Maduka ya dawa Tanzania yanatumika kutuibia, kututesa, kuharibu afya zetu na kutuua?

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Nov 28, 2013
10,129
35,143
Kwa siku za karibuni hapa JF kuna mjadala mkali sana unaendelea kuhusu taaluma ya ufamasia na maduka ya dawa hapa Tanzania. Kupitia mijadala hiyo, nimejifunza mambo kadhaa ambayo hapo kabla sikuyajua kwa kina. Nimegundua mambo haya:

1. Mtu ili kuanzisha na kuendesha biashara ya duka la dawa, huihitaji uwe ni mfamasia kitaaluma bali unahitaji kukodisha cheti cha mfamasia yoyote na kukitundika kwenye duka lako la dawa, na kuanzia hapo utauza dawa yoyote hata kama elimu yako ni darasa la saba! Hii ni sawa na rubani mwenye leseni ya kurusha ndege za abiria kuikodisha leseni yake kwa kampuni ya ndege ili itundikwe ndani ya ndege, halafu mtu yoyote anaweza kushika usukani wa ndege na kuamua kuirusha ndege!

2. Kumbe wafamasia kitaaluma hawajui (hawakufunzwa) na hawapaswi kumpima mgonjwa (examination), kugundua ugonjwa (diagnosis), kuidhinisha dawa za kutumia (Prescription) au kumtibu mgonjwa kwa dawa (drug administration). Mfamasia anapaswa tu kumgawia mgonjwa dawa (drug dispensing) kwa mujibu wa kibali cha Daktari. Ajabu ni kuwa huku mitaani maduka ya dawa ndio hospitali zisizo rasmi, tukiumwa tunaenda na pesa kwenye duka la dawa na kutibiwa faster!

3. Kiujumla karibu dawa zote hazipaswi kuuzwa na duka lolote la dawa mpaka kibali rasmi cha dawa kutoka kwa Daktari (Prescription). Ajabu ni kuwa huku mtaani dawa yoyote unaweza ukauziwa na duka lolote la dawa ukienda na pesa tu!


Baada ya kupitia hayo yote nimegundua wazi kubwa, kiujumla maduka ya dawa hapa Tanzania huenda kwa sehemu kubwa yanatuibia, kutuumiza, kuharibu afya zetu na kutuua!
 
Tuanze kwanza, kuna wangapi wameherabiwa afya na kuuwawa na hayo maduka ya dawa unayoyaongelea? Kuna takwimu zilizokusanywa? Serikali ikikurupuka na kuyabana maduka ya dawa inaweza kuleta matatizo tena haswa kwa wale watu wenye kipato cha chini. Gharama zitaongezeka kwa sababu urasimu unaongozeka.
 
Kuanzisha na kuendesha Pharmacy kisheria si rahisi kama unavyotaka kudanganya hapa , angalia Pharmacy ACT 2013 kama sikosei utajua utaratibu wake , hao wa ADDO wanaovunja sheria usiwafananishe na Pharmacy .
Kuanzisha pharmacy ni jambo moja na kuendesha pharmacy ni jambo lingine. Mimi mgonjwa ninayefika duka la dawa kununua dawa, cheti cha mfamasia kilichotundikwa kinanisaidia nini?
 
Gharama za hospital ni kubwa sana mkuu! Hadi kumuona daktari sio chini ya shilingi 5000, vipimo, foleni, na adha nyingi. Maduka ya dawa yanasaidia sana, japo wanatoa dawa kiholela ila inasaidia.
Kuna kitu kinaweza kuvuka gharama ya uhai au afya ya mtu?
Standard za msingi zinaweza zisiwe na gharama kubwa bali zinahitaji umakini tu.
 
Mengine unayotakiwa kuyajua juu ya taaluma ya ufamasia na maduka ya dawa


MAKUNDI YA DAWA ZA BINADAMU 👇👇

1. Prescription Only Medicines ..(Cheti cha daktari kinahitajika )..hizo zenye "Dose;As directed by Physician".
2. Pharmacy Only Medicines(Cheti cha daktari hakihitajiki).
3. General Sale Medicines(Cheti cha daktari hakihitajiki)..hizi utazikuta hata dukani kwa mangi/mpemba n.k. mfano DAWA TATU/ACTION/HEDEX/PANADOL & PANADOL EXTRA/GLUCOSE /COFTA/TUMBOCID/ MOSQUITO (spray and repperants),CASTROL OIL/GLYCERINE/MEDICATED SOAPS /TOOTH PASTE/CONDOMS n.k.

KUHUSU DAWA ZIAZOTOLEWA KWA CHETI CHA DAKTARI (Prescription Only Medicine);

Dawa hizi zinazotolewa kwa cheti cha daktari kwa sababu zinachukuliwa kuwa hatari ikiwa hazitatumiwa chini ya usimamizi wa mtaalamu wa afya aliyeidhinishwa.
Dawa hizo kwa ujumla zinakusudiwa kutibu matatizo makubwa zaidi ya kiafya. Hii inaweza kujumuisha kisukari, saratani,magojwa ya moyo,bakteria,virusi nk.

Baadhi ya nchi kama vile Uingereza wapo wafamasia na manesi ambao wameidhinishwa kutoa(TO PRESCRIBE) baadhi ya dawa hizo.👇👇👇👇👇Nurses and pharmacists can prescribe as effectively as doctors - NIHR Evidence
 
Gharama za hospital ni kubwa sana mkuu! Hadi kumuona daktari sio chini ya shilingi 5000, vipimo, foleni, na adha nyingi. Maduka ya dawa yanasaidia sana, japo wanatoa dawa kiholela ila inasaidia.
Inabidi kutofautisha kati ya pharmacy na duka la dawa muhimu.
Pharmacy si suala la kubandika cheti, bali ni suala la kuwa na mfamasia anayesimamia uendeshaji wa biashara ya bpharmacy husika kwa mujibu wa sheria.

Kuanzisha huduma ya pharmacy au kumiliki pharmacy si lazima uwe mfamasia, lakini ni lazima upate mfamasia atakayesimamia huduma ya hiyo pharmacy na ndiye anayewajibika kisheria kuhusu uendeshaji wa kila siku wa pharmacy husika, na ndiye atakayehakikisha kuwa pharmacy husika inafanya huduma kwa mujibu wa sheria na kwa mujibu wa taaluma ya famasia.

Maduka ya dawa muhimu huuza dawa ambazo hazihitaji cheti cha daktari na husimamiwa na wenye taaluma ya afya kama wauguzi na madaktari kwa mujibu wa sheria.

Suala la kwenda pharmacy na "kutibiwa" huko ni kinyume cha sheria. Jamii yetu inahitaji elimu sana juu ya hili. Hii ni hatari!! Hata kama hapo pharmacy kuna daktari bado si sahihi kwa daktari kutibia pale pharmacy!! Tiba hutolewa hospitalini au kwenye zahanati!!
 
Kwa siku za karibuni hapa JF kuna mjadala mkali sana unaendelea kuhusu taaluma ya ufamasia na maduka ya dawa hapa Tanzania. Kupitia mijadala hiyo, nimejifunza mambo kadhaa ambayo hapo kabla sikuyajua kwa kina. Nimegundua mambo haya:

1. Mtu ili kuanzisha na kuendesha biashara ya duka la dawa, huihitaji uwe ni mfamasia kitaaluma bali unahitaji kukodisha cheti cha mfamasia yoyote na kukitundika kwenye duka lako la dawa, na kuanzia hapo utauza dawa yoyote hata kama elimu yako ni darasa la saba! Hii ni sawa na rubani mwenye leseni ya kurusha ndege za abiria kuikodisha leseni yake kwa kampuni ya ndege ili itundikwe ndani ya ndege, halafu mtu yoyote anaweza kushika usukani wa ndege na kuamua kuirusha ndege!

2. Kumbe wafamasia kitaaluma hawajui (hawakufunzwa) na hawapaswi kumpima mgonjwa (examination), kugundua ugonjwa (diagnosis), kuidhinisha dawa za kutumia (Prescription) au kumtibu mgonjwa kwa dawa (drug administration). Mfamasia anapaswa tu kumgawia mgonjwa dawa (drug dispensing) kwa mujibu wa kibali cha Daktari. Ajabu ni kuwa huku mitaani maduka ya dawa ndio hospitali zisizo rasmi, tukiumwa tunaenda na pesa kwenye duka la dawa na kutibiwa faster!

3. Kiujumla karibu dawa zote hazipaswi kuuzwa na duka lolote la dawa mpaka kibali rasmi cha dawa kutoka kwa Daktari (Prescription). Ajabu ni kuwa huku mtaani dawa yoyote unaweza ukauziwa na duka lolote la dawa ukienda na pesa tu!


Baada ya kupitia hayo yote nimegundua wazi kubwa, kiujumla maduka ya dawa hapa Tanzania huenda kwa sehemu kubwa yanatuibia, kutuumiza, kuharibu afya zetu na kutuua!
Maumivu yakizidi kunywa sumuart!
 
Maduka ya dawa muhimu huuza dawa ambazo hazihitaji cheti cha daktari na husimamiwa na wenye taaluma ya afya kama wauguzi na madaktari kwa mujibu wa sheria.

Ilikuwa hadi wapate mafunzo ya ADDO kwanza ndipo wanaruhusiwa kuyamiliki na kuuza.

Pia watu ambao walikuwa hawana elimu ya afya walikuwa wanapatiwa mafunzo ya ADDO ya umiliki wa DLDM na walipaswa kuweka mtu anayeweza kuuza ambaye anazitambua dawa.

Sasa ADDO imesinamishwa ndio unaona kelele zote hizi.

Hata hivyo hizi kelele ni kama njia tu, agenda kubwa hapa ni suala la maslahi tu kwenye hii Business of Pharmacy. Imeonekana Wafamasia wanafaidi sana kwenye hii business yao
 
Ilikuwa hadi wapate mafunzo ya ADDO kwanza ndipo wanaruhusiwa kuyamiliki na kuuza.

Pia watu ambao walikuwa hawana elimu ya afya walikuwa wanapatiwa mafunzo ya ADDO ya umiliki wa DLDM na walipaswa kuweka mtu anayeweza kuuza ambaye anazitambua dawa.

Sasa ADDO imesinamishwa ndio unaona kelele zote hizi.

Hata hivyo hizi kelele ni kama njia tu, agenda kubwa hapa ni suala la maslahi tu kwenye hii Business of Pharmacy. Imeonekana Wafamasia wanafaidi sana kwenye hii business yao
Mkuu Kama ADDO imefutwa, vipi waliokuwa watoa dawa kwenye pharmacy na DLDM kwa kutumia cheti cha addo (yaani waliokuwa na cheti cha addo tayari na kufanyakazi kwa cheti cha addo) je wataondolewa wote au inakuwaje ?
 
Kama wenye addo wakiondolewa, vipi kwa DLDM zilizoko vijijini ni wanani wataeuhusiwa kuuza dawa humo kwwnye izo DLDM za vijijini huko.
Ilikuwa hadi wapate mafunzo ya ADDO kwanza ndipo wanaruhusiwa kuyamiliki na kuuza.

Pia watu ambao walikuwa hawana elimu ya afya walikuwa wanapatiwa mafunzo ya ADDO ya umiliki wa DLDM na walipaswa kuweka mtu anayeweza kuuza ambaye anazitambua dawa.

Sasa ADDO imesinamishwa ndio unaona kelele zote hizi.

Hata hivyo hizi kelele ni kama njia tu, agenda kubwa hapa ni suala la maslahi tu kwenye hii Business of Pharmacy. Imeonekana Wafamasia wanafaidi sana kwenye hii business yao
 
Kwa siku za karibuni hapa JF kuna mjadala mkali sana unaendelea kuhusu taaluma ya ufamasia na maduka ya dawa hapa Tanzania. Kupitia mijadala hiyo, nimejifunza mambo kadhaa ambayo hapo kabla sikuyajua kwa kina. Nimegundua mambo haya:

1. Mtu ili kuanzisha na kuendesha biashara ya duka la dawa, huihitaji uwe ni mfamasia kitaaluma bali unahitaji kukodisha cheti cha mfamasia yoyote na kukitundika kwenye duka lako la dawa, na kuanzia hapo utauza dawa yoyote hata kama elimu yako ni darasa la saba! Hii ni sawa na rubani mwenye leseni ya kurusha ndege za abiria kuikodisha leseni yake kwa kampuni ya ndege ili itundikwe ndani ya ndege, halafu mtu yoyote anaweza kushika usukani wa ndege na kuamua kuirusha ndege!

2. Kumbe wafamasia kitaaluma hawajui (hawakufunzwa) na hawapaswi kumpima mgonjwa (examination), kugundua ugonjwa (diagnosis), kuidhinisha dawa za kutumia (Prescription) au kumtibu mgonjwa kwa dawa (drug administration). Mfamasia anapaswa tu kumgawia mgonjwa dawa (drug dispensing) kwa mujibu wa kibali cha Daktari. Ajabu ni kuwa huku mitaani maduka ya dawa ndio hospitali zisizo rasmi, tukiumwa tunaenda na pesa kwenye duka la dawa na kutibiwa faster!

3. Kiujumla karibu dawa zote hazipaswi kuuzwa na duka lolote la dawa mpaka kibali rasmi cha dawa kutoka kwa Daktari (Prescription). Ajabu ni kuwa huku mtaani dawa yoyote unaweza ukauziwa na duka lolote la dawa ukienda na pesa tu!


Baada ya kupitia hayo yote nimegundua wazi kubwa, kiujumla maduka ya dawa hapa Tanzania huenda kwa sehemu kubwa yanatuibia, kutuumiza, kuharibu afya zetu na kutuua!
Mkuu naona unaibuka kama train kwa kas bila reasoning...
1.Business of a Pharmacists inaendeshwa kitaalam sana pengine kuliko biashara nyingine yeyote hapa Tz
2.Mfamasia ni msimamizi tu wa duka na mara nyingi husimamia utoaji na uendeshaj wa maduka husika
3. Watoa dawa ni wataalam wa fundi dawa wa ngaz ya diploma kuendelea..

Hiyo kuua unajitoa ufaham kama chiz tu
 
Kama wenye addo wakiondolewa, vipi kwa DLDM zilizoko vijijini ni wanani wataeuhusiwa kuuza dawa humo kwwnye izo DLDM za vijijini huko.
Kwanza tambua kuwa ADDO ilianzishwa kwa sababu Pharmaceutical Personell walikuwa wachache, kwa sasa wapo wengi. Hizo nafasi zinaenda kwa wahusika.

Angalia hata mahospitalini, manesi walikuwa wanafanya kazi pharmacy kutokana na uhaba wa watu wa famasi. Ila kwa sasa watu wa Famasi wameongezeka na ile namba ya manesi inazidi kupungua kadri wanavyostaafu(maana hawawezi kutolewa kwa nguvu) hatimaye itaisha na nafasi zichukuliwe na wahusika.
 
Kwanza tambua kuwa ADDO ilianzishwa kwa sababu Pharmaceutical Personell walikuwa wachache, kwa sasa wapo wengi. Hizo nafasi zinaenda kwa wahusika.

Angalia hata mahospitalini, manesi walikuwa wanafanya kazi pharmacy kutokana na uhaba wa watu wa famasi. Ila kwa sasa watu wa Famasi wameongezeka na ile namba ya manesi inazidi kupungua kadri wanavyostaafu(maana hawawezi kutolewa kwa nguvu) hatimaye itaisha na nafasi zichukuliwe na wahusika.
Nafikiri Good thing hata nafasi za ajira serikalini kwa kada ya pharmacist zitaongezeka sasa.
 
Gharama za hospital ni kubwa sana mkuu! Hadi kumuona daktari sio chini ya shilingi 5000, vipimo, foleni, na adha nyingi. Maduka ya dawa yanasaidia sana, japo wanatoa dawa kiholela ila inasaidia.
Ingawa sikuungi mkono kusema Maduka ya dawa yanasaidia, yanasaidia kupata short cut tuu ambayo kwa upande wa pili yaweza kuwa hatari zaidi.

Ingawa swali linabaki sasa sisi Hohe hahe tufanyeje?. maana kuna wakati Watawala wetu wanaongea na kutenda kana kwamba wao hawaamini kama Wananchi wao wengi hawana uwezo...ukifuatilia hata kauli zao ni kama hawana habari kabisa.

Miezi kadhaa iliyopita Jamaa yangu mmoja Mwanaye alipata changamoto ya kutokwa damu puani mara kwa mara mpaka akaingia uoga...alipokwenda kumuona Dokta(Mshikaji) baada ya kumsikiliza alimpa machaguo mawili kutokana na hali halisi anayoijua inayomkabili Jamaa...alimwambia kuna hizi dawa unaweza kumpatia Mwanao alafu tuendelee kumfuatilia tuone...au kama utakuwa tayari nenda pale (akataja Hospitali) kuna Mtaalamu wa Pua na Koo amuone mwanao then atakushauri...Jamaa akamuuliza Dokta ni lipi haswa wewe unashauri nifanye?....Dokta akamwambia mpeleke mwanao kwa Mtaalamu...Jamaa akaenda na huu ndio mrejesho wake:-

Kumuona Dokta akaambiwa elfu ishirini...damu ikasisimka, akauma meno akaingia mfukoni akijua ni kuingia tu na kusikiliza ushauri na kutoka.

Baada ya Mtoto kusikilizwa na kuchekiwa akaambiwa asubiri nje...akiwa nje anang'aa macho akasikia anaitwa na Nesi upande mwingine...kwenda akaambiwa inahitajika elfu sitini tumpime Mtoto...hakuamini anachokisikia....akatoa elfu sitini Mtoto akapimwa ndio wanachoita "blood clot" n.k...akarudi kwa Dokta akasomewa matokeo kisha kama mwanzo akaambiwa asubiri nje.

Kama vilevile awali akaitwa tena na Nesi, akaenda akamkuta ameshika box kadhaa za dawa anamwambia naomba laki na ishirini...Jamaa ikabidi amwambie Dada sikuwa nimejiandaa ngoja niende kwanza nyumbani alafu nitarudi....alipotoka getini hakurudi tena pale na aliambiwa ndani ya siku thelathini amrudishe tena Mtoto..na Dawa alizoandikiwa ni kama zilezile alizoshauriwa na Daktari (Mshikaji) wa kwanza tofauti zilikuwa majina tu, na hata alipokwenda Famasi wakamwambia unaweza kutumia moja kati ya hizo.

Na Famasi walipoangalia karatasi ya Dokta na kumtajia bei na kuona alivyoshtuka hawakumuacha aondoke, wakamuuliza wewe una shilingi ngapi..akataja kiasi alichobaki nacho mfukoni, wakamwambia atoe hiyo inatosha dozi ya siku mbili...hakuelewa lakini ikambidi afanye hivyo.

Kiufupi hizo ndio tiba tunazopata huku Mtaani kwetu, na kwenda mbele kwa "Wataalamu" ni kujilipua tu....kwa hiyo kufunga maduka labda mtatusaidia kukimbilia kwa kina Mwampesa, GwaJuma and co...wao Magonjwa yote wanatutibu kwa kutoa tu sadaka elfu kumi au ishirini.
 
Back
Top Bottom