X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,604
- 1,858
Tatizo huna subra, yaani wewe unachotaka ni kupandisha copy/paste kwa haraka kama upo kwenye mashindano ya F1.Sio miye ni ntandao kaka....weye soma tu uone raha ya hayo mahakhma(siyo mahakama)
Tatizo huna subra, yaani wewe unachotaka ni kupandisha copy/paste kwa haraka kama upo kwenye mashindano ya F1.Sio miye ni ntandao kaka....weye soma tu uone raha ya hayo mahakhma(siyo mahakama)
Hii mahakama isimame kama chombo cha Waislamu kwa sababu ni ya dini, Serikali itafanya makosa makubwa kama kodi ya mtanzania itatumika katika uendeshaji wa mahakama hizi.
Tatizo huna subra, yaani wewe unachotaka ni kupandisha copy/paste kwa haraka kama upo kwenye mashindano ya F1.
Mufti mkuu wa waislamu muadhama sheikh simba ametangaza kuwa mahakama ya kadhi kwa ajili ya waislamu itaanza kazi zake hivi karibuni baada ya serikali kukubali kuirudisha tena mahakama hiyo iliyokuweko enzi za nyuma na pia kuiomba serikali kufanya siku kama ya jana tarehe 7 kuwa siku ya mapumziko kwa kuwa ni mwaka mpya wa waislamu!
Source: Gazeti la mwananchi 08.12.10
kama serikali imekubali mahakama hiyo basi naipongeza kwa uamuzi huo wa busara wa kuwapa waislamu kile wanachotaka kwa mujibu wa sheria na kusisitiza hoja ya mufti kufanywa siku ya mapumziko kwa kuingia mwaka mpya wa kiislamu kwa sababu hata dini zingine huwa wanamapumziko siku za mwaka mpya wa tarehe 1.1 kila mwaka hivyo waislamu nao wana haki ya kusherehekea mwaka wao mpya na ifanywe kuwa ni siku ya holliday!!
Kwani waislamu hawalipi kodi? Acheni unazi wenu huo dunia inabidilika wakubwa!!!
Mimi ni christian naomba wakristo tuwe na moyo wa uvumilivu kama waislamu.kwa nini nawaita ni wavumilivu,sababu hizi hapa.
Wakristo 1.jumapili ni mapumziko
2.mwaka mpya
3.ijumaa kuu
4.jumatatu ya pasaka
5.chrismas
6.boxing day
waislam 1.ijumaa siku ya kazi.
2.idd zipo 3 kama sijakosea ni mapumziko.
3.mwaka mpya,kimyakimya.
Kama kweli tunataka amani ya kweli tuwape waislamu haki yao.tz hizi dini zipo karibu sawa sasa kama kuna mmoja ataonewa kwa namna yoyote ile nakwambia amani tutaipoteza.naomba wakristo wenzangu msinishambulie kwani hiyo ndiyo njia ya kweli kwani hata biblia inasema hata mtumwa wako tu unatakiwa kumpa haki yake.
Hii nchi hakuna mwenye mamlaka ya kumtawala mwenzake na kama mmoja wetu atajidanganya kulifumbia macho hili ataona matokeo yake.
Waislamu wapewe mahakama ya kadhi na mapumziko siku ya mwaka mpya wa kiislamu na tuwaombe radhi kwa kutuvumilia
hapo ndipo tutakuwa na amani ya kweli na sikukuu zote tutasherehekea kwa pamoja na amani.
Nawasilisha.
Umesikia wapi!? Wakati mwingine kabla ya kuchangia muwe mnasoma wachangiaji wengine wameandika nini, na sio kukurupuka tu.
Rev Masanilo,
Tunajenga hofu isiyo na msingi katika hili.
Nimechangia hapo juu kuwa lazima tuelewe tofauti baina ya mahakama ya kadhi katika nchi kama yetu, ambayo inaongozwa kwa "common laws", secular laws, na penal code inaongozwa na kuzingatia sheria hizo na mahakama katika nchi za Iran, Saudi Arabia ambazo zinaendesha kesi zao kwa kutumia "sharia"(islamic laws)
Mahakama ya kadhi haitowi hukumu kama mahakama ya Kisutu, zaidi ipo kushughulikia mizozo na suluhu ya ndoa zilizofungwa kiislamu na inaposhindikana kuelekeza jinsi ya utoaji wa talaka, pia kutoa maelekezo kwa waislamu wanaotaka kurithi kiislamu.
Uwepo wa mahakama hii unaongeza option ya pili kwa watu ambao wote ni waislamu kushughulilia, kutatua tofauti zao katika hizo areas mbili; mambo ya ndoa na urithi, kupitia mahakama hii si zaidi ya hapo.
Mambo mengine yote, including haya mawili wanaweza kuyapeleka katika mahakama za kawaida. Ieleweke hapa kuwa ni lazima wote wanaohusika na mgogoro au shauri linalokwenda mahakama ya kadhi ni lazima wawe waislamu na wawe wamekubaliana kwenda huko.
Mahakama ya kadhi haina mamlaka ya kutoa hukumu ya mtu kufungwa gerezani au kuteswa au kukatwa kichwa, mguu, mkono au sikio. Si sehemu ya kushitakiana na kutafuta hukumu. Inafanya kazi zaidi kama advisory body katika hizo areas mbili. wala si kuwa muislamu atalazimishwa lazima aendeke huko ni chaguo lake.
kwa hiyo, vilema hawataongezeka kwa kuanzishwa mahakama hii.
Nafikiri wazo lako la kuanzishwa wizara ya walemavu ni zuri though kwani hizo ajali za barabarani zinatupatia walemavu wengi.
siku njema Mkuu,
amani ya bwana iwe nawe!
Subiri na omba ifunguliwe na ianze kufanya kazi halafu uniulize ulisikia wapi!!! Hp tutapishana brbrn siku moja ukiwa unavuja damu mkono umetoka kukatwa...
U mean kusoma kabla ya kuchangia ili nichangie same opinion au? Basi itakuwa wastage of energy and time!!
Hivi mmesahau enzi za mzee Ruksa? Sikukuu ilikuwa ikiangukia weekend, tunalipa siku ya kazi. Kweli viongozi waislamu safi sanaaa. kwikwiwkiiii:whoo:Xpaster I always admire you, in most cases your wrong. Nadhani tunazungumzia mwaka mpya
Tutakuwa na sikukuu nyingi kitaifa, heko Muadhama sheikh Simba. Kumbuka wenzenu wanafikiria kuanzisha mabenki nyie mnang'ang'ana na mahakama ya kadhi na kuwa na siku nyingi za kupumzika.
Nazidi kuwapongeza mmeliona hilo kwa maendeleo
Mbona kodi za waTanzania kwa miaka mingi tu zimeendesha mashule ya kikatoliki?
Mufti mkuu wa waislamu muadhama sheikh simba ametangaza kuwa mahakama ya kadhi kwa ajili ya waislamu itaanza kazi zake hivi karibuni baada ya serikali kukubali kuirudisha tena mahakama hiyo iliyokuweko enzi za nyuma na pia kuiomba serikali kufanya siku kama ya jana tarehe 7 kuwa siku ya mapumziko kwa kuwa ni mwaka mpya wa waislamu!
Source: Gazeti la mwananchi 08.12.10
kama serikali imekubali mahakama hiyo basi naipongeza kwa uamuzi huo wa busara wa kuwapa waislamu kile wanachotaka kwa mujibu wa sheria na kusisitiza hoja ya mufti kufanywa siku ya mapumziko kwa kuingia mwaka mpya wa kiislamu kwa sababu hata dini zingine huwa wanamapumziko siku za mwaka mpya wa tarehe 1.1 kila mwaka hivyo waislamu nao wana haki ya kusherehekea mwaka wao mpya na ifanywe kuwa ni siku ya holliday!!
X-Paster umesimama kwenye misingi ya kidini nimekufurahia, si Kama Muadhama Sheikh Simba yuko kisiasa zaidi. Nimekubaliana na mchango wako.
Nonda, asante nimejifunza kitu pia kwenye mchango wako.
Lakini tubadili kwanza katiba yetu kukidhi haja ya kuwa na mahakama ya kadhi. Pia Mahakama kuu iwe na uwezo wa kupindua maauzi ya mahakama ya Kadhi
Ni jambo zuri kuwa na uhuru wa dini, ila tu kwa kuwa jamii yetu inadini nyingi basi kila dini ifanye shughuli zake bila kuathiri shughuli za dini nyingine na taifa kwa ujumla. Sikukuu za kidini zipo tayari kwenye kalenda za serikali, na mengine dini zenyewe zijipange zenyewe.Mimi ni kafiri,nailipa kodi serikali yangu,vyanzo vyangu vya mapato ni kama ufugaji na uuzaji wa nyama ya nguruwe,nalipwa riba na mabenki mbalimbali ambapo nakatwa kodi kwa kipato hiki,pia natengeneza na kuuza pombe za kienyeji ambazo pia hutozwa kodi.Mahakama ya kadhi ianzishwe,lakini sitarajii kadhi awe analipwa mshahara kwa kutumia fedha za mimi kafiri.Naamini serikali yangu ni secular government(is not bias in favour of any religion),hivyo sitarajii ijiingize kwenye mambo ya kidini,ikifanya hivyo itakuwa ni kichekesho na itakuwa ni serikali ya kiislamu na itapaswa kuondoka au kuondolewa madarakani mara moja.Mimi ni mfia dini na nipo teyari kufa kwa ajiri ya kutetea dini yangu.
TANZANIA BILA MAHAKAMA YA KADHI INAWEZEKANA HATA KAMA RAIS NA MAKAMU WAKE WOTE NI WAISLAMU :llama::llama::llama:
Kodi ya watanzania imeendesha shule za wakatoriki ambazo hata waislam wamesoma pia. Fikiri kabla ya kuandika!
kwa mara ya kwanza mchungaji umepotoka.
hawa jamaa huwa wanamsururu wa ajenda katika harakati zao za kutaka kuitawala dunia.
hiyo ishu ya kadhi na takataka zake ni moja tu katika mamilioni ya hoja zao.
subiri uone.
wakiruhusiwa kuendesha mahakama ya kadhi lazima wataibua madai mengine mapya.
yakumbukwe maneno yangu hata nijapo kufa.
hoja ni kuzuia kabisa harakati za waislamu wenye msimamo mkali Tanzania
mambo ya kadhi, sijui nini peleka huko kwenye banda la nguruwe. tupa huko!!!!