Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Kikwete hakuacha watu wamsulubu spika bali alihitajia ushahidi kamili ,kama ilivyoonekana kuwa madai ni kuwa sitta anaupendeleo na anatumia nafasi yake kuidhoofisha serikali na Chama chake,lakini ukiangalia kwa makini utaona kuna kundi ambalo ndilo linaloingilia madaraka ya spika ,kundi hili limeshahau kuwa Bunge si mali ya Chama wala serikali iliyopo madarakani ,kundi hili limeshindwa kufahamu kuwa yanayojadiliwa bungeni ni mambo yanayowahusu waTz wote ,hivyo mambo hayo yanaweza kuwa na muelekeo wa kuisema serikali au chama chochote kile bila ya kujali uzito wake.

Kwa ufupi Kikwete amepata uhakika wa yale aliyokuwa akipelekewa vikaratasi kuwa kuwa ndani ya CCM kuna makundi ambayo ndio yanayosababisha mtafaruku ndani ya CCM na kukizidishia maradhi ya kufa chama hicho.

Naona ni bora kusubiri tuone Mheshimiwa Raisi wa CCM na Raisi wa Jamhuri ya (Muungano)Tanzania kutoa tamko lake kitaifa kuhusiana na mkutano uliokwisha ambao ni wa Chama Tawala hapa Tanzania ,hamu ya WaTanzania ni kumsikia Raisi kama Raisi na sio mwenye kiti akiwahabarisha WaTanzania hatma ya nchi yao chini ya Uongozi wa CCM ,letus wait & c.
 
guys,
according to me,it is not easy for j.k to get out of freuds SHADOW!:
-THE FREUDS ARE THE MAKING OF J.K INTO PRESIDENCY EXISTENCE

J.K will just go around and come around
 
sijui ni katiba au ni maamuzi ya ccm kuwa mwenyekiti lazima awe rais, watu wengine hawawezi kushika vyeo viwili kwa wakati mmoja
 
Naye mwenyekiti Kikwete,pamoja na kusema kuwa anampongeza Sitta kwa ujasiri wake, alionyesha wasiwasi wake jinsi spika anavyoendesha shughuli zake.

Alisema mambo ya ufisadi wanayojadili sharti iwe kwenye vikao vya chama na siyo bungeni; kwani yakipelekwa bungeni wanakuwa wameifanyia kazi kambi ya upinzani.

Kwa kauli hii Rais hatuna, mwoga mkubwa tena fisadi huyu. Siku zote nilikuwa namtetea Kikwete na kumtenga na ufisadi lakini kwa habari hizi, huyu naye ni fisadi mkubwa.
 
sijui ni katiba au ni maamuzi ya ccm kuwa mwenyekiti lazima awe rais, watu wengine hawawezi kushika vyeo viwili kwa wakati mmoja
unajua mkuu,haiitaji akili nyingi wewe kufikiria kubadili id yako!unajua kuna mtu anaitwa George Porgie,kwanin usiibadili yako?na ulimkuta!damn it!
 
unajua mkuu,haiitaji akili nyingi wewe kufikiria kubadili id yako!unajua kuna mtu anaitwa George Porgie,kwanin usiibadili yako?na ulimkuta!damn it!
Kwani sheria zinasemaje kuhusu ID na ikitokea memba anatumia ID inayofanana na memba mwengine kwa maandishi na matamshi, Mods plz tusaidieni.
 
Ndugu Pundamilia07,

Kama kweli unaamini kuwa yaliyojiri huko kikaoni ni kama ilivyoripotiwa hapo kwenye tovuti ya CCM, basi Spika Sita asingeweza kuwavaa Makamba na Chiligati kama ilivyoripotiwa hapa chini. Ndiyo maana watu tnasema kuwa tamko la CCM siyo la kuaminika kabisa, na hii inajionyesha pia katika sera zao, kwani waliahidi kuwa serikali ingepambana na rushwa hadi kuundwa kwa Tume kiinimacho ya Warioba lakini ilipofika utekelezaji wakaishia mitini.
.

Mkuu Kichuguu,
CCM ni taasisi na si chombo cha mtu binafsi. Hivyo basi kina utaratibu wake wa kuendesha wa kuwasiliana na wanachama wake pamoja na public. CCM katu haifanyika kazi kupitia magazeti bali ni kwa mujibi wa vikao na maelekezo mengine ya kiutendaji kupitia watendaji wake.
Kwa mantiki hiyo basi, taarifa zinazotolewa na magazeti si taarifa rasmi za yale yaliyofikiwa katika kikao cha NEC kule Dodoma.
Aidha, hayo magazeti yanayomnukuu spika au kuandika habari za Katibu Mkuu wa CCM au watendaji wengine wanafanya hivyo kwa sababu zao binafsi na wameshindwa kuripoti yale hasa yaliyofikiwa katika kikao hicho.
Ni kawaida kwa vyombo vya habari, hasa vya Tanzania kuandika kwa jinsi wanavyotaka wao bila ya kujali maslahi ya watumia habari hizo, matokeo yake ni upotoshaji usiokuwa na maana yeyote.
Kama nilivyosema hapa awali kuwa taarifa ya uhakika ipo wazi kabisa katika tovuti ya Chama Cha Mapinduzi kwa kila mtu aweze kusoma na kufahamu ni nini kilichofikiwa katika kikao kile.
 
Pundamilia07,
Mkuu mimi natoka nje kidogo ya hoja ya Mh. Sitta ila napenda kuelewa nini maana ya maamuzi haya ya chama CCM - wanaposema:-

8. KUHESHIMU VIONGOZI WASTAAFU
Mzee Mkapa anastahili pongezi sio kejeli, anastahili heshima na sio dharau, anastahili kuenziwa na sio matusi.
Kwa kuzingatia hayo, Halmashauri Kuu ya Taifa inatoa wito kwa wana CCM na Watanzania wote wenye nia njema na nchi yetu waache mara moja kumchafua na kumkejeli Mzee Mkapa na badala yake apewe heshima anayostahili na aachwe apumzike kwa amani.

Mkuu haya maneno yanaonyesha wazi kama ni vitisho kwa wananchi! kisha inaonyesha wazi chama hiki hakielewi kabisa nini msimamo wa wananchi na wanachosema kuhusu UFISADI kiasi kwamba malalamiko yao yanaonekana kuwa ni MZAHA na KEJELI..

Hivi kweli kikao kile kinafikiri wananchi wanamkejeli Mkapa kuhusiana na Ufisadi?.. Sidhani kama chama hiki kinaelewa uzito wa Ufisadi wananchi wanaozungumzia..
Ndio maana kila kitu kwao ni mzaha mzaha tu na kutumia maguvu badala ya elimu..Hivi kweli kuna jambazi au criminal yeyote kwa tafsiri fulani, anayeweza kusamehewa mauaji au wizi wake kwa sababu tu aliwahi fanya mazuri fulani before kabla ya ujambazi wake..Na wapi hili neno linasimama mkuu wangu tunaposema - NO one is above the Law!

Mkandara,
Nadhani nchi haiendeshwi kwa emotions bali kwa misingi ya sheria na si vinginevyo. Kitendo chochote cha kumkejeli au kumdharau Rais Mstaafu Mkapa hakiwezi kuvumiliwa na wale ambao wanataka kuendesha mambo kwa kufuata ustaarabu.
Sioni sababu kwani wale ambao wanamkejeli na kumdharau wasijitokeze na kutumia haki zao za kisheria kama wanaona kuwa ana makosa? Haileti Maana yeyote kumvunjia mtu heshima na utu wake kwa kufanya mambo bila ya kufuata sheria na taratibu zilizopo.
Kwa hiyo ni sahihi kabisa kwa Chama Cha Mapinduzi kuhakikisha kuwa kunakuwepo na kusudio maalum la kuzuia wale ambao hawataki au hawapendi kufuata taratibu hasa sheria.
 
Mkuu Kichuguu,
CCM ni taasisi na si chombo cha mtu binafsi. Hivyo basi kina utaratibu wake wa kuendesha wa kuwasiliana na wanachama wake pamoja na public. CCM katu haifanyika kazi kupitia magazeti bali ni kwa mujibi wa vikao na maelekezo mengine ya kiutendaji kupitia watendaji wake.
Kwa mantiki hiyo basi, taarifa zinazotolewa na magazeti si taarifa rasmi za yale yaliyofikiwa katika kikao cha NEC kule Dodoma.
Aidha, hayo magazeti yanayomnukuu spika au kuandika habari za Katibu Mkuu wa CCM au watendaji wengine wanafanya hivyo kwa sababu zao binafsi na wameshindwa kuripoti yale hasa yaliyofikiwa katika kikao hicho.
Ni kawaida kwa vyombo vya habari, hasa vya Tanzania kuandika kwa jinsi wanavyotaka wao bila ya kujali maslahi ya watumia habari hizo, matokeo yake ni upotoshaji usiokuwa na maana yeyote.
Kama nilivyosema hapa awali kuwa taarifa ya uhakika ipo wazi kabisa katika tovuti ya Chama Cha Mapinduzi kwa kila mtu aweze kusoma na kufahamu ni nini kilichofikiwa katika kikao kile.

Pundamilia07 unachokataa ni nini? kwamba Sitta hakujadiliwa NEC? mbona Chiligati ameongea na tukamsikia sauti yake? achilia magazeti. Tena bado tunaimani kubwa na magazeti kama Thisday na Mwanahalisi. Nadhani inakuuma sana kusikia yaliyotokea NEC, hiyo ndo CCM yetu mkuu, ndo maana wengine tumeacha kuisupport kabisa licha ya kuwa tunazokadi za hicho chama.
 
Pundamilia07,
Nitaendeleza zaidi sehemu zenye utata..maanake kila naposoma yaliyoajiri huko Dodoma kama ilivyoandikwa kwenye tovuti ya CCM, ndio kabisa nashindwa hata kuwatetea krtk maamuzi mengi waliyofanya maanake kikao hicho kimevunja sheria ktk maswala mengi sana ya BUnge letu..

Yaani wamejadili sana kazi za Bunge na uendeshaji wake kinyume cha sheria kiasi kwamba Kikao hiicho kimefikia hata MAAMUZI kuhusiana na uendeshaji wa Bunge kwa wabunge wa chama hicho.. Chama kimefikia kuwahoji, kuwataka Wabunge wake ushirikiano Bungeni kwa faida ya chama. Tena basi mnapanga mikakati na kuunda team kuhakikisha wabunge wanakiwakilisha chama na sii wananchi..inatisha kuona chama kikingiza siasa zake bungeni kimabavu badala ya kuhubiri nje kwa wananchi ili wapate waumini..

Hii hatari kubwa mkuu wangu mahitimisho mengi ktk kikao hicho yanawafungia Udikteta kwa sababu kinachotumika ni mawazo ya serikali yenye chama kimoja tu. Sijui kama CCM wanaelewa nini maana ya demokrasia na tofauti zake bungeni ktk utunzi wa sheria kwani sioni tofauti mawazo yao enzi za Ujamaa (chama kimoja) na sasa hivi!..

Mkuu Mkandara,
CCM hakuanzishwa ili ifanye kazi nyingine zaidi ya kushika madaraka ya kuongoza nchi hii. Na CCM haiwezi kuwa Chama kama hakina wanachama wake, viongozi unaowaona wewe ni sehemu tu ya wanachama waliopewa dhamana ya kukionoza chama ili kiweze kufikia malengo yake. Pamoja na mambo mengine mkusanyiko wote huo wa wananchama hauwezi kuwa na mwelekeo kama hakutakuwa na mshikamano, na ndiyo maana NEC imewakumbusha wanachama wake wakiwemo wabunge ambapo spika na mmoja wao kuwa wahimize ushirikiano miongoni mwao. Chama kimeona kuwa kuna mahali kuna utengamano basi ni jukumu lake kuwaweka sawa wanachama wake.
Aidha, Chama kimesisitiza kutumika kikamilifu kwa kamati ya wabunge wa CCM pale ambapo kuna haja ya kujadili kwa kina mambo yanayohusu wabunge wa Chama Cha Mapinduzi. ikumbukwe kwamba wabunge wa CCM mbali ya kuwa wanawajibika kwa wananchi, pia wanawajibika katika Chama Cha Mapinduzi.
 
Pundamilia07 unachokataa ni nini? kwamba Sitta hakujadiliwa NEC? mbona Chiligati ameongea na tukamsikia sauti yake? achilia magazeti. Tena bado tunaimani kubwa na magazeti kama Thisday na Mwanahalisi. Nadhani inakuuma sana kusikia yaliyotokea NEC, hiyo ndo CCM yetu mkuu, ndo maana wengine tumeacha kuisupport kabisa licha ya kuwa tunazokadi za hicho chama.

Mkuu Nemesis,
Mimi siko hapa kutaka kupokea sifa au kupotosha wachangiaji kama ambavyo ilivyofanywa huko nyuma na mmoja wa wanachama wa JF. Nia yangu ni kueleza kuwa yaliyofikiwa katika kikao cha NEC kule Dodoma. Kwa kawaida kufikia mwisho wa kikao huwa ni mchakato, lakini version ya mwisho kabisa inayotolewa ndiyo inayoeleza kikao kile kilikuwa kimejadili nini na kufikia tamati yake.
Sitaki kwenda kwenye ule upotoshaji uliofanywa hapa JF kwa malengo maalum ya kutaka kukipaka matope Chama Cha Mapinduzi, lakini ninachokusudia hapa ni kujaribu kuwaleta katika mazingira ya kuelewa kuwa baada ya kikao huwa ndiyo kunatolewa yale yote kikao hicho iliyokijadili na kufikia mwisho. Kwenye majadiliano si lazima kuwe formula maalum ya kila mtu aseme nini lakini hayo yote hujengea tamati.
Ninaendelea kusupport CCM kwa sababu ni chama changu na kama siridhishwi na jambo lolote chama kimeweka utaratibu wa kufikisha malalamiko yangu.
Ninajivunia kuwa Mwana CCM,
Ninajivunia kuwa Mtanzania.
 
Nafikiri hoja yako kuhusu uspika na uanachama si sahihi japo sina uhakika halisi wa mambo.

Rais si mbunge lakini akijivua uanachama wa ccm outomatically na urais unakoma hii ni kwa sababu aligombea urais kwa ticketi ya chama.Na hisi ndivyo vivyo kwa spika.


MkamaP.

Hili ni jambo gumu kidogo hasa kwetu na linaweza kuleta ubishi sana hasa ukizingatia jinsi katiba na kanuni za bunge zinavyotamka kwa kuzungukazunguka. Nadhani Makamba na Chiligati wanaliangalia jambo hili ama kwa ufinyu au kwa kutumia hii loophole ya Katiba kutokuwa starightforward. Hata hivyo ukiangalia kanuni za bunge na katiba kwa makini, utagundua kuwa mtu akishachaguliwa kuwa spika hawezi kupoteza kiti hicho kwa sababu ya kufukuzwa uanachama labda awe ni spika aliyechaguliwa kutokana na wabunge wa kuchaguliwa. Nadhani Sitta, ambaye ni mwanasheria, analijua hilo vizuri sana. Sina uhakika kama Sitta naye ni mbunge wa kuchaguliwa, mara ya mwisho nilikuwa nafahamu kuwa Msekwa hakuwa mbunge wa kuchaguliwa baada ya kuliachia jimbo lake la Ukerewe kwa mama Mongela. Na nadhani kuwa mbunge wa Urambo huko kwao Sitta ni Profesa Kapuya, kwa hiyo kama Sitta siyo mbunge wa kuchaguliwa basi hawezi kupoteza kiti chake cha uspika kwa kufukuzwa uanachama wa CCMkulingana na Kanuni na Katiba ya nchi kama nitakavyoeleza hapo chini.

Ukiangalia kanuni za Bunge zinasema hivi:

Kanuni za Bunge:


7.-(1) Kutakuwa na Uchaguzi wa Spika katika nyakati zilizowekwa
na lbara ya 86(l) ya Katiba, na Uchaguzi huo utafanywa kwa kura
ya siri kwa kufuata utaratibu uliowekwa na Kanuni hii.

(2) Kila Chama cha Siasa kitakuwa na haki ya kupendekeza jina
moja, ama la Mbunge wa Chama hicho, au la mtu mwingine yeyote
aliye na sifa za kuwa Mbunge, ambaye atakuwa mgombea uchaguzi wa
Spika. Endapo jina moja tu ndilo litakuwa limependekezwa,basi mgombea
huyo atahesabiwa kuwa anaungwa mkono na Vyama vyote
vilivyowakilishwa, Bungeni, kwa hiyo atatangazwa kuwa amechaguliwa
kuwa Spika bila kupingwa.
.
Utaona kuwa ingawa vyama vinapewa nafasi ya kupendekeza mtu kugombea uspika, siyo lazima vifanye hivyo, na siyo lazima wagombea wa uspika wawe wamependekezwa na vyama hivyo. Ndiyo maana kiti cha uspika alichokalia Sitta sasa kiligombewa na watu wawili wa kutoka chama kimoja: Sitta mwenyewe na Msekwa.


Halafu sasa Katiba ya jamhuri wa Tanzania inasema hivi:


84.-(1) Kutakuwa na Spika wa Bunge ambaye atachaguliwa na
Wabunge kutoka miongoni mwa watu ambao ni Wabunge au
wenye sifa za kuwa Wabunge; atakuwa ndiye kiongozi wa Bunge
na atawakilisha Bunge katika vyombo na vikao vingine vyote nje
ya Bunge.
.
.
.
.

(5) Spika atakoma kuwa Spika na ataacha kiti cha Spika
litokeapo lolote kati ya mambo yafuatayo -
(a) iwapo mtu huyo alichaguliwa kutoka miongoni mwa
Wabunge, basi ikiwa atakoma kuwa Mbunge kwa
sababu yoyote ambayo haihusiki na kuvunjwa Bunge;
au
(b) ikiwa kutatokea jambo lolote ambalo, kama
asingekuwa Spika, lingemfanya mtu huyo asiwe na
sifa za uchaguzi au apoteze sifa za uchaguzi wa
Spika; au
(c) Bunge litakapokutana kwa mara ya kwanza baada ya
Uchaguzi Mkuu uliofanywa baada ya Bunge kuvunjwa,
lakini masharti ya aya hii yatatumika bila ya kuathiri
Katiba hii; au
(d) ikiwa mtu huyo ataondolewa kwenye madaraka ya
Spika kwa azimio la Bunge lililoungwa mkono na
Wabunge amabo idadi yao haipungui theluthi mbili ya
Wabunge wote; au
(e) ikiwa mtu huyo atashindwa kuwasilisha kwa Rais
tamko rasmi kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo
(5) ya ibara hii; au
(f) ikiwa mtu huyo atapatikana na hatia kwa kosa la kutoa
habari za uongo, kwa kiapo kinyume cha sheria ya
Kanuni ya jinai, kuhusu tamko rasmi lolote lililotolewa
kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya (3) ya ibara
hii; au
(g) ikiwa mtu huyo atashindwa kuwasilisha kwa Rais
taarifa ya mali kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo
ya (5) ya ibara hii kabla ya kumalizika muda uliowekwa
kwa ajili hiyo kwa mujibu wa sheria iliotungwa na
Bunge;
(h) ikiwa itathibitika kuwa mtu huyo amevunja masharti ya
Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma.
.
.
.
.
(9) Mtu yeyote ambaye si Mbunge atakayechaguliwa kuwa
Spika, atatakiwa, kabla ya kuanza kutekeleza madaraka yake,
kuapishwa katika Bunge kiapo cha uaminifu
Hapa utagundua kuwa mtu kupoteza uachama wa chama chake hakuwezi kumfanya asiwe spika labda tu kama alichaguliwa huku akiwa mbunge wa kuchaguliwa kutoka jimboni, na hivyo amekosa sifa za kuwa mbunge wa kuchaguliwa. Kama nilivyosema huko nyuma, nadhani kuwa Sitta si mbunge wa jimbo lolote, kwa sababu mbunge wa huko kwao Urambo ni Profesa Kapuya. Kama Sitta ni mbunge wa kuchaguliwa basi itabidi afyate mkia kwa CCM.

Hii ni tofauti kabisa na sababu za mtu kupoteza ubunge ambapo katiba imesema wazi kuwa:


71.-(1) Mbunge atakoma kuwa Mbunge na ataacha kiti chake
katika Bunge litokeapo lolote kati ya mambo yafuatayo -

(e) ikiwa Mbunge ataacha kuwa mwanachama wa chama
alichokuwamo wakati alipochaguliwa au alipoteuliwa
kuwa Mbunge;

Nadhani hapa jambo linaloleta utata ni pale Katiba inaposema kuwa Spika anatakiwa awe mtu mwenye sifa za kuwa mbunge. Kuna wabunge waliogombea kupitia vyama vyao ambao wakipoteza sifa za uanachama basi wanakuwa wamepoteza sifa ya ubunge, lakini kuna wabunge ambao hawakugombea kupitia cvhama ambao kupoteza uanachama hakuathiri sifa zao. Katiba hiyo inatoa sifa za mtu yeyote kuwa mbunge kama ifuatavyo:

67.-(1) Bila ya kuathiri masharti yaliyomo katika ibara hii, mtu
yeyote atakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa
kuwa Mbunge endapo-
(a) ni raia wa Jamhuri ya Muungano aliyetimiza umri wa
miaka ishirini na moja, na ambaye anajua kusoma na
kuandika katika Kiswahili au Kiingereza;
(b) ni mwanachama na ni mgombea aliyependekezwa na
chama cha siasa;

(c) katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya
Uchaguzi hakuwahi kutiwa hatiani katika mahakama
yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote
ya Serikali.
Utata upo hapo kwenye kifungu hicho 67-(1)(b) ambacho kilikuwa kimelenga wabunge wa kuchaguliwa. Kwa bahati nzuri katiba hiyo pia inataja aina nyingine za wabunge kama ifuatavyo:
66.-(1) Bila ya kuathiri masharti mengine ya ibara hii, kutakuwa
na aina zifuatazo za Wabunge, yaani-
(a) Wabunge waliochaguliwa kuwakilisha majimbo ya
uchaguzi;
(b) Wabunge wanawake wa idadi inayoongezeka, kuanzia
asilimia ishirini ya Wabunge waliotajwa katika aya ya
(a), (c ) na (d), itakayotajwa mara kwa mara na Tume
ya Uchaguzi kwa taarifa iliyochapishwa katika Gazeti
la Serikali baada ya kupata kibali cha Rais,
watakaochaguliwa na vyama vya siasa
vinavyowakilishwa Bungeni, kwa mujibu wa ibara ya
78, na kwa kuzingatia masharti ya uwiano wa
uwakilishi baina ya vyama hivyo;
(c) Wabunge watano waliochaguliwa na Baraza la
Wawakilishi kutoka miongoni mwa wajumbe wake;
(d) Mwanasheria Mkuu;
(e) Wabunge wasiozidi kumi walioteuliwa na Rais kutoka
miongoni mwa watu wenye sifa kwa mujibu wa ibara
ya 67,isipokuwa sifa iliyotajwa katika ibara ya
67(1)(b)
.
Hebu angalia kifungu 66.-(1)(e) hapo juu kinavyyonyesha kuwa sifa hiyo ya uancahama kama iliyowekwa kwenye 67(1)(b) siyo ya lazima sana katika sifa za ubunge kwa jumla. Ufafanuzi zaidi umetolewa na kifungu cha 67-(2) kinachoorodhesha mambo yanayomkosesha mtu yeyote sifa ya kuwa mbunge ;pia hakitamki upotevu wa uanachama.


67-(1).
Bila ya kuathiri................
.
.
.
(2) Mtu hatakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa
kuwa Mbunge-
(a) ikiwa mtu huyo anao au kwa hiari yake amejipatia
uraia wa nchi nyingine yote; au
(b) ikiwa kwa mujibu wa sheria inayotumika katika
Jamhuri ya Muungano imethibitishwa rasmi kwamba
mtu huyo ana ugonjwa wa akili; au
(c) ikiwa mtu huyo amehukumiwa na Mahakama yoyote
katika Jamhuri ya Muungano na kupewa adhabu ya
kifo au ya kufungwa gerezani kwa muda unaozidi
miezi sita kwa kukutwa na hatia ya kosa lolote,
vyovyote linavyoitwa, linaloambatana na utovu wa
uaminifu; au
(d) ikiwa katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe
ya Uchaguzi Mkuu amepata kuhukumiwa na kupewa
adhabu ya kifungo kwa kosa linaloambatana na utovu
wa uaminifu au kwa kuvunja sheria ya Maadili ya
Viongozi wa Umma;
(e) bila ya kuingilia haki na uhuru wa mtu kuwa na maoni
yake, kuamini dini atakayo, kushirikiana na wengine
na kushiriki shughuli za umma kwa mujibu wa sheria
za nchi, ikiwa mtu huyo si mwanachama na mgombea
aliyependekezwa na chama cha siasa;
 
mkuu Pundamilia07 naona kweli wewe umekunywa maji ya bendera ya CCM yaani huwezi kuona wala kusikia. Mkuu, unataka kanuni za bunge zitumike wapi sasa? yaani wenye uhuru wa kuongea bungeni ni wapinzani tu, CCM wanapswa kuongea kwenye kamati yao siyo bungeni hapo ni kuweka mabunge mawili!

Mbona kipindi kile bunge linamsulubu Idd Simba haya hayakutokea? eti kwasababu sasa wanaguswa akina Rostam na Lowasa ndo nchi inawaka moto!

Dhana ya NEC ni ya upotoshaji sana, inataka kuweka mabunge mawili yaani lile la CCM (wanaita kamati) na ndo liwe bunge la maamuzi chini ya Waziri Mkuu na lile bunge chini ya spika kwa ajili ya kupitisha yaliyoamuliwa na CCM! yaani mkuu Pundamilia ndo unachosisitiza siyo?
 
Mkuu Nemesis,
Mimi siko hapa kutaka kupokea sifa au kupotosha wachangiaji kama ambavyo ilivyofanywa huko nyuma na mmoja wa wanachama wa JF. Nia yangu ni kueleza kuwa yaliyofikiwa katika kikao cha NEC kule Dodoma. Kwa kawaida kufikia mwisho wa kikao huwa ni mchakato, lakini version ya mwisho kabisa inayotolewa ndiyo inayoeleza kikao kile kilikuwa kimejadili nini na kufikia tamati yake.
Sitaki kwenda kwenye ule upotoshaji uliofanywa hapa JF kwa malengo maalum ya kutaka kukipaka matope Chama Cha Mapinduzi, lakini ninachokusudia hapa ni kujaribu kuwaleta katika mazingira ya kuelewa kuwa baada ya kikao huwa ndiyo kunatolewa yale yote kikao hicho iliyokijadili na kufikia mwisho. Kwenye majadiliano si lazima kuwe formula maalum ya kila mtu aseme nini lakini hayo yote hujengea tamati.
Ninaendelea kusupport CCM kwa sababu ni chama changu na kama siridhishwi na jambo lolote chama kimeweka utaratibu wa kufikisha malalamiko yangu.
Ninajivunia kuwa Mwana CCM,
Ninajivunia kuwa Mtanzania.

sawa Mkuu nimekupata vizuri sana, lakini huoni kama maamuzi ya NEC yanapingana na katiba ya nchi? inayotamka kwamba bunge ni mhimili mwingine wa dola?

Mkuu, kumbuka kuwa FMES alipoleta thread yake hapa ilihusu yaliyojiri kwenye kikao cha NEC. Haikuhusu maamuzi ya NEC! Jamaa alikuwa anatoa taswira ya kilichokuwa kimetokea kikaoni, iwe kwa nia mbaya au nzuri. Hapa JF yanatolewa mambo mengi tu juu ya watu au vyema yenye nia mbaya au nzuri. Hivyo, jamaa alikuwa sahihi wala hakulenga kupotosha kwasababu aliyokuwa ameyaleta ndiyo yaliyotokea ktk kikao hicho, rejea yanayoendelea kuandika na kusemwa na Makamba, Chiligati, Sitta na media kwa ujumla. Soma Mwanahalisi ya wiki hii.

Hivyo, naomba utofautishe mambo yaliyojiri/yaliyojitokeza na maazimio.

Mkuu, mantiki na chanzo cha maamuzi ya NEC ni vita dhidi ya ufisadi. Kashfa ya Richmond/Dowans, CIS na EPA ndiyo yaliyosababisha yote hayo. Sasa huoni kama chama kinajiingiza ktk ufisadi? huoni kama wanaoshutumiwa kwa ufisadi ndiyo wanaotuamulia CCM yetu iongozwe namna gani? Hivi kesho tukishinda sisi wanaCCM tunaopinga ufisadi utaipongeza CCM au utaiponda? come on man, huruma kwa Watanzania mkuu.

Kusema kweli NEC imeivuruga sana CCM than anytime before. NEC inataka kuvuruga kabisa bunge, lengo ni kuwafunika malwatani mafisadi.
 
[I said:
Nemesis;562530]Kwa kauli hii Rais hatuna, mwoga mkubwa tena fisadi huyu. Siku zote nilikuwa namtetea Kikwete na kumtenga na ufisadi lakini kwa habari hizi, huyu naye ni fisadi mkubwa[/I].

Taarifa nilizo nazo ni kuwa kuna sentensi aliitoa ambayo iliudhi watu walipomwambia asimpe uwaziri mkuu Lowasa kwa kuwa ni kibaka atakayemletea shida kwenye utawala wake hakusikia akajifanya kiziwi hakuwajibu pale bali alikurupuka akaenda kujichagulia mawaziri wake akina Lowasa na akina Karamagi kinyume na ushauri.Halafu akaamua kuwapiga vijembe waliomwonya asimpe Lowasa uwaziri mkuu kwa kutoa hotuba akijigamba kuwa Uraisi hauna ubia na uwaziri hausomewi alipokuwa akitangaza hilo baraza lake liliokuwa limejaa watuhumiwa vibaka akina Lowasa,Chenge,Karamagi,Msabaha,Basil Mramba na wakwapuaji wengine wa kuanzia mifukoni kwenye mifuko ya hazina hadi mitaani kwenye Richmond n.k

Kutokana na kujigamba kuwa Uraisi hauna ubia na uwaziri hausomewi watu makini wakamwona kuwa ni jeuri asiyejua kuwa uraisi ni taasisi na sio one man show business wakambwaga aendelee peke yake na ujuaji wake.Matokeo yake mafisadi wanampeleka puta hadi kwenye vikao vya chama na kuyumbisha vikao.

Taarifa nilizo nazo ni kuwa mafisadi walikiogopa sana kikao cha NEC Dodoma walikuwa hawalali wakiogopa kuwa huenda watafukuzwa uanachama na kunyang`anywa kadi Dodoma kutokana na tuhuma mbalimbali zinazowakabili zinazokidhalilisha chama.Walikuwa hawaogopi Kikwete,wala Makamba wala Chiligati hofu yao walikuwa wakiogopa kuwa waweza tokea wajumbe wendawazimu wapingao ufisadi wakatoa ajenda ya wao kufukuzwa ndani ya chama na wakaungwa mkono na wengi na ukawa mwisho wao.

Mafisadi Wakapanga mikakati ya kuwahi kuipiga chini hiyo hoja isije ikaibuliwa na wajumbe kwa kuwa outspoken mapema dhidi ya spika na bunge ili kubadili mwelekeo wa upepo upesi usivume kuelekea kwao.Bahati mbaya kutokana na ufinyu wa kufikiri Mwenyekiti,Makamba na akina Chiligati na Msekwa wakapoteza direction ya uendeshaji kikao wakajikuta wanalaani spika na bunge kwa kuishambulia serikali badala ya mafisadi.

Ndio maana mara baada ya kikao kile cha NEC watuhuhumiwa wa ufisadi walikesha wakilewa usiku kucha na kupongezana kusherehekea kitu kimoja kikubwa nacho ni kutofukuzwa uanachama wa CCM na kutonyang`anywa kadi za CCM.Na ndio maana hata Lowasa aliitisha sherehe kubwa ya kuzaliwa kwake kabla ya tarehe yake ya kuzaliwa akaita na viongozi wengi wa dini kusherehekea kutonyang`anywa uanachama na kufukuzwa CCM kwa kisingizio cha birthday.Hakuamini macho yake kuwa katoka salama bila kutimuliwa CCM kwenye kile kikao cha NEC.Viongozi maarufu wa dini mbalimbali nao walikuwepo katika sherehe ile kuitikia AMINAAAAAA ndefu sana kwenye sala kabla ya kula pilau lilogawiwa kwao lilotokana na hela tuhumiwa za ufisadi na walimalizia kwa sala ndefu za kuwaombea dua Mungu wa vibaka awaepushe na wale wanaowataka wawajibike kwa wizi wa pesa za Richmond.Viongozi wa dini nao mmmhhh kwa pilau nao wamo.Hawaangalii pilau limepikwa na Mungu au Ibilisi wakisikia harufu ya pilau tu lazima wakurupukie huko inakonukia maana Pilau haina dini ukiiuliza ni dini gani hata mwehu au mtakatifu atakwambia haina dini kwa hiyo haina ubaya kuipokea hata ikiwa ni ya jambazi lililoua likapora ili likuletee kama sadaka.
 
sawa Mkuu nimekupata vizuri sana, lakini huoni kama maamuzi ya NEC yanapingana na katiba ya nchi? inayotamka kwamba bunge ni mhimili mwingine wa dola?

Mkuu, kumbuka kuwa FMES alipoleta thread yake hapa ilihusu yaliyojiri kwenye kikao cha NEC. Haikuhusu maamuzi ya NEC! Jamaa alikuwa anatoa taswira ya kilichokuwa kimetokea kikaoni, iwe kwa nia mbaya au nzuri. Hapa JF yanatolewa mambo mengi tu juu ya watu au vyema yenye nia mbaya au nzuri. Hivyo, jamaa alikuwa sahihi wala hakulenga kupotosha kwasababu aliyokuwa ameyaleta ndiyo yaliyotokea ktk kikao hicho, rejea yanayoendelea kuandika na kusemwa na Makamba, Chiligati, Sitta na media kwa ujumla. Soma Mwanahalisi ya wiki hii.

Hivyo, naomba utofautishe mambo yaliyojiri/yaliyojitokeza na maazimio.

Mkuu, mantiki na chanzo cha maamuzi ya NEC ni vita dhidi ya ufisadi. Kashfa ya Richmond/Dowans, CIS na EPA ndiyo yaliyosababisha yote hayo. Sasa huoni kama chama kinajiingiza ktk ufisadi? huoni kama wanaoshutumiwa kwa ufisadi ndiyo wanaotuamulia CCM yetu iongozwe namna gani? Hivi kesho tukishinda sisi wanaCCM tunaopinga ufisadi utaipongeza CCM au utaiponda? come on man, huruma kwa Watanzania mkuu.

Kusema kweli NEC imeivuruga sana CCM than anytime before. NEC inataka kuvuruga kabisa bunge, lengo ni kuwafunika malwatani mafisadi.
Haswaa mkuu wangu.. Pundamilia 07, anashindwa kuelewa kwamba yaliyoandikwa ktk tovuti ya chama ni hitimisho la mkutano mzima kwa vifungu vyake. Hakuna maelezo ya yaliyoajiri kabla ya kufikia maamuzi hayo.

Hakuna sehemu inaonyesha hoja, kubishana au hata kutamkwa kwa jina la mwanachama yeyote acha mbali jina la Spika au Mwenyekiti isipokuwa majina matatui tu ya kamati iliyoundwa..hakuna sehemu inaonyesha wazi ni hatua gani zilipitiwa hadi kufikia uamuzi wa kuteua kamati hiyo lakini mtu yeyote akisoma kwa makini report hiyo atagundua kwamba Mheshimiwa Spika Sitta hakuwekwa kiti moto kwa makosa alofanya akiwa kama mwanachama wa chama hicho ila akiwa kama Spika wa Bunge..Haya ni makosa na bila shaka kikao cha NEC CCM wamekiuka Ibara ya 100 ya katiba ya nchi..Na hata Wabunge wameshutumiwa kwa uwakilishi wao bungeni kinyume cha matakwa ya baadhi ya watu wachache na kibaya zaidi wasitumie hata vifungu vya sheria au katiba ya chama hicho kuwalaumu isipokuwa maneno ya dharau na kashfa kwa wabunge na bunge lenyewe ati kwa maslahi ya chama.

Ndio maana mwanzo nilitetea haki ya chama kumsimamisha mtu yeyote na kumweka kitimoto ikiwa swala lenyewe linahusu uwakilishi wake kama mwanachama wa CCM (against Mrengo, Ilani, sera)..Na nikasema ikiwa Spika Sitta akitumia kadi ya chama alijaribu kukigawa chama makusudi kwa kueneza habari za Uongo iwe bungeni au nje ya bunge basi chama kina haki ya kumweka kitimoto lakini kutokana na taarifa ya chama inaonyesha wazi chama kilimweka kitimoto kutokana na utendaji wake wa kazi akiwa Spika wa Bunge...Yaani Spika angenyang'anywa kadi ya chama kutokana na maswala yanayoendeshwa bungeni.

Halafu basi cha ajabu Pundamilia anazidi kusema tunawasikiliza wazushi waandishi wa habari ambao wanaandika habari na hotuba zilizotolewa na viongozi wao. Yaani anataka sisi tuamini kuwa alosema Chiligati, Tambwe, Spika Sitta, rais na wajumbe wengine wote ni Uongo mtupu isipokuwa ukweli upo ktk tovuti ya chama..Yaani hata Chiligati ni mzushi asojulikana wala hawakilishi chama.

Sasa tuseme habari nyingine zoote tunazosikia toka vyombo vya habari bila kuandikwa ktk tovuti ya chama ni Uongo au kuna kitu ambacho mimi sikielewi?..Ni wakati gani tunatakiwa kuamini yaliyoandikwa magazetini yanatokana na yale yaliyoajili ktk kikao cha chama, kabla ya kufikia maamuzi yaliyofikiwa.

Tovuti ya chama haikuandika lolote kuhusu Spika Sitta kuwekwa kitimoto, haikuandika chochote kuhusiana na mtu yeyote, hivyo ndugu yangu Pundamilia anataka sisi tuamini kuwa haikujadiliwa kabisa kuhusu Spika Sittayaliyoandikwa magazeti kuwa hapakuwa na agenda yeyote inayohusiana na Spika Sitta..
 
Last edited:
sawa Mkuu nimekupata vizuri sana, lakini huoni kama maamuzi ya NEC yanapingana na katiba ya nchi? inayotamka kwamba bunge ni mhimili mwingine wa dola?

Mkuu, kumbuka kuwa FMES alipoleta thread yake hapa ilihusu yaliyojiri kwenye kikao cha NEC. Haikuhusu maamuzi ya NEC! Jamaa alikuwa anatoa taswira ya kilichokuwa kimetokea kikaoni, iwe kwa nia mbaya au nzuri. Hapa JF yanatolewa mambo mengi tu juu ya watu au vyema yenye nia mbaya au nzuri. Hivyo, jamaa alikuwa sahihi wala hakulenga kupotosha kwasababu aliyokuwa ameyaleta ndiyo yaliyotokea ktk kikao hicho, rejea yanayoendelea kuandika na kusemwa na Makamba, Chiligati, Sitta na media kwa ujumla. Soma Mwanahalisi ya wiki hii.

Hivyo, naomba utofautishe mambo yaliyojiri/yaliyojitokeza na maazimio.

Mkuu, mantiki na chanzo cha maamuzi ya NEC ni vita dhidi ya ufisadi. Kashfa ya Richmond/Dowans, CIS na EPA ndiyo yaliyosababisha yote hayo. Sasa huoni kama chama kinajiingiza ktk ufisadi? huoni kama wanaoshutumiwa kwa ufisadi ndiyo wanaotuamulia CCM yetu iongozwe namna gani? Hivi kesho tukishinda sisi wanaCCM tunaopinga ufisadi utaipongeza CCM au utaiponda? come on man, huruma kwa Watanzania mkuu.

Kusema kweli NEC imeivuruga sana CCM than anytime before. NEC inataka kuvuruga kabisa bunge, lengo ni kuwafunika malwatani mafisadi.

Nemesis!

Kama bado wewe unafikiri CCM bado ni chama cha siasa nadhani umepotea. Wana- CCM wa leo ni kundi la majambazi under the umbrela of the defunct CCM under Nyerere. Na kama bado unaamini kwamba wewe ni mwanachama imekula kwako! wewe ni kipofu na mtu anapokula na kipofu utaratibu ni kutomgusa asije fikiri chakula kimekwisha.

Mziki unapokaribia mwisho na mara nyingi ndipo utamu hukolea ha-ha-haaa!

The days are numbered for the rulling party kwani hao akina Nemesis watakapofungua macho hapa hapakaliki let us wait and see! Nadhani huu mchama kuna kila dalili utamfia JMK mikononi kama akiendelea kutabasamu. Na kwa taarifa yao kundi la Spika ni kubwa japo hawana pesa!!
 
Kuna mtu mmoja maarufu alikuwa kitumia usemi "Hoja hujibiwa kwa hoja", sasa kama huna hoja ya kujibu hoja ya mwenzako kwani ni lazima uchangie hoja yake?. Regardless na unavyoona wewe huyu mwanzisha thread ameeleza kitu ambacho kila mtu makini atakuwa anakifikiria japo katika uwakilishi wa hoja yake hakuwa consistent kwani katika vitu vitatu ameeleza kimoja tu.

Ila Hoja yake ni nzito na ina ukweli. Ya mangungo au Karl Peters et al ni katika kuweka kivumishi cha hoja yake tu. sasa kama wewe ni mwalimu wa historia ilikuwa ni busara kuweka ukweli badala ya kushutumu

Hili suala la Mangungo mimi kwangu ni personal na nataka kuweka record straight. Mangungo hakuuza nchi na hakuna transaction yoyote iliyotokea. Hila himaya yake ilikuwa ndogo na ilipakana na ya wahehe. Wahehe walikuwa wanafanya expansion yako kwa kuvamia himaya ndogondogo. Na wajerumani walipokuja, himaya ndogo zilichukua protection ya mjerumani. Kilichotokea hapa ni Adui wa rafiki yako ni rafiki yako.

Tukirudi kwenye mada, huwezi kushinda bahati nasibu bila kucheza bahati nasibu. Watu mnataka kujifunza lessons ya Dodoma wakati participation ya yenu ya kisiasa ni ndogo. Nendeni kagombeeni nafasi za kisiasa na mnaweza kuleta mabadiliko.
 
Back
Top Bottom