Maamuzi ya Prof Ndalichako yanashangaza

Maamuzi ya Prof Ndalichako yanashangaza

Alichokiondoa yeye ni utaratibu wa kuchagua masomo form three nadhani ana dhamira nzuri tu tusipende kutafuta baya katika kila zuri
 
Mimi namshangaa sana uyu professor yani afanyi utafiti kabisa anaongea ongea tu kiki nyingi umlazimishe mtu asome science wakati ata hao waalim akuna, wala madarasa maabara yani dah miemuko mingi kweli malipo hapa hapa duniani
 
Hivi humu ndani wote tumesoma secondary school Tanzania kweli?
Yaani watu mnaona ni jambo rahisi tu kumjazia mtoto Physics,Chem,Maths,Bios,Geo,Civics,History,English,Kiswahili,Bookkeeping,Commerce,vyote aende navyo hadi form iv na kufaulu bila shida?!Mtoto apige Abott kuanzia measurement and Physical quantities form one hadi Radioactivity form four,aweke kichwani every detail in each topic,afanye maswali na kusolve equations za topic zile,na shughuli hiyo hiyo kwenye Chemistry,Math etc,halafu unaita hii ni elimu rahisi ya awali,kweli?Hivi mnaotetea haya mmesoma masomo ya sayansi kweli mkaelewa what it takes to be a science student ndani ya elimu ya Tanzania?
Mimi nadhani tulipaswa kujenga mazingira ya watoto kusoma kwa kufuata mikondo tangu chini,yaani hata form three ni mbali sana.
Tunatakiwa kufumua mfumo tangu kindergaten!
Binadamu ni kama maua,kila mmoja na nakshi zake.Tunapaswa kuendeleza vipaji vyote katika varieties zake,na sio kuua baadhi for the sake of others.Hii ni nature,hatuwezi kushindana nayo,bali tuishi tukiifuata inavyotaka.
Tengenezeni mazingira bora ya elimu,mtapata kila mumtakaye,injinia,doctor,pilot,mhasibu,mwanamichezo etc,haihitaji kulazimisha.
Mpaka hapa tulipo Tanzania ni mhanga wa kulazimisha,mazingira yanalazimisha watu kusomea yale ambayo kiasili si namna yao,wanafanya kazi ambazo kielimu hawajasomea,matokeo yake kila msomi nchi hii yuko kwa ajili ya kitu kimoja tu,PESA,na sio kuiletea nchi maendeleo kutokana na utaalamu wake.Sasa Ndalichako anakwenda kuliformalize hili kabisa,tena kwenye very sensitive area,fani zinazozalisha wataalamu ambao wanapaswa kuwa dedicated kweli kwenye utaalamu wao.
Na huyu mtoto anayelundikiwa masomo kutoka aina tofauti za fani,mlifanya research za kutosha kwa wataalamu wa saikolojia,baiolojia na tabia za binadamu wakajiridhisha kuwa aina hii ya ufundishaji inaweza kumjenga mwanafunzi ambaye yuko vizuri kwenye critical thinking and analysis au tunatengeneza wanafunzi ambao ni wazuri kwa vocabulary tu?!
Huku sio kusababisha mzigo mzito kwenye akili ya mtoto na kumpotezea utulivu muhimu kwa ajili ya kufanya critical thinking and analysis?!
 
Prof yupo sahihi kabisa. Hii nchi watoto wetu wengi walikuwa vi. laza kwenye masomo haya. Changamoto ni walimu tu. Lkni tamko lipo sahihi
 
Viongozi wa kisiasa ndio wanao haribu elimu ya nchi hii.
Kila waziri anaekuja anakija na style yake. Iliradi akitoka kesha chafua mtaala anapita hivi....
Wanadhani kila mtu akisoma sayansi hizo fani nyingine ni nani atafanua?
Wana maana jakuna tena wakusoma sjeria, utawala, ualimu, mambo dini nk!! Yaani Tanzamia ya viwanda....
Maigizo tuu hapa.
tatizo la wabongo ni kulalamika tu...nani kakwambia ukisoma sayansi hutasoma sheria..hata hivyo si wamesema anetaka kuchagua art anaruhusiwa akifika fm4....jaribuni kutafiti hata kidogo wanafunzi wanaofaulu asilimia 90 niwale wanaosoma masomo 9..wale wanaokimbilia arts huishia kufeli tu.....kwa mfano ktk shuleyetu tulifaulu watu 7 lakini wote tulikuwa tunasoma masomo ya sayansi na arts..wale wa arts tuwapoteza wote
 
Wengi mmeona habari ya leo kuwa sasa ni lazima wanafunzi wote wasome Sayansi kabla ya hiii zimekuwepo habari nyingi za kushangaza za wizara hii ya elimu. Siku Magufuli aliposema anashangaa fimbo kupigwa marufuku mashuleni, kesho yake tu Wizara hii ikatangaza 'fimbo kurudishwa mashuleni'
yaani halikuwa na mjadala wala kutolewa maelezo labda why fimbo zilizuiwa mwanzo au kuna watalaam gani walihusika kufikia maamuzi.

Halafu yakaja maamuzi ya kuongeza ufaulu ili kujiunga na vyuo, hili nalo limechukuliwa kama Tanzania ni kisiwa vile mpaka sasa wala hakuna maelezo iwapo mwanafunzi wa kitanzania akipata nafasi kusoma nje ya nchi kwa ufaulu ambao hapa nchini haumruhusu, vyeti vyake vitakuwa na 'status' gani hapa nchini mradi maamuzi ya wizara hii sasa ni kama vile Tanzania ndo 'The world'
na kila atakachoamua yeye ndo 'final'

Huyu mama na Mabosi zake wanasahau kuwa tuko katika 'global village' Maamuzi ya ajabu ajabu sanasana yatawaathiri watoto wa masikini tu
wengine wenye options za kusoma nchi jirani na nchi za mbali hayatawagusa na mwishowe watakao 'umizwa na maamuzi' haya ni watoto wa masikini.Sasa hili la lu kulazimisha Sayansi nalo unajiuliza nchi ngapi duniani linatumika?

Je mtoto wa kitanzania akisoma Kenya au Uganda au kwingineko
ambako hakuna 'maamuzi ya aina hii' huyu mama atafanyaje? Hivi why 'tuna invest kwenye kuongeza kero na vizingiti' vya kila aina kwa watanzania? Kwani Tanzania ni kisiwa? Si masuala ya elimu yanapaswa kuwa 'Universally acceptable'? Sasa huyu mama ndo mifano wa maprofessa wetu?

Unaposoma nje ya nchi huwa kuna equivalent inafanyika kwa vyeti ili kuthamanisha vyeti vyako na vya Tz. Pili kwa level ya chuo kikuu, kama huna Uwezo watakusajili wale pesa zako kwa kuwa nao wanataka kumaintain reputation ya vyuo vyao tutaishia kusikia story tu ninasoma nje sijui imekuwaje muda ukiendelea kupita. Hawatakupa cheti. Pia wanapokuajiri kama umesoma vyuo visivyoeleweka waweza pata shida pia. Kuhusu suala la viboko Tz, lilikatazwa kwa kufuata upepo tu wa nchini za magharibi bila kuconsider culture na context yetu. Haiwezekani kwetu bila viboko, hatuna culture ya kuwafunza watoto toka wadogo akapambanua, akaelewa na ukaongea naye ana kwa ana akajua ni kosa akaomba msamaha na akaacha tabia, kuachwa kwa viboko na walimu kukosa njia za kutumia other form za negative reinforcement ndio iliyozalisha kizazi ukionacho sasa, sina Zaidi ya kukwambia sana, soma humu pia waweza elewa kuna nini tumearibu. kama fimbo zilitumika na zikasaidia kuogofya na watoto wakawa disciplined acha tu zitumike hakuna jinsi, ukweli tunahitaji kuwa socialize watoto toka wadogo wabadili tabia.
 
Viongozi wa hii nchi wanapenda shortcut,hawataki kukaa chini na kujadili na wadau wa sekta husika kujua ni njia ipi serikali ipite ili ifikie mafanikio.
Kwanini kusiwe na mjadala huru na research ambazo zitatafuta njia ya kupunguza/kuondoa tatizo la elimu?
Uyu Mama ni mtafiti wa elimu kwa taaluma yake lakini mpaka sasa sijaona sehemu aliyotumia taaluma yake kutatua matatizo ya Elimu hapa nchini.
Napendekeza mjadala huru utakaotatua matatizo ya elimu yetu na sio kutoa matamko yenye ukakasi.
 
sioni tatizo kwa hili la wanafunzi kusoma masomo ya sayansi wote!.kiutaalu hakuna mwanafunzi asieelewa au asie na uwezo wa kusoma sayansi au hakuna somo gumu au rahisi,kikubwa ni maandalizi tu kwa wanafunzi wetu na molari ya walimu wa masomo husika!,mazingira ya kujifunza na kufundishia(miundo.mbinu)kila kitu kitakuwa sawa ila serikali ijipange kwani bado walimu hawatoshi
 
Tatzo la nchi kwasasa kila kiongozi awe ni waziri, naibu waziri katibu mkuu, wakurugenzi, wakuu wa mikoa n.k kila mtu anafanyakazi kwa woga kumridhisha mkuu wa kaya matokeo yake ndo haya tunayoyaona.
 
Hili taifa linadumaa kila uchwao kwa sababu ya kila kiongozi anapoamka anakuja na tamko lake na ndio inakua sera ya serikali,
Na mpaka sasa sioni mwelekeo wa serikali hii zaidi ya matamko tu ambayo ayana tija kwa taifa
 
kwenye Swala Ia fimbo acha liendelee kwani Watoto wa siku hizi ni baraa Sana, by the way Tulia dawa Ikuingie kunako Kama na we we ni miongon MWAO
 
Haihitaji tena elimu ya kiwango cha darasa la saba kugundua kuwa huko tuendako elimu yetu bado itakuwa majanga.Sera ya elimu ni suala mtambuka linayohitaji mjadala wa kina na wadau mbalimbali,tafiti mbali mbali,na maamuzi haya yawe yanatekelezeka kulingana na hali halisi ya nchi yetu.hii leo tamko la kuongeza alama za ufaulu,jioni tamko la kufungia chuo kikuu flani,usiku tamko la kufukuza wanachuo vilaza, mara,kila raia asome sayansi., Umefika wakati sasa wa kupima matokeo ya matamko ya nyuma kwanza, mafanikio yake, na changamoto zake tusiende kama gari lisilo na breki kwenye mteremko wa Sekenke.
 
Mimi ningeacha shule tu...mbagala na gongo la mboto so hawana mwendo kasi? Ningeenda kuwa mpiga tu!
 
Huwa mara kwa mara nawaambia watu kuwa tangu tujitawale hii serikali ndiyo itakayoingia kwenye vitabu vya historia kama serikali mbovu na ya hovyo kuliko zote. Hii ni kwa sababu haina mkakati katika jambo lolote, ni sawa na kusema inaendeshwa toka kijiweni tu.

Elimu yetu ni ya ubaoni na chaki tu badala ya kuwa ya mfumo wa kuibua na kukuza vipaji na mielekeo ya wanafunzi tangu utotoni kama nchi zingine zinavyofanya.
Hatuwezi kuwa na elimu ya maana mpaka pale tutakapoioanisha na maisha halisi, mazingira ya kibinadamu na mahitaji yake.

Ndiyo maana pamoja na JPM kuwa "doctor" na kulundika madaktari wenzie, maprofoo, na mainjinia bado kuna uhaba wa fikra.

Ninyi ni wale mnaolaumu tuu kila kitu kwa kuwa akili yako haitaki. Mambo mengine ni hata kwa force ni ngumu kufanya mageuzi ya elimu kwa kubembeleza wakati mfumo wenywe ilishakuwa corrupt. Mama chapa kazi anayeona kero ahamishe mwanae we tengeneza mfumo bora hata kama inaumiza kwa wakati huu ila baadae tutaenjoy.
 
hofu yangu ni kwamba CCM wameweka madarakani viongozi ambao hufanya maamuzi yasiyokua na upembuzi yakinifu wala ushauri wa wataalamu ama wadau wakuu wenye ueledi uliotukuka..
NI HATARI KUJIONA WEWE NI 'PERFECT' HALAFU ITOKEE KICHWANI KWAKO KUNA MAJI tena YA MTO !
 
Mda sio mrefu wale wenye vyeti vya kuunga unga mtaskia tamko"hakuna kutumia vyeti vya kuunga unga wanaitaj kimoja tu"jipangeni hawa ms prifesa wataka watu wote wanao soma wawe na uwezo ka wao wakati kila mtu anakipaji chake wasilazimishe waliokifanya wao na wengine wakifanye hawa vujana ambao bado wanasoma watafel sana serikal inatafta namna ya kupunguza wasomi wameo wakua wengi zaidi ndo mana kila kunapokucha mifumo inabilika.
 
Sekta ya elimu ipo worldwide, haitakiwi kuichezea kama rede. Umefika wakati sasa WA kutengeneza sera thabiti ya elimu ambapo itumike kipindi vipindi vyote vya serikali..... Kiongozi aingie tu kusimamia sera si kuingiza matashi yake. VIONGOZI wetu MUACHE sifa.... Kama mmepanga kuwaadhibu walala Hoi Mungu yupo atawasimamia adhabu itawafika NYIE kabla ya wao
 
Back
Top Bottom