Kumbukumbu ya Hayati Magufuli isiwe sikukuu ya kitaifa, ifanywe na CCM

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Feb 4, 2009
74,891
155,895
CCM IWEKE KUMBUKUMBU YA JPM NA SIO TAIFA!!!

Kuna wito unatolewa na wabunge na makada wa ccm kuwa Rais mwendazake John P. Magufuli atengewe sikukuu ya kitaifa kuenzi mchango wake kwa taifa,hoja ikiwa kwamba amefanya mambo mengi sana mazuri kiasi cha kumuwekea siku maalum ya kumkumbuka ambayo itakua sikukuu ya kitaifa Kama ilivyo siku ya Karume ama JK Nyerere,hili linapaswa kufanywa zaidi na ccm kuliko taifa zima, nitaeleza!!!

Ukiuangalia uongozi wa Magufuli unamuona mtu aliyetafuta kujijenga yeye zaidi kiutawala na kujenga zaidi chama chake (ccm) kuliko kujenga taifa, taifa sio tu nchi,taifa ni watu,nchi na vyote vilivyomo na labda unaweza kusema angeenda Mbali zaidi kujenga nchi kuliko taifa, ni falsafa pana!

Mtu anayejijenga yeye kiutawala huhakikisha anarundika madaraka mengi mikononi mwake ama kikatiba ama kwa kuvunja Katiba,huzima sauti zote mbadala ambazo zitampinga kufanikisha hilo', huzima bunge, hudhibiti mahakama,huzuia uhuru wa vyombo vya habari na kufunga midomo ya vyama pinzani na wapinzani, miaka mitano ya utawala wa JPM haya yote yakifanyika kwa ufanisi mkubwa.

JPM alijikita katika kuhakikisha ccm inakua haina mpinzani,aliapa kwa kauli zake jukwaani,alitekeleza kwa vitendo, chaguzi za serikali ya mitaa 2019 na uchaguzi mkuu 2020 ulidhihirisha kuwa hakua akitania alipojiapiza kuwa ifikapo 2020 Tanzania itakua haina chama cha upinzani, na kufuta siasa za vyama vingi Tanzania haikua agenda ya kitaifa,ilikua agenda yake binafsi, ikiinufaisha zaidi ccm kuliko kujenga utangamano wa kitaifa

JPM alikua mtetezi na mpigania ccm zaidi kuliko kuwa mjenzi wa taifa,hivyo ccm ndio waweke siku maalum ya kumkumbuka Kama wanavoikumbuka February 5 ya kila mwaka siku chama hicho kilipoundwa!!!

Kama taifa ni nchi,Watu na vyote vilivyomo basi Watu hao ni pamoja na wapinzani, Freeman Mbowe,Zitto Kabwe na wengineo.

Watu ni pamoja na wananchi wa kimara mbezi ambao nyumba zao zilibomolewa bila fidia,mamia wakiachwa bila makazi,Watu ni pamoja na wakulima wa korosho kule kusini ambao soko la zao lao tegemezi liliharibiwa baada ya JPM kuamuru korosho yote ichukuliwe na serikali,watu hao ni wakazi wa Kagera waliopata janga la tetemeko la ardhi wakaachwa bila msaada hata walipochangiwa fedha,fedha hizo zilichukuliwa na serikali ya JPM.

Vipi kuhusu wafanyabiashara ambao fedha zao zilichukuliwa kwa Nguvu benki hata waziri mteule wa fedha Mwigulu Nchemba amelazimika kushawishi Watu kurejesha imani ya kuhifadhi fedha benki,mifano ni mingi,Watu wote hawa sidhani Kama kwao JPM ni shujaa,kuulazimisha ushujaa wa JPM kwao ni kuwaonea na kuutusi ufahamu wao!

Hakuna wakati taifa limepata mpasuko na sintofaham ya kutojua kesho itakuaje Kama wakati wa JPM, hakuna wakati Tanzania imesemwa vibaya kwa ukiukwaji wa haki za kiraia katika vyombo vya kimataifa kushinda watangulizi wote kuliko wakati wa JPM.

Wale wanaotaka tuweke kumbukumbu ya kudumu juu yake nje ya kumbukumbu za jumla za kihistoria,nashauri wafanye hivyo kupitia chama tawala CCM ,chama chake alichokipigania sana,Au waanzishe klabu za kumbukumbu mitandaoni na kwingineko,wamkumbuke huko kwa furaha zao,lakini wengine tuachwe kuwakumbuka Mzee Abeid Amani Karume na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere,waasisi wa taifa letu!!!
 
Mkuu, mazuri yake na mchango wake katika maendeleo ya nchi hii vitakumbukwa siku ya mashujaa. Utitiri wa sikukuu nyingi za kumbukizi za viongozi wa kitaifa haufai kabisa. Pengine upendekeze sanamu yake iwekwe ofisi za CCM Dodoma kama ishara ya kumuenzi
Kweli kabisa huyu anatakiwa kuenziwa siku ya mashujaa, shujaa aliyetaka kuua siasa ya vyama vingi nchini
 
CCM IWEKE KUMBUKUMBU YA JPM NA SIO TAIFA!!!

Kuna wito unatolewa na wabunge na makada wa ccm kuwa Rais mwendazake John P. Magufuli atengewe sikukuu ya kitaifa kuenzi mchango wake kwa taifa,hoja ikiwa kwamba amefanya mambo mengi sana mazuri kiasi cha kumuwekea siku maalum ya kumkumbuka ambayo itakua sikukuu ya kitaifa Kama ilivyo siku ya Karume ama JK Nyerere,hili linapaswa
Mtapinga sana lakini tayari tumeshajenga Makumbusho yake hapo Chato. Hatuwasikilizi wenye vyeti fake na mafisadi tunajua aliwanyoosha sana hamuwezi kumkubali kwa kuwa aliwazuia ulaji wenu wa kiwizi.
 
CCM IWEKE KUMBUKUMBU YA JPM NA SIO TAIFA!!!

Wale wanaotaka tuweke kumbukumbu ya kudumu juu yake nje ya kumbukumbu za jumla za kihistoria,nashauri wafanye hivyo kupitia chama tawala CCM ,chama chake alichokipigania sana,Au waanzishe klabu za kumbukumbu mitandaoni na kwingineko,wamkumbuke huko kwa furaha zao,lakini wengine tuachwe kuwakumbuka Mzee Abeid Amani Karume na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere,waasisi wa taifa letu!!!
Mkuu Bujibuji Simba Nyamaume , tujifunze kudumisha Uafrika wetu na Utanzania wetu wa heshima kwa marehemu wetu!, marehemu hasemwi vibaya!. Mwacheni JPM apumzike kwa amani, na kwa taarifa yenu, kuna vitu wengi hamjui kumhusu JPM ,, saa hizi yuko na Baba yake kule kwa Baba yake!. Voices From Within: Je, wajua yuko Peponi, Mbinguni, Kwa Baba yake? Why kumshutumu, kumsakama na kumsimanga? Aachwe apumzike kwa amani

Maadam alikuwa ni kiongozi wa taifa, ikianuliwa na yeye aenziwe kwa kutengewa siku yake, then itakuwa ni siku ya kitaifa, ila tufanye kwa wote, tuanze na Mwinyi Day, Mkapa Day, Kikwete Day, tuje Magufuli Day na muda wa Samia ukiisha pia tunakuwa na Samia Day na maadhimisho ya siku hizo sio lazima ziwe ni public holiday!.
P
 
Wakifanya huu ujinga Rais Mwingine wa upinzani aje azifutilie mbali huu upuuzi..

Kuna siku ya mashujaa ilishaga puuzwa na maccm na Wala sio public holiday ila ujinga kama huu ndio wanataka uwe public holiday?
Nenda hapo Chato tayari tumeshaweka Makumbusho ya JPM. Utafika mbiguni umechoka sana kwa stress hizi za JPM na kweli aliwanyoosha mafisadi nyinyi!!!
 
Nenda hapo Chato tayari tumeshaweka Makumbusho ya JPM. Utafika mbiguni umechoka sana kwa stress hizi za JPM na kweli aliwanyoosha mafisadi nyinyi!!!
Tatizo sio kuweka makumbusho hata Mkapa ana Mkapa foundation na kila mwaka huwa legacy yake inafanyika tena sio Tanzania bali Afrika yote but hakuna cha public holiday..

Sembuse huyo zero brain ndio afanyiwe public holiday kwa kipi hasa? Umjengee kumbukumbu mwizi

Nasema hivi Rais akija mwingine atafutilia mbali huu upuuzi 👇
 

Attachments

  • Screenshot_20220716-112736.png
    Screenshot_20220716-112736.png
    145.1 KB · Views: 2
  • Screenshot_20220715-185039.png
    Screenshot_20220715-185039.png
    42.3 KB · Views: 1
  • Screenshot_20220715-184917.png
    Screenshot_20220715-184917.png
    146.9 KB · Views: 2
Hebu tueleze 1.5 trilion zilienda wapi , yule aliweza kudanganya wajinga wajinga tu kama wewe
Afadhali kuwa mjinga kuliko kuwa mpumbavu. Mjinga anaweza kufundishwa akaondoa ujinga lakini mpumbavu kama wewe hufundishiki ni sifa kama ufupi na urefu. Wewe tayari Mungu alishakupa upumbafu hivyo utakufa nao hauwezi kubadirika. Hongera kwa kuwa MPUMBAFU.
 
Back
Top Bottom