Kila Mbongo
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 296
- 393
Kwamba Mabula hajawatetea kwa wanavyoondolewa?Hawa wa Mwanza nawafahamu vizuri sana. Nilikuwa mmoja wa watu waliowashauri waipigie kura CCM 2020 kwa Rais na Mbunge Mabula (tena huyu labda aanze kuaga kabisa kama suala la machinga litaendeshwa hivi). Hivyo, kwenye kampeni za 2025 usishangae wanatelekeza mikutano ya kampeni kama walivyotelekeza meza zao leo. Na sijui kama Mh. Mabula atakuwa na ubavj wa kuwashawishi tena nikifikiria kazi kubwa tuliyoifanya ya kumrudisha 2020.