Lukuvi: Standardization ifanyike ili matokeo ya wanafunzi yalingane

Lukuvi: Standardization ifanyike ili matokeo ya wanafunzi yalingane

Hakuna kitu kilichoikera Serikali ya JK kama ule taarifa ya kuwa tangu aingie madarakani elimu imezidi kushuka siku hadi siku ukilinganisha na mtangulizi wake BEN,

Kwanini elimu isishuke wakati nyinyi ndio mnapeleka watoto wetu "gesti hausi" na kuwaachisha masomo?

Mmomonyoko mkubwa wa maadili ndio sababu kubwa inayopelekea matokeo haya.

Hali ya kutopenda shule ndio imetawala akili za vijana wetu wa mashuleni.

Hata kama serikali ikitoa kila kitu, suala la maadili lina nafasi kubwa katika ufaulu, jambo ambalo limetushinda wazazi wengi kulisimamia.
 
Mleta mada inaelekea elimu yako ndogo sana, utambui mhe. Lukuvi ni nani kwenye ripoti ya tume ya Pinda?

Mhe. Lukuvi amekukera kwa lipi? maana alichopeleka bungeni ni maazimio ya serikali na wala sio yake binafsi.

Kuhusu standardization, watakokotoa kiwango ambacho kitaongezwa kwa kila mwanafunzi, mara nyingi kiwango hiko hakibadili sana matokeo, maana ni ongezeko dogo tu linaongezwa.

We ndo huna akili, mleta mada ana akili timamu, na anacho kihoji hapa ni kwa nini wana siasa wanajifanya wataalam wa kila kitu ? Je ku-standardise matokeo ndo suluhisho au ni njia ya kuahirisha tatizo ? Possibly wewe inaonekana hujui kwanini wanafunzi walifeli ?

Sakata la vijana wetu kufeli ni hatari sana kwa mstakabari wa taifa letu, hivyo hatukutarajia wana siasa kama akina Lukuvi ambao elimu zao ni za ku-unga unga kwa bandeji kibao kushughulikia swala mhimu kama hili, bali serikali ingewakabidhi wataalam wa elimu ambao ni Walimu watafute suluhisho la kudumu na siyo zima moto kama serikali ya muishiwa dhaifu ilivyo fanya.

Kwa hiyo baada ya kufuta matokeo, ina maanisha mwaka huu hatutakuwa na form five ? Je wale ambao wamesha chukua result slip na kuendelea na michakato yao ya masomo ikiwemo na kujiunga shule za private wanafanyaje ?

Kwa hili serikali imekurupuka kama nyumbu, and take it from me, madhara yake ni makubwa kuliko unavyo fikiria.
Endapo Dr. Joyce Ndalichako atakubaliana na huu upuuuzi wa wana siasa wanao fanya maamuzi kwa political interest na yeye pia atakuwa ameingia kwenye mtengo na credibility yake aliyo jijengea kwenye jamii yetu itaporomoka kwa kasi ya ajabu, na hata aminika tena.
 
Acha Uzuzu

Hivi mfumo mpya ndo kitu gani?
Mfumo mpya ulikuwa unasema 1+1=3?
Mbona Lukuvi hakusema huo Mfumo Mpya unafanya vipi kazi? na ulichangia vipi katika kufeli kwa wanafunzi???
Je, Serikali Haikushirikishwa na NECTA juu ya Matumizi ya Huo Mfumo Mpya???
Ni nani Developer wa Huo Mfumo Mpya na amechukuliwa hatua gani???
Tender ya Kutengeza Hu Mfumo Mpya alipewa na nani???
Kuleta Siasa kwenye Elimu ni Hatari sana kwa Mustakabali wa Nchi Yetu.
Msingi wa Taifa Lenye wataalamu Dhaifu/Incompetent, Msingi wake ni Maamuzi kama Haya

Umeisoma na kuielewa sheria inayounda baraza la mitihani? au unakurupuka tu na kutuhumu kuwa wamekosea?

Kama sheria imeelekeza NECTA kutumia mbinu au mfumo unaofaa ili kusahisha mitihani, je, wewe ni nani uhoji maamuzi yao?

Mimi sioni kosa lolote la NECTA, sana sana wanapaswa kupongezwa kwa umakini na umahiri wa kusahisha, na pia kwa kubana mianya ya uvujaji wa mitihani ya taifa.

Mimi naamini NECTA wangeanza operesheni hii ya kuzuia uvujaji wa mitihani mapema, mleta mada na watu wote wa aina yako mngekuwa miongoni wa wanafunzi waliozungusha, maana uelewa wenu ni mdogo sana.
 
Kama sheria imeelekeza NECTA kutumia mbinu au mfumo unaofaa ili kusahisha mitihani, je, wewe ni nani uhoji maamuzi yao?
Mimi sioni kosa lolote la NECTA, sana sana wanapaswa kupongezwa kwa umakini na umahiri wa kusahisha, na pia kwa kubana mianya ya uvujaji wa mitihani ya taifa.

Another Lukuvi
Hivi unaelewa kweli wewe???
Ni wapi nimesema kuwa NECTA wako wrong????

Mimi naamini NECTA wangeanza operesheni hii ya kuzuia uvujaji wa mitihani, mleta mada ungekuwa miongoni wa wanafunzi waliozungusha, maana uelewa wako ni mdogo sana.
Hivi kwenye Hii Post, kuna sehemu yeyote nime mention suala la Kuvuja kwa Mitihani???
Naamini kabisa Wewe uwezo wako wa ku Reason Mambo uko Down Kwa Hali ya Juuu Mno
 
Matokeo kufutwa sio kitu cha ajabu,standardization pia sio kitu kipya,form 4 1998 kuna mitihani ilifutwa baada ya kuvuja hivi nyie form 4 wa mwaka huo msiajiriwe kwa kua ni wezi wa mitihani?au mnadhani hao watoto wa form 4 ya mwaka jana hawana nafasi tena kwenye nchi yao kisa wamefeli?nyie mnaoshinda kwenye facebook wakati wakazi hamuoni kua na nyie mmefeli kwenye kazi zenu?
 
we chalii wewe nae mwathirika wa elimu ya lukuvi nini? au kichwa tiktik maji nini maana wenye uwezo mdogo kwa kupenda dezo hamjambo...! n mantic wotev wafanyavyoka kuanza na lukuvi kama kibaraka wao, chanzo ch matatizo!
Mleta mada inaelekea elimu yako ndogo sana, utambui mhe. Lukuvi ni nani kwenye ripoti ya tume ya Pinda?

Mhe. Lukuvi amekukera kwa lipi? maana alichopeleka bungeni ni maazimio ya serikali na wala sio yake binafsi.

Kuhusu standardization, watakokotoa kiwango ambacho kitaongezwa kwa kila mwanafunzi, mara nyingi kiwango hiko hakibadili sana matokeo, maana ni ongezeko dogo tu linaongezwa.
 
Mods,
Naomba msiunganishe Huu uzi na Nyuzi nyingine za Kufutwa kwa Matokeo Ya Kidato Cha Nne
Napenda Kutumia Fursa hii kuonesha Kukerwa Kwetu (Mimi na wakazi wote Mtaa wetu Plus JF Members) na Kauli ya
Lukuvi Juu ya Kufutwa kwa Matokeo ya Kidato cha nne.



Who is Lukuvi By the way???
Je , Kawambwa na Mulugo bado wanapeta???

Kimsingi hii ndo main Point ya Tume ya Pinda.
Serikali inataka kusema kuwa Wasahihishaji wamewaonea Watoto.
Hii ni indication kuwa NECTA na Dr Ndalichako wamekubali (Kwa Kulzimishwa) Kuubeba Msalaba wa Serikali wa kutokujali Kilio Cha Walimu.
Madai ya Msingi ya Walimu ambayo Kimsingi ndo yalipelekea Janga la Mwaka Jana
Hata waki Standardize, Wakisema C Inazia 30% Badala ya 41%, haitakuwa na Tija Kabisa.
Taifa la Wa Taalamu Feki Msingi wake ni Maamuzi ya Kipuuzi Kabisa kama haya.
Standardization ni kitu cha kawaida na kinafanyika duniani kote! Hivyo usione ajabu!

Niliwahi kuandika humu kuwa katika mwaka mmoja wa miaka ya 80 wanafunzi wa third year engineering UDSM karibu wote walifeli hesabu lakini alipokuja external examiner kutoka Makerere 90% ya wanafunzi walipasi!
 
Mbowe ana cheti gani? CHADEMA mnategemea nini?

Kijana acha mzaha,kuna watoto wamekufa kwa sababu ya matokeo haya,na wengine wamekata tamaa kabisa.huenda we ni mkenya,wtz hatuna mtazamo kama wako katika hili.
 
We ndo huna akili, mleta mada ana akili timamu, na anacho kihoji hapa ni kwa nini wana siasa wanajifanya wataalam wa kila kitu ? Je ku-standardise matokeo ndo suluhisho au ni njia ya kuahirisha tatizo ? Possibly wewe inaonekana hujui kwanini wanafunzi walifeli ?

Sakata la vijana wetu kufeli ni hatari sana kwa mstakabari wa taifa letu, hivyo hatukutarajia wana siasa kama akina Lukuvi ambao elimu zao ni za ku-unga unga kwa bandeji kibao kushughulikia swala mhimu kama hili, bali serikali ingewakabidhi wataalam wa elimu ambao ni Walimu watafute suluhisho la kudumu na siyo zima moto kama serikali ya muishiwa dhaifu ilivyo fanya.

Kwa hiyo baada ya kufuta matokeo, ina maanisha mwaka huu hatutakuwa na form five ? Je wale ambao wamesha chukua result slip na kuendelea na michakato yao ya masomo ikiwemo na kujiunga shule za private wanafanyaje ?

Kwa hili serikali imekurupuka kama nyumbu, and take it from me, madhara yake ni makubwa kuliko unavyo fikiria.
Endapo Dr. Joyce Ndalichako atakubaliana na huu upuuuzi wa wana siasa wanao fanya maamuzi kwa political interest na yeye pia atakuwa ameingia kwenye mtengo na credibility yake aliyo jijengea kwenye jamii yetu itaporomoka kwa kasi ya ajabu, na hata aminika tena.

Naona mkuu master peace unavyo endeshwa na hisia na kuukwepa ukweli.

Suala la elimu hasa ili la kushuka kwa ufaulu limefanyiwa utafiti na tume ya Pinda, wajumbe wa hiyo tume ni wadau wakubwa wa elimu hapa nchini, na wala sio wanasiasa.

Lakini vilevile, maamuzi ya kusahisha upya na ku-standardize yametolewa na serikali kufuatia mapendekezo ya tume, sasa hapa siasa iko wapi?

Kinachofanyika hapa sio kibaya, ila ni katika jitihada ya kunusuru hawa watahiniwa, angalau waendelee na masomo ya kidato cha tano na sita, huku jitihada za kuboresha elimu zikiendelea.

Watakao nufaika na utaratibu wa standardization sio waliopata daraja sifuri, la hasha, ila serikali inataka wale wenye daraja la 4 na point 28-29 wafike angalau daraja la 3 na point 25.

Wewe kama mtanzania tena mzalendo utathubutu kukebehi na kukejeli maamuzi haya? hemu tuweke utaifa mbele na tuubariki huu mpango ili vijana waendelee na masomo, hizi dhihaka hazijengi chochote ndugu zangu.
 
Last edited by a moderator:
Yeyote anayebeza uamuzi wa serikali juu ya matokeo ya kdato cha nne atakuwa mpuuzi kwani ni kutokuwa na shukrani na huruma kwa wazazi na wanafunzi ambao walifanya mtihani huo.
 
Serikali dhaifu,inayotaka kuongeza wadhaifu,walau iweze kuongoza wadhaifu!This only happen in Tanzania!Ilitakiwa serikali ijiulize kilichosababisha hali ya ufaulu kuwa duni ukilinganisha na miaka iliyopita!Hawa watu ni sahuni wznaotaka kuangamiza taifa kwa maslahi ya wachache!Wasiposuluhisha tatizo i.iyosababisha wanafunzi kufeli,haitasaidia chochite kwa ufaulu wao xiku za usoni.Watatue kwanza kero zilizosababisha kufeli kwao hasa mishahahara duni kwa walimu na mazingira magumu ka hao wawezeshaji,walimu wa zama hizi siyo wale wa enzi za walimu Nyerere.
 
Hii ndio CV ya Lukuvi, from ualimu wa UPE hadi Degree. Angalia usipokubali nae alifanyiwa Standardization.

MEMBER OF PARLIAMENT CV
GENERAL
Salutation Honourable Member picture
First Name: William
Middle Name: Vangimembe
Last Name: Lukuvi
Member Type: Constituency Member
Constituent: Ismani
Political Party: CCM
Office Location: P.O.Box 980, Dodoma
Office Phone: +255 262 321 151
Ext.:
Office Fax: +255 22 2320046
Office E-mail: wlukuvi@parliament.go.tz
Member Status: Current Member
Date of Birth 15 August 1955
EDUCATION
School Name/Location Course/Degree/Award Start Date End Date Level
Open University of Tanzania Masters in Political Science 2008 2011 MASTERS
DEGREE
Washington International University
- USA BA (Inter. Studies &Diplomacy) 2001 - GRADUATE
Johanesburg - South Africa International Observers Course 1994 - CERTIFICATE
Moscow - USSR Leadership Course 1985 - CERTIFICATE
Moscow - USSR Diploma in Political Science 1982 1983 ADV
DIPLOMA
Lindi Political Course 1976 - CERTIFICATE
Tabora Teacher's Training College Teaching Course - 1975 CERTIFICATE
Iringa Training in Defence and
Security - 1980 CERTIFICATE
Computer Training College-Dar es
Salaam Training in Computer Course - 1998 CERTIFICATE
EMPLOYMENT HISTORY
Company Name Position From To
United Republic of Tanzania Minister Of State(Policy,Coordination
and Parliamentary Affairs) 2010 To date
Dodoma Regional Commissioner Regional Commissioner (RC) 2006 2010
Prime Minister's Office Minister Of State(Policy,Coordination
and Parliamentary Affairs) 2000 2005
Ministry of Labour and Youth
Development Deputy Minister 1995 2000
Bukoba District Commissioner District Commissioner 1994 1995
POLITICAL EXPERIENCE
Ministry/Political Party/Location Position From To
CCM Member of the Central Committee 2010 2012
CCM Member of the National Executive
Committee 1997 To date
CCM Member of the Region/Executive
committee 1995 To date
Chama Cha Mapinduzi - CCM - Head
Office (Youth Organisation) Deputy Secretary General 1992 1993
Chama Cha Mapinduzi - CCM Regional Secretary - Youth
Organisation 1989 1992
Chama Cha Mapinduzi - CCM Head of Department - Youth
Organisation 1984 1989
Chama Cha Mapinduzi - CCM
 
Pitia elimu ya Lukuvi utagundua hata yeye alifanyiwa Standardization. Alifeli form four akaenda kusomea ualimu wa grade A, kupitia mpango wa UPE lakini leo nae anajiita "degree holder" Chuo chenyewe alichosoma hakitambuliki. Hii ndio Tanzania... Ukistaajabu ya Lukuvi utaona ya Agustine Mrema (hajaenda sekondari lakini nae ana degree). Yani huyu ndo funga kazi, ukisia Dar mpaka Moro ndo hii. yani "from Primary to University"
Mwenyekiti wa hii Tume ameshaeleza mipango hii ya kuwapa fursa watu waliomaliza shule ya msingi kutumia uzoefu wa maeneo yao kwenda chuo kikuu. Nafikiri wanaanza mwaka huu.
 
Naona mkuu master peace unavyo endeshwa na hisia na kuukwepa ukweli.

Suala la elimu hasa ili la kushuka kwa ufaulu limefanyiwa utafiti na tume ya Pinda, wajumbe wa hiyo tume ni wadau wakubwa wa elimu hapa nchini, na wala sio wanasiasa.

Lakini vilevile, maamuzi ya kusahisha upya na ku-standardize yametolewa na serikali kufuatia mapendekezo ya tume, sasa hapa siasa iko wapi?

Kinachofanyika hapa sio kibaya, ila ni katika jitihada ya kunusuru hawa watahiniwa, angalau waendelee na masomo ya kidato cha tano na sita, huku jitihada za kuboresha elimu zikiendelea.

Watakao nufaika na utaratibu wa standardization sio waliopata daraja sifuri, la hasha, ila serikali inataka wale wenye daraja la 4 na point 28-29 wafike angalau daraja la 3 na point 25.

Wewe kama mtanzania tena mzalendo utathubutu kukebehi na kukejeli maamuzi haya? hemu tuweke utaifa mbele na tuubariki huu mpango ili vijana waendelee na masomo, hizi dhihaka hazijengi chochote ndugu zangu.

Ninaheshimu sheria za JF, ila wewe ni mtu wa ajabu sana! Sina hakika kama unajua unachokiongelea?
Uamuzi wa kufanya watu wafaulu kutokana na "Standardization ifanyike ili matokeo ya wanafunzi yalingane na juhudi wazizoziweka katika kusoma kwa mazingira, hali halisi ya Tanzania na uamuzi wa taifa kuongeza idadi ya shule na wanafunzi wakati uwekezaji katika ubora unaendelea"

Kweli unauita huu ni uzalendo?! Ee Mungu tunusuru!

Unasema standardization itafanyikaje bila kuathiri wanafunzi wa daraja sifuri? Kigezo gani watatumia? Na kwanini?
Wanatoa wapi hizo maksi za kuwaongezea say, hao daraja la nne hadi wafikie daraja la tatu? Kumbuka sote tuliopita shuleni tunajua maksi zilitokana na mitihani pekee, hayo mengine mtuambie mnayatoa wapi??

Bora wangewapeleka kidato cha tano tu kwa amri kuliko huu usanii wanaofanya, wanamdanganya nani!?

Yule mama Ndalichako ili kuweka heshima yake, ulikua wakati wa kujiuzulu sasa, maana alihubiri kuwa wanafunzi wamefeli na akatoa sababu na kutuonesha hadi mitihani iliyochorwa zombi, leo anaambiwa ifanyiwe standardization?! Kwa hiyo atakapokuja na matokeo yenye ufaulu wa juu zaidi ataomba msamaha kwa yaliyosomwa kabla ama atanyamaza kama halikuwahi kutokea?
Kama anaamini alifanya kitu sahihi na walifuata utaratibu katika mitihani waliyosahihisha basi asimamie maamuzi yake na akubali kuwapisha hao wanaoamini katika kushusha viwango vya madaraja ili wengi waonekane wamefaulu!!

Kwa kuwa serikali imependa kuona wanafunzi wanafaulu bila kuangalia namna inayotumika kuwafanya waonekane wamefaulu, ngoja twende!

Naomba Mungu atupe maisha marefu tushuhudie kinachotengenezwa na hawa wanasiasa.
 
Standardization ni kitu cha kawaida na kinafanyika duniani kote! Hivyo usione ajabu!

Niliwahi kuandika humu kuwa katika mwaka mmoja wa miaka ya 80 wanafunzi wa third year engineering UDSM karibu wote walifeli hesabu lakini alipokuja external examiner kutoka Makerere 90% ya wanafunzi walipasi!

Unataka kusema NECTA hawajui standardization.? Au magoli yanapanuliwa ili kila mtu afunge?. Maana magoli madogo wagungaji wachache hivyo serikali imeona ni vyema milingoti ya magoli kutanuliwa ili wafungaji wawe wengi, badala ya kuhangaika kuwafundisha wafunga magoli!.

Sent using wireless by wire
 
Hakuna kitu kilichoikera Serikali ya JK kama ule taarifa ya kuwa tangu aingie madarakani elimu imezidi kushuka siku hadi siku ukilinganisha na mtangulizi wake BEN,

mumeshaanza ud.......
 
Back
Top Bottom