Halisi
JF-Expert Member
- Jan 16, 2007
- 2,802
- 617
Sitta afyatuka tena
• Amshukia Makamba, Chiligati wanaomshambulia nje ya NEC
na Mwandishi Wetu, Tabora
SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Samuel Sitta, amesema anakerwa na kauli za upande mmoja zinazoendelea kutolewa na viongozi wa ofisi ndogo ya Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na baadhi ya wajumbe wa Halmashari Kuu ya chama hicho (NEC), badala ya kusubiri ripoti ya kamati iliyoundwa na NEC, imalize kazi yake.
Sitta ambaye hii ni mara yake ya pili kuzungumza hadharani tangu aliposulubiwa na NEC, mjini Dodoma wiki moja iliyopita, alisema hayo jana kwenye mkutano wake na waandishi wa habari, uliofanyika jimboni kwake Urambo, mkoani Tabora.
Ingawa hakuwataja majina, lakini ni wazi kwamba Sitta alikuwa akimlenga Katibu Mkuu wa CCM, Luteni Yusuf Makamba na Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa, Kapteni John Chiligati na baadhi ya wajumbe wa NEC ambao kwa nyakati tofauti, wamekaririwa na vyombo vya habari wakitetea uhalali wa CCM kumshughulikia Sitta na wabunge wanaojifanya wapiganaji wa vita dhidi ya ufisadi wakati wa mkutano wa NEC.
"Nilitarajia watu wa makao makuu ya CCM, kuzingatia na kusubiri uamuzi wa kamati iliyoundwa na NEC ambayo inaongozwa na mzee Mwinyi pamoja na wajumbe wengine, hivyo si busara kwa namna yoyote kwamba kama hutaki malumbano, kwanini unaendelea kutoa maneno?" alihoji Sitta.
Sitta ambaye siku za hivi karibuni amekuwa akiandamwa na kashfa mbalimbali, huku akijizolea umaarufu kutokana na msimamo wake wa kuliendesha Bunge kwa stahili yake ya viwango, alisisitiza kuwa hataki kujibu lolote, lakini anakerwa na hali ya malumbano inayoendelea sasa.
"Mimi nadhani sasa tuache maneno na kejeli nje ya NEC wakati tayari kuna kamati imeundwa kuchunguza malumbano ndani na nje ya Bunge, ningeshauri watu wa makao makuu ya chama, waiachie kamati hiyo ifanye kazi yake ili ijue tatizo, kama ni mimi au kama kuna tatizo pana zaidi," alisisitiza.
Kuhusu yaliyotokea ndani ya NEC, Sitta alisema kuna kundi la watu linalojaribu kumwekea maneno mdomoni ili kumletea picha mbaya mbele ya jamii na kuonyesha kwamba hafai.
Akitolea mfano wa baadhi ya maneno aliyodai amewekewa mdomoni na kundi hilo la wabaya wake, ni pamoja na kauli kwamba aliomba radhi ndani ya kikao cha NEC, na kwamba kamati iliyoundwa ni kwa ajili ya kuchunguza mwenendo wake.
"Hayo yamekolezwa tu na baadhi ya magazeti, mimi daima nitasimamia katika ukweli na niwaambie tu kwamba tume iliyoundwa ipo kwa ajili ya kusuluhisha makundi yanayohasimiana ndani ya chama, si kwa ajili ya uendeshaji wa Bunge,"
"Mimi sikuomba radhi na kama niliomba, niliomba kwa kosa lipi? Mimi sikuwa na tuhuma yoyote na kama ingekuwapo, wangeipeleka kwenye Kamati ya Maadili, kwani ndani ya CCM, upo utaratibu wa kumtuhumu mwanachama pamoja na kumpelekea barua inayoonyesha tuhuma zake, mimi sikuletewa barua yoyote kwamba ninatuhumiwa kwa yanayoenezwa," alisema Sitta.
Kwa mujibu wa Sitta, kamati iliyoundwa itakuwa na kazi ya kupokea maoni mbalimbali kutoka kwa wabunge wa CCM ili kujua matatizo yao, jambo ambalo litasaidia kujua kiini cha malumbano ili kuchukua hatua za kudhibiti hali hiyo.
Akizungumzia madai ya NEC kwamba amekuwa akipanga watu wa kuzungumza bungeni, Sitta alisema madai hayo si ya kweli, kwani kila mbunge amekuwa akifuata utaratibu ambao ni kujaza fomu kwa Katibu wa Bunge, ambaye naye humpelekea Spika huku kila kitu kikiwa kimekamilika.
"Zipo fomu za kuchangia mjadala, ndizo zinatumika kwa wabunge wanaotaka kuchangia mjadala, hivyo mimi siwezi kujua mbunge anataka kuchangia nini au kwenye swali la nyongeza anataka kuongeza nini," alisema Sitta.
Juzi Sitta aliwasili mkoani hapa na kuweka bayana msimamo wake kwamba ataendeleza kasi ile ya mapambano dhidi ya ufisadi, pasipo kutetereka.
Akihutubia mamia ya wananchi waliojitokeza kumsikiliza katika viwanja vya CCM mjini Urambo, Sitta alisema yeye ni mzima wa afya na yuko imara na kusisitiza kuwa ataendelea na kasi ile ile.
Hivi karibuni, Makamba alisema chama hicho kina haki ya kumhoji Sitta na wabunge wote wa chama hicho, kwani wote ni mali ya chama hicho tawala.
Alipoulizwa juu ya mkanganyiko wa kauli mbili za viongozi wa juu wa chama hicho, Chiligati na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Propaganda, Tambwe Hizza, zilizotofautiana, Makamba alisema kauli halali ya chama ni ile iliyotolewa na Chiligati.
Wakati Makamba akitamba kuwa chama hicho kina haki ya kumhoji Sitta kama kilivyofanya katika vikao vyake vilivyopita, wiki iliyopita Tambwe alitoa tamko kwa vyombo vya habari linaloonyesha dhahiri kupindisha tafsiri ya maamuzi ya vikao hivyo, baada ya maamuzi hayo kuonekana kupata upinzani mkubwa kutoka kwa wadau mbalimbali nchini.
Katika tamko hilo, Tambwe alisema vikao hivyo havikujadili ajenda yoyote iliyowahusu Sitta na wabunge wenzake, wala iliyomhusu Makamba, aliyedaiwa kuwa ilikuwa nusura ang'olewe.
Wiki moja iliyopita, Sitta alibanwa ndani ya NEC na ilidaiwa aliomba radhi na kunusurika katika hatari ya kupoteza uanachama.
Hatua hiyo ya Sitta kuomba radhi ilikuja baada ya wajumbe takriban wote wa vikao viwili vya juu vya Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) vya chama hicho kujenga hoja za kumshambulia, wakipinga namna anavyoliendesha Bunge katika mwelekeo wa kukidhalilisha chama hicho na serikali yake.
Tukio hilo baya kabisa kuwahi kumfika Sitta ambaye amekuwa akijinadi kuwa ni spika wa kasi na viwango, lilihitimishwa na uamuzi wa NEC kuunda kamati maalumu kuchunguza kiini cha kufikia hapo.
Kamati hiyo maalumu inaongozwa na Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi na wajumbe wengine ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Tanzania Bara), Pius Msekwa na mwanasiasa mkongwe, Abdulrahman Kinana.
Kwa mujibu wa habari hizo, mwelekeo wa wana CCM hao kutaka kumwadhibu Sitta, ambaye katika siku za hivi karibuni amejizolea umaarufu wa kisiasa ndani na nje ya Bunge, hata kuwa na uwezo wa kumnyoshea kidole mtu au taasisi yoyote, ulianza kujitokeza tangu wakati wa kikao cha Kamati Kuu mjini Dodoma.
http://www.freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=8034
• Amshukia Makamba, Chiligati wanaomshambulia nje ya NEC
na Mwandishi Wetu, Tabora
Sitta ambaye hii ni mara yake ya pili kuzungumza hadharani tangu aliposulubiwa na NEC, mjini Dodoma wiki moja iliyopita, alisema hayo jana kwenye mkutano wake na waandishi wa habari, uliofanyika jimboni kwake Urambo, mkoani Tabora.
Ingawa hakuwataja majina, lakini ni wazi kwamba Sitta alikuwa akimlenga Katibu Mkuu wa CCM, Luteni Yusuf Makamba na Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa, Kapteni John Chiligati na baadhi ya wajumbe wa NEC ambao kwa nyakati tofauti, wamekaririwa na vyombo vya habari wakitetea uhalali wa CCM kumshughulikia Sitta na wabunge wanaojifanya wapiganaji wa vita dhidi ya ufisadi wakati wa mkutano wa NEC.
"Nilitarajia watu wa makao makuu ya CCM, kuzingatia na kusubiri uamuzi wa kamati iliyoundwa na NEC ambayo inaongozwa na mzee Mwinyi pamoja na wajumbe wengine, hivyo si busara kwa namna yoyote kwamba kama hutaki malumbano, kwanini unaendelea kutoa maneno?" alihoji Sitta.
Sitta ambaye siku za hivi karibuni amekuwa akiandamwa na kashfa mbalimbali, huku akijizolea umaarufu kutokana na msimamo wake wa kuliendesha Bunge kwa stahili yake ya viwango, alisisitiza kuwa hataki kujibu lolote, lakini anakerwa na hali ya malumbano inayoendelea sasa.
"Mimi nadhani sasa tuache maneno na kejeli nje ya NEC wakati tayari kuna kamati imeundwa kuchunguza malumbano ndani na nje ya Bunge, ningeshauri watu wa makao makuu ya chama, waiachie kamati hiyo ifanye kazi yake ili ijue tatizo, kama ni mimi au kama kuna tatizo pana zaidi," alisisitiza.
Kuhusu yaliyotokea ndani ya NEC, Sitta alisema kuna kundi la watu linalojaribu kumwekea maneno mdomoni ili kumletea picha mbaya mbele ya jamii na kuonyesha kwamba hafai.
Akitolea mfano wa baadhi ya maneno aliyodai amewekewa mdomoni na kundi hilo la wabaya wake, ni pamoja na kauli kwamba aliomba radhi ndani ya kikao cha NEC, na kwamba kamati iliyoundwa ni kwa ajili ya kuchunguza mwenendo wake.
"Hayo yamekolezwa tu na baadhi ya magazeti, mimi daima nitasimamia katika ukweli na niwaambie tu kwamba tume iliyoundwa ipo kwa ajili ya kusuluhisha makundi yanayohasimiana ndani ya chama, si kwa ajili ya uendeshaji wa Bunge,"
"Mimi sikuomba radhi na kama niliomba, niliomba kwa kosa lipi? Mimi sikuwa na tuhuma yoyote na kama ingekuwapo, wangeipeleka kwenye Kamati ya Maadili, kwani ndani ya CCM, upo utaratibu wa kumtuhumu mwanachama pamoja na kumpelekea barua inayoonyesha tuhuma zake, mimi sikuletewa barua yoyote kwamba ninatuhumiwa kwa yanayoenezwa," alisema Sitta.
Kwa mujibu wa Sitta, kamati iliyoundwa itakuwa na kazi ya kupokea maoni mbalimbali kutoka kwa wabunge wa CCM ili kujua matatizo yao, jambo ambalo litasaidia kujua kiini cha malumbano ili kuchukua hatua za kudhibiti hali hiyo.
Akizungumzia madai ya NEC kwamba amekuwa akipanga watu wa kuzungumza bungeni, Sitta alisema madai hayo si ya kweli, kwani kila mbunge amekuwa akifuata utaratibu ambao ni kujaza fomu kwa Katibu wa Bunge, ambaye naye humpelekea Spika huku kila kitu kikiwa kimekamilika.
"Zipo fomu za kuchangia mjadala, ndizo zinatumika kwa wabunge wanaotaka kuchangia mjadala, hivyo mimi siwezi kujua mbunge anataka kuchangia nini au kwenye swali la nyongeza anataka kuongeza nini," alisema Sitta.
Juzi Sitta aliwasili mkoani hapa na kuweka bayana msimamo wake kwamba ataendeleza kasi ile ya mapambano dhidi ya ufisadi, pasipo kutetereka.
Akihutubia mamia ya wananchi waliojitokeza kumsikiliza katika viwanja vya CCM mjini Urambo, Sitta alisema yeye ni mzima wa afya na yuko imara na kusisitiza kuwa ataendelea na kasi ile ile.
Hivi karibuni, Makamba alisema chama hicho kina haki ya kumhoji Sitta na wabunge wote wa chama hicho, kwani wote ni mali ya chama hicho tawala.
Alipoulizwa juu ya mkanganyiko wa kauli mbili za viongozi wa juu wa chama hicho, Chiligati na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Propaganda, Tambwe Hizza, zilizotofautiana, Makamba alisema kauli halali ya chama ni ile iliyotolewa na Chiligati.
Wakati Makamba akitamba kuwa chama hicho kina haki ya kumhoji Sitta kama kilivyofanya katika vikao vyake vilivyopita, wiki iliyopita Tambwe alitoa tamko kwa vyombo vya habari linaloonyesha dhahiri kupindisha tafsiri ya maamuzi ya vikao hivyo, baada ya maamuzi hayo kuonekana kupata upinzani mkubwa kutoka kwa wadau mbalimbali nchini.
Katika tamko hilo, Tambwe alisema vikao hivyo havikujadili ajenda yoyote iliyowahusu Sitta na wabunge wenzake, wala iliyomhusu Makamba, aliyedaiwa kuwa ilikuwa nusura ang'olewe.
Wiki moja iliyopita, Sitta alibanwa ndani ya NEC na ilidaiwa aliomba radhi na kunusurika katika hatari ya kupoteza uanachama.
Hatua hiyo ya Sitta kuomba radhi ilikuja baada ya wajumbe takriban wote wa vikao viwili vya juu vya Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) vya chama hicho kujenga hoja za kumshambulia, wakipinga namna anavyoliendesha Bunge katika mwelekeo wa kukidhalilisha chama hicho na serikali yake.
Tukio hilo baya kabisa kuwahi kumfika Sitta ambaye amekuwa akijinadi kuwa ni spika wa kasi na viwango, lilihitimishwa na uamuzi wa NEC kuunda kamati maalumu kuchunguza kiini cha kufikia hapo.
Kamati hiyo maalumu inaongozwa na Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi na wajumbe wengine ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Tanzania Bara), Pius Msekwa na mwanasiasa mkongwe, Abdulrahman Kinana.
Kwa mujibu wa habari hizo, mwelekeo wa wana CCM hao kutaka kumwadhibu Sitta, ambaye katika siku za hivi karibuni amejizolea umaarufu wa kisiasa ndani na nje ya Bunge, hata kuwa na uwezo wa kumnyoshea kidole mtu au taasisi yoyote, ulianza kujitokeza tangu wakati wa kikao cha Kamati Kuu mjini Dodoma.
http://www.freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=8034