NAMBA MOJA AJAYE NCHINI
JF-Expert Member
- Oct 29, 2019
- 8,526
- 17,433
Ni hivi majuzi tu matokeo ya Darasa la Saba yametoka ya Shule mbalimbali nchini. Kuna baadhi ya Shule zimefutiwa matokeo kutokana na uzembe na ulaji rushwa wa wasimamizi, tuseme wanafunzi wameingizwa mkenge na waliowaamini kama wasimamizi na walimu wao.
Kuwafutia wanafunzi matokeo ni adhabu kali sana tena ya maisha na kuteketeza ndoto zao za kuwa wataalamu wa kada mbalimbali. Mi nadhani umefika wakati wa kufikiria mbadala wa janga hili napendekeza yafuatayo!
1. Warudie kufanya mtihani mwingine na gharama zifidiwe na wazembe waliosababisha usimamizi mbovu. Ikiwezekana wazazi walipe ada ya kuendesha mitihani ya watoto wao! Wasimamizi mali zao zipigwe mnada kufidia gharama za mtihani walioshiriki kuvujisha.
2. Wanafunzi waliofutiwa matokeo warudi tena darasani kwa mwaka mmoja zaidi yaani wasome kwa miaka minane elimu ya msingi ili wafanye mtihani kama watahiniwa wengine wa mwaka huo!
Kumbukeni kuendelea kuboresha maslahi ya walimu waondokane na rushwa ndogo ndogo kama 25000/= ambazo zinakosti utumishi wao na kudhalilisha kada za elimu nchini.
Kuwafutia wanafunzi matokeo ni adhabu kali sana tena ya maisha na kuteketeza ndoto zao za kuwa wataalamu wa kada mbalimbali. Mi nadhani umefika wakati wa kufikiria mbadala wa janga hili napendekeza yafuatayo!
1. Warudie kufanya mtihani mwingine na gharama zifidiwe na wazembe waliosababisha usimamizi mbovu. Ikiwezekana wazazi walipe ada ya kuendesha mitihani ya watoto wao! Wasimamizi mali zao zipigwe mnada kufidia gharama za mtihani walioshiriki kuvujisha.
2. Wanafunzi waliofutiwa matokeo warudi tena darasani kwa mwaka mmoja zaidi yaani wasome kwa miaka minane elimu ya msingi ili wafanye mtihani kama watahiniwa wengine wa mwaka huo!
Kumbukeni kuendelea kuboresha maslahi ya walimu waondokane na rushwa ndogo ndogo kama 25000/= ambazo zinakosti utumishi wao na kudhalilisha kada za elimu nchini.