Maandamano makubwa Songea!

Maandamano makubwa Songea!

Mkanganyiko wa aina yake uko kwenye taarifa
zenyewe kuhusu idadi sahihi ya majeruhi na wale waliokufa huko mkoani Songea.Kulingana na gazeti la Mwananchi:
1.Polisi inasema waliokufa ni wawili na majeruhi
ni 10.
2.Uongozi wa hospitali ya mkoa umesema
umepokea maiti 4 na majeruhi 41 wawili kati ya
hawa majeruhi wakipelekwa chumba cha
upasuaji kutokana na kuwa na majeraha ya
risasi.
3.Ofisi ya Mkuu wa Mkoa inasema waliokufa ni wawili na majeruhi 20.
Kwa kawaida ukipata taarifa za ''casualties''
kwenye maafa yeyote hasa yanayoweza kuitia
serikali matatani(RC ndiye mwakilishi wa serikali
hapo) zidisha mara 2 angalau utakuwa umefikia kwenye idadi kamili.

My take:
Mfumo wa kushughulikia maandamano ya
wananchi na namna ya utoaji taarifa juu ya maafa ya kizembe yanayotokea unahatarisha the so called ''amani nchini''.
Yaliyotokea Zanzibar kipindi cha Mkapa hasa ule wakati wa uchaguzi yana nafasi kubwa ya
kujirudia tena lakini sasa kwa kiwango kikubwa
hapa Tanzania Bara kwenye uchaguzi ujao.
Kama Jeshi la Polisi limeshindwa kushughulika
vizuri na idadi ndogo ya watu katika sehemu tu
ya mkoa wa Songea pata picha machafuko yakiwa katika kiwango cha kitaifa.
''Massacre in the making''

Napenda kuwapa pole wakazi wa Songea waliofikwa na huu unyama wa Polisi na wale waliofiwa ndugu na wapendwa wao.
 
HUU ITAKUWA NI MGOMO WA POLISI KWANI POLISI WANAGOMAJE AAAT!a
 
Hayo ndo mafunzo ya polisi wale wasiokua na kazi (FFU)waliyopata pale ccp moshi tuwalaumu wale waliowapa mafunzo huenda ndo waliwaelekeza njia ya kuzima maandamo ya raia wasiokua na silaha ni kutumia silaha za moto tu
Mi napendekeza hawa askari wasiokua na kazi (FFU) wawawepeleke somalia wakambanane na Al shabab maana hapa bongo hakuna kazi ya kuwapa

Ndugu yangu;

Jeshi la Polisi siku hizi ukimuona Askari amevaa sare za FFU siyo kile kikosi tulichokizoea miaka yote ambao walikuwa na kazi ya kutuliza ghasia.

Hawa siku hizi ni askari wale ambao wapo vituo vya polisi ndio wamevalishwa magwanda yale ili wafanye kazi ya FFU. Hawana uzoefu wowot na ndio maana vitendo vya kialifu vinaongezeka siku hadi siku. Hawa walishazoea kukaa vituoni na kupokea milungula toka kwa vibaka na wapiga debe wa madaladala, sasa wakipewa pikipiki wanajiona wamefanikiwa sana na wamepanda cheo kwa kukaa katika pikipiki tu. Siku wakipangiwa kukaa katika patrol (defenders) hapo ndio usiseme!!!!!!!!!!! balaa tupu anaona amekuwa mkuu wa majeshi!!!!!!!!!

Na huu mchezo ulianza toka ilipoanzishwa kitengo cha pikipiki (TIGO)

ukitaka kuhakikisha nisemayo:- chunguza utendaji wa kazi wa askari TIGO na fuatilia jinsi wanavyoua raia pasipo makosa. Mimi nawaomba ndugu zangu wasamaria wema tusiwalaumu Askari kwa kuua raia katika matukio kama haya kwa sababu hawa askari wanaokaa katika Defender na pikipiki wengi wao walishazoea kukaa vituoni na kushika fimbo na filimbi. Leo unampa Bunduki na alisha sahau kuitumia miaka mingi. Hivyo akiishika badala ya kutishia yeye anafyatua. Wengi wao wanakuwa hawakudhamiria kuua lakini kutokana na umbumbumbu wa kutumia Bunduki wanafikia hapa.

Na pia leo wanatembea mitaani na kukutana na watu wengi, hivyo wanatamani kupata pesa kwa kutumia Bunduki waliyopewa. Mfano tukio la Mbeya la juzi kifo cha mwanafunzi ambaye alikuwa yupao bar. Kulikuwa na sababu gani kwa askari kufyatua risasi.

Ni umbumbumbu tu ule. Inabidi IGP aliangalie vizuri jeshi lake na askari vinginevyo watakuwa wanamuharibia CV yake. Kwani uozo kama huu ukitokea raia tunamuangalia IGP atasema nini. Ukizingatia kamada wa Mkoa naye ametoa pumba, je na IGP atasema nini.

kuna sababu kubwa sana ya Jeshi la Polisi kuangaliwa upya na hawa makamanda wa mikoa wabadilishwe kila baada ya muda fulani kwani wanazoeana na askari wa chini kisha lawama zitaenda kwa Serikali na IGP.

Tulitegemea baada ya mauaji ya Arusha na Zanzbar, jeshi la Polisi litajirekebisha na kutafuta mbinu nyingine ya kupambana na wananchi wasio na siraha za moto. Kumbe bado wanaendeleza mchezo ule ule wa kutumia silaha za moto.

je hapa kuna tofauti gani na mapambano ambayo Babu zetu walikuwa nayo kati ya Wakoloni na Wafrika waliopinga kutawaliwa. Mkoloni alikuwa na Bunduki na Mwafrika alikuwa na Fimbo. Tena ndugu zangu Wangoni ndio usiseme kwani wao Mkoloni akipiga Risasi wao silaha yao ni kusema "MAJI, MAJI, MAJI......"

Je tunarudi kule enzi za vita vya Maji Maji??? (Mkoloni na Kinjekitile, Mkoloni na Isike, Mkoloni na Mirambo n.k)

Ni wakati sasa kwa JEshi la Polisi Tanzania Kufanya "TAFAKARI NA KUPATA MBINU YA KUPAMBANA NA RAIA WASIO NA SILAHA"


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!



Sasa kutokana na ulimbukeni huu
 
RC, RPC, wa Mkoa wa RUVUMA waachie ngazi mapema wameendekeza Imani za kishirikina na siasa
 
Wikipedia inavyomjadili Kikwete na utawala wake

Corruption and other controversies


Kikwete's presidency has been marked with wide range of corruption, some of which happened during the presidencies of his predesesors. Some of his supporters claim that to be a sign of transparency that was brought in by Mr Kikwete.

Other cases, like deaths, have also been brought up such as
Tanzanian police killing people on Tanzanian streets and getting away with it.

Also, President Kikwete has been blamed for choosing his friends to the cabinet, a result of which he has no power to condemn them for their irresponsibility.

The example of two consecutive bomb blasts at Mbagala and Gongo la Mboto arm base respectively in 2009 and 2011 where General Mwamunyange as well as the defense minister, Mwinyi, were in charge, but they insisted that it was not their fault for the blast and denied to brief the country about the reason for the blasts.

The President himself kept praising to the two officials that they are working to secure a country something that raised anger among the victims of blasts.
 
Kwanza wanao haribu amani Tanzania ni CCM akiwemo JK na Nape halina ubishi, na yakitokea madhara yeyote wajiandae kujibu hii damu ya watanzania wanayomwaga kwa ajili ya kuwalazimisha kula ugali wa kiporo wakati wanajua kiporo kimeshapitwa na wakati, kila mtanzania anataka kunywa chai ya maziwa, supu, mkate wa bluu bend kwa ajili ya afya zao.

Tukija Songea, ninadhani wananchi hawakuwa na nia mbaya ilikuwa DC atafute njia ya kukutana na wananchi wake hata kwa kuchagua wawakilishi asikilize ujumbe wao na awaombe ushikiano wa kufanya hiyo kazi kwa ushikiano na polisi na raia, ninadhani hapo wananchi wasingefanya fujo na wangefanya kazi kwa pamoja ili kuondoa huo mlolongo wa mauaji na vikwazo vilivyokuwa vinawakwaza hao wanananchi.

Sasa tujiulize ikifikia kila askari akipewa pistola yake kama wanavyofanya nchi nyingine je sisi wananchi tutapona kweli? Tunaomba IGP na RPC kabla ya kupewa hii nafasi wawe na kozi hata ya miezi sita nje ya nchi ilikuona wenzao wanafanikiwa namna gani kuzima hasira za wananchi mara inapotokea. Kazi ya polisi sio ya kibabe na ndio maana wananchi wanakuwa na imani na polisi kuwa ni wasuluhishi.

Anakotupeleka huyu Mwema damu ya watanzania itamfikisha pabaya na wenzake wa CCM watamkimbia. Kuna msemo unaosema "kidogo kidogo hujaza kibaba" sasa tumeona Arusha Igunga na sasa Songea mnafikiri wananchi wataendelea kuwavumilia hao Polisi kweli? Sasa ninadhani hata polisi wamestuka kuwa hata wananchi wanajipanga, sio watoto wa shule.
 
Ah! Najuta kupigia kura CCM mwaka 2005. Ewe mwenyezi natubu dhambi zangu leo. Ni heri ya makaburu wa A/kusini enzi zile kuliko utawala wa CCM na serikali yake inayoua wanaowaongoza.

Leo ndiyo umejua na unajuuuuuuuuuuta, pole mkuu, tukio hili liwe fundisho na chachu ya kuwaamsha na wengine wanaodhani kuwa ccm inaweza kuwakomboa au hata kuwaletea maisha bora. Sambaza ujumbe kwa wenzio kumi, kisha nao kwa kumi wengine na kisha kumi tena na tena............... Poleni wafiwa na wana Songea kwa ujumla.
 
Kwanza poleni sana ndugu zetu wa Songea na Tanganyika kwa jumla. Habari ya kusikitisha sana.

Sipendi kusema haya kwa furaha lakini inabidi niseme kama ukumbusho kwa yaliopita, yaliopo na yajayo kwa nchi yetu au Tanganyika na Zanzibar. Huko nyuma wenzetu wa Tanganyika walizowea kusikia mauwaji ya kikatili yaliyoendeshwa na utawala wa Muungano na jeshi lake la polisi kwa upande wa Zanzibar tu. Ndugu zetu wa Tanganyika, bila kuchanganuwa, walikuwa wanatuita Wazanzibari wakorofi na majina tele yakuonesha kuwa Wazanzibari ni watu wakorofi sana. Wazanzibari waliouliwa hawakufanya ukorofi wa aina yeyote na wala hawakuchukuwa silaha yoyote. Walichokifanya ni kudai haki zao za msingi. Matokeo yake, vyombo vya dola likiwemo jeshi la polisi viliwafanyia raia ukatili wa hali ya juu. Raia waliuwawa kikatili, walivunjiwa majumba, wengine walinajisiwa, na wengine kuishia vilema wa maisha kutokana na ukatili huo wa vyombo vya dola. Hili ndilo jeshi la polisi la Tanzania na vyombo vya dola. Hii yote ni mbinu ya mtawala wetu Tanganyika na Zanzibar, CCM, kutawala kwa thamani yoyote ile. Hata iwe ni kutoa roho za watu lakini lazima itawale. Kwa ninanvyowafahamu CCM na utashi wao wa madaraka ni kuwa ni lazima watawale wao au nchi utumbukie katika janga lolote lile. Wao ni lazima wawe viongozi. Hii ni kutanabahisha tu kuwa tuweni makini, mtawala wetu ni kuwa abakie madarakeni au ale roho za Watanzania kwa wale watakaodai haki zao. Siku zote mtawala huyu umridhie vile anavyotaka tu ukimuulize basi wewe ni mbaya na adui na ndiyo kama hivyo mnavyoona kwa raia maskini na wanyonge wa Songea. Haya yananikumbusha mauwaji ya Pemba.

Poleni sana ndugu zetu wa Songea. Naomba roho zenu ziwe ni chachu ya ukombozi na mabadiliko ya nchi nzima kutokana na mtawala huyu na vyombo vyake katili.
 
Saa hizi 1.20 maeneo ya stand ya Songea yameanza tena kupigwa mabomu hata tunaogopa kutoka nje kwani hutujajua kumetokea nini tena. Maana toka asubuhi kulikuwa shwari kabisa na kila mtu aliendelea na mambo yake. Subirini tutawajulisha kinachoendelea
 
Nimemsikia RPC Songea anasema maaskari wanne wanachunguzwa kuhusu vifo vya waandamanaji...... pia anasema yale hayakuwa maandamano kwani maandamano yana sehemu yanakoelekea...... anazidi kusema kwamba waandamanaji walikuwa wanarusha mawe kwenye magari, ofisi za serikali na polisi.
 
Wikipedia inavyomjadili Kikwete na utawala wake

Corruption and other controversies


Kikwete's presidency has been marked with wide range of corruption, some of which happened during the presidencies of his predesesors. Some of his supporters claim that to be a sign of transparency that was brought in by Mr Kikwete.

Other cases, like deaths, have also been brought up such as
Tanzanian police killing people on Tanzanian streets and getting away with it.

Also, President Kikwete has been blamed for choosing his friends to the cabinet, a result of which he has no power to condemn them for their irresponsibility.

The example of two consecutive bomb blasts at Mbagala and Gongo la Mboto arm base respectively in 2009 and 2011 where General Mwamunyange as well as the defense minister, Mwinyi, were in charge, but they insisted that it was not their fault for the blast and denied to brief the country about the reason for the blasts.

The President himself kept praising to the two officials that they are working to secure a country something that raised anger among the victims of blasts.

This means that principles of constitutionalism never apply in this country. I am worried that we won't get consensus constitution.
 
Back
Top Bottom