Mabere Marando awania Uspika kupitia CHADEMA

Mabere Marando awania Uspika kupitia CHADEMA

Asante Rutashubanyuma, nina swali dogo.....ni kwa nini CCM wanaruhusiwa kuchagua watu watatu kugombea na upinzani wanatoa mmoja tu?

Clarification kidogo itasaidia sana kuelewa hili suala kwani nilitegemea CCM wasimamishe mtu mmoja.

Lengo ni kwa kamati ya CCM inayoundwa na wabunge kuyapunguza majina mawili na kubaki na jina moja tu..kwa kupiga kura lakini zoezi zima tayari ni uchakachuaji kwa sababu wabunge wa CCM sasa wanabanwa na mapendekezo ya CC na wao yawezekana wote hao 3 wataona hawafai lakini hawana cha kufanya...................labda ......................
 
Omarilyas sidhani kwamba ni CUF ndiyo inayoombwa bali ni wabunge wote wale wenye uzalendo na wanaotanguliza maslahi ya taifa mbele ya chama. Nina hakika kwamba ukiwaacha viongozi wachache wa CUF waliotanguliza maslahi na wako tayari kushirikiana hata na shetani kulinda maslahi hayo, wapo ambao wana mtizamo tofauti. Na sidhani kama wote ndani ya CCM watampa kura mgombea huyo Ana Makinda na hivyo hivyo kwa CUF na vyama vingine kama NCCR. Janja ya CCM ni kuwa huenda wakatumia njia za hila katika zoezi hilo kama vitisho na kura za wazi kwa nia ya kufanikisha sera yao ya uchakachuaji wa kura.

Achana na chuki zako dhidi ya Chadema.

Endeleeni kujidanganya....Hivi ni mbunge yupi wa CUF unayemjua? Hivi ni lini uliona kuna kiongozi ama mbunge wa CUF anaside tofauti na maamuzi ya Chama? Hivi unajua feelings za CUF dhidi ya Chadema katika masuala ya Ushirikiano na uhusiano wake na siasa na hisia za udini kama ilivyo kwa upande wa Chadema? Hivi chini ya uenyekiti wa Mbowe ambaye aliwahi kusema hadharani kuwa hawezi kushirikiana na CUf kwa kuwa ni chama cha udini kweli unategemea any collaboration kutoka kwa CUF? Na vipi propaganda za uchaguzi ambapo Chadema walishikilia kuwa CUF wanandoa ya kubaka demokrasia na CCM na hata kukebehi mafanikio ya CUF Zanzibar? Hivi unajua ni watu wangapi ndani ya CUF ambao walikuwa wazito serikalini na wanamjua vilivyo Mabere Marando ambao hawatakuwa tayari kuona akifanikiwa kupata nafasi hiyo?

Mazingira ya kushirikiana yanatakiwa yajengwe kabla lakini sio kutegemea sentiments na mahitaji ya muda mfupi......Kuheshimiana na kuthaminiana ni moja ya hatua muhimu ya kujenga mazingira hayo hata kama mnatofautiana lakini kama ambavyo wapambe, wafuasi na baadhi ya viongozi wa Chadema wanavyopenda kufanya.......siasa za chuki, fitina na kebehi sio siasa endelevu zinazohitajika kulikomboa taifa letu kwa maana halisi ya ukombozi (sio our turn to eat kind of Ukombozi ambao tunauona sasa)

Sichukii Chadema lakini nachukia mwenendo wao wa kukosa uthubutu wa kujisahihisha na kuharibu all the potentials walizonazo kuwa Chama Mbadala Makini mradi waweze kufanikisha matamanio ya muda mfupi kisiasa na maslahi ya Mbowe.......

Lakini pia humu ndani kuna watu wanapenda kuongozwa na emmotions zao bila hata kuthubutu kujua undani wa siasa za nchi yetu, na bahati mbaya wapo baadhi ya viongozi wa Chadema wanachukulia jukwaa hili kama uwanja wa ushauri kwao na kujikuta wanaingia mkenge kila wakati............
 
icon1.gif
Re: Mabere Marando sasa uspika wamnukia...........


ivi hakuna uwezekano wa wabunge wa ccm kukataa mapendekezo ya central committee??
Uwezekano upo lakini shida ni kuwa wengi wa wabunge wa CCM moja ya sifa ya kuteuliwa na hiyo hiyo CC ni kutokuwa na moyo wa kuthubutu................CC wakikuona ni machachari na unaweza kuwa na ushawishi mkubwa kwenye jamii watahakikisha jina lako halirudi.......................mfano ni Dr. Slaa ambavyo CC ililichakachua jina lake mwaka 1995 na kumweka Bw. Patrick Qorro ambaye walijua ni Bw. "Yes".....................Kama wabunge watatofautiana na CC na kuweka jina lao jipya kwenye nafasi ya Uspika huo utakuwa mwanzo wa ukombozi wa Bunge letu ambalo CC huliendesha kwa "remote control"........................na Bunge litaanza kujali masilahi ya raia wa kawaida wa nchi hii badala ya wale wenye kipato cha juu tu...............
 
Marando!!!!!!!!!!!!!!!! Spika wa bunge lipi. Na uchafu woooooooooote alionao leo akawe Spika. You guys are really not serious.
Tuache ushabiki wa kisiasa. Marando hana sifa za kuongoza bunge. Msitake tuanze kumuumbua hapa.
 
Maoni yangu....

quote_icon.png
Originally Posted by omarilyas
Acheni kujidanganya.

Kwanza majina hayo matatu yakitoka hapo yanakwenda katika caucas ya CCM ambapo watachangua mtu mmoja tu na ni wazi atakuwa Anna Makinda. Ukweli ni kuwa kati ya wote hao ni Anna Makinda tu mwenye uwezo, ukomavu na uhusiano mzuri na wabunge walio wengi kiasi cha kumuwezesha kushinda katika party caucus na pia bungeni

Pili, baada ya kuwatukana, kuwakejeli na kuwakashifu CUF kwa miezi yote hii na sasa mnalazimisha bingwa wa utengano katika upinzani Mbowe kuwa kiongozi wa upinzani bado mnajidanganya kuwa CUF hao hao ndio watakaowabebea mgombea wa wenu..Marando?

Acheni siasa za kujidanganya...

Majibu yako.....

Cjui ni lini hawa watu wenye siasa za kihafidhina za nchi za jangwani wataelimika na kuona siasa na utumishi wa wananchi na si uhasama wa kidini na ukanda. Utakuta kanda zao ndo zinapigwa umaskini wa kufa mtu lakini hawajifunzi. Wanajilipua mabomu na kuachwa wanaungua wenyewe huku wengine wakiendelea na maisha lakini hawajifunzi. Amkeni ndugu zangu tunataka Spika mzuri, Spika wa upinzani atakuwa wa watanzania wote kwa faida yetu sote. Spika huyo atfaidisha tanzania wote wakiwepo CCM, CHADEMA, CUF na wote watanznia wasokuwa na vyama.

Sasa kwa mtazamo kama huu sijui nani mwenye sentiments za udini kati yako na mimi?
 
Uwezekano upo lakini shida ni kuwa wengi wa wabunge wa CCM moja ya sifa ya kuteuliwa na hiyo hiyo CC ni kutokuwa na moyo wa kuthubutu................CC wakikuona ni machachari na unaweza kuwa na ushawishi mkubwa kwenye jamii watahakikisha jina lako halirudi.......................mfano ni Dr. Slaa ambavyo CC ililichakachua jina lake mwaka 1995 na kumweka Bw. Patrick Qorro ambaye walijua ni Bw. "Yes".....................Kama wabunge watatofautiana na CC na kuweka jina lao jipya kwenye nafasi ya Uspika huo utakuwa mwanzo wa ukombozi wa Bunge letu ambalo CC huliendesha kwa "remote control"........................na Bunge litaanza kujali masilahi ya raia wa kawaida wa nchi hii badala ya wale wenye kipato cha juu tu...............

Angalao wao wanaita CC na kujadiliana na sio wengine wanageuza Secretariat kuwa kikao cha maamuzi na sio utekelezaji tu kama ambavyo katiba ya chama chao inavyosema....
 
Nategemea kura sita,mkewe Anna Kilango,Mwakyembe zitaenda kwa Marando
 
Endeleeni kujidanganya....Hivi ni mbunge yupi wa CUF unayemjua? Hivi ni lini uliona kuna kiongozi ama mbunge wa CUF anaside tofauti na maamuzi ya Chama? Hivi unajua feelings za CUF dhidi ya Chadema katika masuala ya Ushirikiano na uhusiano wake na siasa na hisia za udini kama ilivyo kwa upande wa Chadema? Hivi chini ya uenyekiti wa Mbowe ambaye aliwahi kusema hadharani kuwa hawezi kushirikiana na CUf kwa kuwa ni chama cha udini kweli unategemea any collaboration kutoka kwa CUF? Na vipi propaganda za uchaguzi ambapo Chadema walishikilia kuwa CUF wanandoa ya kubaka demokrasia na CCM na hata kukebehi mafanikio ya CUF Zanzibar? Hivi unajua ni watu wangapi ndani ya CUF ambao walikuwa wazito serikalini na wanamjua vilivyo Mabere Marando ambao hawatakuwa tayari kuona akifanikiwa kupata nafasi hiyo?

Mazingira ya kushirikiana yanatakiwa yajengwe kabla lakini sio kutegemea sentiments na mahitaji ya muda mfupi......Kuheshimiana na kuthaminiana ni moja ya hatua muhimu ya kujenga mazingira hayo hata kama mnatofautiana lakini kama ambavyo wapambe, wafuasi na baadhi ya viongozi wa Chadema wanavyopenda kufanya.......siasa za chuki, fitina na kebehi sio siasa endelevu zinazohitajika kulikomboa taifa letu kwa maana halisi ya ukombozi (sio our turn to eat kind of Ukombozi ambao tunauona sasa)

Sichukii Chadema lakini nachukia mwenendo wao wa kukosa uthubutu wa kujisahihisha na kuharibu all the potentials walizonazo kuwa Chama Mbadala Makini mradi waweze kufanikisha matamanio ya muda mfupi kisiasa na maslahi ya Mbowe.......

Lakini pia humu ndani kuna watu wanapenda kuongozwa na emmotions zao bila hata kuthubutu kujua undani wa siasa za nchi yetu, na bahati mbaya wapo baadhi ya viongozi wa Chadema wanachukulia jukwaa hili kama uwanja wa ushauri kwao na kujikuta wanaingia mkenge kila wakati............
The answer is simple no permanent enemy in politics nani alitegemea CUF na CCM waongee lugha moja kule Zanzibar.
 
'juock ping' ( mabere marando) anachukua kiti
 
Ndg Ruta uliyosema ni kweli kabisa hawa watu wameisha poteza dira, sasa wangoje hukumu ya wabunge vijana, bila kujali vyama vyao. Na hao wabunge pia wasitungushe sisi tulio wachagua, vita ya ufisadi haitazimwa mpaka kieleweke, kumekucha! Aluta continua.
 
Ushabiki ni kitu hatari sana. Watu wanaacha kutumia akili zao walizopewa na Allah kwa sababu ya ushabiki. Mabere Marando of all the people mnataka awe speaker. Dude's client is Jitu Patel for effin sake. He destroyed NCCR Mageuzi. He has no spine, whose political affiliations changes with the current upepo wa siasa.

Also, unafiki wenu utawasuta. CCM used kura za maoni kuchukua wagombea wa ubunge, you guys went behind closed doors. CCM used central committee kuchuja maspika, nyie mmetuletea jina tu la Mabere Marando hata hatujui kapitaje. CCM is more democratic than chama chenu cha kizushi. Ila kwa ushabiki wenu mmekuwa vipofu wa kujadili and you just hate, hate, and hate.

You used to hate on CUF, and now you want their votes. wtf? mmeshatuona sie waTanzania wapumbavu eeh?


nenda ukalale wewe!

nani alikwambia kwenye siasa kuna uadui wa milele wewe?
 
Kila mtu atakubaliana na mimi kuwa Bunge hili la 10 litakuwa ni moto na lenye changamoto za kila aina baada ya upande wa Upinzani kuingiza Wabunge wengi zaidi kuliko wakti wowote tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi. Kwa maana hiyo basi Bunge hili linahitaji Spika makini,asiye na tuhuma yoyote,msomi na anayejua sheria na taratibu zote za kusimamia na kuendesha Bunge.

Kwa vile CCM wamemng'oa Samwel Sitta ambaye ndiye angeweza kulimudu Bunge hili kwa kisingizio cha kuweka Mwanamke awe Spika kwa mara ya kwanza tangu tupate uhuru basi Upinzani utakuwa umepata nafasi nzuri ya kuchukua kiti hicho kupitia Mhe. Mabere Marando wa CHADEMA.



Nina sababu kuu 4 za kutaka Mabere Marando apewe kiti hicho:
  1. Kwa vile Rais Kikwete kwenye hotuba yake baada ya kuapishwa alisema kwamba HAKUNA ALIYESHINDA BAALI NI WATANZANIA WOTE TUMESHINDA na akaahidi kuanza kutibu majeraha yaliyotokana na kampeni za Uchaguzi basi huu ni wakti wa kuonyesha hiyo DHAMIRA. Kuwa CHADEMA ambao wameporwa USHINDI WAO MEZANI WAPEWE KITI CHA USIPIKA ili kutibu majeraha yaliyosababishwa na harakati za Uchaguzi.
  2. Kwa vile Bunge la hili la 10 litakuwa la moto na Changamoto za kila aina inatakiwa Spika makini,mwenye msimamo na asiyeyumbishwa na hoja ya namna yoyote. Kwa vile CCM wameweka MWANAMKE nachelea sana kama ataweza KUKABILIANA NA MIKIKIMIKIKI ya Bunge la 10. Kweli wanawake wanaweza siyo sehemu zote na mambo yote!Niwaulize CCM mbona hawajawahi kuweka Rais Mwanamke, IGP mwanamke,Mkuu wa JWTZ mwanamke au Jaji Mkuu. Kwanini iwe kwa Spika tena kwa Bunge hili?Hapa CCM wameamua kumkomoa Sitta kiujanjaujanja. Ukweli ni kwamba Mwanamke hataliweza hili Bunge. Sana sana atakuwa anaongozwa kwa REMOTE CONTROL na MAFISADI waliosuka huu mpango wa kumng'oa Sitta. Nahofia kuwa tutashuhudia vilio vya Spika mwanamke na malalamiko ya kuburuzwa na kuonewa. Hivyo Mabere Marando anafaa.
  3. Kwa vile tayari ndani ya CCM kuna mgawanyiko au Makundi yaliyosabaishwa na Chenge na Sitta haitakuwa busara kuchagua Spika kutoka ndani ya CCM kwa vile kutaendeleza mgawanyiko uleule maana hata hawa wanawake wa CCM wana makundi yao. Nawaomba Wabunge wa CCM wampigie Kura mgombea wa CHADEMA Mhe. Marando kwa nafasi ya SPIKA na naibu wa Spika wampe huyo wa CCM bila kujali kama atakuwa mwanamme au mwanamke ili ku-neutralise situation.
  4. CCM wenyewe wanajua kabisa wakti wa Spika Sitta kulikuwa na mijadala na Miswada ambayo ilikuwa inaahirishwa kama Sitta amesafiri nje ya Bunge mpaka anaporudi mfano ni mjadala wa Richmond, Anne Makinda hakuweza kuuendesha mpaka Sitta alipokuwepo. Hii ina maana kwamba CCM wanajua mwanamke hawezi kumudu kusimamia mijadala mijadala na hoja nzito za Bunge.
Nahitimisha kwa kusema kuwa safari hii Spika atoke upinzani kwa sababu kuu nilizozitaja hapo juu. Kama CCM watalazimisha mwanamke wao apite whether atakuwa Anne Makinda,Anne Abdulla au Kate Kamba wajue kabisa ITAFIKIA SIKU WABUNGE WATAPIGA KURA YA KUTOKUWA NA IMANI NA SPIKA WA BUNGE KWA KUSHINDWA KUSIMAMIA BUNGE KWA KUTOKUWA NA MSIMAMO.

Hii ndiyo picha ninayoiona.
 
What the hell, Hivi Mabere Marando si ndio wakili wa Valambhia ambaye pamoja na yule haramia wa Ireland waliingiza mkenge serikali katika manunuzi ya silaha miaka ya themanini na sasa wanapigania kulipwa zaidi ya bilioni hamsini kutoka katika hazina yetu na yeye Marando anawazuia wanafamilia wa Valambhia kusettle case for 3 Bilion ili yeye na wenzake wa BOT waendelee kula malipo ya uwakili?


This is too much............
 
Wabunge wa CCM, kama mnataka ukombozi, na mtaji wa kurudi 2015, basi kataeni kuburuzwa na kamati, sijui kamata kuu ya chama. Wekeni spika wa upinzani! Mtakuwa huru!
 
Acheni kujidanganya.

Kwanza majina hayo matatu yakitoka hapo yanakwenda katika caucas ya CCM ambapo watachangua mtu mmoja tu na ni wazi atakuwa Anna Makinda. Ukweli ni kuwa kati ya wote hao ni Anna Makinda tu mwenye uwezo, ukomavu na uhusiano mzuri na wabunge walio wengi kiasi cha kumuwezesha kushinda katika party caucus na pia bungeni

Pili, baada ya kuwatukana, kuwakejeli na kuwakashifu CUF kwa miezi yote hii na sasa mnalazimisha bingwa wa utengano katika upinzani Mbowe kuwa kiongozi wa upinzani bado mnajidanganya kuwa CUF hao hao ndio watakaowabebea mgombea wa wenu..Marando?

Acheni siasa za kujidanganya...

Mkuu hapo umenena Marando hana nafasi kabisa bora angegombea ubunge jimbo la Rorya ningemwelewa kidogo Uspika ni ndoto za mchana.
 
Baada ya CC ya CCM kujitwanga risasi ya begani kufuatia uteuzi wa wanawake wanaofahamika kwa udhaifu wa kutopambana na ufisadi...........nyota ya gwiji wa kupambana na ufisadi Mheshimiwa Mabere Marando yaelekea kuwa na mvuto mkali kwenye kinyang'anyiro hicho.............

Ikumbukwe Marando aliwahi kuwa Mbunge wa Afrika Mashariki na wabunge wa CCM walimwona ndiye anayefaa kuiwakilisha kambi ya upinzani...........

Wabunge karibu wote wa upinzani watamchagua Marando na wabunge vijana wa CCM wanatarajiwa kufanya hivyo kwa nia ya kutuma ujumbe mzito kwa wapigakura bunge hili halitaki utani na ufisadi kama CC ilivyojidhalilisha............

Mheshimiwa Anna Makinda pamoja na kuwa alikuwa Naibu Spika lakini anafahamika kwa kuvunja mijadala mizito ndani ya bunge hilo..................kwa visingizio vya kanuni za bunge au maswali kutoka nje ya sera husika................wabunge wengi hawampendi kwa sababu ya kuliendesha bunge hilo kwa ridhaa yake binafsi au kuwafurahisha wanamtandao..................Ikumbukwe mwaka 1995 alikuwa Mwenyekitebe wa Kampeni za JK na jina lake lilikuwa linatajwa kuwa angelikuwa PM....................yawezekana hizi sasa ni wakati wa kulipwa fadhila ............

Anna Abdallah ni mkongwe wa siasa lakini wengi wanamwona hana upeo wa kuhimili matarajio ya wapigakura wa Karne hii ya 21..........Hivyo hauziki hata kidogo........

Kate Kamba ni msomi mzuri lakini katika Ukatibu Mkuu wake wa UWT hajawahi kupambana na ufisadi au hata kuukemea na hivyo si jemedari wa kutumainiwa..........................

Kama nia ilikuwa ni wanawake mbona mpambanaji mzuri wa ufisadi Mheshimiwa Anne Kilango mbona kaachwa?

Sababu nzito ya wabunge wa CCM kuyakataa mapendekezo ya CC ni kupinga udikteta wa wazi wa kugeuzwa mhuri kwa wabunge wa CCM.................ungelitegemea CC ya Karne ya 21 kuwaachia wabunge wenyewe wajichagulie wampendaye lakini hizi mbeleko za hao akina mama zina lenga kudhoofisha vita dhidi ya ufisadi na huu ni uthibitisho mwingine JK ni kinara wa ufisadi hapa nchini na kamwe tusimtegemee kuutokomeza................
Kwani Anne kilango alikuwa kwenye kinyang'anyiro cha kugombea Uspika wa bunge?
 
Kila mtu atakubaliana na mimi kuwa Bunge hili la 10 litakuwa ni moto na lenye changamoto za kila aina baada ya upande wa Upinzani kuingiza Wabunge wengi zaidi kuliko wakti wowote tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi. Kwa maana hiyo basi Bunge hili linahitaji Spika makini,asiye na tuhuma yoyote,msomi na anayejua sheria na taratibu zote za kusimamia na kuendesha Bunge.

Kwa vile CCM wamemng'oa Samwel Sitta ambaye ndiye angeweza kulimudu Bunge hili kwa kisingizio cha kuweka Mwanamke awe Spika kwa mara ya kwanza tangu tupate uhuru basi Upinzani utakuwa umepata nafasi nzuri ya kuchukua kiti hicho kupitia Mhe. Mabere Marando wa CHADEMA.



Nina sababu kuu 4 za kutaka Mabere Marando apewe kiti hicho:
  1. Kwa vile Rais Kikwete kwenye hotuba yake baada ya kuapishwa alisema kwamba HAKUNA ALIYESHINDA BAALI NI WATANZANIA WOTE TUMESHINDA na akaahidi kuanza kutibu majeraha yaliyotokana na kampeni za Uchaguzi basi huu ni wakti wa kuonyesha hiyo DHAMIRA. Kuwa CHADEMA ambao wameporwa USHINDI WAO MEZANI WAPEWE KITI CHA USIPIKA ili kutibu majeraha yaliyosababishwa na harakati za Uchaguzi.
  2. Kwa vile Bunge la hili la 10 litakuwa la moto na Changamoto za kila aina inatakiwa Spika makini,mwenye msimamo na asiyeyumbishwa na hoja ya namna yoyote. Kwa vile CCM wameweka MWANAMKE nachelea sana kama ataweza KUKABILIANA NA MIKIKIMIKIKI ya Bunge la 10. Kweli wanawake wanaweza siyo sehemu zote na mambo yote!Niwaulize CCM mbona hawajawahi kuweka Rais Mwanamke, IGP mwanamke,Mkuu wa JWTZ mwanamke au Jaji Mkuu. Kwanini iwe kwa Spika tena kwa Bunge hili?Hapa CCM wameamua kumkomoa Sitta kiujanjaujanja. Ukweli ni kwamba Mwanamke hataliweza hili Bunge. Sana sana atakuwa anaongozwa kwa REMOTE CONTROL na MAFISADI waliosuka huu mpango wa kumng'oa Sitta. Nahofia kuwa tutashuhudia vilio vya Spika mwanamke na malalamiko ya kuburuzwa na kuonewa. Hivyo Mabere Marando anafaa.
  3. Kwa vile tayari ndani ya CCM kuna mgawanyiko au Makundi yaliyosabaishwa na Chenge na Sitta haitakuwa busara kuchagua Spika kutoka ndani ya CCM kwa vile kutaendeleza mgawanyiko uleule maana hata hawa wanawake wa CCM wana makundi yao. Nawaomba Wabunge wa CCM wampigie Kura mgombea wa CHADEMA Mhe. Marando kwa nafasi ya SPIKA na naibu wa Spika wampe huyo wa CCM bila kujali kama atakuwa mwanamme au mwanamke ili ku-neutralise situation.
  4. CCM wenyewe wanajua kabisa wakti wa Spika Sitta kulikuwa na mijadala na Miswada ambayo ilikuwa inaahirishwa kama Sitta amesafiri nje ya Bunge mpaka anaporudi mfano ni mjadala wa Richmond, Anne Makinda hakuweza kuuendesha mpaka Sitta alipokuwepo. Hii ina maana kwamba CCM wanajua mwanamke hawezi kumudu kusimamia mijadala mijadala na hoja nzito za Bunge.
Nahitimisha kwa kusema kuwa safari hii Spika atoke upinzani kwa sababu kuu nilizozitaja hapo juu. Kama CCM watalazimisha mwanamke wao apite whether atakuwa Anne Makinda,Anne Abdulla au Kate Kamba wajue kabisa ITAFIKIA SIKU WABUNGE WATAPIGA KURA YA KUTOKUWA NA IMANI NA SPIKA WA BUNGE KWA KUSHINDWA KUSIMAMIA BUNGE KWA KUTOKUWA NA MSIMAMO.

Hii ndiyo picha ninayoiona.

tatizo marando ni kuwa katika pande mbili moja ni uspika na knyingine ni kataasisi ka serikali ka kujificha, vikazi hivi vya taasisi ya kujificha vinamaslahi makubwa na vinaondoa uhuru wa mtu
 
Back
Top Bottom