Mabere Marando ni nani?

Watu wanauliza maswali, ndipo wajibiwe, sasa wewe unauliza majibu, ujibiwe nini?. Ni wasiojua tuu ndio wanaoaminishwa kwenye ule siye yeye, na sauti sio yake, yaani mkanda ni fake, nilipowaambia ni "bonafide genuine!", wala hakurekodiwa kwa kificho!, alikuwa anajua kila kitu!, watu hamuamini!.

Ila sishangai, hata alipokuja YEYE, akawaambia wale alio waijia kuwa yeye ndiye YEYE!, hawakumwamini, na badala yake, ...
Hata ninavyowaeleza watu humu "jiwe walilolikataa waashi, litafranywa kuwa jiwe kuu la pembeni!". hamuamini!.
Nawaambia kuwa kuna kiongozi mmoja alielezewa kuwa "wewe ni mwamba, na juu ya mwamba huu, nitalijenga taifa langu!" watu hawaamini, ameufanya mioyo yao iwe migumu, ili mshuhudie utukufu wake!, aliyepo mnaemdhanie ndiye siye! na yule msiye mdhania kabisa ndiye!.
Pasco.
Pasco kwa mafumbo bwana uko vizuri sana!
 
Binafsi hupenda sana uchambuzi wa Pasco , maana huwa hauna bias zozote zaidi ya uhalisia. Japo wengi hum'beza kwa kutoendana na baadhi ya wayapendayo au wapendayo kuyasikia.
Kudos to you Pasco
Mie pia kuna wakati humvulia kofia huyu Pasco lakini haupiti muda mrefu anaweza kuja na hoja ya kufikirika hadi mtu unahisi labda kuna mtu ameiba pass word yake!
 
Kwan wewe pasco ni nani mbona wanishawishi kirahisi rahisi hv? vp naweza kukufamu live ????.......

Mtafute katika vipindi vya promo vya Shirika La Nyumba Tanzania na katika baadhi ya mifuko ya hifadhi ya jamii kama mtangazaji kwenye baadhi ya vituo vya televisheni,ni mtu mwenye kichwa kizuri tangu Ilboru na baadaye kwa kuchelewa pale UDSM, ingawa alikuwa kijana mtundu sana!
 
Mkuu, Tamim hajawahi kupindua nchi ila alishiriki katika mpango ya kupindua nchi 1982 ila haukufanikiwa. Baadhi ya wenzie Tamimi walikuwa akina Rodric Roberts, Zakaria Hans Poppe na nduguye, Hamza Kadege, Banyikwa nk.
a.k.a S. A SEIF
 
Mtafute katika vipindi vya promo vya Shirika La Nyumba Tanzania na katika baadhi ya mifuko ya hifadhi ya jamii kama mtangazaji kwenye baadhi ya vituo vya televisheni,ni mtu mwenye kichwa kizuri tangu Ilboru na baadaye kwa kuchelewa pale UDSM, ingawa alikuwa kijana mtundu sana!

mkuu unamaanisha pascal mayala?
 
Mwanasheria mkuu wa serikali mtarajiwa, atasimamia show za kuwafunga na kuwafilisi mafisadi............., mwanasheria mkongwe, jasusi mkongwe, ni product za udsm na wakina marehemu advocate maira
 
1. Alisomea sheria kwenye kile chuo cha sheria na kuhitimu mwaka ule aliohitimu.

2. Yeye kutamka hadharani kua ni mwanausalama ni athari mzuri za kisiasa ndani ya chadema kwa sababu na "rais" wa watu naye anapata ile daily S-briefing na ndio maana anashuka na nondo za kiuhakika za kufa mtu.

3. Amewahi kufikia rank juu kabisa ndani ya usalama na operesheni zote muhimu ameshiriki.

4. Mchango wake katika kuinusuru NCCR Mageuzi ni mkubwa, ila tatizo iliisha athirika beyond repair ndio maana ikasambaratisha yenyewe tuu!.

5. Uwepo wake CHADEMA ni kwa ajili ya kuuimarisha, ila ikitokea Chadema ikaathirika, beyond repair, this time atautumia uzoefu wa NCCR kuhakikisha Chadema, kamwe haiwezi kusambaratika!. itaishi milele!.
6. Mafunzo ya ujasusi aliyapatia wapi?

7. Yeye kwa ngazi aliyofikia, hawezi kuwa bado ni agent wa TISS mpaka sasa, maagent ni wale samaki wadogo wadogo, hawa wakubwa sio maajenti, hao ndio wenyewe!.

NB. Kwa wapenzi wa Chadema, ili Chadema iweze kukabidhiwa nchi mwaka 2015, kama ikishinda uchaguzi, then kwanza ni lazima Chadema kipate vetting ya TISS, hivyo Marando ni muhimu sana kwa Chadema kuliko kiongozi mwingine yoyote!. Ikulu haikabidhiwi kwa siasa za majukwaani, by voting, bali by vetting!.

Na mnaodhania ni Marando peke yake, mjinue hamjui chochote kuhusu siasa za nchi hii!, sisi tunaowaambia ukweli kuwa 2015 ni CCM tena!, mnatuchukia, na badala yake mnawapenda wale wanaowadanganya kuwa 2015 ni Chadema!.

Endeleeni kufuatilia watu!, laiti mngelijua "politics is just a game!" wala msingejisumbua kujiuliza, ila kwa vile ni kwa lengo la kufurahisha nafsi zenu, endeleeni kujifurahisheni tuu.
Pasco.

Sijawaig kuwa na shaka na maandishi yako mkuu, cdm bado iko low sehemu kubwa kukamata serikali. I wish ungeweka uzi ukalizungumzia hili ili watu waelewa wanakoelekea kwa wanaotaka na watakaopinga potezea.
 
Sijawaig kuwa na shaka na maandishi yako mkuu, cdm bado iko low sehemu kubwa kukamata serikali. I wish ungeweka uzi ukalizungumzia hili ili watu waelewa wanakoelekea kwa wanaotaka na watakaopinga potezea.

Aweke Uzi?Si ungeweka wewe halafu ukoleze kabisa na "Bonafide Genuine"?
 
may be historia ya kanchi kangu imenipiga kando.ilikuwaje hadi leo hii hawa mahaini wapo uraiani wanadunda?au ulipita msamaha wa Rais?
Huyu si ndiyo alikuwa anachampion mgomo wa mafuta? Ama hakika hakushughulikiwa ipasavyo, natumai asingekuwa na jeuri hii. Anavyoongea tu anaonekana ni MKOROFI sana na anajeuri ya FEDHA tena nina imani ni CHAFU labda hata alizopewa kuasisi mapinduzi hayo yaliyofail. Watu wa usalama na Intelijensia ya Taifa mumchunguze huyu mtu anaweza kuwa behind something
 
Inawezekana, make kama ametaja namba zote, lakini mpaka leo sijasikia mtu akitishia kwenda mahakamani. Riz1 alimtishiaka Slaa kwamba asipothibitisha yeye (riz) ni bilionea atamburuza mahakamani, kwenye hii naona hajasikia bado.
Hapo ndio pa kuanza kujiuliza,Mwanahalisi limemtaja Rama MLA VICHWA VYA MAITI limefungiwa mpaka KIAMA,Tanzania Daima limemwaga kila kitu lakini marando ndio kwanza akula bata town!
 
Mkuu,
Ahsante sana kwa ufafanuzi huu ambao unaanza kutoa mwanga juu ya huyu comrade.

Lakini je, unadhani viongozi wa juu pale Chadema hawazijui sifa za huyu mwanakondoo wao aliye na ngazi za juu pale mtaa wa Togo? Na iwapo wanamjua, je kuna makubaliano yoyote miongoni mwao au tahadhari ipo juu ya huyu kamanda kwa wenye chama?

Ila nadhani, kwa vyovyote vile iwavyo, zipo faida kwa huyu Marando kuwepo Chadema.
Hivi kwa akili yako unafikiri hawa jamaa wa masuti meusi wakitaka kitu pale CDM wanakosa?Hakuna kitu wanaachokosa pale CDM,wanapata kila kitu,nani alikuwa anajua ludovick anatumika?kaa ukijua kuwa pale ndani ya CDM kuna watu wanamahusaino mazuri tu na hawa jamaa wa makoti meusi,haiwezekani kwa taasisi kubwa kama ile ikose watu wa kuwapa taarifa za nini kinaendelea hasa kwenye Chama kikubwa kama CHADEMA,tatizo lao ni moja tu,kuwa sehemu ya magamba,kuchukua taarifa za CDM na kuwapa Magamba hilo ndio kosa,au kuwasaidia Magamba kuwamaliza CDM hapo ndipo wanapokosea,lakini hii inatokana na ushabiki na kulipa fadhila za vyeo na marupurupu wanayopata kutoka kwa magamba,njaa hizi na tamaa zinawafanya waache miiko ya kazi na wakosi kujiamini kwa kusema hiki fanyeni wenyewe (magamba) na hiki wafanye wao kama kina maslahi kwa taifa.lakini kaa ukijua hakuna kitu wasichokijua hawa jamaa,na wana watu wanashirikiana nao vizuri tu,na pia si kitu kibaya,taasisi kama ile lazima ijue,isipojua basi inakuwa imeshindwa kazi!
 
CDM fanyeni kazi,hata huyo Pasco anamumunya tu maneno,hakuna mtu anaejua utendaji wa hawa jamaa,woote tuna bahatisha tu story za hapa na pale,kikubwa huwezi kukimbia watu wa system maana "HATA MKEO ANAWEZA AKAWA NI ARGENT WA SYSTM NA USIJUE"kuwa makini endelea kuipenda CHADEMA.
 
Last edited by a moderator:
Pasco kamaliza ......Mi naamini vyama vya upinzani vimekuwa vinashinda chaguzi zote esp 1995 na 2010 lakini hawa watu wa system hawawezi kukabidhi nchi kwa watu wasiowakubali .......na kwa hili marando ni muhimu .........
 
Watu walidhani Marando zile namba kafanya kazi kubwa sana kuzipata ! Hata mimi kama TISS na nnataka namba za watu flani nampigia simu tu jamaa yangu wa makao makuu ya kampuni yoyoote ya simu na kumpa shida yangu na baada ya muda kila kitu nakipata kwakuwa hata wao TISS wana agents wao kule, ni rahisi sana mbonaa....

uwezo wako wa kufikiri ni mdogo sana
 
Kwa kukusaidia tuu, matokeo halali ni yale ya kura zilizoandikwa na sio zilizopigwa!, hata Chadema ikipata kura asilimia 95% na CCM ikapata asilimia 05%, kura zikiandikwa CCM 95%, Chadema 05%!, matokeo halali ni yanayotangazwa na sio kura zilizopigwa!. Kama vetting ikisema no Chadema, then its no Chadema, hata kama votting itaipigia kura za yes Chadema, kupitia vetting, matokeo yakayokatangwa ni yale ya karatasi!.

Pasco.

Haaa haaa....mbona 'vetting' ilisema 'No Malaika' lakini ikawa.....!
 
Back
Top Bottom