Pamoja na uzuri anaopambwa nao huyo Balozi, lakini kwa mwendo wake huo atalisalimisha jahazi tulilotaka lizame moja kwa moja.
CCM ilivyo sasa hivi kamwe haiwezi kufanyiwa ukarabati wa juu juu kwa matumaini ya kurudisha ile ya zamani.
Balozi anajaribu kuweka bandage kwenye donda ndugu, akifikiri litapona!
Anapoza maumivu ya muda mfupi tu, huku donda ndugu likiwa bichi kabisa ndani kwa ndani.
Acha nikupe na mfano hai kabisa kama bado unamashaka kuhusu ninaloeleza hapa.
CCM ya Magufuli; uliiona? Mara PAAAA, Samia kaingia,.... Donda likaanza kutoa usaha kabisa.
Balozi anaweza kulituliza kidogo. Haliponi hilo!