Maamuzi ya Prof Ndalichako yanashangaza

Maamuzi ya Prof Ndalichako yanashangaza

Anadhani kusoma Physics na Chemistry ndo kuweza kuoperate viwanda!
Kwanza machine za siku hizi siyo manual ni automated computerized.

Nimesoma mimi physics na chemistry lakini sijawahi kuiapply popote!, hata huko viwandani hawaangalii physics umefauluje
Haya mambo mimi nayatazama kwa jicho la tatu.
Unapolazimisha watu washikilie kitu ambacho hujakiboresha kiwe cha maana kwao,mantiki yake ni nini?Hutaki watu wawe na kitu cha maana na hiyo ni janja yako kuwakosesha,sivyo?
Tunalalamika kila siku humu jinsi mfumo wetu wa elimu usivyofaa kwa elimu ya sayansi,badala ya kushughulika kuuboresha,ndio kwanza tunazidi kuufanya utuletee majanga zaidi,sasa tukisema hii ni makusudi tunakosea?Hawa wazee na usomi wao hawayaoni haya?
Mimi najiuliza sana,wanachokitaka watoto wasome sayansi au watoto wafeli?Kwanini vikwazo hivi?Watu wasome Physics,Chemistry,Bios,Maths kwa lazima ndani ya mfumo mbovu hivi halafu unawaambia wapate division one na two form six ili wasome bachelor,na wale watakaoshindwa hapo wapitie njia ya certificates,diplomas,kwa GPA ya 3.5!
Wenye akili mmeelewa hidden message hapo!
 
Elimu ya Tanzania huwa miaka yote iko mikononi mwa Waziri wa Elimu. Tungekuwa na sera madhubuti ya elimu na sheria zinazoilinda mifumo ya elimu haya yasingekuwepo. Nikiwaza toka enzi na Mzee Munga aliye amini katika elimu isiyo na sayansi na kisha yule wa awamu ya nne ambaye ufaulu wa kisiasa ndio ilikuwa kipaumbele kuliko uwezo wa mwanafunzi na huyu naye kaja na yake. Tusubiri atakaye kuwa waziri wa elimu 2020 au 2025 naye atakuja na Lipi! tanzania ni ajabu sana Duniani! labda kwa sababu ilipatikana kwa kuchanganya udongo.
 
Haya mambo mimi nayatazama kwa jicho la tatu.
Unapolazimisha watu washikilie kitu ambacho hujakiboresha kiwe cha maana kwao,mantiki yake ni nini?Hutaki watu wawe na kitu cha maana na hiyo ni janja yako kuwakosesha,sivyo?
Tunalalamika kila siku humu jinsi mfumo wetu wa elimu usivyofaa kwa elimu ya sayansi,badala ya kushughulika kuuboresha,ndio kwanza tunazidi kuufanya utuletee majanga zaidi,sasa tukisema hii ni makusudi tunakosea?Hawa wazee na usomi wao hawayaoni haya?
Mimi najiuliza sana,wanachokitaka watoto wasome sayansi au watoto wafeli?Kwanini vikwazo hivi?Watu wasome Physics,Chemistry,Bios,Maths kwa lazima ndani ya mfumo mbovu hivi halafu unawaambia wapate division one na two form six ili wasome bachelor,na wale watakaoshindwa hapo wapitie njia ya certificates,diplomas,kwa GPA ya 3.5!
Wenye akili mmeelewa hidden message hapo!

Wasomi hawatakiwa TZ na ccm inatekeleza ilani yake hio.
 
Basi mkuu physics uliitupa pembeni au hukuielewa vizuri au unachokifanya ni kuoperate vitu ambavyo ni already made na huna passion ya kubuni kitu chako mwenyewe, we unadhani hizo automation ya hizo machines anayefanya ni nani? ambaye hajasoma physics? tukitaka kuwa na viwanda tusitegemee tutanunua kila product nje, vitu vingine ni custom built lazima tuweze kuvitengeneza sisi wenyewe, we unataka hadi machine ya kupima vitu na kukata twende nje tukanunue huku its very basic physics?

Physics ni muhimu sana, mimi niliisoma na hadi leo hii ninaitumia kwenye kazi zangu mara kibao tu, siku nyingine narudi kuchimba vitabu vya university physics kuangalia principles nikiwa nimezisahau. Kama ni kutengeneza viwanda tunahitaji watu waliosoma physics, huwezi tengeneza engine ya gari bila physics, huwezi tengeneza game la computer, hata kiatu bora cha kuvaa unapima strength ya material, heat absorption na dissipation, hadi vitu basic kama rangi nyeupe inafanya reflection na nyeusi inafanya complete absorption ni concepts nyepesi lakini very important ikija kwenye decisions ya rangi ipi itumike sehemu flani. We idea yako ya viwanda kumbe ni kununua kila kitu nje alafu tukaoperate wenyewe? Hehehe, mimi idea yangu ni kununua vichache nje, alafu vingi tukatengeneza sisi wenyewe.
Nimekuelewa vema, haya nambie toka tuanze kufundishwa science niambie tumegundua au kutengeneza nini kikawa na impact hapa East Africa achilia mbali huko Duniani kama sio ma end user wa kila kinachogunduliwa nje ona sasa hadi IT expert's tuna import India & now Rwanda wakati kuna watu hapa wamesoma hyo hyo computer science
 
Elimu ya Tanzania huwa miaka yote iko mikononi mwa Waziri wa Elimu. Tungekuwa na sera madhubuti ya elimu na sheria zinazoilinda mifumo ya elimu haya yasingekuwepo. Nikiwaza toka enzi na Mzee Munga aliye amini katika elimu isiyo na sayansi na kisha yule wa awamu ya nne ambaye ufaulu wa kisiasa ndio ilikuwa kipaumbele kuliko uwezo wa mwanafunzi na huyu naye kaja na yake. Tusubiri atakaye kuwa waziri wa elimu 2020 au 2025 naye atakuja na Lipi! tanzania ni ajabu sana Duniani! labda kwa sababu ilipatikana kwa kuchanganya udongo.
Na udongo wenyewe kachanganya mtu mmoja tu......Ndalichako ameweka TAALUMA yake pembeni naye anacheza mdundo wa NGOSHA.
 
MITAALA YETU ni mibovu sana kuanzia ngazi ya msingi mpaka vyuo vikuu! Mwanafunzi wa TELECOMMUNICATION anasoma module ambayo inamfunsisha kuhusu TV yenye Chogo zile za kwanza kabisa na kwenye uhalisia wa maisha zinatumika flat screen!!! Huwezi kukwepa kuomba msaada wa wataalamu toka nje
 
Basi mkuu physics uliitupa pembeni au hukuielewa vizuri au unachokifanya ni kuoperate vitu ambavyo ni already made na huna passion ya kubuni kitu chako mwenyewe, we unadhani hizo automation ya hizo machines anayefanya ni nani? ambaye hajasoma physics? tukitaka kuwa na viwanda tusitegemee tutanunua kila product nje, vitu vingine ni custom built lazima tuweze kuvitengeneza sisi wenyewe, we unataka hadi machine ya kupima vitu na kukata twende nje tukanunue huku its very basic physics?

Physics ni muhimu sana, mimi niliisoma na hadi leo hii ninaitumia kwenye kazi zangu mara kibao tu, siku nyingine narudi kuchimba vitabu vya university physics kuangalia principles nikiwa nimezisahau. Kama ni kutengeneza viwanda tunahitaji watu waliosoma physics, huwezi tengeneza engine ya gari bila physics, huwezi tengeneza game la computer, hata kiatu bora cha kuvaa unapima strength ya material, heat absorption na dissipation, hadi vitu basic kama rangi nyeupe inafanya reflection na nyeusi inafanya complete absorption ni concepts nyepesi lakini very important ikija kwenye decisions ya rangi ipi itumike sehemu flani. We idea yako ya viwanda kumbe ni kununua kila kitu nje alafu tukaoperate wenyewe? Hehehe, mimi idea yangu ni kununua vichache nje, alafu vingi tukatengeneza sisi wenyewe.
You are very right ni deed.
But the problem here is,... watoto wetu hawa wa siku hizi jamani hawawezi kusoma phyisics, chemistry au hata biology kwa madhumuni hayo ambayo wewe leo yanakusaidia.
Wanafunzi wachche wenye utayari wa kusoma hayo basi waendelezwe, na wapewe ujuzi wa juu kabisa kiasi kwamba waweze ku - apply katika maisha yao ya kawaida na kuweza kutengeneza vitu hivyo kwa ajili ya viwanda vyetu... Ila sio kulazimisha kila mtu afanye sayansi.
Chukulia mfano mzuri somo la hisabati, ambalo wao kama serikali wamefanya ni la lazima kwa O level, watoto wengi wanasoma tuu kwa kuwa wameambiwa wasome, ila hawalitilii maanani, na wanafeli sana... Na wenyewe hawana shida kabisaaaa, wanaona sawa tuu... Ukimshauri mwanafunzi umuhukmu wa kusoma hesabu anakuambia sio wote tunajuwa hesabu, wengine tunasindikiza tuu..
Yaani kwa maamuzi hayo, watoto watasoma masomo hayo kama vile wanavyosoma hesabu, wataingia darasani, ila hawatasikiliza na watapuuza wakiwa tayari washajuwa kuwa watapata F....
Kwa hiyo jambo hilo litakuwa ni kuongeza mzigo tuu kwa waalimu wachache wa sayans ila product hapo itakuwa ni F tuuu.
Ni mawazo yangu tuu kaka..
 
Lowasa angekua raisi haya yote yangekuwepo.
 
Angeboresha technical schools, kama moshi tech,tanga tech,iyunga,bwiru,mtwara tech na kuanzisha nyingine au kuteua shule moja wapo kila mkoa ingekuwa bora zaidi. Shule za ufundi huwa hazina mchepuo wa sanaa, huko ni combinations za science. Msingi uliotumiwa kuchaguliwa huko ni ufaulu wajuu kabisa hasa katika hisabati. Hizi shule zetu za kawaida za sekondari kumlazimisha mtoto nikupoteza rasilimali tu,maana nauhakika watakuwa wanafunzi wa science hewa. Waziri anawaongezea msongo wa mawazo walimu wa science hata hao wachache waliopo,tusubili lawama za wakubwa na vikao kujadili hatua zakuwachukulia walimu wanafunzi watakapokuwa wanapata marks 0 kwenye haya masomo.
 
H
Anasema eti kuelekea Tanzania ya viwanda Sayansi ni lazima
nimejiuliza USA na China huko kote walilazimisha wanafunzi wote kusomea Sayansi?
au hii yetu ni 'ubunifu mpya'?
Alafu sayansi yenyewe tunasoma historia ya sayansi, Tangu masomo ya sayansi yaanze nchi tumegundua nini na hiyo sayansi.
Mi nadhani hata angeanza kuboresha mitaala ya hiyo sayansi wahitimu wetu watengeneze hata toroli basi.
 
Hua ni muhimu sana kua na long discussions ikiwezekana muda mwingine kuinvolve public au education institutions kwenye these kinda choices ili tu kupata maoni ya pande zote, personally I think wanafunzi kusoma sayansi hadi form 4 sio kitu kibaya, kwa kua ni basic stuffs wanasoma, na wanafunzi wengi hua wanaregret kudrop science wakiwa form 2 simply because unakuta bado uelewa ni mdogo wa kumake the right choice, mambo kawaida hua yanaanza kua tight form 5. Ofcoz vipo vichwa vingi ambavyo vitafeli Tanzania, hasa arts hua wanafeli sana pamoja na kua na idadi kubwa still wana kauvivu fulani wakiamini arts ni kitu rahisi.

Nadhani tatizo kubwa hasa lipo kwenye system yetu, wanafunzi wengi ni wavivu, they don't study at all, ingia darasa lolote la form 4 uliza pythagoras theorem utakuta almost 50% hawajui kitu ambacho marekani mtoto wa grade 6 anakujibu hata akiwa usingizini, unless upo kwenye shule special.

Ila una valid point pia, I think what we need is long discussions kuweigh njia ipi ni sahihi, na challenges zake ni zipi, kama tutaintroduce sayansi kwa system iliyopo kuna probability kubwa ya kuongeza F kwenye vyeti vya form 4. Tuige nchi kama USA ambazo kitu kama kuintroduce Computer science kwenye curriculum walitumia almost miaka 4 kudiscuss, research zikafanyika, wakafuatilia hadi kwenye big companies Sillicon valley ili tu kujiridhisha kua its the right choice. Sisi hizi decisions ni kama tunazifanya overnight, we are experimenting on people.[/Q
Sio mjadatia tu peke yake kaka panatakiwa kuboresha maslahi ya walimu na vitendea kazi kwa ujumla. Masomo ya sayansi vitabu walimu na vifaa vya maabara ndio njia pekee ya kuileta sayansi katika uhai wake..Serikali hijali waimu wanawekeZa katika miundombinu bila kuwwezesha walimu na hata wanafunzi pia. Siasa inaharibu Elimu ziachiwe Taasisi za elimu kushauri sio wapiga porojo majukwaani..
 
H

Alafu sayansi yenyewe tunasoma historia ya sayansi, Tangu masomo ya sayansi yaanze nchi tumegundua nini na hiyo sayansi.
Mi nadhani hata angeanza kuboresha mitaala ya hiyo sayansi wahitimu wetu watengeneze hata toroli basi.

hivi hujawahi kuona watoto wakijenga toroli la mbao?hehe
 
Nyie mnaoleta na kutetea thread za namna hii tumeshawajua ni wamiliki wa vyuo binafsi na wale wenye watoto wasio na ufahulu mzuri. Vyuo vyenu binafsi mliwategemea sana wanafunzi wenye ufahulu hafifu ili mneemeke lakini ndo hivyo tena hakuna janja janja tena huku mkijifanya mnawatetea watoto masikini wakati huwa hawaji kwenye hivyo vyuo vyenu vyenye gharama kubwa.
Unavyoongea km una uhakika vile..halaf ni ufaulu sio ufahulu mkuu..ungekua unajua kuiandika ufaulu vizuri mbona tungekoma[emoji23][emoji23]
 
Nimekuelewa vema, haya nambie toka tuanze kufundishwa science niambie tumegundua au kutengeneza nini kikawa na impact hapa East Africa achilia mbali huko Duniani kama sio ma end user wa kila kinachogunduliwa nje ona sasa hadi IT expert's tuna import India & now Rwanda wakati kuna watu hapa wamesoma hyo hyo computer science

Mkuu labda unadhani huduma kama M-pesa, MaxMalipo, au hata server za simu za mitandao zinajiendesha zenyewe? Huduma mpya zinazokua introduced kila siku zimetengenezwa na nani? Kwenye software side tunaweza vizuri tu.
Kwenye hardware ndipo kuna challenge, watanzania wanaoweza electronics vizuri wengi wanafanya kazi nje, wanaofanya kazi bongo wachache wanatengeneza enterprise devices ambazo wewe kama normal consumer huwezi kutana nazo, kwa kua manufacturing costs ni kubwa zinakua manufactured for specific companies peke yake ambao wanaweza kulipia.

Vitu kama door lock systems tunategeneza, devices za kukeep mfano employees data, kwenye baadhi ya manufacturing industries vimashine vidogovidogo, hatujafikia uwezo wa kumanufacture consumer devices kwa kua hatuna manufacturing industries hadi twende china, pili hata kufanya prototyping pia inahitaji pesa, ni kazi sana kupata investment Tanzania, haya ukisema utegemee kufanya labda Kickstarter kukuza kamtaji bado ni challenge sana kwa kua ili uende kickstarter bado unahitaji prototype, na electronic devices unlike software zinahitaji team kubwa, watu angalau kuanzia watatu wanne ili kila mtu achukue part yake kidogo kazi iende kwa haraka, kitu kidogo kinaweza chukua hata miaka miwili kudesign, sio kazi ndogo. Wapo watanzania wenye huo uwezo mimi moja wapo ila sio rahisi kiasi hicho kufanyia Tanzania, kazi hizi tunazifanyia nje. Tukikua polepole itafika stage tutaazifanyia nyumbani tu, kwa sasa hailipi.
 
You are very right ni deed.
But the problem here is,... watoto wetu hawa wa siku hizi jamani hawawezi kusoma phyisics, chemistry au hata biology kwa madhumuni hayo ambayo wewe leo yanakusaidia.
Wanafunzi wachche wenye utayari wa kusoma hayo basi waendelezwe, na wapewe ujuzi wa juu kabisa kiasi kwamba waweze ku - apply katika maisha yao ya kawaida na kuweza kutengeneza vitu hivyo kwa ajili ya viwanda vyetu... Ila sio kulazimisha kila mtu afanye sayansi.
Chukulia mfano mzuri somo la hisabati, ambalo wao kama serikali wamefanya ni la lazima kwa O level, watoto wengi wanasoma tuu kwa kuwa wameambiwa wasome, ila hawalitilii maanani, na wanafeli sana... Na wenyewe hawana shida kabisaaaa, wanaona sawa tuu... Ukimshauri mwanafunzi umuhukmu wa kusoma hesabu anakuambia sio wote tunajuwa hesabu, wengine tunasindikiza tuu..
Yaani kwa maamuzi hayo, watoto watasoma masomo hayo kama vile wanavyosoma hesabu, wataingia darasani, ila hawatasikiliza na watapuuza wakiwa tayari washajuwa kuwa watapata F....
Kwa hiyo jambo hilo litakuwa ni kuongeza mzigo tuu kwa waalimu wachache wa sayans ila product hapo itakuwa ni F tuuu.
Ni mawazo yangu tuu kaka..

Hii akili mbovu kwa hawa watoto ni sisi wenyewe tunawajaza, tunaenda kimazoea kwenye elimu. Tatizo la watoto kutokusoma huanzia chini kabisa kwenye ngazi ya familia, wazazi hawajali, wao wanachojua mtoto kaenda shule basi, mengine yote wanamuachia yeye ku~make decisions, ni vigumu mtoto kujitambua kama hasukumwi, tatizo kubwa pia ni kua wazazi wenyewe wengi hawajasoma hata sekondari hawajafika, wanajiona kama hawana la kuchangia kwa watoto kwa kua watoto wenyewe tayari wanawashinda elimu, hapa sasa ndipo mwalimu anatakiwa aingie kati, afundishe vizuri lakini pia atoe motivation kwa watoto, kama hawaoni value yoyote kwenye elimu na hamna cha kuwasukuma lazima watafeli tu.

Nawakumbuka sana walimu wangu wa Chemistry na Physics Olevel, walikua wanatusukuma kwa nguvu, mwisho wa siku mambo yalivoanza kueleweka wote tulijikuta tunayapenda haya masomo, wengi tulikua tunatoka na A wa mwisho alikua na C, I'm thankful hadi leo hii nimekua mtu wa sayansi moja kwa moja, ningefeli haya masomo nisingekua hapa nilipo. Naamini inawezekana kabisa, ni system iliyopo tu imewaacha wanafunzi na wazazi wajijue kivyao, no direction zaidi ya curriculum tu, hata walimu hawana motisha ya kupiga kazi vizuri, hawaipendi kazi yao, wanaenda darasani ilimradi tu liende.
 
brigedia mafia hakuna ufaulu wa jumla kwa wanafunzi kitaifa?

pic+mtoto.jpg

Huyu alikuwa wa kwanza Kitaifa kwenye mitihani ya kidato cha sita mwaka 2015. Anaitwa Ramadhamani Gembe. Alisoma Fizikia Kemia na Bailojia (Physic, Chemistry and Biology - PCB)
Yah huwa hakuna ufaulu wa jumla mfano huyo uliomuweka ndugu ramadhan gembe kutoka feza boys yeye ameongoza masomo ya sayansi vilevile ambao wanachukua masomo ya sanaa wana namba wao
 
Alisifiwa sana tena na wengi wa humu jukwaani ijapokuwa wachache waliompinga walionekana watu wa mrengo wa aina fulani, nadhani huu ni mwanzo tu maana hata huko necta kwangu mm aliharibu pia.
Analazimisha wadogo zetu waparangane wasome hiyo historia ya sayansi ilihali waliopo mitaani anashindwa pa kuwapeleka,
analazimisha wadogo wasome sayansi wakati hao wanaosoma huko mashuleni hawana walimu,kama ameshindwa kupata walimu wa kusomesha hao wachache ,hawa anawaongeza watafundishwa na nani...???
Analazimisha watoto wasome sayansi ,papo hapo waliofaulu hiyo sayansi halafu wakafeli English language amewanyima nafasi za vyuo,
RIP IN ADVANCE TZ
 
Back
Top Bottom