Magufuli bila madaraka yukoje?

mkuu mwanakijiji kuna maswali mazuri ya waberoya ambayo majibu yake yatakuwa elimu tosha na pengine mjadala kutoa changamoto zaidi.

ukiangalia maswali hayo nimeyajibu tayari vinginevyo itakuwa ni kurudia rudia au kufafanua zaidi. Nilichokisema siyo kigumu hivyo kueleweka.
 
Wakati naandika makala ambayo itatoka kwenye gazeti moja la leo kuhusu Magufuli na kwanini hana chaguo jingine lolote isipokuwa kujiuzulu nilijadiliana na ndugu yangu mmoja na tukajikuta tunakabiliwa na swali ambalo hatukuweza kulipatia jibu: Hivi nje ya madaraka Dr. Magufuli anaweza kukumbukwa vipi katika kusimamia sheria nchini na kupigania maslahi ya wananchi?<br />
<br />
Hapa sizungumzii mambo ambayo alikuwa anauliza kama mbunge kwa ajili ya jimbo lake tu nazungumzia kitaifa ana jambo lolote ambalo tunaweza kusema alilisimamia kitaifa nje ya yale ambayo amewahi kuyafanya akiwa na madaraka?<br />
<br />
Yawezekana ujasiri wa Magufuli hautokani na msimamo au mtazamo uliosahihi bali unatokana na kuwa na madaraka kwamba kwake madaraka na siyo kanuni ya kuongozwa na uadilifu ni chombo kwake cha kutimiza mambo mbalimbali? <br />
<br />
Je amewahi kusimama akiwa Mbunge kuhoji na kutaja uwajibikaji wa serikali kwenye jambo gani ambalo lilikuwa na taswira au matokeo ya kitaifa? <br />
<br />
Ni wazi kwamba amekuwa Waziri toka wakati wa Mkapa na wakati wote wa Kikwete yawezekana madaraka yamemjengea pazia ambalo ni kwa hilo tu anaweza kuonekana? Je Magufuli bila ya madaraka ni nani? Bila kuwa na cheo - yaani akiwa Mbunge wa kawaida anaweza kupigania sheria isimamiwe Bungeni bila kucompromise? Je akiwa MBunge wa kawaida yuko tayari kubanwa na mawaziri na wabunge wengine? <br />
<br />
Katika kujitahidi kupata majibu binafsi nilifikia mahitimisho yafuatayo - mengine nimeandika kwenye makala hiyo:<br />
<br />
a. Dr. Magufulu hawezi kuwa mpiganaji wa raslimali za taifa bila ya madaraka. Madaraka ni kinga kwake ya kuweza kufanya mambo mbalimbali.<br />
<br />
b. Dr. Magufuli hana historia ya kujivunia ya kujitofautisha kuwa ni mtetezi wa raslimali za wananchi nje ya ofisi yake. Kwa kiasi kikubwa anakumbukwa kwa mamboa ambayo yamemjengea sifa ya kuwa ni &quot;askari wa mwamvuli&quot; wakati wa Mkapa lakini bila kuwa na uwaziri ni mtu ambaye yuko very docile. <br />
<br />
Haya mawili yanajibu maswali mawili - kwa uzuri na kwa ubaya:<br />
<br />
a. Itakuwa vigumu sana kwa Magufuli kujiuzulu on principle hasa baada ya kutofautiana na RAis na Waziri Mkuu wake na vile vile kwa viongozi hao wawili kuonesha wazi kuwa hawana imani na uwezo, nia na sababu ya maamuzi ya waziri wao. Kwa vile hawezi kukaa bila ya madaraka na kupigania anachoamini ataendelea kuwa waziri na tushangae akiwa mkimya mno kwani alichofanyiwa juzi si kidogo kwa kipimo chochote.<br />
<br />
b. Endapo atakuja kutaka kupewa madaraka makubwa zaidi nchini; kuna watu wanaweza kujikuta wanakimbia nchi kwani ni wazi kuwa anaweza kutumia madaraka aliyonayo kufikitia masuluhisho ya mambo kadha wa kadha kuliko baadhi ya viongozi wengine ambao wamebakia kuja na sura za huruma na upole wakikwepa kusimamia sheria.<br />
<br />
my two cents plus the other fifty
<br />
<br />
MM,
Sio Magufuli tu bali ni karibu kila Kiongozi ana matatizo ulioyasema. Mfumo uliopo hauruhusu Nyota kung'ara
 
Wataalam kama Jatropha mpo lakini mnaacha watu kama Maghufuli wanatufanyia mambo kijanja hivo kama akina Kakobe wanavyofanya na Biblia yetu!

Mimi sio mtaalamu, ila ni mhanga turned mtaalamu baada ya kuchimba kutafuta haki yetu. Ndio maana CDM waliweza kutwaa jimbo la Ubungo kwa kuwa Charles Keenja alipokuwa mbunge wa Jimbo la Ubungio alipuuza kuchukua hatua zozote. Hebu fikiria Kilwa maeneo kama Mbagla, Kongewe n.k zipo huduma za kibenki, ATM n.k lakini kati ya Ubungo hadi Kibaha hakuna huduma kama hizo kwa sababu ya ukandamizaji wa mtu mmoja nayetumia madaraka yake vibaya. Unafikiri ni watu wangapi wameathirika kijamii na kiuchumi?
 
Hizo sheria zilipitishwa na vikao halali vya Bunge. Isitoshe ignorance of the law is no excuse... Bila barabara bora hatuwezi kurealize maendeleo lazima tuunge mkono jitihada za Magufuli, watakaoathirika waombe kudra kwa JK walipwe japo fidia kiodogo.


Panapokuwa na mgongano kati ya sheria na Katiba ya Jamhuri, mara moja Katiba lazima iprevail yaani Katiba itabaki juu. Sasa anachotumia Magufuli ni Kanuni za Sheria ya barabara za 1930, 1967 na 2009, Kanuni ambazo hutungwa na Waziri wa Ujenzi. Kanuni zote hizo kwa eneo la Ubungo hadi Kibaha zinapingana na Sheria ya Ardhi ya Vijiji namba 5 iliyotungwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. HKifungu cha 15 cha sheria hiyo kinatamka hivi UGAWAjI WA ARDHI ULIOFANYWA KWA MTU AU KUNDI LA WATU WAISHIO AU WALIOTAKIWA KUHAMIA NA KUISHI KATIKA KIJIJI WAKATI WOWOTE KATI YA 01 JAN 1970 HADI 31 DES 1977 , KAMA UGAWAJI HUO ULIFANYWA KWA MUJIBU WA SHERIA AU KINYUME CHA SHERIA AU BILA KUZINGATIA SHERIA YOYOTE, SASA INATHIBITISHWA KUWA UGAWAJI HUO NI HALALI NA KWAMBA DAIMA NI WENYE NGUVU YA KUTOA HAKI NA WAJIBU WA KISHERIA KWA KUNDI LA WATU WALIOGAWIWA ARDHI HIYO....." Aidh Kifungu cha 16 Kinatamka .......... MASHARTI YA KIFUNGU 15 YATATUMIKA KILA MARA UGAWAJI WA ARDHI YA KIJIJI ULIPOFANYWA NA HALMASHAURI YA KIJIJI AU MAMLAKA NYINGINE YOYOTE MNAMO NA BAADA YA 01 JAN 1978 HADI TAREHE YA KUANZA KUTUMIKA KWA SHERIA HII.

Ndio maana wakubwa wake wametambua kuwa upana wa hifadhi ya barabara ni Mita 22.86 kila upande. Upana huo unatosha kuzalisha njia (lane) 14; 7 zikielekea Kibaha na 7 zikija Dar zote zikiwa na upana wa Mita 3.25 kama inaelekezwa na Kanuni hio hizo. Hivyo nafasi ya kutosha ya kutekeleza maendelo ya barabara Magufuli anayo, kwanini anawafuata walioko MIta 120 kutoka katikati ya barabara? Kama hujui hilo ndio tatizo.

Yeyote aliyeko ndani ya Mita 22.86 ndio mteja halali wa Mhe John Magufuli, laikini kwa kuwa Magufuli anafahamua kuwa akishghulika na hao wachache ambao wengi wao ni vibanda vya muda vya biashara hawezi kuzuo sifa anazotaka ndio maana nawaburuza hata wasiokuwemo/ Nafikiri nimekuelewesha wewe usiyesoma hata hizi thread vizuri kabal haujachangia.
 
Hivi kwa nini kwa wakati mmoja Raisi na PM wanamwandama Magufuli katika utendaji wake tena hadharaniiiii????????????????????????????
Jamani watanzania tunasifa moja kuu, nayo ni kutosoma na kurukia vitu. Gazeti la Tanzania Daima liliropoti kuwa PM alimwita na kuka na Magufuli mara mbili na kumtaka asitishe bomaa bomoa holela hii kabala hata ya hajaenda katik ziara Kagera. Akakaidi na kutunga msamiati kuwa nimeapa na kumtaja Mungu.

Kwa hakika kilichotakiwa ni Magufuli kufukuzwa kazi na si lingine kwa kuwa watanzania wako very linient, Serikali ingeweza kudaiwa lot of money kwa kitendo tu cha kuchafua nyumba za watu wenye title deeds halali kama Tanesco na wengineo.
 
we Jatropha inaelekea ni mmoja wa waathirika wa bomoabomoa ndiyo maana unaongea even out of context. Nijuavyo mimi ipo ramani ya jiji zima la Dar, ukiangalia ramani hiyo na hali halisi on the ground ni kichekesho. Yaani watu wamejenga kiholela sana na walifanya hivyo kwa kudanganywa na maafisa ardhi kuwa ramani ingebadilishwa in their favour, hiyo ilikuwa miaka kama 10 au 20 iliyopita, hatua zisipochukuliwa basi daima hatutakuwa na barabara zenye ubora. njia pekee ni kubomoa baadhi ya nyumba ili kupisha ujenzi wa barabara, na hatua hii ni kwa faida ya taifa lote kwa ujumla. As I see it labda muombe fidia kidogo kwa JK.

Nakubaliana na wewe 100%, lakini kwanza itumike hifadhi halali ya barabara ya Mita 22.86 ambayo ina uwezo wa kuzalisha njia (lane) 14, yaani 7 za kuelekea Kibaha na 7 za kuja Dar. Kama eneo hilo halitatosha ndipo tuwavamie wananchi wengine. Tatizo lenu wengi mnadandia treni ya hifadhi ya barabara bila ya kujua hata nini maana ya hifadhi ya abarabara. Tembelea Magomeni pale Llilipojengwa jengo jipya la Benki ya wananchi wa Dar es Salaam au uzio wa DIT uliorudishwa nyuma ndipo utaona eneo waliloacha kutoka barabara ya sasa ilipoishia ndilo linalohitajika kwa ajili ya mradi wa mabasi ya kwenda kasi na si vinginevyo.

Kwingine kote Magufuli anakovamia yaani Mita 100 kutoka katikati ya barabara ni uvamizi wa ardhi na makzi ya wananchi.
 
Magufuli sio kiongozi wa Principle, na hii imejidhihiriasha sasa. Magufuli ni kama robbot unaliprogram halafu linafanya kazi kulingana na ulivyo liprogram, nasema hivyo kwa sababu kila wizara anayoenda anakariri sheria na miongozo yake na kuanza kutekeleza bila kuipa nafasi akili yake kupambanua. Na ndio maana nje ya uongozi hana kitu anachoweza kufanya. Hana principle zake anazozisimamia.

Youre exactly right. Mwak 2008 Magufuli akiwa Waziri wa Ardhi katik mgogoro wa Luguruni, watendaji wake walikuwa wanadai kuwa Serikali ilitwaa eneo la Kilomita 2 kutoka Morogoro road both sides kupitia GN Notice mwaka 1993. Hivyo watu wote waliokuwapo katika eneo hilo mwaka 2007 Wizara ya Ardhi ilipoanza kutekeleza mradi wa Satellite City ya Luguruni hawastahili fidia hata kidogo kwa kuwa ni eneo la Serikali.

Arguement ikawa nbaada ya Serikali kutwaa eneo hilo 1993 mboana hata waliokuwepo wakati huo hawakuarifiwa? Mbona Serikali za Mitaa zenye ziliendelea kusimamia land transfer na watu kujenga. Based on those facts akaamua watu walipwe fidia. Alitoa uamuzi huo January 2008, Februari 2008 Baraza la Mawaziri likavunjwa baada ya EL kujiuzulu. Mafisadi waliotanda wizara ya ardhi hadi Ikulu kw akuona Magufuli yuko upande wa wananchi wakamshauri president kuwa kuna tatizo kubwa katika fisheries hivyo iundwe wizara ya kitoweo na hakuna waziri mwingine anayefaa ila Magufuli tu, lenmgi likiwa ni kumuondo pale wizara ya Ardhi kwa kuwa walikuwa wameshatafuna Bil 3 kwa njia ya fidia na alikuwa amewakalia kooni. Hivyo akakabidhiwa akahamishiwa wizara ya kitoweo na kukabidhiwa statistics za samaki ambazo halianza kucharuka nazo ili ajipatie sifa na kusahau hata kukabidhi ushahidi wa wizi aliokuwa akishughulika nao pale ardhi.
 
Kwa maelezo uliyoyatoa,he will make a good president pindi tukishabadili katiba...Kwasababu ameonyesha sifa nzuri ya usimamiaji wa sheria,then tubadili katiba halafu kama atasimama kwa sera nzuri,then he will make a good contender for presidency.Good kwa maana ya good for the country.

WHATA ARE YOU TALIKING ABOUT, SOMEBODY WHO FAILS TO ADHERE TO REGULATIONS PUT IN PLACE BY HIS OWN MINISTRY AND APPLIES FOCE AND COHESION TO FULFILL HIS MINISTRY'S OBLIGATION. SOMEBODY WHO KNOWS NOTHING ABOUT COORDINATION AND CHAIN OF RESPONSIBILITIES BETWEEN CENTRAL AND LOCAL GOVERNMENT TO MAKE A PRESIDENTIAL MATERIAL. KINDLY FOLLOW

Sababu za magufuli kukaripiwa ni kuvunja sheria za barabara alizoapa kulinda kwa kumtaja mungu
Sasa imebainika sababu za Mhe John Pombe Magufuli kukaripiwa na wakubwa wake serikalini ni kutokana na kuwa mbumbumbu wa sheria za barabara ambazo amekuwa akitamba kuwa aliapa kuzilinda.

Kama ambavyo Mhe John Magufuli aliliambia bunge lililoisha wakati akijibu swali kuhusu hifadhi ya barabara, alisema upana wa hifadhi hiyo nchi nizma ilikuwa ni Mita 22 kila upande kutoka katikati ya barabara, lakini upana huo uliongezwa kufikia Mita 30 kwa Kanuni za Sheria ya barabara namba 13 ya 2007 zilipopitishwa kwa Tangazo la Serikali namba 21 la Tar 23 Januari 2009 ibara ya 29 . Na akaongeza kuwa wananchi wanaoguswa na ongezeko hilo wana haki ya kulipwa fidia.

Ibara ya 27 (2) ya Kanuni za Sheria hiyo inamtaka Waziri wa Ujenzi atakaporidhika kuwa ardhi fulani inahitajika kwa ajili ya maendeleo ya barabara atawasiliana na Wizara wa Ardhi, kwa ajili ya ardhi hiyo kuhifadhiwa. Kutokea upana wa hifadhi ya barabara kuongezwa kwa MIta 8 kupitia Kanuni za 2009, hakuna Waziri yoyote wa Ujenzi wala Mhe John Magufuli mwenyewe aliyewasiliana na Wizara ya Ardhi ili itimize wajibu wake wa kuhifadhi eneo hilo kwa mujibu wa sheria? Kitendo cha Magufuli kuwatuma wafanyakazi wa TANROAD kuweka alama ya X katika nyumba zilizoko katika upana wa MIta 8 kimekiuka sheria, tena alizojitungia mwenyewe?.

Ibara ya 27 (3 na 4 ) inamataka Waziri wa Ujenzi baada ya kufanya mawasiliano na Waziri wa Ardhi atahakiksha ananunua ardhi hiyo kutoka kwa wananchi hao. Je Mhe John Magufuli alifanya hivyo? Badala yake Mhe Magufuli alitumia ubabe na kuwatuma kwa lazima na vitisho vya kufukuzwa kazi wafanyakazi wa TANROAD kuvamia nyumba za wananchi na kuweka alama za X katika Mita 8 zilizoongezeka 2009, huku kulikuwa ni kukiuka sheria ya barabara.

Ibara ya 27 (5) inatamka kuwa baada ya siku 60 tokea wananchi kulipwa fidia Wizara wa Ujenzi kupitia TANROAD atawataka wananchi husika kuhama au kutoendeleza chochote. Je wananchi ambao nyumba zao zilizowekewa alama za X wamewahi kuarifiwa chochote na Wizara ya Ardhi, sembuese kulipwa fidia? kwakuwa wananchi walioko ndani ya Mita 8 hawajalipwa fidia hawakutakiwa kubughudhiwa kwa lolote hadi hapo watakapokuwa wamelipwa fidia. Na Magufuli anafahamu hivyo ndio maana alijibu hivyo bungeni, lakini akafanya tofauti alipotoka bungeni.

Ibara ya 27 (6) inatamka kuwa baada ya wananchi kuarifiwa kuhusu ardhi hiyo kutwaliwa na Serikali watalipwa fidia. Kwa kuwa hakuna fidia zozote zilizolipwa ndio maan Waziri Mkuu Pinda na Raisi Kikwete wakamkaripia.

Kwa hali hii ni lazima tukubaliane kuwa Mhe John Pombe Magufuli ni mbumbumbu wa sheria, aidha ameshindwa hata kutafsiri na kutekeleza sheria alizojitungua mwenyewe. Je atawezaje kutekeleza sheria zingine?

Kwa hali hiyo Mhe JohnPombe Magufuli alistahili kufukuzwa kazi kwa kukiuka sheria za barabara na kuiletea aibu serikali.

 
Jatropha ndio maana bado kwa kipimo chochote kile Magufuli hana budi kujiuzulu:

a. Kama alikuwa sahihi (kwamba yote uliyoyasema juu yake si kweli) na Rais alimtaka asiendelee namna ile alipaswa kujiuzulu
b. Kama hakuwa sahihi (kama unavyoonesha) na Rais amemuacha anaendelea na kuvuruga wizara hiyo na kutumia madaraka vibay abado alitakiwa kujiuzulu na kama kuna ushahidi mzito kushtakiwa kabisa kwa kutumia madaraka vibaya na kulisababisha taifa hasa.
 
Wakati naandika makala ambayo itatoka kwenye gazeti moja la leo kuhusu Magufuli na kwanini hana chaguo jingine lolote isipokuwa kujiuzulu nilijadiliana na ndugu yangu mmoja na tukajikuta tunakabiliwa na swali ambalo hatukuweza kulipatia jibu: Hivi nje ya madaraka Dr. Magufuli anaweza kukumbukwa vipi katika kusimamia sheria nchini na kupigania maslahi ya wananchi?

Hapa sizungumzii mambo ambayo alikuwa anauliza kama mbunge kwa ajili ya jimbo lake tu nazungumzia kitaifa ana jambo lolote ambalo tunaweza kusema alilisimamia kitaifa nje ya yale ambayo amewahi kuyafanya akiwa na madaraka?

Yawezekana ujasiri wa Magufuli hautokani na msimamo au mtazamo uliosahihi bali unatokana na kuwa na madaraka kwamba kwake madaraka na siyo kanuni ya kuongozwa na uadilifu ni chombo kwake cha kutimiza mambo mbalimbali?

Je amewahi kusimama akiwa Mbunge kuhoji na kutaja uwajibikaji wa serikali kwenye jambo gani ambalo lilikuwa na taswira au matokeo ya kitaifa?

Ni wazi kwamba amekuwa Waziri toka wakati wa Mkapa na wakati wote wa Kikwete yawezekana madaraka yamemjengea pazia ambalo ni kwa hilo tu anaweza kuonekana? Je Magufuli bila ya madaraka ni nani? Bila kuwa na cheo - yaani akiwa Mbunge wa kawaida anaweza kupigania sheria isimamiwe Bungeni bila kucompromise? Je akiwa MBunge wa kawaida yuko tayari kubanwa na mawaziri na wabunge wengine?

Katika kujitahidi kupata majibu binafsi nilifikia mahitimisho yafuatayo - mengine nimeandika kwenye makala hiyo:

a. Dr. Magufulu hawezi kuwa mpiganaji wa raslimali za taifa bila ya madaraka. Madaraka ni kinga kwake ya kuweza kufanya mambo mbalimbali.

b. Dr. Magufuli hana historia ya kujivunia ya kujitofautisha kuwa ni mtetezi wa raslimali za wananchi nje ya ofisi yake. Kwa kiasi kikubwa anakumbukwa kwa mamboa ambayo yamemjengea sifa ya kuwa ni "askari wa mwamvuli" wakati wa Mkapa lakini bila kuwa na uwaziri ni mtu ambaye yuko very docile.

Haya mawili yanajibu maswali mawili - kwa uzuri na kwa ubaya:

a. Itakuwa vigumu sana kwa Magufuli kujiuzulu on principle hasa baada ya kutofautiana na RAis na Waziri Mkuu wake na vile vile kwa viongozi hao wawili kuonesha wazi kuwa hawana imani na uwezo, nia na sababu ya maamuzi ya waziri wao. Kwa vile hawezi kukaa bila ya madaraka na kupigania anachoamini ataendelea kuwa waziri na tushangae akiwa mkimya mno kwani alichofanyiwa juzi si kidogo kwa kipimo chochote.

b. Endapo atakuja kutaka kupewa madaraka makubwa zaidi nchini; kuna watu wanaweza kujikuta wanakimbia nchi kwani ni wazi kuwa anaweza kutumia madaraka aliyonayo kufikitia masuluhisho ya mambo kadha wa kadha kuliko baadhi ya viongozi wengine ambao wamebakia kuja na sura za huruma na upole wakikwepa kusimamia sheria.

my two cents plus the other fifty

With due respect to your opinion....tunao viongozi wengi sana ambao wameshindwa kutimiza majukumu yao katika scenario zote mbili ulizo zieleza. Namaanisha wakiwa na madaraka hata bila madaraka. Kama Magufuli ameweza kutumia madaraka yake kusimamia taratibu na kanununi alizozikuta kwa ukamilifu lakini akashindwa kufanya hivyo nje ya madaraka , yeye bado ni bora sana kum-compare a na walioshindwa kote ( wakiwemo mabosi zake kikwete na Pinda).

Kwangu mimi Magufuli ni miongoni mwa viongozi wachache wa kuigwa. Kuweza kufanya vizuri katika nyanja zote mbili kama unavyotaka sikitu kidogo. Ni viongozi wachahe sana wameweza hilo, wengi walipofanya vizuri nje walipoingia katika Madaraka walizorota kabisa ( Mfano Keenja). Tumpe stahili yake, vinginevyo tutakuwa wanafki wenye kuvunja nguvu viongozi wetu wanoajitahidi kufanya kazi kwa moyo na uadilifu....

Tchao!
 
Jatropha ndio maana bado kwa kipimo chochote kile Magufuli hana budi kujiuzulu:

a. Kama alikuwa sahihi (kwamba yote uliyoyasema juu yake si kweli) na Rais alimtaka asiendelee namna ile alipaswa kujiuzulu
b. Kama hakuwa sahihi (kama unavyoonesha) na Rais amemuacha anaendelea na kuvuruga wizara hiyo na kutumia madaraka vibay abado alitakiwa kujiuzulu na kama kuna ushahidi mzito kushtakiwa kabisa kwa kutumia madaraka vibaya na kulisababisha taifa hasa.

Mkuu MMKJJ mambo mengi anayoonge Jatropha tumekwisha yaongeea na kuyarudia mara nyingi sana katika threads zilizopita, tatizo ninaloliona mimi humu JF kuna watu wa Magufuri na baadhi ya Wafanyakazi wa Wizara yake ambao labda walishauriana naye hili swala kisiasa zaidi, na sasa wanapoona kuna wataalam wanaolijua zaidi wanakimbia na hawa jibu hoja yoyote badala yake wanafungua thread mpya, wewe subiri utaona wanakimbia humu katika hii thread kabisa na wataanzisha nyingine, lakini kitu wanachotakiwa kujua ni kuwa Tanzania hivi sasa ina wataalam tena wazuri sana katika kila kona za Dunia hii, pia inaonekana hata hapo Wizarani kwao kuna wataalam wazuri ambao mawazo yao yanapuuzwa kwasababu wao hawapo katika malengo ya Magufuri ya kisiasa, nasema hivi kwasababu ukichambuwa vyema hili swala mi naona dalili ya kuwa Waziri Mkuu alitonywa na wataalam wa Wizara hiyohiyo kuwa huyu jamaa anatengeneza bomu hapa wizarani ebu zueni haraka sana!

We angalia kwa mfano walijenga Jengo la Meneja wa TANROADS kwa gharama za walipa kodi alafu anakuja kulibomoa haraka haraka kwa ajili ya sifa, lakini Mwanakijiji ukae ukijua hii yote ni kuumiza walalahoi na walipa kodi kwasababu ya uzembe wa wachache, kwanini hatujaambiwa sababu ya hasara hiyo na imetugharimu kiasi gani?, maana kama unajenga nyumba ya serikali sehemu amabayo baadae unakuja kubomoa maana yake nini? na sehemu kubwa ya ujenzi uliobomolewa pale ulifanyika Magufuri akiwa Waziri wa wizara hiyo. kwanini watanzania wasiambiwe nini kilitokea mpaka fedha za serikali zikawekezwa sehemu ambayo haiitajiki?, na waliosababisha wamechukuliwa hatua gani? Sisi tunatakushabikia kubebeshwa mzigo ambao sio wa kwetu, maana ki ukweli ubomoaji wa jengo la TANROADS ulipaswa kwenda na hatua za kinidhamu dhidi ya Muhusika aliyeleta hasara hiyo! kwani Tanzania tunashida ya ardhi kiasi cha kuingiza serikali hasara kiasi hicho? kama walijua watabomowa baadae kwanini hawakuweka majengo ya temporary kama mbao, kontena nk. Hii peke yake inatosha kutia shaka juu ya walichokuwa wanafanya maana kama lile eneo ni Right of Way na wao ndio watunzanji wa RoW ilikuwaje wajenge jengo la kudumu ndani ya RoW?! na kwa hasara ya nani?

Mambo ya kitaalam hayapaswi kufanywa kisiasa hata siku moja, watanzania tunataka wanasiasa kutatua matatizo ya kitaalam ndio maana hatuendi mbele badala yake ni kurudi nyuma kila siku.
 
Mkuu MMKJJ mambo mengi anayoonge Jatropha tumekwisha yaongeea na kuyarudia mara nyingi sana katika threads zilizopita, tatizo ninaloliona mimi humu JF kuna watu wa Magufuri na baadhi ya Wafanyakazi wa Wizara yake ambao labda walishauriana naye hili swala kisiasa zaidi, na sasa wanapoona kuna wataalam wanaolijua zaidi wanakimbia na hawa jibu hoja yoyote badala yake wanafungua thread mpya, wewe subiri utaona wanakimbia humu katika hii thread kabisa na wataanzisha nyingine, lakini kitu wanachotakiwa kujua ni kuwa Tanzania hivi sasa ina wataalam tena wazuri sana katika kila kona za Dunia hii, pia inaonekana hata hapo Wizarani kwao kuna wataalam wazuri ambao mawazo yao yanapuuzwa kwasababu wao hawapo katika malengo ya Magufuri ya kisiasa, nasema hivi kwasababu ukichambuwa vyema hili swala mi naona dalili ya kuwa Waziri Mkuu alitonywa na wataalam wa Wizara hiyohiyo kuwa huyu jamaa anatengeneza bomu hapa wizarani ebu zueni haraka sana!

We angalia kwa mfano walijenga Jengo la Meneja wa TANROADS kwa gharama za walipa kodi alafu anakuja kulibomoa haraka haraka kwa ajili ya sifa, lakini Mwanakijiji ukae ukijua hii yote ni kuumiza walalahoi na walipa kodi kwasababu ya uzembe wa wachache, kwanini hatujaambiwa sababu ya hasara hiyo na imetugharimu kiasi gani?, maana kama unajenga nyumba ya serikali sehemu amabayo baadae unakuja kubomoa maana yake nini? na sehemu kubwa ya ujenzi uliobomolewa pale ulifanyika Magufuri akiwa Waziri wa wizara hiyo. kwanini watanzania wasiambiwe nini kilitokea mpaka fedha za serikali zikawekezwa sehemu ambayo haiitajiki?, na waliosababisha wamechukuliwa hatua gani? Sisi tunatakushabikia kubebeshwa mzigo ambao sio wa kwetu, maana ki ukweli ubomoaji wa jengo la TANROADS ulipaswa kwenda na hatua za kinidhamu dhidi ya Muhusika aliyeleta hasara hiyo! kwani Tanzania tunashida ya ardhi kiasi cha kuingiza serikali hasara kiasi hicho? kama walijua watabomowa baadae kwanini hawakuweka majengo ya temporary kama mbao, kontena nk. Hii peke yake inatosha kutia shaka juu ya walichokuwa wanafanya maana kama lile eneo ni Right of Way na wao ndio watunzanji wa RoW ilikuwaje wajenge jengo la kudumu ndani ya RoW?! na kwa hasara ya nani?

Mambo ya kitaalam hayapaswi kufanywa kisiasa hata siku moja, watanzania tunataka wanasiasa kutatua matatizo ya kitaalam ndio maana hatuendi mbele badala yake ni kurudi nyuma kila siku.

FOR YOUR INFORMATION HAKUNA JENGO LOLOTE LA TANROAD LILILOBOMOLEWA, PALE UBUNGO. ZILIKUWA NI MBINU ZA MAGUFULI KUWATISHA WATU WABOMOE NYUMBA ZAO ILI AJIPATIE SIFA. KILICHOBOMOLEWA NI MAJENGO MAKUU MAKUU YALIYORITHIWA NA TANROAD KUTOKA KWA UJENZI, AMBAYO NAYO ILIYARITHI KUTOKA KWA CONTRACTOR ALIYEIFANYIA BARABARA YA DAR-MLANDIZI UKARABATI MWAKA 2001 ALIYEITWA SCANPHIL KOLAS.

hIVYO HIYO ILIKUWA NI YADI YA CONTRACTOR, HIVYO TANROAD HAIJAWAHI KUJENGA JENGO LOLOTE HAPO UBUNGO. KWA KAWAIDA CONTARACTOR HUCHAGUA MAHALI PAZURI NA KUJENGA YADI KATIKA SITE YAKE. KWA TAARIFA YAKO MARA TU BAADA YA CONTRACTOR KUKABIDHIWA KANDARASI YA BARABARA ENEO LOTE LITAKALOKUWA CHINI YA UJENZI HUITWA BUILDING SITE. HIVYO UKWELI NI KWAMBA CONTARACTOE AITWAYE SCANPHIL KOLAS ALIJENGA YADI YAKE KATIKA SITE ALIYOKUWA AKIFANYA KAZI ZA UJENZI.

BAADA YA KUKAMILISHA KAZI ZA UJENZI, NA SITE HIYO KUFUNGWA. MAJENGO, MAKONTENA NA UZIO VILIVYOKUWA VIKITUMIWA NA CONTRACTOR HUYO VILIRIITHIWA NA MHANDISI WA TANROAD PWANI NA DAR.

HIVYO HAIKUWA SAHIHI KWA MAGUFULI KULIDANGANYA TAIFA KUWA TANROAD IMEJENGA KATIKAHIFADHI YA BARABARA. ALITAKIWA KUSEMA UKWELI KUWA MAJENGO HAYO YALIKUWA NI MALI YA CONTRACTOR SCANPHIL KOLAS.
 
Wakati naandika makala ambayo itatoka kwenye gazeti moja la leo kuhusu Magufuli na kwanini hana chaguo jingine lolote isipokuwa kujiuzulu nilijadiliana na ndugu yangu mmoja na tukajikuta tunakabiliwa na swali ambalo hatukuweza kulipatia jibu: Hivi nje ya madaraka Dr. Magufuli anaweza kukumbukwa vipi katika kusimamia sheria nchini na kupigania maslahi ya wananchi?

JIBU: Kwa kumfukuza yule CEO wa TANROADS


Yawezekana ujasiri wa Magufuli hautokani na msimamo au mtazamo uliosahihi bali unatokana na kuwa na madaraka kwamba kwake madaraka na siyo kanuni ya kuongozwa na uadilifu ni chombo kwake cha kutimiza mambo mbalimbali?

JIBU:L Hapana. CEO wa TANROADS or rather chini ya uongozi wake gharama ya kutengeneza kilometa moja ilipanda hadi ilikofika leo, 1.5billion. Extra hiyo ndo mgawo kwa walomweka madarakani. Wamechukizwa na hilo na consequences, tunaziona

Je amewahi kusimama akiwa Mbunge kuhoji na kutaja uwajibikaji wa serikali kwenye jambo gani ambalo lilikuwa na taswira au matokeo ya kitaifa?

JIBU: Indirectly Mrema amekula meza moja na waliomweka pale. Mafisadi wenzake.

...
...


Katika kujitahidi kupata majibu binafsi nilifikia mahitimisho yafuatayo - mengine nimeandika kwenye makala hiyo:

a. Dr. Magufulu hawezi kuwa mpiganaji wa raslimali za taifa bila ya madaraka. Madaraka ni kinga kwake ya kuweza kufanya mambo mbalimbali.

b. Dr. Magufuli hana historia ya kujivunia ya kujitofautisha kuwa ni mtetezi wa raslimali za wananchi nje ya ofisi yake. Kwa kiasi kikubwa anakumbukwa kwa mambo ambayo yamemjengea sifa ya kuwa ni "askari wa mwamvuli" wakati wa Mkapa lakini bila kuwa na uwaziri ni mtu ambaye yuko very docile.

... Not true Sir!!

Haya mawili yanajibu maswali mawili - kwa uzuri na kwa ubaya:

a. Itakuwa vigumu sana kwa Magufuli kujiuzulu on principle hasa baada ya kutofautiana na RAis na Waziri Mkuu wake na vile vile kwa viongozi hao wawili kuonesha wazi kuwa hawana imani na uwezo, nia na sababu ya maamuzi ya waziri wao. Kwa vile hawezi kukaa bila ya madaraka na kupigania anachoamini ataendelea kuwa waziri na tushangae akiwa mkimya mno kwani alichofanyiwa juzi si kidogo kwa kipimo chochote.

JIBU: Akijiuzulu ni wazi watam-Kolimba! Hakuna ubishi kwamba he is very popular kule kanda ya ziwa. Ni asset kubwa sana. Thanks to his contributions, leo hii unachanja mbuga toka Mwanza all the way to Kampala. Lami tupu. Likewise, hadi Kigoma

b. Endapo atakuja kutaka kupewa madaraka makubwa zaidi nchini; kuna watu wanaweza kujikuta wanakimbia nchi kwani ni wazi kuwa anaweza kutumia madaraka aliyonayo kufikitia masuluhisho ya mambo kadha wa kadha kuliko baadhi ya viongozi wengine ambao wamebakia kuja na sura za huruma na upole wakikwepa kusimamia sheria.
KWELI

my two cents plus the other fifty

... kwa watafiti angalieni contract alizopewa EXIM Construction halafu jiulizeni nani OWNERS. Walewale!!! Trace na COWI pia. Connect the dots halafu mezea na hii. Ilitoka pepa ofisi ya .... kwamba Mrema aachwe ikawa too late, Magufuli alishatoa marching orders, previous Sunday. Magufuli kudhalilishwa ni pamoja na hii. Hawa mafisadi si mchezo. Tuko pabaya sana
 
Kwa hilo jamaa anaweze hata asipokuwa na uwaziri kwani tumeona kuna wabunge walikuwa wakali lkn pindi wakipewa uwaziri inakuwa kama wamezimwa, hawafanyi kitu. Huyu jamaa yuko vizuri na anasimamia sheria ila wakuu wake wameona kwa kufuata sheria basi huenda kiasiasi chama kingeenda mrama na hili ni kutokana na watendaji ndani ya serikali kutokuwa makini na majukumu yao ya kila siku, hivyo basi anachokifanya Magu ni kujitoa mhanga kwa kufanya yale ambayo wengine wameshindwa kuyafanya kwani kwa kuyatekeleza yanahatarisha na maisha ya mtu pia.
Cku zote ukifuata haki utachukiwe na wachache na kupendwa na wengi ila wanaseme ubaya unavuma kuliko wema.


Wakati naandika makala ambayo itatoka kwenye gazeti moja la leo kuhusu Magufuli na kwanini hana chaguo jingine lolote isipokuwa kujiuzulu nilijadiliana na ndugu yangu mmoja na tukajikuta tunakabiliwa na swali ambalo hatukuweza kulipatia jibu: Hivi nje ya madaraka Dr. Magufuli anaweza kukumbukwa vipi katika kusimamia sheria nchini na kupigania maslahi ya wananchi?

Hapa sizungumzii mambo ambayo alikuwa anauliza kama mbunge kwa ajili ya jimbo lake tu nazungumzia kitaifa ana jambo lolote ambalo tunaweza kusema alilisimamia kitaifa nje ya yale ambayo amewahi kuyafanya akiwa na madaraka?

Yawezekana ujasiri wa Magufuli hautokani na msimamo au mtazamo uliosahihi bali unatokana na kuwa na madaraka kwamba kwake madaraka na siyo kanuni ya kuongozwa na uadilifu ni chombo kwake cha kutimiza mambo mbalimbali?

Je amewahi kusimama akiwa Mbunge kuhoji na kutaja uwajibikaji wa serikali kwenye jambo gani ambalo lilikuwa na taswira au matokeo ya kitaifa?

Ni wazi kwamba amekuwa Waziri toka wakati wa Mkapa na wakati wote wa Kikwete yawezekana madaraka yamemjengea pazia ambalo ni kwa hilo tu anaweza kuonekana? Je Magufuli bila ya madaraka ni nani? Bila kuwa na cheo - yaani akiwa Mbunge wa kawaida anaweza kupigania sheria isimamiwe Bungeni bila kucompromise? Je akiwa MBunge wa kawaida yuko tayari kubanwa na mawaziri na wabunge wengine?

Katika kujitahidi kupata majibu binafsi nilifikia mahitimisho yafuatayo - mengine nimeandika kwenye makala hiyo:

a. Dr. Magufulu hawezi kuwa mpiganaji wa raslimali za taifa bila ya madaraka. Madaraka ni kinga kwake ya kuweza kufanya mambo mbalimbali.

b. Dr. Magufuli hana historia ya kujivunia ya kujitofautisha kuwa ni mtetezi wa raslimali za wananchi nje ya ofisi yake. Kwa kiasi kikubwa anakumbukwa kwa mamboa ambayo yamemjengea sifa ya kuwa ni "askari wa mwamvuli" wakati wa Mkapa lakini bila kuwa na uwaziri ni mtu ambaye yuko very docile.

Haya mawili yanajibu maswali mawili - kwa uzuri na kwa ubaya:

a. Itakuwa vigumu sana kwa Magufuli kujiuzulu on principle hasa baada ya kutofautiana na RAis na Waziri Mkuu wake na vile vile kwa viongozi hao wawili kuonesha wazi kuwa hawana imani na uwezo, nia na sababu ya maamuzi ya waziri wao. Kwa vile hawezi kukaa bila ya madaraka na kupigania anachoamini ataendelea kuwa waziri na tushangae akiwa mkimya mno kwani alichofanyiwa juzi si kidogo kwa kipimo chochote.

b. Endapo atakuja kutaka kupewa madaraka makubwa zaidi nchini; kuna watu wanaweza kujikuta wanakimbia nchi kwani ni wazi kuwa anaweza kutumia madaraka aliyonayo kufikitia masuluhisho ya mambo kadha wa kadha kuliko baadhi ya viongozi wengine ambao wamebakia kuja na sura za huruma na upole wakikwepa kusimamia sheria.

my two cents plus the other fifty
 
Hawezi simama peke yake bila ya uwaziri kwani hana ujasiri kama wa kina selelii, lembelii na hata akina ole sendeka ktk kusimamia maslahi ya tz ila akipewa rungu(uwaziri) utasikia wavuvi haramu, bomoabomoa, zuia magari ya serikali na mengineyo.

Mkuu hapo kwenye RED si kwamba unatoa hitimisho bila kutueleza ni kwanini?

Kumbuka;
Sifa aliyonayo Magufuli ni kuelewa kazi anayotakiwa kufanya na kuipenda kazi yake. Kama hilo ni kweli sioni kwanini asiweze kutimiza wajibu wake kama Mbunge endapo atakuwa si waziri!

TAFAKARI...!

 
Hii ni subortage vs comred Maguduli. Kwa speed aliyonayo wanafahamu jinsi itakavyokuwa vigumu kumzuia atakapojitosa kugombea urais kwani wananchi tunamkubali. Wanachofanya sasa ni kum'frustrate n kum weaken' tu ili aonekane hafai kwa wananchi. Mtoa mada anaonekana kubabaisha napata tabu kufikiria juu ya makala yake kama haitajaa ubabaishaji. Umaskini wa watz umeletwa na mafisadi, na upanuzi wa barabara ni njia muhimu wa kuinua uchumi wa watz. Huhitaji kuwa na degree kujua hii. Kejeli za jk ni muendelezo wa udhaifu alionao'inherently' n might mean is not president material.
 
FOR YOUR INFORMATION HAKUNA JENGO LOLOTE LA TANROAD LILILOBOMOLEWA, PALE UBUNGO. ZILIKUWA NI MBINU ZA MAGUFULI KUWATISHA WATU WABOMOE NYUMBA ZAO ILI AJIPATIE SIFA. KILICHOBOMOLEWA NI MAJENGO MAKUU MAKUU YALIYORITHIWA NA TANROAD KUTOKA KWA UJENZI, AMBAYO NAYO ILIYARITHI KUTOKA KWA CONTRACTOR ALIYEIFANYIA BARABARA YA DAR-MLANDIZI UKARABATI MWAKA 2001 ALIYEITWA SCANPHIL KOLAS.

hIVYO HIYO ILIKUWA NI YADI YA CONTRACTOR, HIVYO TANROAD HAIJAWAHI KUJENGA JENGO LOLOTE HAPO UBUNGO. KWA KAWAIDA CONTARACTOR HUCHAGUA MAHALI PAZURI NA KUJENGA YADI KATIKA SITE YAKE. KWA TAARIFA YAKO MARA TU BAADA YA CONTRACTOR KUKABIDHIWA KANDARASI YA BARABARA ENEO LOTE LITAKALOKUWA CHINI YA UJENZI HUITWA BUILDING SITE. HIVYO UKWELI NI KWAMBA CONTARACTOE AITWAYE SCANPHIL KOLAS ALIJENGA YADI YAKE KATIKA SITE ALIYOKUWA AKIFANYA KAZI ZA UJENZI.

BAADA YA KUKAMILISHA KAZI ZA UJENZI, NA SITE HIYO KUFUNGWA. MAJENGO, MAKONTENA NA UZIO VILIVYOKUWA VIKITUMIWA NA CONTRACTOR HUYO VILIRIITHIWA NA MHANDISI WA TANROAD PWANI NA DAR.

HIVYO HAIKUWA SAHIHI KWA MAGUFULI KULIDANGANYA TAIFA KUWA TANROAD IMEJENGA KATIKAHIFADHI YA BARABARA. ALITAKIWA KUSEMA UKWELI KUWA MAJENGO HAYO YALIKUWA NI MALI YA CONTRACTOR SCANPHIL KOLAS.

Nafahamu sana Jetropha, lakini yote ni majibu sahihi, ama akiri kuwa alidanganya kwa mujubu wa maelezo yako, au atwambie hakudangaya basi atwambie ilikuwa vipi wajenge sehemu ambayo baadaye watavunja ili kuipa serikali hasara.

Ila umenipa taarifa nyinge ambayo sikuwanayo! kuwa hakuna jengo lilibomolewa wakati alijaza TV pale konyesha kuwa anabomoa nyumba kwa kuanza na ofisi zake? huyu Mtu wa ajabu sana!

Anatakiwa ajiunge Comedy
 
Utaona kumbe hatumjadili mtu kama mtu bali mtu na kanuni inayomuongoza; ndiyo maana sijasema "Magufuli yukoje?"; swali ni Magufuli bila ya madaraka. Na utaona wachangiaji karibu wote wanachangia - ukiwemo wewe- kwa kuangalia kiongozi aitwaye magufuli akiwa na madaraka au pasi na madaraka. Huku si kumjadili mtu kama mtu.

M/Kijiji, this is too narrow to handle MM. At the end tutajikuta tuko palepale, ku-discuss mtu.
 
sn2139 - ndio maana naamini ya haya maswali na uchokozi wangu hapa.. of course tunajua mawaziri wanafanya kazi at the pleasure of the president.. kwa hiyo upande mmoja ni kuwa ili aweze kuendelea kuwa madarakani na kufanya anayotaka hana budi kulamba miguu ya bosi wake. Swali langu ambalo ndio msingi wa hoja (natumaini Waberoya naye ataliona) ni kuwa viongozi hawa wanapotofautiana hivi ni nani ajiuzulu on principle? Swali langu halihusiani na upiganaji n.k linahusu kutawala na kuwabika kama kiongozi pale tofauti za msingi zinapotokea.

Kuhusu swali lako, si Waberoya, hata mimi pia nimeliona, lakini tutakuwa tuna deal na hoja ambayo ni tricky sana kiasi kwamba uwezekano ni mkubwa kuishia kujadili mhusika zaidi kuliko swali la utawala na uwajibikaji. Hata hivyo, sio lazima kila mara njia ya kuwajibika kwa kujiuzulu ndio the only option, kuna njia zingine za ku-adjust situation na kusonga mbele.
 
Magufuli ni mnyanyasaji wa walalahoi tu ni shabiki wa mafisadi na mtumiaji mbaya wa madaraka! Bomoabomoa zisizo na fidia kwa watu waliojinyima kwa miaka nenda rudi kujenga na bila kupmiwa viwanja au kuelekezwa pa kujenga! Ni waziri gani anaweza kutoa maauzi yaszingatia akili ya kawaida kama hiyo? Kwa hilo naona bora Rostam kuliko yeye anayeua watu kwa vihoro vitokanavyo na makosa ya serikali.
Alichomea watu makokoro na nyavu watu walojinyima wakanunua bila kuwachukulia hatua wenye viwanda vya nyavu hizo, hiyo akili au matope na ubinadamu? kwani wavuvi walizipata wapi ambako magufuli hana mkono?
Uuzaji wa nyumba za serikali alosimamia halafu baadaye serikali ikaghalamika kuweka mawaziri majaji na waurugenzi wapya hotelini ni akili hizo au matope. watanzania tunajua kupngeza wasanii hata wanapotumaliza eti kwa vile kakalili kilometa za kutoka Chato hadi Chalinze mnampigia makofi! Akiwa raisi nusu yetu tutakuwa wakimbizi maana hatutaweza kutawaliwa na zoba kama huyu
 
Back
Top Bottom