mkuu my web, tukiamua kuwataja magamba hapa wenye kasoro hizo zote ulizozitaja hapo juu hapatatosha hapa. wengine wana mpaka ushahidi wa picha kuwa nani kamzalisha mwanafunzi yupi. bahati mbaya au nzuri ni kuwa sisi CDM si chama cha matusi, kazi yetu si kutangaza matusi bali kutangaza sera za ukombozi wa mtanzania anayetawaliwa kisiasa, kiuchumi na kijamii katika nchi yake mwenyewe tena na watu wake mwenyewe. nyie magamba pelekeni matusi kwa jamii sisi makamanda tunapeleka ujumbe wa ukombozi na faraja ili tulete mwanga palipo na giza, tulete matumaini kwa waliokata tamaa na faraja kwa walioonewa. magamba ni vema mngeelewa sasa mkalisikiliza neno roho aliambialo kanisa. Lakini kama mnajifanya kichwa ngumu na hamtaki kunisikiliza mimi basi shauri yenu, jililieni ninyi wenyewe na watoto wenu kwa maana upanga na juu yenu. after all mimi siye, ila mimi ni sauti tu iliayo nyikani, wapo wajao nyuma yangu(lwakatare, zito, lema, slaa, mboye msigwa nk) ambao sistahili hata kufungua kamba za viatu vyao. hao watawanyoosha tu...mene mene tekel peres...