Magufuli bila madaraka yukoje?

Kwa mfano kama ni kweli Magufuli alitaka Jengo la TANESCO-UBUNGO libomolewe, ilibidi afikirie kua lile jengo limejengwa kwa pesa yetu na ujenzi uliidhinishwa na Mawaziri husika walikokuwepo kabla yake Magufuli kwenye wizara hiyo. Likibomolewa leo, kesho kuna uwezekano atakuja waziri mwingine anayembadili Magufuli na akaidhinisha ujenzi tena katika sehemu hiyo - sasa utaona kua sisi ndio tunaliwa tokana na maamuzi ya kibabe toka kwa hao mawaziri wa CCM.

Magufuli angetufaa sana kama angesimamia na kuwakaba walioidhinisha ujenzi wa hilo jengo. Pia atatufaa kama atadhibiti ujenzi holela unaoendelea kukua na hapo hapo kupigania raia kupata viwanja vilivyopimwa haraka - bomoa bomoa is too easy kumpa sifa Magufuli. Vilivyofanywa kwa makosa na wenzake kabla yake, basi na waadhibiwe kwanza ili makosa yasirudiwe.

Kimsingi Magufuli si kiongozi mzuri, anafanya mambo kama kuruta - utafikiri amekatazwa kufikiri. Ni kweli tunaweweza kumlaumu magufuli kwa kutaka kubomoa jengo la TANESCO kwa kigezo cha kula hasara walipa kodi wa tanzania. Sasa tujiulize ni kifanyike ili barabara iweze kutanuliwa?
 
Kuhusu swali lako, si Waberoya, hata mimi pia nimeliona, lakini tutakuwa tuna deal na hoja ambayo ni tricky sana kiasi kwamba uwezekano ni mkubwa kuishia kujadili mhusika zaidi kuliko swali la utawala na uwajibikaji. Hata hivyo, sio lazima kila mara njia ya kuwajibika kwa kujiuzulu ndio the only option, kuna njia zingine za ku-adjust situation na kusonga mbele.

SN, unafikiri Magufuli anaweza kusema bado anayo imani ya Rais na Waziri wake Mkuu? Mimi ninaamini kuwa kitakachoendelea sasa siyo "kuadjust situation na kusonga mbele" bali itakuwa ni "kucompromise on a principle". Nyerere alisema vizuri "ukivunja kanuni katika jambo dogo, kanuni itakuvunja katika jambo kubwa".
 
SN, unafikiri Magufuli anaweza kusema bado anayo imani ya Rais na Waziri wake Mkuu? Mimi ninaamini kuwa kitakachoendelea sasa siyo "kuadjust situation na kusonga mbele" bali itakuwa ni "kucompromise on a principle". Nyerere alisema vizuri "ukivunja kanuni katika jambo dogo, kanuni itakuvunja katika jambo kubwa".

Yes nimekuelewa sana japo maada yako ni ngumu sana na kama tutatumia chekeche hili kuwakaanga CCM, masafi ya mtume! hapiti mtu!...usiseme wapinzani , ndio kabisa!

Mkuu unajua tumbo na principle haviendani! unajua ukiwa na njaa sana unaweza kusahau kunawa mikono?

Yes Magufuli he is compromising with the situation because he dont have options/alternative n.k, njaa mbaya na ukiingia kwenye siasa LENGO lao ni hilo kula kwanza mengine baadaye.

I think we need rich leaders, I mean they have to prove they are rich before being leaders !!!! sound strange??

Rafiki yangu mmoja alisema tunapowachagua viongozi na kuwa -install lets ask them HOW MUCH THEY NEED BEFORE commencing their jobs! mfano lets say JK kabla ya kuanza kazi tungempa sh. bilioni 100! ili afanye kazi nyingi na kwa uhakika, maana yeye kujiingiza kwenye dubius deals lime-cost taifa trillions, wakati tunge-save kwa kumpatia yeye bilioni 100, achilia mbali mshahara wake, then same to mawaziri, wakurugenz n.ki!! nilikaa kimya na kutafakari...kidogo ...

If we will reach stage that politics is not a platform to earn money but is a chance to show how one human can increase value of life to other people then we are 'THERE'! kwa sasa bado, are we??
 
Yes nimekuelewa sana japo maada yako ni ngumu sana na kama tutatumia chekeche hili kuwakaanga CCM, masafi ya mtume! hapiti mtu!...usiseme wapinzani , ndio kabisa!

Mkuu unajua tumbo na principle haviendani! unajua ukiwa na njaa sana unaweza kusahau kunawa mikono?

aisee nimeipenda hiyo thanks! - kunawa mikono is the principle..

Yes Magufuli he is compromising with the situation because he dont have options/alternative n.k, njaa mbaya na ukiingia kwenye siasa LENGO lao ni hilo kula kwanza mengine baadaye.

I think we need rich leaders, I mean they have to prove they are rich before being leaders !!!! sound strange??

Lakini tunao hao tayari; lakini swali ambalo ni gumu lini mtu tajiri aliacha kutaka kuwa tajiri zaidi? Yaani alisema "imetosha"?

Rafiki yangu mmoja alisema tunapowachagua viongozi na kuwa -install lets ask them HOW MUCH THEY NEED BEFORE commencing their jobs! mfano lets say JK kabla ya kuanza kazi tungempa sh. bilioni 100! ili afanye kazi nyingi na kwa uhakika, maana yeye kujiingiza kwenye dubius deals lime-cost taifa trillions, wakati tunge-save kwa kumpatia yeye bilioni 100, achilia mbali mshahara wake, then same to mawaziri, wakurugenz n.ki!! nilikaa kimya na kutafakari...kidogo ...

Ni wazo la kufikiria ni jinsi gani ukimpa hizo fedha hatozitumia vibaya halafu akatafuta mahali pa kupata zaidi?

If we will reach stage that politics is not a platform to earn money but is a chance to show how one human can increase value of life to other people then we are 'THERE'! kwa sasa bado, are we??

Ndio maana pamoja na yote wanayomsema Nyerere nadhani anabakia an enigma - najiuliza kuwa kwanini muda wote ule hakutaka kutumia nafasi yake kama kina Mobutu na wenzao? Nadhani tungekuwa na Rais tajiri sana na sasa.. Sijui alikuwa na kitu gani kinamzuia kutumia nafasi yake ile kujijengea mavila ya kupumzikia huko Zanzibar na ndege za kumpeleka kunywa Chai Dodoma. Maana siku hizi kuna ndege huwa zinaondoka JNIA usiku kwenda baadhi ya sehemu ambazo Watanzania wangejua - ingekuwa ni vurugu ya mwaka.
 
aisee nimeipenda hiyo thanks! - kunawa mikono is the principle..



Lakini tunao hao tayari; lakini swali ambalo ni gumu lini mtu tajiri aliacha kutaka kuwa tajiri zaidi? Yaani alisema "imetosha"?



Ni wazo la kufikiria ni jinsi gani ukimpa hizo fedha hatozitumia vibaya halafu akatafuta mahali pa kupata zaidi?



Ndio maana pamoja na yote wanayomsema Nyerere nadhani anabakia an enigma - najiuliza kuwa kwanini muda wote ule hakutaka kutumia nafasi yake kama kina Mobutu na wenzao? Nadhani tungekuwa na Rais tajiri sana na sasa.. Sijui alikuwa na kitu gani kinamzuia kutumia nafasi yake ile kujijengea mavila ya kupumzikia huko Zanzibar na ndege za kumpeleka kunywa Chai Dodoma. Maana siku hizi kuna ndege huwa zinaondoka JNIA usiku kwenda baadhi ya sehemu ambazo Watanzania wangejua - ingekuwa ni vurugu ya mwaka.

Ha ha haa! watoto wa Nyerere utawajua tu!

MKJJ Nyerere alikuwa special he was not just a man, he was superman!, and visionary he had his own ideas , TATIZO ni waliobeba gari la Tanzania baada ya Nyerere! inakuwa kama dereva wa bajaj unampa treni! au tax driver asiyejua kurusha ndege unampa Boeing 737 (tuishie hapo!)

Ni kweli hata kama ukitaka kuwapa fedha nyingi hawataridhika na watatumia vibaya sana, because it is 'free money'! ni kama fedha za urithi.

The question is what can we do? do we have leaders wenye character kama Nyerere? where things went wrong , why we are where we are? what should be done...unajua bila kurudi kwenye foundations , tumekwisha, who will take us back there? to be honest I dont see!! labda mtu anipe moyo!
 
Kumtetea asijiuzuru ni uvivu wa kufikiri.Katika hali kama hiyo mwenye akili sawasawa lazima angejiuzuru.Nakubaliana na msemaji mmoja hapo juu uongozi kwa ccm sio utumishi ni ajira.Akijizuru atakula nini?Atapata wapi tena ajira yenye mafao ya muda mfupi lakini ni manono?
 
Kimsingi sheria na kanunu zimemwongezea ujasiri akiwa kiongozi, la sivyo hana tofauti na wabunge wengine so called man or woman of yes's
 
Yes nimekuelewa sana japo maada yako ni ngumu sana na kama tutatumia chekeche hili kuwakaanga CCM, masafi ya mtume! hapiti mtu!...usiseme wapinzani , ndio kabisa!

Mkuu unajua tumbo na principle haviendani! unajua ukiwa na njaa sana unaweza kusahau kunawa mikono?

Yes Magufuli he is compromising with the situation because he dont have options/alternative n.k, njaa mbaya na ukiingia kwenye siasa LENGO lao ni hilo kula kwanza mengine baadaye.

I think we need rich leaders, I mean they have to prove they are rich before being leaders !!!! sound strange??

Rafiki yangu mmoja alisema tunapowachagua viongozi na kuwa -install lets ask them HOW MUCH THEY NEED BEFORE commencing their jobs! mfano lets say JK kabla ya kuanza kazi tungempa sh. bilioni 100! ili afanye kazi nyingi na kwa uhakika, maana yeye kujiingiza kwenye dubius deals lime-cost taifa trillions, wakati tunge-save kwa kumpatia yeye bilioni 100, achilia mbali mshahara wake, then same to mawaziri, wakurugenz n.ki!! nilikaa kimya na kutafakari...kidogo ...

If we will reach stage that politics is not a platform to earn money but is a chance to show how one human can increase value of life to other people then we are 'THERE'! kwa sasa bado, are we??

Priciple ya tumbo inaweza kutofautiana ktk levels zake. Sidhani principle hiyo inaaply ktk kiwango cha Magufuri, yeye anaweza asiwe na njaa kama ya kwangu, na pia njaa yangu haiwezi kufikia kiwango cha Somalia na Ethiopia. Njaa yangu ina nafasi ya kumhurumia mtu na kumsaidia, lakini njaa ya kiwango kilichowahi kutokea Ethiopia haiwezi kuwa na huruma hata kama mtu anakaribia kufa. Kwahiyo kama Magufuri ana njaa sidhani itakuwa katika kiwango cha kumzuia kuchukua hatua katika mazingira kama aliyopo sasa hivi. Nionavyo mimi kuna principle nyingine inayoweza kuapply hapa.

Kila mtu ana aspirations zake, kupata pesa za kutosha (sifahamu ni pesa kiasi gani ni kiwango cha pesa ya kutosha?), then kupata madaraka na utukufu. Principle hii ina cut across kwa kila mtu, kuanzia mimi, wewe hadi yeye. Hata hizi kelele za kujadili watu zinaweza kuwa zinasababishwa na principle hii.

Ukiangalia vizuri kabisa, viongozi wengi sio effective katika majukumu yao, lakini hawajadiliwi na mtu yeyote. Kosa ni pale mtu anapoonesha dalili za kupata sifa au kutaka madaraka, hapo discussion zinaanza. Hata wale wasio na uwezo kabisa wataibuka na kutoa criticism zao. Pengine hii ni kanuni ya kibinadamu...

Kuhusu kuwa na viongozi matajiri (need of rich leaders) kama suluhisho la tatizo la ulaji au ufisadi, sidhani kama hilo ni tiba sahihi. Wengi tunaweza kukubaliana kuwa Nyerere alianza uongozi akiwa maskini na amestaafu akiwa hivyohivyo, lakini amefanya mambo makubwa sana kwa nchi yetu na nchi zingine. Je Lowasa akiwa rais atakuwa mwadilifu kama Nyerere? Mimi sijui! Je Kikwete amejikusanyia utajiri mwingi kwake na kwa mwanaye, je sasa ataweza kuonesha uzalendo zaidi ya Nyerere? Pia hapo sijui. Kitu kikubwa tunachohitaji kwa viongozi wetu ni dhamira ya mtu kuweza kujikana nafsi. Pamoja na ukweli kwamba kujikana nafsi ni jambo gumu kwa watu wengi maskini na tajiri, lakini ni jambo muhimu. Kujikana nafsi ndio sifa kubwa ya uongozi. Kwa upande mwingine sifaya kujikana nafsi ndio sababu ya viongozi wazuri duniani kuwa wachache. Watu wengi wanapenda kutumia madaraka kama nafasi ya kustarehe na kujifurahisha. Utakuta kiongozi aliyezunguka kila sehemu akiomba kura na akishapewa anaishia kwenda kubembea na kutalii kwenye vivutio vya starehe huku akisahau umaskini na shida za watu waliompa kura. Hili ni tatizo kubwa sana na dawa yake mimi siifahamu.
 
Kinachonifurahisha kwa masikitiko ni pale unapokuta waliomkoromea magufuli wanajulikana kwa kukosa meno na nguvu kiasi cha kuwa bendera ambayo hutikiswa hata na pumzi badala ya upepo! Mifano ipo mingi hasa kwenye epa,meremeta, kagoda, na hivi karibuni tuzo ya dowans ambapo tumewashuhudia watawala wakubwa kabisa wakigeuka kuwa bendera.
 
Pamoja na mapungufu yake ambayo kila binadamu ana yake, Magufuli anaweza kusimamia kitu na kikaenda, the guy delivers, analeta uwajibikaji pale anapokuwa, Tanzania tuna tatizo kubwa sana hapa, viongozi wengi sio wa kudeliver, much less kwa caliber ya Magufuli! Tena ukitilia maanani anatoka kwenye chama cha magamba! Anajitahidi sana kwa kweli!
 
Haya sasa...huyo naye ni Fisadi!hahaha
 

Attachments

  • magufuli.jpg
    magufuli.jpg
    120.7 KB · Views: 35
Mkuu magufuli bila madaraka yukoje:

Magufuli ni aina ya watu ambao wanaweza kutumwa tu period; yaani unamuwekea job description; time na unampa fedha na mamlaka anapasua mlima no doubt about that..

Magufuli hawezi kuwa mbunifu, hawezi kuwa kiongozi (leader) kwasababu sidhani kama kuna kitu anakiamini na kusimama nacho kama tabia au msimamo wake..

Msimamo wake ni utekelezaji wa majukumu aliyopewa; mimi nilishanga sana JK kumpa Pinda bada JPM nafasi ya U-PM
 
Ndugu MM, topic yako hii, inaweza kukuweka mahali pabaya hata wewe, kwa sababu inaonekana kama kumjadili mtu. Tukumbuke kuwa simple minds discuss people...

Kuhusu Pombwe Magufuri, ni mwana sayansi. Watu wengi waliosoma sayansi wana namna yao ya utendaji. Wakijua principle inasema hivi..wao huanza kutekeleza kulingana na hiyo principle inavyosema. Si waongeaji sana kama wewe MM, au kama walivyo wanasiasa per se. Hawaongei sana kama wansheria, au watu waliosoma sana historia. Hawa ni watu, katika aina za watu, wenye kundi lao, ni watendaji.

Kuhusu uuzaji wa nyumba, ilikuwa ni maamuzi ya pamoja katika baraza la mawaziri, kipindi cha serikali ya BW Mkapa. Mkapa alikuwa na utaratibu wa kufanya vikao na mawaziri wake ili waweze kuwa na uamuzi wa pamoja. Naona Kikwete hilo si muhimu sana, yeye anawatembelea huko huko wizarani kwao mmoja mmoja. Kwahiyo baada ya uamuzi huo, Magufuri alianza kutekeleza kwa kishindo principle ya baraza la mawaziri.

Kuhusu hili la bomoa bomoa, naona lina sababu tatu (1) sheria ndio inataka hivyo (2) ilani ya uchaguzi inatao ahadi ya kujenga fly overs na usafiri wa kasi (3) alipelekwa wizara hiyo kwenda kuondoa malalamiko mengi yaliyokuwepo ikiwa ni pamoja na ufisadi.

Kwasababu hizo tu rais alitakiwa kumpa special treatment, yaani kuwa naye karibu ili kuweza kumrekebisha pale anapoharibu na kumpa moyo ili afanye ile kazi aliyompa aifanye katika hiyo wizara ngumu.

Magufuri, amejijengea jina, ambalo hata asipokuwa na madaraka, wengi mtamkumbuka. Ndiyo maana leo tunamjadili yeye na siyo Dr Kawambwa. Ndio maana Lyatonga Mrema ambaye hana madaraka ya uwaziri, lakini nchi nzima tunakumbuka utendaji wake. Hata Hayati Moringe Sokoinne, pia hatasahaulika kwa uwezo wa kutekeleza na kufuatilia utekelezaji katika serikali ya awamu ya kwanza.

Mwisho, kila mtu anaweza kuwa na taswira yake kutegemea na kazi anayofanya, madaraka aliyopewa na aina ya mkuu wake wa kazi alivyo. Kama Dr JP Magufuri angekuwa anafanya kazi chini ya rais Nyerere au Dr Slaa, nadhani angeweza kuwa na manufaa makubwa sana kwa taifa hili.

mtu avurunde kisha umuache ujadili uvundo wake? Hata hao waliosema kuwa simple minds discuss people wanaweza kosolewa pia. Kuna ubaya gani kumjadili hitler kwa mfano. Mbona kuna documentary na filamu kibao zinazomuhusu yeye? Magufuli achafue hali ya hewa then tujadili uchafuzi wa hali ya hewa pekee? Hauko sahihi
 
sasa kwa mfano akiwa Rais Magufuli atatuongozaje?

Hawezi kuwa Rais; hana ideas; urais ni zaidi ya utekelezaji; nafikiri education background imemfanya alivyo..

Maximum he can be ni U-PM ..beyond that mnamuonea bure mzee wa watu..hana hana hana.(empy ideas) period
 
Yes nimekuelewa sana japo maada yako ni ngumu sana na kama tutatumia chekeche hili kuwakaanga CCM, masafi ya mtume! hapiti mtu!...usiseme wapinzani , ndio kabisa!

Mkuu unajua tumbo na principle haviendani! unajua ukiwa na njaa sana unaweza kusahau kunawa mikono?

Yes Magufuli he is compromising with the situation because he dont have options/alternative n.k, njaa mbaya na ukiingia kwenye siasa LENGO lao ni hilo kula kwanza mengine baadaye.

I think we need rich leaders, I mean they have to prove they are rich before being leaders !!!! sound strange??

Rafiki yangu mmoja alisema tunapowachagua viongozi na kuwa -install lets ask them HOW MUCH THEY NEED BEFORE commencing their jobs! mfano lets say JK kabla ya kuanza kazi tungempa sh. bilioni 100! ili afanye kazi nyingi na kwa uhakika, maana yeye kujiingiza kwenye dubius deals lime-cost taifa trillions, wakati tunge-save kwa kumpatia yeye bilioni 100, achilia mbali mshahara wake, then same to mawaziri, wakurugenz n.ki!! nilikaa kimya na kutafakari...kidogo ...

If we will reach stage that politics is not a platform to earn money but is a chance to show how one human can increase value of life to other people then we are 'THERE'! kwa sasa bado, are we??
Mkuu wangu mimi nitatofautiana sana na wewe pamoja na Mwanakijiji ktk hili....Kwa maana yangu na mtazamo wangu. Kiongozi anatakiwa kwanza UZALENDO hata ukiwa na njaa maadam kuna uzalendo haijalishi kama umenawa mikono au hukunawa maadam wewe na uzalendo wako unajiamini kwamba ni msafi.

Yesu alisema wazi ktk hili kupima nia za waumini wake ambao walimuuliza kama kutonawa mikono kabla ya kula ni haramu... Na akawajibu uharamu upo ktk nafsi zenu maana kama wewe unajua kutonawa mikono ni vibaya na haramu kwa nini usinawe?.. na kama hutanawa na wewe unajiamini msafi kwa nini uulize uharamu wa kutonawa....Kwa maana hiyo, Usafi wa binadamu ni wa kiroho yaani imani - amini kwanza mengine yote yatajipanga.. Mtanisamehe ikiwa biblia haisemi hivyo lakini tukubaliane in general kwamba unapokuwa msafi kiroho mengine yote ya haramu hukaa mbali nawe.

Utajiri wa mtu sio kigezo kabisa kwa sababu bado tunarudi palepale kwamba hakuna utafiti wowote wa kisayansi wala kienyeji unaoithibitisha kwamba mtu mwenye Utajiri hatakuwa na njaa kama maskini asiyekuwa nacho... Na swala likiwa Ufisadi basi tajiri ni hatari zaidi kwa sababu huyu mtu hana kipimo cha UTU hadi kutajirika vile wakati jirani zake maskini. Mtu huitwa tajiri tu ikiwa wenzake ni maskini maana hakuna mtu tajiri mbele ya matajiri.. Huyu tajiri lazima ameisha jenga imani ya utajiri (kuwa ni mbora zaidi ya wengine kifedha) na kwa bahati mbaya hakuna kipimo cha ujazo. yaani tajiri hawezi fikia mahala akasema basi sasa nimeshakua tajiri sina haja ya kuendelea kutajirika..Jamani tabnzania ni nchi ya tatu duniani kupokea misaada ya maendeleo (kiuchumi) lakini wapi mabillioni yanaliwa na kundi lilelile la matajiri..

As to say, wakati tajiri anagombea Urais fikra zake ni kuongeza zaidi na maskini anapogombea Urais fikra zake ni kutoka, hawa wote hata wakinawa mikono yao bado ulafi uko pale pale watalirukia sinia kutafuta nyama kubwa kubwa ..Hivyo kuwana kwao hakuna sababu hata kama wasingenawa bado swala ni kuondoka kwa pande kubwa la nyama ktk sahani..

Tunahitaji kiongozi Mzalendo, mimi nafikiria tunahitaji kumpata CHE wetu au Chavez ambaye yuko tayari kusulubiwa kwa mashali ya wakulima na wafanyakazi maana ule wimbo wa nchi hii ni ya WAKULIMA na WAFANYAKAZI umekwisha kabisa japokuwa kweli tunajenga asilimia 99 ya Population. Wawekezaji wa ndani hawafiki hata millioni moja maana Dr.Slaa alikwisha sema walipa kodi hawafiki hata millioni 3..Utajiri umeshikwa na asilimia ndogo sana na wananchi na matabaka yanaziodi kukua baada ya kuondokana na malengo....
 
Hilo daraja wasisahau tu njia za waenda kwa miguu, Guta, baiskeli na Bajaj....maanake isiwe linajengwa kwa malengo ya kundi fulani la watu wa Kigamboni mji mpya (wenye magari)..
 
Nchi ilishavulundwa muda mrefu na watendaji wabovu, ili kuweka mambo sawa kwa nchi iliyovulugwa kama hii tunahitaji viongozi wenye vulugu, kwa hili Magufuli anafaa. Watu wanahitaji maamuzi magumu, maamuzi magumu yakianza kutekelezwa tena tunakuwa watu wa kwanza kulalamika. Katika lundo la vigogo wote wanaong'ang'ania kuongoza mzoga huu (Tanzania), at least Pombe ndio anafaa. Mtoa maada umeonyesha bias kwenye topic hii. Kamwe sitaweza support eti Magufuli ajiuzuru kwa kuwa tu anasimamia bomoabomoa au kwa kuwa tu kawaambia watu wapige mbizi. Au kwa kuwa tu maamuzi yake huwa nayapingana na Rais na PM, I don't see any rationality on this , Unless utwambie kuwa hao viongozi walio juu yake ni watendaji wazuri kuliko yeye, then anawavuruga. Lakini kama Magufuli anafanya kwa manufaa ya Tanzania, na akiwa kati ya watu wachache ambao walisomeshwa bure enzi za Mwalimu ili waje walipe fadhira kwa taifa kwa kulitumikia, Magufuri hana haja ya kujiudhuru unless tuaminishwe kuwa JK, PM and others are doing well for this poor nation. Wapo watu wakujizuru wengi tu huko kwenye system wachafu kuliko Magufuli. Kama sheria zilikosewa watu walipwe na nyumba zibomolewe na hayo ndio wanaita maamuzi magumu. Magufuri anahitaji blending ndogo tu ila kazi anaiweza kwa watu wapenda soga kama sisi watanzania.
Katika kipindi hiki mpaka 2015 tutayasikia mengi sana na waandishi uchwara wanaotumia kalamu kuchumia tumbo wataonekana.
Watu kama Magufuli ambao hawajatumia muda wao kisiasa kujijenga Kichama wala hawajishughurishi kuwapa visenti waandishi wa habari ili waandikwe vizuri kwenye magazeti bali kutegemea utendaji wao kujijenga kisiasa wanapata shida sana kwenye mazingira ya Tanzania ambayo yamejaa waandishi wachumia tumbo.
Sasa nimeanza kuamini ni kwa nini Mpaka alimpa ulinzi wa ziada Magufuli, kweli mazingira ya Tanzania yamejaa predetors kwa watu wa aina ya Magufuli. Tunakoenda kazi iko
 
Back
Top Bottom