lift gharama
Senior Member
- Apr 11, 2015
- 107
- 66
'Hapa kazi tu' sasa imekuwa 'Hapa ujinga tu'.
Ujinga gani? namshaka na wewe ni wale waliozoea elimu ni kwa Sadala hata mwenye div 4 nina mashaka unaweza kuwatetea waende chuo kikuu.
'Hapa kazi tu' sasa imekuwa 'Hapa ujinga tu'.
Ndalichako atatuachia majanga kama ya Mungai..huyu mama kaukamia kweli Uwaziri ngoja tuone time will tellAnasema eti kuelekea Tanzania ya viwanda Sayansi ni lazima
nimejiuliza USA na China huko kote walilazimisha wanafunzi wote kusomea Sayansi?
au hii yetu ni 'ubunifu mpya'?
Yule bwana alikuwa na vituko vyenye vivuko. 1. Yule ndiye aliesema hatambui special schools. Tukakaa kimya. 2. Akachakachua shule nyingi za boys ziwe na girls, mf Azania. Tukakaa kimya. Hakukoma. 3. Akasema geography, history na nini sijui, ni somo 1 liitwalo: SOCIAL SCIENCES. Tukakaa kimya. 4. Akafuta UMISSETA! Daaah, Yule jamaaaa yule!
I miss you Mumbai, sorry, sio Mumbai.
mi nimejiuliza swali moja tuu....kwa kutumia walimu wa sayansi hawa walioko mashuleni?Haya mambo mimi nayatazama kwa jicho la tatu.
Unapolazimisha watu washikilie kitu ambacho hujakiboresha kiwe cha maana kwao,mantiki yake ni nini?Hutaki watu wawe na kitu cha maana na hiyo ni janja yako kuwakosesha,sivyo?
Tunalalamika kila siku humu jinsi mfumo wetu wa elimu usivyofaa kwa elimu ya sayansi,badala ya kushughulika kuuboresha,ndio kwanza tunazidi kuufanya utuletee majanga zaidi,sasa tukisema hii ni makusudi tunakosea?Hawa wazee na usomi wao hawayaoni haya?
Mimi najiuliza sana,wanachokitaka watoto wasome sayansi au watoto wafeli?Kwanini vikwazo hivi?Watu wasome Physics,Chemistry,Bios,Maths kwa lazima ndani ya mfumo mbovu hivi halafu unawaambia wapate division one na two form six ili wasome bachelor,na wale watakaoshindwa hapo wapitie njia ya certificates,diplomas,kwa GPA ya 3.5!
Wenye akili mmeelewa hidden message hapo!
Nilishasema toka awali kua huyu mama anakurupuka sana watu wakapinga vikali. Mpaka hapa sijaona mwelekeo wa mafanikio kwa uwepo wa huyu mama Wizara ya Elimu. Wizara ya ELIMU sio NECTA, sio taasisi ndogo! Hii wizara ndio moyo wa nchi.
Sijui mwaka huu vyuo vikuu vingapi vitakavyopokea wanafunzi wa fani za Sayansi. Utaratibu wa kizamani sana huu.
NDUGU HUJAELEWA MAADA AU?kwa hali hii kiingereza chetu kinaenda kufa kabisa maana hawa wa art walitusave sana
Nani atafaulu physics na chemistry kama hesabu anafeli?KUSOMA SAYANSI HADI KIDATO CHA NNE IWE NI LAZIMA. ACHENI UOGA NDUGU WANANCHI NI KWA FAIDA YA VIZAZI VIJAVYO. HIVI HAMJIULIZI KWANINI LEO HII UOGA UMESABABISHA TUKAWA NA RUNDO LA WALIMU WA SANAA MASHULENI NA KUWA NA UHABA WA WATAALAM WA SAYANSI?
Ndugu, kuna watu wanafanya siasa hapa, kazi yao kupinga kila kitu, hakuna hoja inayoonyesha ni uamuzi mbaya bali kuna hoja zinazoonyesha kuna changamoto, ambacho si kitu kibaya. Ni lazima jitahida za maksudi zifanyike ili kizazi kijacho kiweze kupata wataalamu wa Sayansi wa kutosha.KUSOMA SAYANSI HADI KIDATO CHA NNE IWE NI LAZIMA. ACHENI UOGA NDUGU WANANCHI NI KWA FAIDA YA VIZAZI VIJAVYO. HIVI HAMJIULIZI KWANINI LEO HII UOGA UMESABABISHA TUKAWA NA RUNDO LA WALIMU WA SANAA MASHULENI NA KUWA NA UHABA WA WATAALAM WA SAYANSI?
Nani kakuambia watu wote wasiosoma Physics na Chemistry kidato cha 3-4 hawana uwezo huo, toa hizo fikra hasi.Nani atafaulu physics na chemistry kama hesabu anafeli?
chilumendo watu wa Sanaa wataendelea kuwepo kama zamani, tofauti tu soma la Physics na Chemistry halitakuwa tena la kuchagua, litakuwa la lazima kama yalivyo baadhi ya masomo mengine saivi kama Maths na Kiswahili.kwa hali hii kiingereza chetu kinaenda kufa kabisa maana hawa wa art walitusave sana