Mahakama ya kadhi hii hapa!

Hahahaah usianze kuchukia tunajadilia ndugu yangu, hata haya mazungumzo ya kwenye mtandao si lazima yafanyiwe kazi.
Kuna sehemu nimeonyesha kuchukia!? hayo ni mawazo yako tu, huwa sina kuchukia kujadiliana na mtu yoyote yule katika maisha yangu, na haswa humu ndani ya JF.
 
Naona umuhimu wa katiba ya sasa kufanyiwa marekebisho makubwa, ili hii mahakama ya kadhi ya ndugu zetu iweze kuingizwa bila kuvunja katiba. Ningependa pia kuona mahakama kuu inakuwa na uwezo wa kupindua maamuzi ya mahakama ya kadhi pale inapoonekana kuna uamuzi wa mangumuyu.

Katiba mpya tunaitaka sasa kuliko wakati wowote!
 
Acha ujinga huo wewe nani kakuambia waislamu wanataka fedha za makafiri na wakristo? Ila tatizo ni kwamba mmeweka katika vichwa venu wakristo pekee ndio walipa kodi endelee kuota tu. Tanzania walipa kodi ni waislamu na wakristo na kama kutahitajika pesa ya kuiendesha itatokea katika fungu la kodi za waislamu. Wewe na kodizako za nguruwe endeleeni na ujinga wenu. Kujitegemee hakumaanishi nguvu ya kisheria sisi tunataka mahakama ya kadhi iwe na nguvu ya kisheria basi. Kuhusu kuendeshwa itaendeshwa tu but msifikiri hii serikali ni ya wakristo peke yenu tuondolee ujinga wako hapa!!

Watch your language!
 
Sitaki tufike mbali, najua mahakama ya kadhi ina mambo mazuri pia kiimani ya kiislam kama mirathi, haki za wanawake, Talaka na Ndoa etc....lakini je mumejiandaa vizuri, wale watakao misinterpret sharia huoni kutakuwa na ukiukwaji wa haki za binadamu? Hii Kitu ipo kwenye katiba?

soma hapa

Somali Islamists Chop Off Thieves' Hands as Sharia Law Takes Hold

Somali Islamists Chop Off Thieves' Hands as Sharia Law Takes Hold

Misinterpretation na misconception inatokana na upeo wa kielimu walionao baadhi ya wanasheria kuhusiana na shariah law. La msingi ni watu kujifunza na kuteua jopo la majaji wenye kujua hili basi.
 
Wrong again hebu soma hapa pole pole post ya mtani wangu Kadogoo

Soma maandishi hayo mekundu! Usijifanye hutaki kuelewa, asante sana

Kuhusu kalenda soma hapa

Julian calendar - Wikipedia, the free encyclopedia
Masanilo, Ngoja nikupe faida moja kuhusiana na sikukuu za Kiislam:

Waislam tuna sikukuu mbili tu kwa mwaka mzima, nazo ni Eid Al-Fitr, sikuu hii usheherekewa baada ya Sisi Waislam kumaliza mfungo wa Ramadhani, ambao ni mwezi wa tisa katika kalenda ya Kiislam (Hijria) na sikukuu nyingine ya pili na ya mwisho ni sikukuu ya Eid Al-Adha. Ambayo tunasheherekea baada ya mahujaji kumaliza Hijja...! Zaidi ya hapo Waislam hawana tena sikukuu nyingine.

Waislam hatuitaji sikukuu nyingine zaidi ya hizo mbili hapo juu!
 
Watch your language!

Mkuu mtu mjinga ni mtu anayezungumza vitu without making any sense at all sijamtukana mtu. Ningelimuita mpumbavu nadhani ningelikuwa nimemtusi but mjinga sijamkosea. Ila nakushukuru mkuu kwa kuliona hilo.
 
Mufti mkuu wa waislamu muadhama sheikh simba ametangaza kuwa mahakama ya kadhi kwa ajili ya waislamu itaanza kazi zake hivi karibuni baada ya serikali kukubali kuirudisha tena mahakama hiyo iliyokuweko enzi za nyuma na pia kuiomba serikali kufanya siku kama ya jana tarehe 7 kuwa siku ya mapumziko kwa kuwa ni mwaka mpya wa waislamu!
Source: Gazeti la mwananchi 08.12.10

kama serikali imekubali mahakama hiyo basi naipongeza kwa uamuzi huo wa busara wa kuwapa waislamu kile wanachotaka kwa mujibu wa sheria na kusisitiza hoja ya mufti kufanywa siku ya mapumziko kwa kuingia mwaka mpya wa kiislamu kwa sababu hata dini zingine huwa wanamapumziko siku za mwaka mpya wa tarehe 1.1 kila mwaka hivyo waislamu nao wana haki ya kusherehekea mwaka wao mpya na ifanywe kuwa ni siku ya holliday!!

Mbona kwenye ilani ya CCM iliondolewa? au ndio Udini anausema JK
 
Mimi ni christian naomba wakristo tuwe na moyo wa uvumilivu kama waislamu.kwa nini nawaita ni wavumilivu,sababu hizi hapa.
Wakristo 1.jumapili ni mapumziko
2.mwaka mpya
3.ijumaa kuu
4.jumatatu ya pasaka
5.chrismas
6.boxing day

waislam 1.ijumaa siku ya kazi.
2.idd zipo 3 kama sijakosea ni mapumziko.
3.mwaka mpya,kimyakimya.
Kama kweli tunataka amani ya kweli tuwape waislamu haki yao.tz hizi dini zipo karibu sawa sasa kama kuna mmoja ataonewa kwa namna yoyote ile nakwambia amani tutaipoteza.naomba wakristo wenzangu msinishambulie kwani hiyo ndiyo njia ya kweli kwani hata biblia inasema hata mtumwa wako tu unatakiwa kumpa haki yake.
Hii nchi hakuna mwenye mamlaka ya kumtawala mwenzake na kama mmoja wetu atajidanganya kulifumbia macho hili ataona matokeo yake.
Waislamu wapewe mahakama ya kadhi na mapumziko siku ya mwaka mpya wa kiislamu na tuwaombe radhi kwa kutuvumilia
hapo ndipo tutakuwa na amani ya kweli na sikukuu zote tutasherehekea kwa pamoja na amani.
Nawasilisha.

Nakubaliana nawewe kwa asilimia 100%. Vilevile tusiwasahau ndugu zetu wahindu. maana na wao pia ni raia wa tanzania, wana haki ya kuheshimiwa na kutambuliwa utu, imani na itikadi yao. Na hata waislamu tutenganishe sherehe za shia, sun, ahmadiya, kadiria, kadian, sufian. Wote hawa sherehe zao na siku zao za kupumzika tuzitambue. Na ndugu zetu wasabato wanasherehe zao za makambi ama sikukuu ya vibanda. Ni vyema tuwatambue hawa na kupumzika kwa wiki mbili. Siku hizi wachina wameanza kuomba uraia wa tanzania. Chinese new year ni tofauti ya hii tunayoifuata. Inabidi tuwatambue vilevile. Yangu ni hayo tu.
 
Misinterpretation na misconception inatokana na upeo wa kielimu walionao baadhi ya wanasheria kuhusiana na shariah law. La msingi ni watu kujifunza na kuteua jopo la majaji wenye kujua hili basi.

Niko pamoja na wewe kwa hili, theres is no need of rushing at all maandalizi yanatakiwa wakati huo huo tunarekebisha katiba yetu kuweza kuingiza hii Mahakama ya Kadhi.
 
Ok, kana sherehe fulani za wasabato huwa zinachukua wiki mzima na zinafanyika kwa kanda, kwahiyo ni mwezi mzima mapumziko, sijawahi wasikia wakilalamika kwani wanajua mambo ya kale hayana nafasi katika kaisha ya sasa
 
Masanilo, Ngoja nikupe faida moja kuhusiana na sikukuu za Kiislam:

Waislam tuna sikukuu mbili tu kwa mwaka mzima, nazo ni Eid Al-Fitr, sikuu hii usheherekewa baada ya Sisi Waislam kumaliza mfungo wa Ramadhani, ambao ni mwezi wa tisa katika kalenda ya Kiislam (Hijria) na sikukuu nyingine ya pili na ya mwisho ni sikukuu ya Eid Al-Adha. Ambayo tunasheherekea baada ya mahujaji kumaliza Hijja...! Zaidi ya hapo Waislam hawana tena sikukuu nyingine.

Waislam hatuitaji sikukuu nyingine zaidi ya hizo mbili hapo juu!

Tusiende kwenye Imani tutaacha hoja ya msingi. Nakubaliana na wewe ila hapo mwisho umecontradict kila kitu.

Mufti Muadhama Sheikh Simba amesema
pia kuiomba serikali kufanya siku kama ya jana tarehe 7 kuwa siku ya mapumziko kwa kuwa ni mwaka mpya wa waislamu!
 
Nakubaliana nawewe kwa asilimia 100%. Vilevile tusiwasahau ndugu zetu wahindu. maana na wao pia ni raia wa tanzania, wana haki ya kuheshimiwa na kutambuliwa utu, imani na itikadi yao. Na hata waislamu tutenganishe sherehe za shia, sun, ahmadiya, kadiria, kadian, sufian. Wote hawa sherehe zao na siku zao za kupumzika tuzitambue. Na ndugu zetu wasabato wanasherehe zao za makambi ama sikukuu ya vibanda. Ni vyema tuwatambue hawa na kupumzika kwa wiki mbili. Siku hizi wachina wameanza kuomba uraia wa tanzania. Chinese new year ni tofauti ya hii tunayoifuata. Inabidi tuwatambue vilevile. Yangu ni hayo tu.

ndio maana JK (Orijino sio photocopy) serikali haina dini, ila watu wana dini zao
 
Mimi ni christian naomba wakristo tuwe na moyo wa uvumilivu kama waislamu.kwa nini nawaita ni wavumilivu,sababu hizi hapa.
Wakristo 1.jumapili ni mapumziko
2.mwaka mpya
3.ijumaa kuu
4.jumatatu ya pasaka
5.chrismas
6.boxing day

Hivi mwaka mpya ni siku wa wakristo?
Na boxing day wanasherehekea kitu gani vile??
 
Mufti mkuu wa waislamu muadhama sheikh simba ametangaza kuwa mahakama ya kadhi kwa ajili ya waislamu itaanza kazi zake hivi karibuni baada ya serikali kukubali kuirudisha tena mahakama hiyo iliyokuweko enzi za nyuma na pia kuiomba serikali kufanya siku kama ya jana tarehe 7 kuwa siku ya mapumziko kwa kuwa ni mwaka mpya wa waislamu!
Source: Gazeti la mwananchi 08.12.10

kama serikali imekubali mahakama hiyo basi naipongeza kwa uamuzi huo wa busara wa kuwapa waislamu kile wanachotaka kwa mujibu wa sheria na kusisitiza hoja ya mufti kufanywa siku ya mapumziko kwa kuingia mwaka mpya wa kiislamu kwa sababu hata dini zingine huwa wanamapumziko siku za mwaka mpya wa tarehe 1.1 kila mwaka hivyo waislamu nao wana haki ya kusherehekea mwaka wao mpya na ifanywe kuwa ni siku ya holliday!!

wekeni mfano wa nchi zinazopunzika duniani!
 
Na sie akina mwanamalundi wapagani tusiofuata dini zenye ustaarabu za nchi za magharibi na mashariki, tunaomba mtutambue siku zetu za kupumzika. Maana wote sie ni raia wa tanzania na nchi hii tumepewa na mwenyezi mungu. Msitubague, maana mungu mwenyewe hajatubagua ndio maana tumechanganyikana na wastaarabu wanaomini dini za kimagaribi na kiarabu. asanteni.
 
hapa km kila mmoja akija na mwaka wake tz tutakuwa na miaka mingapi ndani ya mwaka mmoja?......kudadadeki..........

NIKIKUMBUKA KWA HARAHA NI KUWA WATZ TUMEKATAA KUTULETEA UOZO HUU WA MAHAKAMA YA KADHI SASA SIJUI NI KWA IDHINI YA NANI?

Tusiende kwenye Imani tutaacha hoja ya msingi. Nakubaliana na wewe ila hapo mwisho umecontradict kila kitu.

Mufti Muadhama Sheikh Simba amesema
 
Masanilo, Ngoja nikupe faida moja kuhusiana na sikukuu za Kiislam:

Waislam tuna sikukuu mbili tu kwa mwaka mzima, nazo ni Eid Al-Fitr, sikuu hii usheherekewa baada ya Sisi Waislam kumaliza mfungo wa Ramadhani, ambao ni mwezi wa tisa katika kalenda ya Kiislam (Hijria) na sikukuu nyingine ya pili na ya mwisho ni sikukuu ya Eid Al-Adha. Ambayo tunasheherekea baada ya mahujaji kumaliza Hijja...! Zaidi ya hapo Waislam hawana tena sikukuu nyingine.

Waislam hatuitaji sikukuu nyingine zaidi ya hizo mbili hapo juu!

Nadhani huwa zipo sikukuu kadhaa ambazo zinaitwa maulidi (maana yake siijui) in addition to those you have mentioned.
 
Yote maisha tu. After all mahakama inawahusu waumini ambao kwa hali ya Kibongo, ni wazi kuwa wengi sana watakuwa na mkono mmoja maana kwa kupenda kwao ********** watahukumiwa sana. Tujiandae kupata walemavu wengi zaidi.:embarrassed:


Ndugu yangu Mzalendo umenichekesha sana mpaka nikasahau tabu zangu kwa muda

manahakama ya kazi haitakuwepo kwa ajili ya kukata watu mikono hata serekali isingeweza kuruhusu jambo hili unadhani serekali hawana ufahamu mpaka waruhusu jambo hili.

Lengo kuu la mahakama ya kazi ni kuto suluhisho la mambo yanayoizunguka jamii yetu kwa kufuata misingi ya kiisilamu hasa migogoro ya ndoa, mirathi n.k ili kuleta jamii yenye utulivu, amani na kuheshimiana.

swala la kuhukumu wezi litabaki kuwa la mahakama zetu za kawaida, so hakuna kukatwa mikono ndugu yangu.
 
Back
Top Bottom