Zanzibar 2020 Maalim Seif asema licha ya kuapishwa madai yao ICC yako pale pale!

Hussein Ally Hassan Mwinyi ana busara kama ya Baba yake

Kiliponuka 1984 Mzee Mwinyi akapewa Urais wa Znz akaituliza hali ya Zanzibar ndani ya muda mfupi sana hadi ikashangaza Tanganyika...
Kiliponuka 1984 Mzee Mwinyi akapewa Urais wa Znz akaituliza hali ya Zanzibar.

Nadhani ni 1983
 
Ni kweli bonge ya madini, kwa mara ya kwanza nimesikia shughuli ya kiserekali ikifanyika bila jiwe kutajwa! Hii inamaanisha kuwa yeye ndio chanzo cha chuki hapa nchini.
Chadema ndio waeneza chuki bwashee!
 
Unampelekaje mahakamani mtu anaekulisha,kukulinda na kukupa huduma zote zinazostahiki!
Ujinga wa nyie wanaCCM umeleta madhara makubwa kwa jamii kwa kuficha na kusifia maovu yanayotendwa na wanachama wenzenu hasa walio madarakani eti kwa kuwa wanalisha, wanalinda na kutoa huduma kwa jamii. Sasa tunashuhudia baba mzazi anambaka mtoto wake anabambwa lakini hapelekwi Mahakamani wala Polisi eti kwa sababu baba ndo mkuu wa familia.

Mtoto wa nyumba anaiba mamilioni ya familia lakini hashitakiwi na wanafamilia lakini mtoto wa jirani aliyeiba kuku mmoja wa familia hiihii kwa sababu ya njaa yuko lupango anatumikia kifungo cha miaka mingi. Mwanachama mwenzenu aliyepewa madaraka ya kuongoza ofisi ya Umma au Shirika la Umma anaiba mali za mamilioni ya Umma, anatumbuliwa au kutenguliwa na kupata haki?

Zake zote na kuachiwa makasli na mali zingine zilizopatikana kwa wizi huo. Mwananchi wa mawazo mbadala anabambikiziwa kesi anapelekwa Mahakamani, anasota miaka mahabusu mwisho kwa agizo toka juu anahukumiwa miaka lupango. Mifano ni mingi lakini CCM, CCM, CCM!
 
Siku nikisikia huyu mzee anaokota makopo siwezi kushangaa kabisa.
Nimemsikia BBC Swahili haeleweki anachokizungumza kabisa. .
His mental capacity is waning pretty fast ! Soon he will black out intellectually!
 
Akihojiwa na Zuhura Yunus wa BBC Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif amesema licha ya ACT Wazalendo kujiunga na SUK bado madai yao ICC yapo pale pale...

Panadol panadil pain killer.

Lazima watu wanyweshwe pain killer, panadol 2x3
 
Sijafahamu mahusiano ya nilichoeleza na wewe ulichokasirika hadi kutukana!

Nmekueleza Serikali ya umoja wa kitaifa Znz ni matokeo ya maelekezo ya NEC ya CCM kwa SMZ mwaka 2009 japo wakati huo kina Ally Shamhuna Senior Minister walikuwa wanakejeli wazo hilo hadharan kwa kusema Wanajua Mseto wa chakula sio wa Serikali, wapi nmeandika kuwa Amani Karume alikuwa hajulikani?

Lakin pia nakupa taarifa nyingine hata huyo Amani Karume alipata Urais kwa nguvu ya CCM bara mwaka 2000 kwa kuwa CCM Znz mgombea wao alikuwa Dr Gharib Bilal na ndie alieongoza kwny kura za Znz na Aman Karume akawa wa pili toka mwisho akimshinda Fatma Said Ally,

ilipofika Dodoma Meza ikapinduliwa akachaguliwa Amani, na ilipofika 2005 bado Dr Bilal akamkabili tema Amani Karume akalazimishwa na Mkapa pamoja na Philip Mangula ajitoe

Siku nyingine ntakutajia Team ya Kampen ya Amani Karume mwaka 2000 iliongozwa na kina Nani, ila kwa taarifa yako tu secretariet ya Team ya Ushindi wa karume 2000 kwny Kikao cha NEC Dodoma haikuwa na Mzanzibar hata mmoja kwa kuwa wote mgombea walievuka nae bahari kwenda kumpigania Dodoma alikuwa Bilal!


Unajua kilichomchefua Karume mwaka 2010 hadi kugeuka Inactive Member wa CCM? ni kupinduliwa tena Meza kwa kupigwa chini mtu wake Shamsi na kuwekwa Dr Shein

Mwongo mkubwa wewe na JK! Amani alijulikana hata alipokuwa waziri wa komandoo! Acha kudanganya watoto na JK wako
 
Maalim atakupa jibu rahisi sana kwa hili swali lako; atakuambia hiyo ni haki yake kwavile ni matakwa ya katiba na si hisani.
 
Akihojiwa na Zuhura Yunus wa BBC Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif amesema licha ya ACT Wazalendo kujiunga na SUK bado madai yao ICC yapo pale pale.

Maalim Seif amesisitiza kuwa anamwamini Rais Hussein Mwinyi na ana imani naye katika kujenga Zanzibar mpya.

Nadhani hizi zitakuwa ni habari njema kwa Chadema, Tundu Lisu na Robert Amsterdam.

Maendeleo hayana vyama!
Kwako haiwezi kuwa habari njema,labda kama umeamua kuturidhisha.
 
Akihojiwa na Zuhura Yunus wa BBC Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif amesema licha ya ACT Wazalendo kujiunga na SUK bado madai yao ICC yapo pale pale.

Maalim Seif amesisitiza kuwa anamwamini Rais Hussein Mwinyi na ana imani naye katika kujenga Zanzibar mpya.

Nadhani hizi zitakuwa ni habari njema kwa Chadema, Tundu Lisu na Robert Amsterdam.

Maendeleo hayana vyama!
Robi na Lisu wanahara uharo wa mavi ya kijani
 
Akihojiwa na Zuhura Yunus wa BBC Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif amesema licha ya ACT Wazalendo kujiunga na SUK bado madai yao ICC yapo pale pale.

Maalim Seif amesisitiza kuwa anamwamini Rais Hussein Mwinyi na ana imani naye katika kujenga Zanzibar mpya.

Nadhani hizi zitakuwa ni habari njema kwa Chadema, Tundu Lisu na Robert Amsterdam.

Maendeleo hayana vyama!
kuna njia nyingi za maridhiano, hata tume ya maridhiano, settle out of court n.k siolazima icc
 
Back
Top Bottom