Maandamano makubwa Songea!

Maandamano makubwa Songea!

Kweli hiiiiiiiiii ni hali zaidi,nguvu zaidi,na kasi mpya ya wanaccm kwa kuua raia wasio kuwa na hatia.
Kumbuka Waziri wa Mambo ya ndani Mheshimiwa Shamsa Vuai Nahodha na MHESHIMIWA KAGASHEKI pamoja na Mkuu wa POLISI Saidi Mwema !!!! Tafadhari Wakuu mawaziri shuka huko Ruvuma kabla watu hawajamalizana na Polisi!!!!!!!! Kwani watu wakiandamana kama Senegal wakatoa duku duku lao inakuwaje, kwani lazima wazimwe kwa risasi?????

 
kutokana na ufirauni wa ccm,sasa ya leo songea ni CV jingine kujiongezea,washeni helcopa yenu sasa na paeni to Songea faster,we Zitto kabwe mpigie Mdee na mnyika.

Aaah wapi, humpati mtu hapo. Chadema itakwenda Songea kwa wakati muafaka, si kama unavyofikiria na kutaka wewe.
 
viongozi+wetu.jpg


wapiga kura wenu wanakufa mpo wapi nyie?
Mheshimiwa Nchimbi na Jenesta Mhagama si mumshinikize Shamsa Vuai Nahodha atelemke Ruvuma, au kwa vile Songea sio watu????? Mwishowe mtalazimisha watu watengeneze mabomu ya kienyeji sijui mtawazui vipi moto ukiwaka?????

 
Jambo ambalo badi sijaelewa ni kwa nini polisi wa Tanzania wanatumia silaha za moto? Na kwa nini wanawatanya watu badala ya kusikiliza? Kama wana uwezo wa kutawanya watu na hata kuua raia wasio na hatia kwa nini washinde kuwakamata majambazi?
 
Hakuna asiyejua,alieidhinisha mauaji haya nchi nzima ni Amiri Jeshi Mkuu,Mh Jakaya Mrisho Kikwete,hana huruma na wananchi wake,anaruhusu mauaji ili wananchi wasidai haki zao,anawatisha wanachi wanapokuwa mikono mitupu bila silaha wakionyesha kuto kuridhishwa na utendaji wa serikali yake,watoto,vijana,wanawake wanaume,wanauawa kila siku kwenye nchi hii bila hatua yeyote

Damu ya hawa wazalendo wa kweli ambao wamekataa kuingia msituni na kushika bunduki,ambao wanaonyesha kutokuridhishwa kwa njia ya wazi,ambao hawajavunja sheria yeyote ya nchi iko mbele ya uso ya mheshimiwa sana Raisi wa nchi hii majibu ya dhuluma anayowafanyia wananchi atakuja kuyapata kabla hajaondoka 2015
Poleni wana Songea ,Majonzi yenu,vilio vyenu,damu yenu itafungua mlango wa haki ,karibuni ,mungu awape ujasiri mukatae kuonea na kunyanyaswa na Jeshi la Polisi lililoagizwa kuua raia wasio na hatia na Kikwete
Atakwenda kwenye misiba Ruvuma sijui atahudhuria mingapi, mzee wa sanaa!!!!!

 
Picha ziko kwenye hii blog,songeayetu.blogspot.com nashindwa kuzi upload anayeweza afanye hivyoo!!!!!!!!!!!!!!!!!

Mwandishi wa TBC akiwa anajihami na risasi za polisi



Mmoja kati ya waliouawa na polisi










Polisi wakifyatua risasi kwa raia





Dimbwi la damu














picha na habari zaidi zitawajia soon!​
 
Ni takribani wiki 2 sasa mji wa SONGEA umekumbwa na MAUAJI ambayo chanzo chake haijulikani kuwa ni kwa ajili ya nini.
Mahojiano na RPC kweny vyombo vya habari siku za nyuma alisema mauaji hayo unasababishwa na wivu wa kimapenzi,na si wananchi wengi ambaowameuwawa.Taarifa hiyo ILIKANUSHWA VIKALI NA WANANCHI kwa kuwa kuna wanafunzi wengine wadogo kabis wameuwawa ambao kwa umri wao,hawajaanza kuwa na mahusiano.

Takribani zaidi ya watu kumi wameuwawa ktk mikasa hiyo na jeshi la police halijachukua hatua yoyote.....

Kwa takribani muda wa siku saba kila siku mtu mmoja alikuwa anauwawa,juzi waliuwa,jana wameua,leo wameuwa,Hivyo wanchi wamechoka kwa mauaji hayo na wananchi wameamua kuandamana kulikumbusha jeshi la polise wjibu wake,hata hivyo wakati maandamano yanaendelea kuna mtu mwingine alimenusurika kuuwawa maeneo ya RUHWIKO kw kuokolea na mpita njia ambaye alikuja kutoa taarifa kwa RAIA WEMA na kuanza kuwafuatilia watu hao ambao wlishtukia na kukimbia. kuna taarifa raia zaidi ya 2 wameuwawa kwenye maandamano hay na wengine wengi wemejeruhiwa na risasi
A%20S%20465.gif
 
Hali ni tete hapa songea polisi imejeruhi watu na sita nimeshuhudia wakiwa wamekufa ni hali ngumu sana kwani ni mabomu na risasi ndo zinarindima kuzuia maandamano ya wananchi wanaolitaka jeshi la polisi kuwajibika kwa vifo vya raia vinavyofanywa na kundi la siri toka msumbiji!

tupe habari vizuri nini tatizo imekuwaje hadi kufukia hali hiyo?
 
Saa 9.40 alasiri hii kidogo kumetulia, asubuhi kulikuwa hakufai wachache saa hii wanafungua maduka yao. Asubuhi ilikuwa kama usiku kwamba maduka yote, stand, soko kuu vilifungwa. Maandamano yalikuwa ya bodaboda na raia wengine kwenda kwa mkuu wa wilaya na hapo ndipo ilitokea patashika kubwa hadi risasi za moto zikatumika na watu wawili wakapoteza maisha. wanaofanya kazi karibu na maeneo hayo waliamriwa wakae ndani ya ofisi zao japo athari ya mabomu hayo iliwakumba. Askari walipiga marufuku mkusanyiko wowote wa watu zaidi ya watatu na wakiwaona walirusha bomu. Kwa muda kama masaa matatu hivi milio ya mabomu ilitawala mji wa songea kila upande hasa zaidi mtaa wa Lizaboni. Kilio kikubwa cha wengi ni hatua hafifu zinazochukuliwa na jeshi la polisi kudhibiti mauaji yanayoendelea hapa mjini. Mbaya zaidi kilichowaudhi wananchi wengi ni kauli aliyoitoa kamanda wa polisi wa mkoa kudharua mauaji yanayoendelea. Hadi naandika habari hii mitaani kote askari wanakatishakatisha
Nionavyo mimi kuna haja jeshi letu la polisi lijifunze hata kwa kuangalia jinsi nchi zingine zinavyoweza kudhibiti maandamano ya wananchi hasa wanapokuwa hawana silaha yeyote. Ni aibu kudhibiti idadi ndogo ya waandamanaji kama waliokuwapo hapa songea leo kwa nguvu kubwa namna hii na kuuwa raia asiye na silaha yeyote.
 
Back
Top Bottom