Maamuzi ya Prof Ndalichako yanashangaza

Maamuzi ya Prof Ndalichako yanashangaza

The Boss na katika hii global village tunahitaji watu watakao weza ku communicate effectively kwa Kiingereza tukiwa kama moja ya nchi za jumuiya ya madola, tunahitaji malawyer wazuri wakuweza kusimimia mikataba ya rasilimali zetu, sasa kama nguvu zote zikitupwa kwenye physics na chemistry huko kwingine tutaendelea kuumizwa.
 
Sijui nani atakuja kuikomboa elimu ya nchi hii maana kila anae kabidhiwa ofisi anakuja na yake kwa kumsikiliza mpiga zumali wake.

Sijui kwanini kuna kua na ugumu wa kuja na sera moja makini ya kitaifa iliyochambuliwa na wadau wote wa elimu na ikapitishwa na pasiwe na mwingine wa kuja kuivuruga.

Ndugu yetu kaililia wee "Mama Tanzania" wameishia kumpuuza badala ya kumshika mkono tupate mchango wake.

Hawa wasomi wetu sijui wanatupeleka wapi.
Kwel aisee mzee wa mama yetu Tanzania James Mbatia,anamengi sana kuhusu elim sema ndo ivyo 2.
 
Sijui nani atakuja kuikomboa elimu ya nchi hii maana kila anae kabidhiwa ofisi anakuja na yake kwa kumsikiliza mpiga zumali wake.

Sijui kwanini kuna kua na ugumu wa kuja na sera moja makini ya kitaifa iliyochambuliwa na wadau wote wa elimu na ikapitishwa na pasiwe na mwingine wa kuja kuivuruga.

Ndugu yetu kaililia wee "Mama Tanzania" wameishia kumpuuza badala ya kumshika mkono tupate mchango wake.

Hawa wasomi wetu sijui wanatupeleka wapi.
Soon tutasikia masomo yasiyokuwa ya sayansi yamefutwa!
 
Mimi nimeipenda hii. Wote tusome sayansi(masomo) yote mpaka form 4, then hapo ndio kila mtu achague mchepuo
Safi sana Dr
 
Huwa mara kwa mara nawaambia watu kuwa tangu tujitawale hii serikali ndiyo itakayoingia kwenye vitabu vya historia kama serikali mbovu na ya hovyo kuliko zote. Hii ni kwa sababu haina mkakati katika jambo lolote, ni sawa na kusema inaendeshwa toka kijiweni tu.

Elimu yetu ni ya ubaoni na chaki tu badala ya kuwa ya mfumo wa kuibua na kukuza vipaji na mielekeo ya wanafunzi tangu utotoni kama nchi zingine zinavyofanya.
Hatuwezi kuwa na elimu ya maana mpaka pale tutakapoioanisha na maisha halisi, mazingira ya kibinadamu na mahitaji yake.

Ndiyo maana pamoja na JPM kuwa "doctor" na kulundika madaktari wenzie, maprofoo, na mainjinia bado kuna uhaba wa fikra.
 
Wengi mmeona habari ya leo kuwa sasa ni lazima wanafunzi wote wasome Sayansi kabla ya hiii zimekuwepo habari nyingi za kushangaza za wizara hii ya elimu. Siku Magufuli aliposema anashangaa fimbo kupigwa marufuku mashuleni, kesho yake tu Wizara hii ikatangaza 'fimbo kurudishwa mashuleni'
yaani halikuwa na mjadala wala kutolewa maelezo labda why fimbo zilizuiwa mwanzo au kuna watalaam gani walihusika kufikia maamuzi.

Halafu yakaja maamuzi ya kuongeza ufaulu ili kujiunga na vyuo, hili nalo limechukuliwa kama Tanzania ni kisiwa vile mpaka sasa wala hakuna maelezo iwapo mwanafunzi wa kitanzania akipata nafasi kusoma nje ya nchi kwa ufaulu ambao hapa nchini haumruhusu, vyeti vyake vitakuwa na 'status' gani hapa nchini mradi maamuzi ya wizara hii sasa ni kama vile Tanzania ndo 'The world'
na kila atakachoamua yeye ndo 'final'

Huyu mama na Mabosi zake wanasahau kuwa tuko katika 'global village' Maamuzi ya ajabu ajabu sanasana yatawaathiri watoto wa masikini tu
wengine wenye options za kusoma nchi jirani na nchi za mbali hayatawagusa na mwishowe watakao 'umizwa na maamuzi' haya ni watoto wa masikini.Sasa hili la lu kulazimisha Sayansi nalo unajiuliza nchi ngapi duniani linatumika?

Je mtoto wa kitanzania akisoma Kenya au Uganda au kwingineko
ambako hakuna 'maamuzi ya aina hii' huyu mama atafanyaje? Hivi why 'tuna invest kwenye kuongeza kero na vizingiti' vya kila aina kwa watanzania? Kwani Tanzania ni kisiwa? Si masuala ya elimu yanapaswa kuwa 'Universally acceptable'? Sasa huyu mama ndo mifano wa maprofessa wetu?
Sijaona penye huo ULAZIMA maana ukimaliza form four utaendelea na choice yako.Primary ndio sayansi lazima
 
Anadhani kusoma Physics na Chemistry ndo kuweza kuoperate viwanda!
Kwanza machine za siku hizi siyo manual ni automated computerized.

Nimesoma mimi physics na chemistry lakini sijawahi kuiapply popote!, hata huko viwandani hawaangalii physics umefauluje

Basi mkuu physics uliitupa pembeni au hukuielewa vizuri au unachokifanya ni kuoperate vitu ambavyo ni already made na huna passion ya kubuni kitu chako mwenyewe, we unadhani hizo automation ya hizo machines anayefanya ni nani? ambaye hajasoma physics? tukitaka kuwa na viwanda tusitegemee tutanunua kila product nje, vitu vingine ni custom built lazima tuweze kuvitengeneza sisi wenyewe, we unataka hadi machine ya kupima vitu na kukata twende nje tukanunue huku its very basic physics?

Physics ni muhimu sana, mimi niliisoma na hadi leo hii ninaitumia kwenye kazi zangu mara kibao tu, siku nyingine narudi kuchimba vitabu vya university physics kuangalia principles nikiwa nimezisahau. Kama ni kutengeneza viwanda tunahitaji watu waliosoma physics, huwezi tengeneza engine ya gari bila physics, huwezi tengeneza game la computer, hata kiatu bora cha kuvaa unapima strength ya material, heat absorption na dissipation, hadi vitu basic kama rangi nyeupe inafanya reflection na nyeusi inafanya complete absorption ni concepts nyepesi lakini very important ikija kwenye decisions ya rangi ipi itumike sehemu flani. We idea yako ya viwanda kumbe ni kununua kila kitu nje alafu tukaoperate wenyewe? Hehehe, mimi idea yangu ni kununua vichache nje, alafu vingi tukatengeneza sisi wenyewe.
 
We inao
...ndio wasome sayansi...

ukizungumzia maskini,ungejua maskini ndio wanachimba(wanasoma Zaidi) ...usingesema wataumia Zaidi...

sayansi wakati ule,ilikua lazima kwa wote mpk form two,form three na kuendelea ndio wanaanza kuspecialize....

ssijajua alikua anamaanisha nini sasa hivi?mwenye kujua anifafanulie

Wewe inaonesha kabisa umekimbia umande...

Hamna kitu, yaani mweupee... Empty kabisa.
 
Nafikiri mama Ndalichako alikua na lengo zuri ila namna ya kuliwasilisha imekua tamko lenye ukakasi.

Mtoto wa kidato cha pili kuchagua asome nini wengi huchagua kwa kufuata marafiki zao na hivyo ushawishi wa kusoma arts hua mkubwa kuliko sayansi kwa sababu anaaminishwa masomo 7 ni rahisi kuliko 9 ama 11, lakini uwezo wanao kusoma sayansi au biashara.

Serikali ipitishe hili ila iwe masomo tisa ya lazima, isipokua biashara iwe sayansi kuliko kusema iwe sayansi pekee tutaua biashara ambayo ni uti wa uchumi popote duniani.

Naunga mkono hoja.
 
Mkuu naunga hoja yako kwa 100%.Ujue nchi yetu hii ina mambo ya ajabu sana inang'ang'ania wanafunzi wote wasome sayansi wakati hata mazingira ya utolewaji wa sayansi yenyewe ni duni mfano baadhi ya nyenzo muhimu za kujifunzia hakuna,vilevile idadi ya vyuo vinavyotoa kozi mbalimbali za sayansi ni ndogo sana kwa mfano kozi ya pharmacy ina umuhimu mkubwa sana hapa Tz lakini inatolewa kwenye vyuo vinne tu Tz nzima chuo kimojawapo ni chuo cha kampala ambacho nacho kimejaa mizengwe.
Vilevile kozi kama optometry,prothetics&orthotics zinatolewa chuo kimoja tu ambacho ni Kcmc.Alaf kitu kingine baadhi ya kozi hapa Tz hazipo.Sasa vitu vingine wanavyolazimisha ni kupotezeana muda tu.

Kikubwa ambacho wizara ya elimu walibidi wakifanye ni kuongeza idadi ya vyuo kama itawezekana au ikiwezekana vyuo vilivyokuwepo vitanuliwe ili baadhi ya kozi ziongezwe.
 
Ofcoz vipo vichwa vingi ambavyo vitafeli Tanzania, hasa arts hua wanafeli sana pamoja na kua na idadi kubwa still wana kauvivu fulani wakiamini arts ni kitu rahisi.
Ingawa bandiko lako umelijaza Kiingereza bila ya sababu za msingi kuna hoja hapa umeianzisha naona na mimi nichangie. Kwenye mfumo wetu wa kufundishia darasani kuna tatizo kidogo. Mwalimu inaaminika anajua kila kitu wakati mwanafunzi anachukuliwa ana ubongo ulio wazi wa kujazwa kila kitu toka kwa mwalimu. Aina hii ya ufundishaji iko mpaka kwenye vyuo vyetu vikuu.

Wanafunzi wengi wanaosoma masomo ya mchepuo wa sanaa wanafeli zaidi kuliko wale wanaosoma masomo ya mchepuo wa sayansi, na sababu yake ni rahisi kueleweka. Masomo ya Mchepuo wa Sanaa ni rahisi lakini mitihani yake ni migumu wakati masomo ya sayansi ni magumu lakini mitihani yake ni rahisi. Na ndiyo maana mara nyingi wanaoshika nafasi kumi za kwanza kitaifa kwa Mitihani ya Kidato cha Nne na cha Sita huwa wanatoka kwenye mchepuo wa Sayansi.
 
Huwa sikubaliani na watu wanaosema "mbona USA/Ulaya/China hawafanyi hivi kwanini sisi tufanye" au "mbona wao wanafanya kwanini sisi tusifanye". Sio Lazima tuige kila kitu, Tz ni nchi yenye maamuzi yake kama nchi za Ulaya zilivyo na maamuzi yao bila kuiga au shurti ya nchi nyingine

That being said, sikubaliani na uamuzi wa huyu Mama. Hili swala linahitaji utafiti na kushirikisha wadau kabla ya uamuzi, inaonyesha kajiamulia mwenyewe tu akiwa akiwa na mume wake kama Mungai alipoamua kutoa commerce na bookkeeping na kuunganisha phy na chem baada ya mtoto wake kusema anachukia hayo masomo.

Tayari kuna uhaba wa walimu wa sayansi nchini. Hakuna vitendea kazi kama maabara, vitabu nk. Badala ya kuboresha haya kwanza ili kuweka mazingira rafiki ili watoto wachague sayansi kwa hiari waziri anatumia nguvu kuwalazimisha. Kama huu sio uchizi I don't know what is

Hili linchi sasa limeshindikana
 
Basi mkuu physics uliitupa pembeni au hukuielewa vizuri au unachokifanya ni kuoperate vitu ambavyo ni already made na huna passion ya kubuni kitu chako mwenyewe, we unadhani hizo automation ya hizo machines anayefanya ni nani? ambaye hajasoma physics? tukitaka kuwa na viwanda tusitegemee tutanunua kila product nje, vitu vingine ni custom built lazima tuweze kuvitengeneza sisi wenyewe, we unataka hadi machine ya kupima vitu na kukata twende nje tukanunue huku its very basic physics?

Physics ni muhimu sana, mimi niliisoma na hadi leo hii ninaitumia kwenye kazi zangu mara kibao tu, siku nyingine narudi kuchimba vitabu vya university physics kuangalia principles nikiwa nimezisahau. Kama ni kutengeneza viwanda tunahitaji watu waliosoma physics, huwezi tengeneza engine ya gari bila physics, huwezi tengeneza game la computer, hata kiatu bora cha kuvaa unapima strength ya material, heat absorption na dissipation, hadi vitu basic kama rangi nyeupe inafanya reflection na nyeusi inafanya complete absorption ni concepts nyepesi lakini very important ikija kwenye decisions ya rangi ipi utumike sehemu flani. We idea yako ya viwanda kumbe ni kununua kila kitu nje alafu tukaoperate wenyewe? Hehehe mimi idea yangu ni mbali na kununua vichache nje, vingi tunatengeneza sisi wenyewe.
Sema taratibu kabla hujasikia katazo la kutengeneza kitu kama hujapewa kibali na mamlaka husika
 
Hivi kuna mtaala unaoeleweka unaotumika????

Vile vitabu vinavyotumika siku hizi mashuleni walishapitia kuona maajabu yake?

Hizo maabara zipo za kutosha?????

Walimu wapo wa kutosha?????


Vitabu na vitendea kazi vingine???




Kazi ipo aisee.......
 
Back
Top Bottom