Mganguzi
JF-Expert Member
- Aug 3, 2022
- 1,032
- 2,769
Ndugu zangu kuna hili janga linalowakumba wamiliki wa Maduka ya Dawa Nchini, kuna ukiritimba na unyanyasaji wa hali ya juu kwa Wafanyabiashara za Dawa! Hawa watu wanafanya biashara kama wakimbizi, ukaguzi kila siku kwa nia ya kujipatia rushwa!
Madawa yote hata yale ya kawaida ambayo tulizoea kuyakuta madukani kwa sasa yamepigwa marufuku, wanaoruhusiwa kuuza ni wamiliki wa Pharmacy kubwa tu.
Mfano dawa kama Erythromacn, Ciproxacin, Flaggy, dawa za Malaria aina zote, Doxaclin, Muvera Plus, na nyingine kibao kwa sasa haziruhusiwi kuuzwa madukani mpaka uitafute pharmacy iliko.
Kwa sisi ambao tunaishi vijijini haya maduka ndio salama yetu, pharmacy tutazikuta wapi? Ukienda hospitali hupewi dawa unaambiwa kanunue, ukienda kununua tumekatazwa kuuza dawa zote za Antibiotic.
Akina mama wanakimbizana na wakaguzi kama Traffic wa barabarani na madereva, ukaguzi umekuwa wa holela na hongo imetawala hasa mikoani kila wiki ni ukaguzi.
Ofisi ya Mfamasia Mkuu iache kunyanyasa Wafanyabiashara kwa maslahi binafsi, mnawalinda mapapa na kutafuna vidagaa, Waziri wa Afya, Waziri Ummy unataka maduka ya dawa tuuze maandazi?
Nilichogundua hapo ni Wamiliki wa pharmacy kulindwa na sio usalama wa watumiaji, pili hizo ndio dawa zinazohitajika kila siku ni watumiaji wa kawaida kwa sasa mmiliki wa Duka la Dawa hana dawa za kuuza maana zote zimepigwa marufuku.
Madawa yote hata yale ya kawaida ambayo tulizoea kuyakuta madukani kwa sasa yamepigwa marufuku, wanaoruhusiwa kuuza ni wamiliki wa Pharmacy kubwa tu.
Mfano dawa kama Erythromacn, Ciproxacin, Flaggy, dawa za Malaria aina zote, Doxaclin, Muvera Plus, na nyingine kibao kwa sasa haziruhusiwi kuuzwa madukani mpaka uitafute pharmacy iliko.
Kwa sisi ambao tunaishi vijijini haya maduka ndio salama yetu, pharmacy tutazikuta wapi? Ukienda hospitali hupewi dawa unaambiwa kanunue, ukienda kununua tumekatazwa kuuza dawa zote za Antibiotic.
Akina mama wanakimbizana na wakaguzi kama Traffic wa barabarani na madereva, ukaguzi umekuwa wa holela na hongo imetawala hasa mikoani kila wiki ni ukaguzi.
Ofisi ya Mfamasia Mkuu iache kunyanyasa Wafanyabiashara kwa maslahi binafsi, mnawalinda mapapa na kutafuna vidagaa, Waziri wa Afya, Waziri Ummy unataka maduka ya dawa tuuze maandazi?
Nilichogundua hapo ni Wamiliki wa pharmacy kulindwa na sio usalama wa watumiaji, pili hizo ndio dawa zinazohitajika kila siku ni watumiaji wa kawaida kwa sasa mmiliki wa Duka la Dawa hana dawa za kuuza maana zote zimepigwa marufuku.