Magufuli sio mtu anayefuata sheria hata kidogo, anatumia kauli mbiu ya "sheria" kujijengea umaarufu tu, kwa kuwa anafahamu watanzania wengi ni wavivu kusoma sheria hivyo wataamini kauli aake kuwa ni waziri. Mfano hai wa Magufuli kutofuata sheria na kukandamiza hali za wananchi ni case ifuatayo:- Mwaka 1999 wakati inatungwa Sheria ya Ardhi ya Vijiji ya 1999, Magufuli alikuwa miongonji mwa wabunge walioipitisha. Kifungu cha 15 cha sheria hiyo kinatamka hivi UGAWAjI WA ARDHI ULIOFANYWA KWA MTU AU KUNDI LA WATU WAISHIO AU WALIOTAKIWA KUHAMIA NA KUISHI KATIKA KIJIJI WAKATI WOWOTE KATI YA 01 JAN 1970 HADI 31 DES 1977 , KAMA UGAWAJI HUO ULIFANYWA KWA MUJIBU WA SHERIA AU KINYUME CHA SHERIA AU BILA KUZINGATIA SHERIA YOYOTE, SASA INATHIBITISHWA KUWA UGAWAJI HUO NI HALALI NA KWAMBA DAIMA NI WENYE NGUVU YA KUTOA HAKI NA WAJIBU WA KISHERIA KWA KUNDI LA WATU WALIOGAWIWA ARDHI HIYO....." Aidh Kifungu cha 16 Kinatamka .......... MASHARTI YA KIFUNGU 15 YATATUMIKA KILA MARA UGAWAJI WA ARDHI YA KIJIJI ULIPOFANYWA NA HALMASHAURI YA KIJIJI AU MAMLAKA NYINGINE YOYOTE MNAMO NA BAADA YA 01 JAN 1978 HADI TAREHE YA KUANZA KUTUMIKA KWA SHERIA HII.
Wakati wa opersheni vijiji miaka ya 1970's maenEo kati ya Ubungo hadi Kiruvia pia vilianzishwa vijiji vya Kimara, Mbezi Kibamba na Kiruvia ambavyo vilibadsilishiwa hAdhi na kuwa chini ya Mipango Miji mwaka 1985. Kwa mujibu wa vifungu vy sheria iliyotajwa hapo juu ambayo Mhe John magufuli lishiriki kuipitisha wananhci wote waliokuwa wakiishi katika vijiji hivyo hadi mwaka 1985 wana haki na ardhi wanayoimiliki na kama Serikali inaitaka ardhi hiyo ni lazima kuwalipa fidia. Kwa maneno mengine ukisoma kwa makini maneno in bold sheria feki anazotumia Magufuli za 1930's na 1967 ziliisha uhai katika maeneo yaliyokuwa vijiji vya ujamaa kutokea mwaka 1999.
Kwa kuwa Mhe John Magufuli alifahamua kuwa Serikali huchulewa kuchapa, kusambaza na kutoa elimu kwa wananchi ya sheria mbali mbali zinazopitishwa na bunge kutoakana na ukosefu wa fedha, mwaka 2000 alipochaguliwa kuwa waziri wa ujenzi kwa mara ya kwanza (ikiwa ni miezi michache baada ya kupitishwa kwa sheria hiyo) bila huruma wala ubinadamu wowote Magufuli akaagiza kupandwa kwa mawe na mabango yanayoonyesha mwisho wa hifadhi ya barabara Mita 120 kutoka katikati ya barabara ya Morogoro pande zote mbili, kati ya Ubungo hadi Kibaha. Upana halali wa hifadhi ya barabara ni Mita 22 tu. Hata kama sheria ya vijiji ilifuta hata sheria ya barabara, kama Magufuli angekuwa amedea na Upana halali wa Road Reserve wa Mita 22 pande zote mbili kidogo wananchi wangeweza kumwelewa kuwa ana nia njema.
Hivyo Magufuli alitoa maagizo na kuwatendea wananchi mambo yaliyo kinyume cha sheria ya Ardhi ya Vijiji vifungu nilivyovitaja hapo juu. Na ili kuhakikisha wananchi kati ya Ubungo hadi Kibaha wanakosa haki yao kabisa kwa ubabe wake wa kawaidia aliingia katika ardhi na makazi halalai ya wananchi chini ya sheria zilizotungwa na bunge bila ya kushirikisha ngazi za Mkoa, Wilaya, Manispaa, Tarafa, Kata wala Serikali za Mitaa na mpaka sasa hataki majadiliano ya iana yoyote yanayohusu haki za wananchi hawa. Je huu ndio mfano wa kiongozi bora mnayemtaka? Viongozi kama hawa Mwalimu Nyerere alisema hawafai hata kupewa Ujumbe wa shina.
Magufuli aliamua kuwatendea unyama huo wananchi wanaoishi kati ya Ubungo hadi Kibaha kwa kuwa alifahamu wananchi wana ufahamu mdogo wa haki zao chini ya sheria ya vijiji. Kutokana na kuwa na ufahamu mdogo wananchi wanaomiliki ardhi na makazi ndani ya eneo hilo walikaa kimya na kuathirika kijamii na kiuchumi kwa miaka 9 mpaka 2010 alipoanzsiha zoezi la kutaka kubomoa nyumba hizo kwa kisingizio cha kutekeleza mradi wa mabasi yaendayo kasi na msongamnao wa magari.
Cha ajabu upana unaohitajiwa na mradi wa mabasi yaendayo kasi hauzidi Mita 10, mfano hai ni upana ulioachwa na jengojipya la Benki ya Wananchi ya Dar es Salaam (DCB) lililojengwa hivi karibuni pale Magomeni na ukarabati wa kusogeza nyuma uizo wa Chuo cha DIT. Kwa hali hiyo, Je ni kweli nyumba zilizoko Mita 100 kutoka katikati ya barabara kati ya Ubungo hadi Kimara Magufuli alizoagizi ziweweke alama ya X na kuagiza zibomolewe zinazuia ujenzi wa barabara za mabasi yaendayo kasiau zinachanmgia vipi msongamano wa magari?
Ndio maana wakubwa wake wameagiza historia ya maeno izingatiwe na wananchi walipwe fidia kama kuna hajaya nyumba kubomolewa.
Kuhusu Magufuli kusemwa hadharani ni haki yake kwa kuwa Gazeti la Tanzania Daima liliripoti kuw kabla ya Waziri Mkuu kumsema hadharani alimwita na wakakaa mara mbili kuhusu suala hilo lakini Magufuli akakaidi na kutunga msamiati kuwa ameapa kulinda sheria. Hivuo ili kulinda haki za wananchi na kulinda serikali ili ni lazima ashughulikiwe kidogo.