya kimila lazima wawe wamebobea kwenye mila, desturi na utamaduni wa kabila letu. Kabila jingine haruhusiwi kuingilia mambo yetu tutakayokuwa tukijadili.
 
Mimi ni christian naomba wakristo tuwe na moyo wa uvumilivu kama waislamu.kwa nini nawaita ni wavumilivu,sababu hizi hapa.
Wakristo 1.jumapili ni mapumziko
2.mwaka mpya
3.ijumaa kuu
4.jumatatu ya pasaka
5.chrismas
6.boxing day

waislam 1.ijumaa siku ya kazi.
2.idd zipo 3 kama sijakosea ni mapumziko.
3.mwaka mpya,kimyakimya.
Kama kweli tunataka amani ya kweli tuwape waislamu haki yao.tz hizi dini zipo karibu sawa sasa kama kuna mmoja ataonewa kwa namna yoyote ile nakwambia amani tutaipoteza.naomba wakristo wenzangu msinishambulie kwani hiyo ndiyo njia ya kweli kwani hata biblia inasema hata mtumwa wako tu unatakiwa kumpa haki yake.
Hii nchi hakuna mwenye mamlaka ya kumtawala mwenzake na kama mmoja wetu atajidanganya kulifumbia macho hili ataona matokeo yake.
Waislamu wapewe mahakama ya kadhi na mapumziko siku ya mwaka mpya wa kiislamu na tuwaombe radhi kwa kutuvumilia
hapo ndipo tutakuwa na amani ya kweli na sikukuu zote tutasherehekea kwa pamoja na amani.
Nawasilisha.

Waislam hufuata kitabu cha qurani na katika quran tukufu ni sikukuu mbili tu zilizotamkwa mtanisahihisha kama nimekosea Idd el fitr na idd al hija(adh)

hayajesemwa maylidi wala mwaka mpya kwenye quran kama ni sikukuu kwa waislam sasa sijui tunafuata ipi maana hata Ijumaa yenyewe imetamkwa kuwa baada ya sala basi nendeni mkaendelee na kazi
 
Back
Top Bottom