Magufuli bila madaraka yukoje?

Magufuli bila madaraka yukoje?

Mkuu maada yako ni tata sana! hasa ukidefine neno mamlaka na wajibu wa aliyepewa mamlaka! kama kwajibika kwa magufuli kwa mamlka aliyonayo ni tatizo then we have problem somewhere

Je unaweza kutoa mfano wa asiye na mamlaka na yet ni mpiganaji au mtetezi wa mali ya umma
Pili je ulitaka magufuli afanye nini bungeni ili aonekane kuwa anapigania haki na kufabya unavyotaka wewe?

Baada ya majibu hayo je ili uonekane mpiganaji lazima

1. uandike article sana
2. useme sana bungeni (kama mbunge)
3. Jamii yote ijue wewe ni mpiganaji?

Je wale wasio na nafasi ya kujulikana kwa vigezo utakavyoonyesha wanaweza kuwa wapiganaji?

Je unaweza kutoa mfano mmoja wa waziri mmoja wa sasa na serikali zilizopita ambaye ni mpiganaji from bungeni mpaka serikalini na OUTPUT yake imeonekana?

Magufuli ulivyo-m-rate umetumia standard gani? job descritption yake inasemaje?

cheers

Heshima Mkuu! Mimi nilivyomwelewa MM, ni vigumu sana kujua msimamo wa Magufuli, anasimamia nini hasa katika masuala ya kitaifa. sawa, anaonekana mchapa kazi sana, lakini so far ukipiga picha, anaonekana kufaulu akiwa katika madaraka tu. sasa MM amejenga hoja hapo, na binafsi nimeikubali. conclusion yake pia, kwamba kwa maana hiyo itakuwa ni vigumu sana Magufuli kujiuzulu, kwa sababu hawezi kusimama kama yeye na msimamo wake, aka-flourish. na hoja hii ya MM inakuwa urgent kwa sababu kama asemavyo MM, PM na JK wamemlima jamaa kisawasawa, kiasi kwamba unabaki unashangaa huyu jamaa bado yupo. nadhani kwa mtu mwenye msimamo hasa, alitakiwa ajiuzulu na kama ni mtu mwenye misimamo inayojitokeza kitaifa, bado anaweza kuwa relevant and effective katika kusimamia yale anayoyaamini katika taifa hili. ndivyo anavyofanya Dr. Slaa, kwa mfano. sasa hivi sio mbunge, lakini akisimama mahala akaongea, watu wanamsikiliza na serikali inatetemeka
 
Heshima Mkuu! Mimi nilivyomwelewa MM, ni vigumu sana kujua msimamo wa Magufuli, anasimamia nini hasa katika masuala ya kitaifa. sawa, anaonekana mchapa kazi sana, lakini so far ukipiga picha, anaonekana kufaulu akiwa katika madaraka tu. sasa MM amejenga hoja hapo, na binafsi nimeikubali. conclusion yake pia, kwamba kwa maana hiyo itakuwa ni vigumu sana Magufuli kujiuzulu, kwa sababu hawezi kusimama kama yeye na msimamo wake, aka-flourish. na hoja hii ya MM inakuwa urgent kwa sababu kama asemavyo MM, PM na JK wamemlima jamaa kisawasawa, kiasi kwamba unabaki unashangaa huyu jamaa bado yupo. nadhani kwa mtu mwenye msimamo hasa, alitakiwa ajiuzulu na kama ni mtu mwenye misimamo inayojitokeza kitaifa, bado anaweza kuwa relevant and effective katika kusimamia yale anayoyaamini katika taifa hili. ndivyo anavyofanya Dr. Slaa, kwa mfano. sasa hivi sio mbunge, lakini akisimama mahala akaongea, watu wanamsikiliza na serikali inatetemeka
mkuu, hapo kwenye red umenikuna hasaaaaa!
 
Kwa upande wangu sijui kama nitamweka wapi huyu mheshimiwa. Naweza nikasema kuwa ni "mtendaji" anayetaka kuacha legacy kila aendako.Haijalishi ni aina gani ya legacy!
Namkumbuka vizuri sana kwenye maswala yafuatayo:

  • Kufuatilia "uporaji" wa magari ya serikali alipokuwa wizara inayohusika na Ujenzi na magari ya serikali.Alitetemesha watu pale alipothubutu kuwanyang'anya magari wazito walioandikisha magari ya serikali namba za binafsi na kuwapa wapendwa wao!
  • Aliposimamia uvuvi haramu hadi kukamata tani kadhaa za samaki waliovuliwa pasipo uhalali ndani ya maji yaliyomo ndani ya mipaka ya Tanzania - alipokuwa katika wizara inayohusika na uvuvi ( sijui kama mwisho wa sekeseke hili ulikuwa mzuri ama la hii ni ishu nyingine!)
  • Aliposimamia uuzwaji wa nyumba za serikali kwa watumishi wa umma ( wengine hawakuwa watumishi wa umma bali walikuwa wako karibu na watumishi wa umma) bila kujali malalamiko yaliyokuwa yakitokea ndani ya jamii - huenda kwa vile Serikali nzima iliunga mkono uamuzi huu na hivyo kupata confidence kuendelea bila kutetereka.
  • Uamuzi wake wa sasa wa kubomoaboamoa majengo ya watu binafsi na hata ya umma ya gharama kubwa kwa vile anasimamia sheria - japo hapa kuna kukosekana kwa support ya bosi wake.
Kitu kimoja ninachoona ni kuwa bila kujali "public policy" ya wakati husika, huyu kiongozi hufanya maamuzi ambayo wakati mwingine huwaacha watu wabaki wakijiuliza maswali mengi mno.Inawezekana anasimamia sheria na taratibu.Lakini kama anaonyesha double standards siwezi kumtafsiri na kumweka upande wowote.Kama ni msimamizi wa haki - ingetegemewa asitishe lile zoezi la kuuza nyumba za serikali kwa bei ya kutupwa kwa kisingizio cha kuwasaidia watakapostaafu wasiadhirike wapate makazi.Siyo siri nyumba nyingi zimeuzwa kwa wahindi na wamejenga ma apartments - apartment moja yenye vyumba vitatu vya kulala kwa mfano Masaki inauzwa kuanzia dola za kimarekani 200,000 hadi 700,000 na hii ndio bei wenzetu waliouziwa kwa bei ya kutupa wameuza nyumba zile.Jengo moja linaweza kuwa na apartment hata 20! Piga hesabu.Ingetegemewa basi awe sharp zaidi kuona hili na kuhakikisha serikali hapati hasara kwa uuzwaji wa mali zake! Simuelewi kabisa huyu Mheshimiwa!
 
Kimsingi magufuli ataonesha taswira ya uzalendo na upiganaji wa haki ya matumizi endelevu ya rasilimali za taifa kwa maslahi ya watanzania pale ambapo atajiuzulu-kuonesha ishara ya kukerwa na wakubwa wake! Vinginevyo: Bado hana taswira ya uzalendo, kimsingi akishindwa kujiuzulu ni ishara tosha kuwa ..yeye bila "pazia la madaraka hawezi kuzuia upepo na vumbi kuingia ndani"
 
Kiongozi anayeamini katika kanuni na sheria tunamhitaji katika nchi hii kwa sasa. Nchi yetu haihitaji kiongozi wa kuwafurahisha watu bali mwenye 'discipline, vision, goals and action'.


you are right absolutely! Na mimi ni miongoni mwa watu ambao nilikuwa ninaamini Magufuli ni kiongozi wa principle... lakini hili bado linanisumbua.
 
Binadamu tumetofautiana sana.kuna watu wanaweza kuhoji wakiwa tu hawana madaraka pindi wakiyapata huwA KIMYA.kuna watu wengine huwa kinyume chake.Nafikiri hapa cha msingi ni je alikuwa sahihi kwenye yale aliyofanya akiwa madarakani?kama alikuwa sahihi apongezwe kama hakuwa hivvyo atalaumiwa.


ni wazi kwamba haya aliyoyafanya hivi karibuni hayakuwa sahihi - kwa mtazamo wa viongozi wake wa juu kitu ambacho kikanuni ilimpasa kuachia ngazi.
 


Kuhusu kufuata sheria, kwa kuwa anatambua kuwa watanzania wengi wana kiu ya kuona sheria zikifuatwa basi Magufuli hutumia kauli mbiu hiyo kujipigia chapuo lakini ukichunguza kwa makini yeye sio muumini mzuri wa utawala wa sheria na kanuni za utawala bora.

Neno la leo.
 
Ndugu MM, topic yako hii, inaweza kukuweka mahali pabaya hata wewe, kwa sababu inaonekana kama kumjadili mtu. Tukumbuke kuwa simple minds discuss people... .

Utaona kumbe hatumjadili mtu kama mtu bali mtu na kanuni inayomuongoza; ndiyo maana sijasema "Magufuli yukoje?"; swali ni Magufuli bila ya madaraka. Na utaona wachangiaji karibu wote wanachangia - ukiwemo wewe- kwa kuangalia kiongozi aitwaye magufuli akiwa na madaraka au pasi na madaraka. Huku si kumjadili mtu kama mtu.
 
a. Dr. Magufulu hawezi kuwa mpiganaji wa raslimali za taifa bila ya madaraka. Madaraka ni kinga kwake ya kuweza kufanya mambo mbalimbali.

b. Dr. Magufuli hana historia ya kujivunia ya kujitofautisha kuwa ni mtetezi wa raslimali za wananchi nje ya ofisi yake. Kwa kiasi kikubwa anakumbukwa kwa mamboa ambayo yamemjengea sifa ya kuwa ni "askari wa mwamvuli" wakati wa Mkapa lakini bila kuwa na uwaziri ni mtu ambaye yuko very docile.

Haya mawili yanajibu maswali mawili - kwa uzuri na kwa ubaya:

a. Itakuwa vigumu sana kwa Magufuli kujiuzulu on principle hasa baada ya kutofautiana na RAis na Waziri Mkuu wake na vile vile kwa viongozi hao wawili kuonesha wazi kuwa hawana imani na uwezo, nia na sababu ya maamuzi ya waziri wao. Kwa vile hawezi kukaa bila ya madaraka na kupigania anachoamini ataendelea kuwa waziri na tushangae akiwa mkimya mno kwani alichofanyiwa juzi si kidogo kwa kipimo chochote.

b. Endapo atakuja kutaka kupewa madaraka makubwa zaidi nchini; kuna watu wanaweza kujikuta wanakimbia nchi kwani ni wazi kuwa anaweza kutumia madaraka aliyonayo kufikitia masuluhisho ya mambo kadha wa kadha kuliko baadhi ya viongozi wengine ambao wamebakia kuja na sura za huruma na upole wakikwepa kusimamia sheria.

my two cents plus the other fifty

MMKJJ sijakuelewa una maana gani kusema magufuri anatete maslahi ya Umma, labda uende detail kuelezea kama ikiwa maana yako ni kuwa kubomoa hizo nyumba ndio maslahi ya Umma kwako wewe, si mbaya pia ukatwambia hiyo tafsiri una-evidence wapi?

Labda kama kuna kitu mnajadili kuhusu magufuri hamja kiweka wazi pia ni vyema mkatwambia na sisi maana kama ni swala la Bomobomoa Mimi na Jatropha tumelieleza kinagaubaga na kihalisia pia tumeanisha taratibu ambazo zilitakiwa zifuatwe ambazo Magufuri alizikiuka, tokea awali tumejitahidi na kujitolea kufafanua hili swala kwa upana wake hadi sasa hamna mtu aliyediriki kuzijibu hata hoja moja. Jana nilisoma comments zako katika thread ya "Magufuri tumeelewa" Nilikuandia na kukuomba kupata muda usome michango ya Jatropha na yangu binafsi katika threads zote za magufuri humu ndani ukianzia na ile "PM anatumiwa kumchafuwa Magufuri" hadi ile ya "Serikali ya kanusha kujizuru kwa Magufuri" nilikwambia usome hizo threads na pia kama utaweza tafuta "legal Opion" nilikushauri kama una fahamiana na Mhe.Lissu muombe ushauri wake maana lazima atakuwa Live cases za Bomobomo za Magufuri, nilikuwa naamini kuwa hujapitia michango ya baadhi ya members na hivyo nilidhani ingekusaidia sana. Hii threads yako imenioyesha au bado hujazisoma hizo hoja au la kama umeyasoma basi kuna jambo juu ya magufuri ambalo labda mnalijadili kwa kutumia neno bomoabomoa, na hivyo kutuacha kwenye mataa sisi tunaochangia na kutoa ushahidi kuwa Magufuri alikosea katika hili la kutaka kubomoa nyumba za watu wenye haki kisheria bila kufuata utaratibu na kwa mabavu.

Tunaomba mtwambie kuna nini? maana hata hivyo hizi threads za Magufuri zinafurika humu kila baada ya dk.5 na Mods pia hawaoni kama zinarudiwa bila tija yoyote wakati wanazileta wamegoma kujibu wala kutoa hoja yoyote.

Pia Naami unajua mambo mengi na wewe ni mfuatiliaji, kama utapata muda na kusoma hizo threads nilizokuomba kusoma naomba uje tena hapa katika hii threads yako utusaidie mambo yafuatayo:

  1. Magufuri anasimamia sheria ipi ya nchni inayompa mamlaka ya kuvunja nyumba za halali za raia tena wenye haki milki ya ardhi bila notice na fidia yeyote?
  2. Uje tushauriane katika hii nchni yetu nani ana mamlaka ya kupanga na kugawa matumizi ya ardhi, kama ukiwa na hisia kama zangu kuwa mwenye mamlaka ya kugawa ardhi ni Wizara ya Ardhi, basi tushauriane pia kuwa inakuwaje mwenye mamlaka agawie mlalahoi ardhi, ateseke kuuza mchicha karikoo na kujenga nyumba yake then aje mwingine katika serikali hiyohiyo iliyokupa ardhi aje tena nyuma kuibuka na kubomoa nyumba yako kwa ubabe na lazima bila taarifa wala fidia yeyote? Huku akinadi kuwa haijui wala haitambui hiyo sheria iliyokupa ardhi, tushauriane kama ikiwa tafsi ya sheria kwenu wenzetu ndio hiyo.
  3. Lakini cha Msingi kinacho pindisha hapa ambalo na hitaji tujadiliane Mkuu, ni iwapo Magufuri ana simamia sheria au ana chukua sheria mikono mwake? nataka tufafanue na kuchambua iwapo kumchoma moto kibaka ni kusimamia sheria au ni kuchukua sheria mikononi!? na inatofauti gani kwa upande wa shillingi katika hili Magufuri?

Mkuu nashukuru sana, naamini wote tunajenga nyumba moja ila tofauti ni kuwa Mimi na changanya ugongo na Wewe unakata fito, nasubiri fito uje nazo.
 
you are right absolutely! Na mimi ni miongoni mwa watu ambao nilikuwa ninaamini Magufuli ni kiongozi wa principle... lakini hili bado linanisumbua.
Magufuli sio kiongozi wa Principle, na hii imejidhihiriasha sasa. Magufuli ni kama robbot unaliprogram halafu linafanya kazi kulingana na ulivyo liprogram, nasema hivyo kwa sababu kila wizara anayoenda anakariri sheria na miongozo yake na kuanza kutekeleza bila kuipa nafasi akili yake kupambanua. Na ndio maana nje ya uongozi hana kitu anachoweza kufanya. Hana principle zake anazozisimamia.
 
Waberoya, umetoa maswali na hoja nzuri. Hatujatenda haki kwa huyo jamaa anayejaribu kutumikia jamii. Tena kuna kitu ambacho kimeniuma sana...yaani mtu anaomba kwa raisi aruhusiwe kutekeleza majukumu na sheria alizoapa? Yaani kutenda haki na wajibu sasa hivi mpaka ulambe miguu ya kiongozi wa mfumo unaotawala??? Hii ni hatari na hapo lazima nguvu itokayo juu iingilie kati

sn2139 - ndio maana naamini ya haya maswali na uchokozi wangu hapa.. of course tunajua mawaziri wanafanya kazi at the pleasure of the president.. kwa hiyo upande mmoja ni kuwa ili aweze kuendelea kuwa madarakani na kufanya anayotaka hana budi kulamba miguu ya bosi wake. Swali langu ambalo ndio msingi wa hoja (natumaini Waberoya naye ataliona) ni kuwa viongozi hawa wanapotofautiana hivi ni nani ajiuzulu on principle? Swali langu halihusiani na upiganaji n.k linahusu kutawala na kuwabika kama kiongozi pale tofauti za msingi zinapotokea.
 
Magufuli sio kiongozi wa Principle, na hii imejidhihiriasha sasa. Magufuli ni kama robbot unaliprogram halafu linafanya kazi kulingana na ulivyo liprogram, nasema hivyo kwa sababu kila wizara anayoenda anakariri sheria na miongozo yake na kuanza kutekeleza bila kuipa nafasi akili yake kupambanua. Na ndio maana nje ya uongozi hana kitu anachoweza kufanya. Hana principle zake anazozisimamia.

Hapo kwenye bold, naomba ufafanue.

Nijuavyo mimi, Waziri ana majukumu 1. Kusimamia sera za serikali iliyomweka madarakani 2. Ni political commissar hivyo anasimamia sera za chama na ilani ya uchaguzi ya chama chake. Ina maana hawezi kutenda nje ya mandates hizi.

Swali linakuja hivi: Je ni kazi yake kwenda frontline na kusimamia kama afanyavyo? Je katika kusimamia sera ( pamoja na Sheria) huyu waziri angeweza kuwa tofauti kiutendaji na akawa na tija? Kuna nafasi ipi itakayomwezesha kutenda effectively nje ya 'madaraka" yake?( madaraka ilivyotumiwa na MMKJJ ni sawa na mandate?)
 
sn2139 - ndio maana naamini ya haya maswali na uchokozi wangu hapa.. of course tunajua mawaziri wanafanya kazi at the pleasure of the president.. kwa hiyo upande mmoja ni kuwa ili aweze kuendelea kuwa madarakani na kufanya anayotaka hana budi kulamba miguu ya bosi wake. Swali langu ambalo ndio msingi wa hoja (natumaini Waberoya naye ataliona) ni kuwa viongozi hawa wanapotofautiana hivi ni nani ajiuzulu on principle? Swali langu halihusiani na upiganaji n.k linahusu kutawala na kuwabika kama kiongozi pale tofauti za msingi zinapotokea.
Kimsingi hii inaonyesha kwa namna fulani viongozi anaowatumikia JPM hawana imani nae au hawakubaliani na jinsi anavyo endesha mambo yake, inapofikia kwamba kiongozi wako anaonyesha kutokubaliana na wewe hadharani ina maana aliisha kaa na wewe pembeni akakushauri na hukusikiliza ushauri wake. Sitaki kuamini kwamba JK na PM waliamua kumkosoa hadharani bila kuwa waliisha kaa nae na kumpa muongozo wao, huenda anachofanya JPM sicho walichokubaliana kwenye baraza la mawaziri na vikao vyo vingine na hivyo wameamua kumtolea uvivu hadharani. Kama kweli JPM is the man of principle ilibidi awaachie wizara yao, ili asije akaongo wizara kinyume na kile anacho amini.
 
Swali linakuja hivi: Je ni kazi yake kwenda frontline na kusimamia kama afanyavyo? Je katika kusimamia sera ( pamoja na Sheria) huyu waziri angeweza kuwa tofauti kiutendaji na akawa na tija? Kuna nafasi ipi itakayomwezesha kutenda effectively nje ya 'madaraka" yake?( madaraka ilivyotumiwa na MMKJJ ni sawa na mandate?)

Hapana; mandate is more a political notion ya kile mtu anachotarajiwa kufanya na inakuwa na nguvu pale inapoanishwa. Ninapozungumzia madaraka ninazungumzia - nguvu zinazotokana na mamlaka ya cheo au ofisi fulani - powers that comes with the authority of a rank or authority. Kwa hiyo Waziri wa Miundo Mbinu - ni cheo - na kutoka hapo kinakuja na nguvu fulani (kama Waziri generally, na kama Waziri wa Miundo Mbinu specifically).
 
Hapo kwenye bold, naomba ufafanue.

Nijuavyo mimi, Waziri ana majukumu 1. Kusimamia sera za serikali iliyomweka madarakani 2. Ni political commissar hivyo anasimamia sera za chama na ilani ya uchaguzi ya chama chake. Ina maana hawezi kutenda nje ya mandates hizi.

Swali linakuja hivi: Je ni kazi yake kwenda frontline na kusimamia kama afanyavyo? Je katika kusimamia sera ( pamoja na Sheria) huyu waziri angeweza kuwa tofauti kiutendaji na akawa na tija? Kuna nafasi ipi itakayomwezesha kutenda effectively nje ya 'madaraka" yake?( madaraka ilivyotumiwa na MMKJJ ni sawa na mandate?)
Ninacho zungumzia ni kwamba nje ya madaraka hajawahi kuwa mwanaharakati/mkereketwa katika kuonyesha kuisukuma serikali iendeshe mambo kulingana na sheria zake
 
Dr. Magufuli atakumbukwa kwa misimamo ya KIJINGA eti anasimamia SHERIA kwa kuwafanya watu wazidi kuwa mafukara...tayari zaidi ya nusu yetu tunatumia CHINI YA DOLA MOJA kwa siku.....anampango sasa tutumiae CHINI YA NUSU DOLA kwa siku....

Hapa sijakuelewa, unaweza kufafanua tafadhali.
 
Wakati naandika makala ambayo itatoka kwenye gazeti moja la leo kuhusu Magufuli na kwanini hana chaguo jingine lolote isipokuwa kujiuzulu nilijadiliana na ndugu yangu mmoja na tukajikuta tunakabiliwa na swali ambalo hatukuweza kulipatia jibu: Hivi nje ya madaraka Dr. Magufuli anaweza kukumbukwa vipi katika kusimamia sheria nchini na kupigania maslahi ya wananchi?

Hapa sizungumzii mambo ambayo alikuwa anauliza kama mbunge kwa ajili ya jimbo lake tu nazungumzia kitaifa ana jambo lolote ambalo tunaweza kusema alilisimamia kitaifa nje ya yale ambayo amewahi kuyafanya akiwa na madaraka?

Yawezekana ujasiri wa Magufuli hautokani na msimamo au mtazamo uliosahihi bali unatokana na kuwa na madaraka kwamba kwake madaraka na siyo kanuni ya kuongozwa na uadilifu ni chombo kwake cha kutimiza mambo mbalimbali?

Je amewahi kusimama akiwa Mbunge kuhoji na kutaja uwajibikaji wa serikali kwenye jambo gani ambalo lilikuwa na taswira au matokeo ya kitaifa?

Ni wazi kwamba amekuwa Waziri toka wakati wa Mkapa na wakati wote wa Kikwete yawezekana madaraka yamemjengea pazia ambalo ni kwa hilo tu anaweza kuonekana? Je Magufuli bila ya madaraka ni nani? Bila kuwa na cheo - yaani akiwa Mbunge wa kawaida anaweza kupigania sheria isimamiwe Bungeni bila kucompromise? Je akiwa MBunge wa kawaida yuko tayari kubanwa na mawaziri na wabunge wengine?

Katika kujitahidi kupata majibu binafsi nilifikia mahitimisho yafuatayo - mengine nimeandika kwenye makala hiyo:

a. Dr. Magufulu hawezi kuwa mpiganaji wa raslimali za taifa bila ya madaraka. Madaraka ni kinga kwake ya kuweza kufanya mambo mbalimbali.

b. Dr. Magufuli hana historia ya kujivunia ya kujitofautisha kuwa ni mtetezi wa raslimali za wananchi nje ya ofisi yake. Kwa kiasi kikubwa anakumbukwa kwa mamboa ambayo yamemjengea sifa ya kuwa ni "askari wa mwamvuli" wakati wa Mkapa lakini bila kuwa na uwaziri ni mtu ambaye yuko very docile.

Haya mawili yanajibu maswali mawili - kwa uzuri na kwa ubaya:

a. Itakuwa vigumu sana kwa Magufuli kujiuzulu on principle hasa baada ya kutofautiana na RAis na Waziri Mkuu wake na vile vile kwa viongozi hao wawili kuonesha wazi kuwa hawana imani na uwezo, nia na sababu ya maamuzi ya waziri wao. Kwa vile hawezi kukaa bila ya madaraka na kupigania anachoamini ataendelea kuwa waziri na tushangae akiwa mkimya mno kwani alichofanyiwa juzi si kidogo kwa kipimo chochote.

b. Endapo atakuja kutaka kupewa madaraka makubwa zaidi nchini; kuna watu wanaweza kujikuta wanakimbia nchi kwani ni wazi kuwa anaweza kutumia madaraka aliyonayo kufikitia masuluhisho ya mambo kadha wa kadha kuliko baadhi ya viongozi wengine ambao wamebakia kuja na sura za huruma na upole wakikwepa kusimamia sheria.

my two cents plus the other fifty
Kwa maelezo uliyoyatoa,he will make a good president pindi tukishabadili katiba...Kwasababu ameonyesha sifa nzuri ya usimamiaji wa sheria,then tubadili katiba halafu kama atasimama kwa sera nzuri,then he will make a good contender for presidency.Good kwa maana ya good for the country.
 
mkuu mwanakijiji kuna maswali mazuri ya waberoya ambayo majibu yake yatakuwa elimu tosha na pengine mjadala kutoa changamoto zaidi.
 
Magufuli bado namfagilia kwa ushupavu wake wa kusimamia sheria kwa vitendo. Suala la je, anapokuwa hana madaraka yukoje, to me is irrelevant. Kwani kuna mijitu ndani ya serikali ya kifisadi ya ccm imepewa madaraka yote lakini imekaa kimya na kuacha nchi inachezewa kama haina mwenyewe. Kikwete anamweka magufuli madarakani kwa kinyongo.

Anachoogopa ni kunyoshewa vidole na watanzania endapo ataamua kumwacha kwa sababu utendaji wake wa kazi hakuna mtanzania asiyeujua. Aliwahi hata kumtia ndani kiongozi mmoja wa ccm kwa kukutwa na kokolo ya kuvulia samaki kwenye bwawa la nyumba ya Mungu.

Mimi mwenyewe namfagilia sana huyu jamaa aisee.....nilitamani sasa awe waziri mkuu ingekuwa powa sana inaonekana kazi zake mkuu mwenyewe anakubali na hafichi huyu jamaa......zaidi atarudi tu madarakani....ni mchapa kazi wa kweli....
 
a. Itakuwa vigumu sana kwa Magufuli kujiuzulu on principle hasa baada ya kutofautiana na RAis na Waziri Mkuu wake na vile vile kwa viongozi hao wawili kuonesha wazi kuwa hawana imani na uwezo, nia na sababu ya maamuzi ya waziri wao. Kwa vile hawezi kukaa bila ya madaraka na kupigania anachoamini ataendelea kuwa waziri na tushangae akiwa mkimya mno kwani alichofanyiwa juzi si kidogo kwa kipimo chochote.

MwanaKijiji,

Kwa hali ilivyo ya nchi yetu kama Rais, Waziri mkuu na wazari wa kawaida wanapisha wadhania kuwa ni kuwa magufuli hana uwezoooo? Just think wide to that matter,

Nchi viongozi kama rais anashindwa kuitetea katiba ya nchi JK kama yeye tu hana maaamuzi mazito at least kwa magufuli aamabaye anajitahidi kukaa kwenye sheria lakini serikali inazipindisha tena na kumwona magufuli ni mbaya kwanini ?? nikuwa nchi haina KATIBA imara na hakuna usimamizi makini wa sheria zilizopo na ndio kunakuwa na hali hiyo kama rais anafika anawaambia watendaji jamani angalieni na Utu khaaaa wakati walipokuwa wakifanya mipango mini hakujua hilo huyo rais?? mbona viongozi wengi wameji patia mali kiholela na hajasema hawaionei huru pesa ya walipa kodi??

JK anaendekeza siasa na anashindwa kukaaa kwa maneno yake ambayo anawaambia wapinzani ati tuachane na siasa tufanye kazi sasa hapo ndio anafanya nini kwa kuwa piga mkwara wizara ya miundombinu?? Hapo ni Rais JK na Pinda ndio hawna msimamo its simple calculation watanzania sio mazuzu please

 
Back
Top Bottom