M-Pesa sio salama

M-Pesa sio salama

Suppose namba zangu ni 075423678 na niliyokosea inasoma 0754233978 . sometime ni ngumu kuona hiyo namba hapo katikati haswa ukizingatia mazingira niliyotumia hela yalikuwa kwenye gari linalotembea.
Sasa hapo makosa ni ya nani??
 
Kwa nini Mng'ang'ane kwenye maumivu ..piga chini huo mtandao.

Angalau Tigo wao wana njia mbadala ya kurudisha muamala wako ..

Kosa ulilofanya ni kuukubali muamala wakati ukijua kabisa unaweza 1 kubali au 2 kukataa.

Kuw makini Bro nyie ndiyo mnazingua ata wakati wa uchaguzi mnaharibu kura zenu.
 
Tatizo la Mitandao yetu ya simu inatumia cheap labour na na watu ambao wamezoea kufanya kazi kimazoea na very short foresight kiasi kwamba kufikiri beyond the horizon ya meza zao ni ngumu sana
Tatizo jingine, baadhi ya wateja wa M Pesa wamezoea kutuma pesa kimazoea bila kuzingatia maelekezo. A slightly mistake inasababisha muamala usomeke kwa mtu mwingine!
 
Aliwahi kuchangia member mmoja humu kuwa alikosea kutuma pesa TIGO, ila akawa tigo wanamzungucha, hivyo akaamua kwendaTCRA, majibu aliyopewa tcra kuwa ni mzembe maana kabla kuweka namba ya siri inakuja Jina, ikabidi awe mpole harudi Tena tigo kufuatilia sijui halifanikiwa
 
huo ni uzembe wa vodacom pia. sasa nini maana ya kusajili namba za watumiaji wa mtandao? kama wao wanaona shida wangekupa taarifa zake alizojisajili nazo umsake vizuri mwenyewe.
Ambacho hamjakitambua ni kuwa kwenye kanuni na taratibu hawaruhusiwi kutoa taarifa za mteja unless wanazihitaji watu wa upelelezi au vyombo vya usalama kama polisi na ndomana akashauriwa aende (akashtaki) kutoa taarifa polisi

Kingine ni kwamba huyo mhudumu yeye ametimiza majukumu yake ya kazi kwa kiwango anachostahili kuishia hayo ya kutaki wateja ni mengine tena ni kinyume na majukumu yake


Tatu, je alishajaribu kuchukua hatua walau moja katika zile alizoshauriwa zikagonga mwamba? Kama hapana hakuna haja ya kuwapakazia vodacom kusema mpesa sio salama mana ikitokea umesaidiwa kivyovyote vile ukarudishiwa hela yako au kwa namna yoyote ile itakubidi uombe radhi au upigwe faini kwa shambulio la uzushi/kupakaza. Mana hicho ukitakacho yawezekekana pengine hawafanyi mpaka kutolewe kibali na baadhi ya mamlaka (kutraki simu sio kirahisirahisi hivyo- it's illegal)

Nne, huyo jamaa anavyomuanika huyo mwenzake hivyo (ambapo yeye anamuita mwizi) je haoni kuwa inawezekana ikamrudi yeye mwenyewe akawa hatiani kwa kufanya shambulio la aibu uzushi au kumvunjia mtu heshima

Mwisho niseme tu kwamba voda ni mtandao makini na unategemewa sana na vyombo vya usalama wa mitandaoni kwahiyo jambo lako dogo tu hilo haliwezi kuwa the big deal
Vinginevyo fuata taratibu halali
 
Daah pole sana mkuu ila hapa nadhan umewashushia faida kwa asilimia 20 maana wateja watapungua.
 
Kama hizi ndizo comments za watanzania walio wengi basi niamini tu nchi inakokwenda ni gizani kuliko tuliko toka.
Washa taa ili uwaangazie watanzania. Kosa ni lako kutokuwa makini kwenye miamala.
 
Sheria za nchi zinasemaje juu ya hilo?
Hapana huu si ushauri mzuri. Nadhani ipo haja ya vodacom kuboresha mifumo ya ulinzi wa fedha ili kuwalinda wateja wema. Ulinzi huu ni pamoj
a na kuweka deni kwenye akaunti ya mteja aliyetumiwa kimakosa ili atakapoweka fedha akatwe. Tunailalamikia Vodacom kwa kuwa ndiyo walengwa katika thread hii, lakini ukweli ni kwamba mitandao yote ina ulinzi hafifu dhidi ya mali za wateja wao.
 
Pole sana mkuu. Nakushauri usambaze ujumbe facebook na namba yake ikiwa na caption. Huko watu wanajuana zaidi kuliko hapa JF na nakuhakikishia atajutia sana. Nimewahi kuona kesi nyingi za namna hiyo na hiyo njia ilitatua kwa ufanisi. Voda hawatakupa msaada zaidi ya kuweka deni kwenye namba yake au labda endapo utafungua jalada police na police ndio waamuru voda watoe taarifa za huyo mteja wao aliyechukua hiyo pesa
 
Hv sasa Vodacom na Airtel wanayo hiyo huduma ya kurudisha pesa iliyo tumwa au ulio tumiwa kimakosa.
 
Nimetuma hela kwa mtu anaitwa Samweli Deus kimakosa na in ten minutes nikawapigia MPesa kwa dial 100 na niliongea na dada aliyeko kitengo cha lugha ya Kiingereza na akaniambia nimpe receipt number ya hiyo transaction. Amekuwa fasta kucheki na kuniambia niliyemtumia hela ameshazichukua kwa wakala na THEY CAN DO NOTHING na itanibidi mimi nimpigie mwizi wa hela zangu na akikataa niripoti polisi. Hii ilikuwa accident na sijawahi kosea tangu nianze kutumia hii huduma. Nimesikitika kuwa MPESa haina mechanism ya security kuhakikisha watumiaji wa huduma hawaibiwi. Kwao wanahesabu wamefanya business bila kujali mteja kaibiwa;. Nimejiuliza maswali yafuatayo:
1. VODA hawana uwezo wa kumtrack mteja wao aliyewaibia wateja wengine?
2. Namba ya aliyechukua hela zangu ni 0759548521 inakuwaje Vodacom wanashindwa kunisaidia kupata hela zangu na badala yake kuniambie is non of their business.
3. TCRA inawabanaje hawa wenye kutoa hizi huduma kuhakikisha fedha za mteja hazichopolewi hata pale anapokosea namba au ni kilio cha samaki.
4. Im sure voda wanamjua hata wakala aliyetoa hela na ni rahisi kwa wao kumtumia kumtia mbaroni mwizi ; how come hawataki kujishughulisha na kumwachia aliyeibiwa afanye negotiation na mwizi?

5. Aliyeibiwa yuko Arusha na aliyeiba yuko kanda ya Ziwa na wao wana muscles za kufuatilia nchi nzima ni kwa nini tusione kuwa MPESA siyo salama?

Naomba tusaidiwe hata kama tulikosea ili kupata hela zangu na bado ninaamini wana uwezo wa kufanya hivyo onlu nimekutana tu na VERY WRONG IRRESPONSIBLE AND SHORTSIGHTED STAFF.
Haya ndio tunaita matumizi mabaya ya akili,


Lakini usijali , swala lako linafanyiwa kazi,
 
Tunatumia pia Paypal kuagiza vitu nje kwa mtu usiyemfahamu kabisa na kama akichukua fedha zako bila kutuma item anafuatiliwa popote alipo duniani na atakamatwa
Kama una ujuzi wa PayPal, wape wenzako faida km vp. Inapatkn wapi na jinsi ya kuipata
 
makosa ni ya mtumaji maana kuna kuhakiki no ya unayemtumia mpaka jina sasa kama hukuweza kuona basi .Huwezi kutuma hela then unasema umekosea no kivipi? Tuache lawama ambazo hazina miguu wala kichwa.Hawa Mobile money wameweka kabisa kabla ya kutuma wanaonyesha jina la unayemtumia na no kama zipo sahihi ina maana hukuziona????
Mimi nilifikiri labda kuna shida nyingine kama kuibiwa hela yako iliyoko kwenye akaunti kumbe ni usembe
Pole sana lakini huo ni ujinga na ulipaswa kuwa serious linapokuwa jambo la muamala wa hela
 
Back
Top Bottom