Maamuzi ya Prof Ndalichako yanashangaza

Maamuzi ya Prof Ndalichako yanashangaza

namkumbuka mwalimu wangu kwa mfano ambao hata leo hupenda kuurejea. alifananisha huduma yetu ya elimu na ugojwa wa malaria ambapo daktari anataka kuwatibu wagonjwa wengi lakini vidonge ni vichache. sasa badala ya daktari kutoa full dose kulingana na uchache wa dawa anaamua kugawa kidonge kimoja kimpoa ili mradi kila mtu apate dawa japo hatapona. sasa ukiangalia shida ya elimu yetu halafu unasema kila mtoto asome sayansi badala ya kuwafundisha wachache vizuri kwa resources zilizopo je mfano haulandani? nijibuni! msitukane au kukashifu
 
Hivi nani alikuambia kwenye sayansi hakuna sheria ni nani? Serikali imesema wanafunzi wasome masomo yote; sayansi na Sanaa hadi kidato cha 4. Baada ya hapo ichepuko itaendelea. Lengo la serikali ni kubadili hadhi ya sasa ambapo wanafunzi wanaomaliza kidato cha 4 wengi wao wanakuwa wamesoma masomo ya sanaa na lugha na wachache wao wanakuwa wamesoma sayansi.
Hebu nitajie faida za kusoma masomo Tisa. Kisha mimi nitakutajia faida za michepuo
 
ili tupunguze wapuuzi nchi hii ni lazima tuongeze ufaulu wa hisabati ili wakina #tundu kabla ya kuropoka wawe wanafanya hesabu ngumu kwanza wanajiridhisha kama tunahitaji kuta kwa sasa au tunahitaji #mabadiliko ? lazima wanafunzi wote wasome sayansi ambayo ziada ni masomo mawili tu, chemistry na physics
 
namkumbuka mwalimu wangu kwa mfano ambao hata leo hupenda kuurejea. alifananisha huduma yetu ya elimu na ugojwa wa malaria ambapo daktari anataka kuwatibu wagonjwa wengi lakini vidonge ni vichache. sasa badala ya daktari kutoa full dose kulingana na uchache wa dawa anaamua kugawa kidonge kimoja kimpoa ili mradi kila mtu apate dawa japo hatapona. sasa ukiangalia shida ya elimu yetu halafu unasema kila mtoto asome sayansi badala ya kuwafundisha wachache vizuri kwa resources zilizopo je mfano haulandani? nijibuni! msitukane au kukashifu
Exactly

Nadhan serikali wamekurupuka pakubwa sana
 
Anasema eti kuelekea Tanzania ya viwanda Sayansi ni lazima
nimejiuliza USA na China huko kote walilazimisha wanafunzi wote kusomea Sayansi?
au hii yetu ni 'ubunifu mpya'?
Uko sahihi na huenda naye yuko sahihi kwa kiasi fulani. Kuna mambo ambayo kila nchi inahitaji wannachi wake wayafahamu ktk maisha yao. China hata usome historia na art ya aina yoyote, lazima usome hesabu (Mathematics). wanayo sababu yao. KUna nchi pale europe hata ungependa kusoma nini, lazima usome biology na wanasema biology ni maumbile lazima kila mtu ajifahamu. hata binti anayevunja ungo, akiambiwa contraceptive ni nini anelewa wazi.

Sisi Tz miaka ile ilikuwa Siasa, kiswahili na hesabu. Kwa sasa sijui ni nini au ni huria. kwa nini kila mtu asome Kiswahili? Kweli unahitaji kiswahili cha darasani ili uzungumze kiswahili? Hesabu imesahaulika hadi Bungeni maana ukitaka ubunge ni kusoma na kuandika hata kama hujui kuhesabu!

Nadhani akijipanga, anaweza kuja na maelekezo sahihi zaidi kuliko matamko ya jukwaani. Wizara ile ina madudu mengi tangu chini hadi vyuo vikuu ambako tulidhani wanajiongoza vizuri, kumbe pumbafu kabisa! Angalia wanafunzi wanavyoteseka kwa wizi wao!
 
Huyu ndiye aliyetufelisha 4m4 2012 nchi nzima halafu akatuita et wa kubustiwa! None sense! Cmuamin hadi keshokutwaaaa, nakumbuka alifanya utumbo 1 hadi nilicheka chumba cha pratical ya chemistry, ktk paper kuna HCL acid halafu iliyoandaliwa Salphuric acid haaahaaa et nifanye titration!
 
HUU uoga ndiyo hugandisha wanafunzi wengi na kudumaza fikra zao kwamba hawawezi kujifunza.Kujifunza ni UTAYARI,MAZOEZI,MAJARIBIO,UZOESHI na MTIHANI.Huko nyuma wanafunzi walisoma michepuo yote na walimudu.F5 mwanafunzi alielekea kwenye mchepuo alioupenda kusoma zaidi.
 
Tanzania ni ya kwetu wote lakini baadhi tuliowapa dhamana wamefanya kuwa mali yao. Haoni haja ya kuwasikiliza wenzao wanasema nini. Wanaamini wao wanajua kila kitu. Poor Tanzania.
 
Huyu ndiye aliyetufelisha 4m4 2012 nchi nzima halafu akatuita et wa kubustiwa! None sense! Cmuamin hadi keshokutwaaaa, nakumbuka alifanya utumbo 1 hadi nilicheka chumba cha pratical ya chemistry, ktk paper kuna HCL acid halafu iliyoandaliwa Salphuric acid haaahaaa et nifanye titration!
Wewe kijana, Prof Ndalichako ndiyo anakuandalia vifaa vya Prac, mlalamikie mwalimu wako kilaza aliyeshindwa kuandaa material sahihi.
 
Tatizo sio kuwa hakuna wanafunzi wa kusoma ualimu wa sayansi, tatizo vyuo vikuu nyetu ndio havifundishi walimu wa sayansi, hebu tizama tumaini saut cbe ekenford hao ndio wanatoa 80% ya walimu na wote ni walimu wa book keeping history na kiswahili, tuanze hao kuwaambia wadahili na walimu wa sayansi, sasa kumfundisha mtoto somo ambalo halina mwalimu ni kuongeza idadi ya zero tu.
Wadahili kutoka wapi kama wahitimu wa Sayansi kidato cha nne na sita ni wachache, ni wanafunzi wachache sana wa Sayansi waliofaulu wanaokosa chuo. Tunahitaji kuongeza idadi ya wahitimu wa Sayansi, tuwaondoe vijana uoga wasome basic Sayansi kama mtu anataka kuendelea na Sanaa na biashara ataendelea nayo A level ila kuwa na pool kubwa ya wahitimu wa Sayansi ni kitu sahihi.
 
Wadahili kutoka wapi kama wahitimu wa Sayansi kidato cha nne na sita ni wachache, ni wanafunzi wachache sana wa Sayansi waliofaulu wanaokosa chuo. Tunahitaji kuongeza idadi ya wahitimu wa Sayansi, tuwaondoe vijana uoga wasome basic Sayansi kama mtu anataka kuendelea na Sanaa na biashara ataendelea nayo A level ila kuwa na pool kubwa ya wahitimu wa Sayansi ni kitu sahihi.
kwahiyo hata wenye ziro wataenda udom?
 
Sijui nani atakuja kuikomboa elimu ya nchi hii maana kila anae kabidhiwa ofisi anakuja na yake kwa kumsikiliza mpiga zumali wake.

Sijui kwanini kuna kua na ugumu wa kuja na sera moja makini ya kitaifa iliyochambuliwa na wadau wote wa elimu na ikapitishwa na pasiwe na mwingine wa kuja kuivuruga.

Ndugu yetu kaililia wee "Mama Tanzania" wameishia kumpuuza badala ya kumshika mkono tupate mchango wake.

Hawa wasomi wetu sijui wanatupeleka wapi.
Itabidi tubadilishe katiba kuzuia kuvuruga elimu yetu na mawazo ya watu wachache
 
Huyu ndiye aliyetufelisha 4m4 2012 nchi nzima halafu akatuita et wa kubustiwa! None sense! Cmuamin hadi keshokutwaaaa, nakumbuka alifanya utumbo 1 hadi nilicheka chumba cha pratical ya chemistry, ktk paper kuna HCL acid halafu iliyoandaliwa Salphuric acid haaahaaa et nifanye titration!
Unavyosimulia ni kama Ndalichako ndo alikuwa anasimamia practical yako..
 
Tatizo la JF ni kila mchangaji kuamini kuwa anavyoona na/au kuzungumza ndivyo suala husika linavyotakiwa kuwa. Wachangiaji wengi wanatoa ushuhuda badala ya utaalam katika Nyanja husika. hapa kuna walakini.

Mwl. Ndalichako amesoma, amefundishwa na kufundisha - shule za chini hadi vyuo vikuu. Amesoma masomo ya sayansi na elimu (UDSM), kufaulu kisha kubakizwa pale asome zaidi na kuwa mhadhiri kufundisha wengine katika taaluma za elimu na hisabati (vipimo).

Mwl. Ndalichako anajua kwamba mwanafunzi hapashwi kupewa fursa ya kupenda masomo kadhaa ili achague kusoma masomo ya sanaa au sayansi. La hasha. Mwanafunzi anapotoka nyumbani anapelekwa shule kusoma masomo yote. Huko anakutana na Mwalimu, mazingira, ya kusoma na zana za kusoma, basi. Anafundishwa na kupimwa ufaulu mara kwa mara. Atashauriwa na kuelekezwa namna ya kujifunza na malengo ya taifa kwa elimu anayoipata. Ni pale tu mwanafunzi akifika elimu ya juu anapata fursa ya kuoanisha malengo yake binafsi na malengo ya taifa ya elimu anayoipata. Akifika hapo anaweza kuchagua eneo mahsusi la kujifunza umahili katika fani yoyote.

Kwa hiyo, katka madarasa ya awali, mtoto hawezi kupewa fursa ya kuchagua masomo kwa kigezo cha urahisi. Mwanafunzi anatakiwa asome masomo yote. Na hili ndio tamko la sera la Serikali. Kwamba kwa kuwa lengo la serikali ni kuzalisha wataalam watakaokuja kufanya kazi katika maeneo mbali mbali ya viwanda (kipaumbele cha sera kuu ya serikali kwa sasa), basi watoto wasome masomo yote, sayansi na sanaa, hadi kidato cha nne. Kwa namna hii watoto ambao hawataweza kuendelea na masomo ya kidato cha 5 na 6, na hata watakaoendelea hadi kidato cha 6, lakini wasiendeleaa na elimu ya juu zaidi ya hapo, basi wawe na fursa ya kufanya mafunzo katika vyuo vya elimu ya ufundi, wapate ujuzi unaotakiwa kukamilisha lengo la taifa la kujitosheleza kwa nguvukazi viwandani.

Tunatakiwa kufahamu kuwa elimu siyo mali ya mtu binafsi, ni mali ya umma/taifa (public good). Kwa hiyo elimu ni rasilimali ya taifa ambayo mtu hastahili kujiamulia kuipata na kuitumia kwa namna anavyotaka mwenyewe au familia yake. Kwa kuwa elimu ni rasilimali ya taifa, basi serikali inawajibika kuifanyia mipango, uratibu na maboresho ya mara kwa mara. Kwa hiyo, alichofanya Mwl. Ndalichako ni jukumu lake la kusimamia mipango ya serikali katika elimu - rasilimali ya taifa kwa ajili ya maendeleo ya viwanda - kipaumbele cha sera kuu ya serikali kwa sasa. Sasa akina The Boss and the like wanataka kuaminisha umma wa JF kuwa kila kaya ina fursa ya kuwa na mipango na maamuzi yake ya rasilimali-elimu nje ya mipango ya nchi/serikali, la hasha. Huo ni upotoshaji. Tangazo la serikali kupitia waziri Ndalichako ni la kisera na ni sahihi.
 
Itabidi tubadilishe katiba kuzuia kuvuruga elimu yetu na mawazo ya watu wachache
Kweli kabisa. Elimu sio kitu cha kila mtu kuja kujifunzia umahili wake....wanaharibu taifa alafu baadae wanakuja kuwaita vijana wetu vilaza wakati ni zao la ubabaishaji wao.
 
Back
Top Bottom