Maajabu ya bongo movie..

Na kaa na dogo nalazimika tu kuziangalia lakini hamna wanachofanya...bora hata vichekesho
 
ukichunguza vizuri utagundua hao si wakristo. ni waoslam ambao kwa 'bahati mbaya' wamekumbana na hiyo scene na walawa reluctant kuigiza uhalisia. sijaiona ila ni mtazamo wangu
 
Ingefaa hata hawa wenye Tv station kabla hawajazirusha hewani waziangalie kama ulivyosema dosari yoyote itskayoonekana wapewe wakarekebishe,ni wendawazimu watu wanaigiza vitu wasivyovijua then wanaita eti movie,movie my foot..kuna kale kakipande mama yuko jikoni anakaanga kuku,wanapoteza mda kuonyesha jinsi mpishi anavyogeuza vipande vya kuku,kutoa kuweka kwnye sinia kisha kurudia tena hivyo hivyo yan sehem isiyokuwa na mpango wwte inachukua dk4,kikawida tungeona tu mama yuko jikon akipika kisha sekunde 10 tungeona wako mezani wanakula,wanachosha wasanii wetu.

hahahaha nilicheka pale yule mama anatoa vipande vya kuku jikoni at moja kwa moja kaviweka kwenye hotpot hata hajaweka somewhere kwenye chombo cha kuchuja kwanza yale mafuta lol
 
Kuna movie nilikua nikiangalia hapa EATV inaitwa CHOZI LA BABA duuuh yaaan kuna kipande kimenishangaza sana yan mtu ameshindwa ata kupiga ishara ya msalaba kweli duuuh kwa style hii kweli uigizaji gani huu...

Kwa atakayeipata angalia kipande kile mama mtu na mwanae wa kike walipo kwenda kaburini kuangalia kabur la baba yao kilicho tokea ni kwamba wote wawili izo ishara tu za msalaba zimekuwa tatizo...

Movie za bingo soko la kimataifa bado sana

Labda ndo lilikuwa kusudio ktk eneo hilo.
 
Mkuu hata mimi niliona nikashangaa sana,kuwaje watake kufanya ishara ya msalaba ilhal hawakufundishwa hivyo ktk kile wanachokiamini,na kwanini wahusika wasingeruhusiwa kwamba wafanye maombi kwa kuzingatia walichofundishwa ktk imani zao,wasanii wetu badilikeni hizo movie zenu hawaangalii wa Tz tu jaribuni kuigiza hali halisi ya mnachoigiza sio mnakariri then mkikosea hamfanyi hata editing kuondoa au kurekebisha kile mlichokosea,sijui ni njaa inawasumbua maana mnataka kuachia movie 10 ndani ya mwezi mmoja but ubora ni sifuri yaani zero,badilikeni mna-bore.

Low budget na mategemeo ya returns kubwa. Hapo mwendo ni "one take" only, no retakes!
 
Matatizo ya filamu za bongo ni mengi. Mojwapo ni kuwa, scripts zake haziko detailed, na hata wasanii hawajitumi kuinternalize scripts na mbaya zaidi directors hawazingatii kuhakikisha kuwa scripts zinazingatiwa. Kinachoshangaza kingine filamu ina kuwa imeshikilkiwa na mtu mmoja huyohuyo (director, script writer, actor, editor, producer etc). Na mbaya zaidi mradi mzima wa film hauna contuinuity director!!!
 
Ndiyo maana inaitwa "acting", hata kama haufungani na upande unaoigiza unatakiwa uuvae uhusika! Wenzetu wanaigiza madaktari, akiwa anaongea na mgonjwa (muigizaji mwingine) unasahau kama ni "movie". Mtu anaigiza Rais, hiyo "speech" anayotoa (ya kuigiza) hata Rais wa ukweli wa nchi fulanifulani hawezi toa. Kwetu mijitu inaamka tu na "kushoot", kumbe mnatakiwa muipitie "script" nzima na kufanya "consultation" kwa watu wenye taaluma halisi wawaelekeze,,,Oshh kutoa "movie" si rahisi hivi!

ukichunguza vizuri utagundua hao si wakristo. ni waoslam ambao kwa 'bahati mbaya' wamekumbana na hiyo scene na walawa reluctant kuigiza uhalisia. sijaiona ila ni mtazamo wangu
 
Kuna moja nilicheka miaka ya nyuma sana eti steringi alimfytulia mkuu wa maadui risasi na kioo kilikuwa kimewatenga mkuu wa maadui baada ya kufytulia risasi upande mwengine wa kioo akaanguka na kufa na damu kibao kuchuruzika lakin kioo hakikuvunjika kilikuwa vile vile.
 
Nyingine eti jini kuvuka barabara anaangalia kushoto kulia kushoto na kuhakikisha hamna magari anavuka
 
Kuna moja nilicheka miaka ya nyuma sana eti steringi alimfytulia mkuu wa maadui risasi na kioo kilikuwa kimewatenga mkuu wa maadui baada ya kufytulia risasi upande mwengine wa kioo akaanguka na kufa na damu kibao kuchuruzika lakin kioo hakikuvunjika.

Duuuuh bado sanaa bongo yetu afu tunawaza soko la kimataifa kweli
 
Mnakumbuka na zile za action et sterling na jambazi wanavyo pigana bac ni vituko tu akipiga teke mmoja nae nangoja mwenzie arudishe ndo anapiga tena na wlmwenzie anamngoje ivo ivo kweli bongo bwana
 
Nasikia the young billionaire ya kanumba the legindary (rip) waliekti masaa kumi na moja tu kwa anzia asubuhi had jion
 
Mnakumbuka na zile za action et sterling na jambazi wanavyo pigana bac ni vituko tu akipiga teke mmoja nae nangoja mwenzie arudishe ndo anapiga tena na wlmwenzie anamngoje ivo ivo kweli bongo bwana
inspekta seba nini?? Kwa upande flan alijitahid inspekta seba hasa ile last scene fight mkuu wa maadui alikuwa noma kweli nilimkubali alikuwa anaruka sarakas wewe anabwaka hapa na kuibukia upande wa pili anaweza pia kuzama hapa na kuchomoza kwengine. Ilimchukua muda mrefu sana inspekta seba kumzibit kwenye hule mjengo chakavu. Walijitahid sana kibongobongo kwenye hii movie
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom