Magwangala
JF-Expert Member
- Oct 4, 2011
- 2,413
- 1,534
Pasco kwa mafumbo bwana uko vizuri sana!Watu wanauliza maswali, ndipo wajibiwe, sasa wewe unauliza majibu, ujibiwe nini?. Ni wasiojua tuu ndio wanaoaminishwa kwenye ule siye yeye, na sauti sio yake, yaani mkanda ni fake, nilipowaambia ni "bonafide genuine!", wala hakurekodiwa kwa kificho!, alikuwa anajua kila kitu!, watu hamuamini!.
Ila sishangai, hata alipokuja YEYE, akawaambia wale alio waijia kuwa yeye ndiye YEYE!, hawakumwamini, na badala yake, ...
Hata ninavyowaeleza watu humu "jiwe walilolikataa waashi, litafranywa kuwa jiwe kuu la pembeni!". hamuamini!.
Nawaambia kuwa kuna kiongozi mmoja alielezewa kuwa "wewe ni mwamba, na juu ya mwamba huu, nitalijenga taifa langu!" watu hawaamini, ameufanya mioyo yao iwe migumu, ili mshuhudie utukufu wake!, aliyepo mnaemdhanie ndiye siye! na yule msiye mdhania kabisa ndiye!.
Pasco.