Lukuvi akwepa mdahalo na Lissu

Lukuvi akwepa mdahalo na Lissu

Ha ha ha!Wenzie walishajua ratiba yake ya ziara ilikuwa inamalizikia jana Ijumaa na ndio maana Mdaharo ukapangwa ufanyike Jumapili lakini kwakuwa Mkuu alijua ataumbuliwa akaamua kujipangia ziara nyingine ya Iringa lengo likiwa ni kuhalalisha hoja yake ya kukwepa mdaharo na Lissu


Kha ha ha ha ha haaaaaa! Tulitegemea mambo yangekuwa hivi hivi.
 
Waziri Lukuvi amekataa kushiriki katika mdaharo ulioandaliwa na asasi moja juu ya kilichojiri Bungeni kuhusiana na mchakato wa Katiba mpya.Mdaharo huo ambao ulipangwa kufanyika Jumapili kuanzia saa Saba mchana hadi saa Kumi na mbili jioni ungewashirikisha Waziri Lukuvi na Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bwana Tundu Antipasi Lissu.Katika maelezo yake ya kwanini hatashiriki kwenye mdaharo huo Waziri Lukuvi alidai kuwa hana taarifa kutoka ofisini kwake juu ya mwaliko huo kwasababu alikuwa ziarani mikoani kwa shughuli za kikazi na kwamba anapanga kuelekea Mkoani Iringa leo kama mwendelezo wa ziara zake za Mikoani za kikazi.

Najua LUKUVI atakuwa amewaumiza sana kutokana na ukweli kwamba CHDEMA mlikuwa mmejipanga na attackers wa government kama akina mkuu wa SAUT mkisaidiana na mwendesha mdahalo, bila shaka angekuwa ROSE KITWANGA , sijui lakini. Jipangeni upya Serikali ina mkono mrefu itakuwa imegundua imebonyezwa hiyo janja. Cha msingi andaeni maandamano kupinga LUKUVI kujitoa mdahalo
 
nili-bet kichwa changu kuwa kilaza lukuvi hawezi kutokea,si mnaona!
 
Ningeshangaa sana kama Lukuvu angekubali kwenda kwenye mdahalo na Tundu Lissu wakati anajua nini kilimpata Ndugai...

Ingekuwa sawa na kupima ukubwa wa Kinywa cha mamba kwa kuingiza mkono...
 
Hapa kweli walinoa labda wangemleta mnafiki 6 lakini yko tofauti nao sana.
 
Vitu vingine ni kuwatafuta watu maneno tu,...Sasa Lukuvi jamani ataongea nini kwa Tundu Lissu jamani....! Waandaaji wa midahalo muwe mnatenda haki..... Nikisikia neno mdahalo nakumbuka kampeni za uchaguzi 2010,Namkumbuka Mwasisi wa kutimua mbio akisikia mdahalo ndugu yetu JK na sasa vijana wake wanaiga tabia ya baba!!!!!
 
Najua LUKUVI atakuwa amewaumiza sana kutokana na ukweli kwamba CHDEMA mlikuwa mmejipanga na attackers wa government kama akina mkuu wa SAUT mkisaidiana na mwendesha mdahalo, bila shaka angekuwa ROSE KITWANGA , sijui lakini. Jipangeni upya Serikali ina mkono mrefu itakuwa imegundua imebonyezwa hiyo janja. Cha msingi andaeni maandamano kupinga LUKUVI kujitoa mdahalo

darasa la saba lukuvi hawezi kusimama na msomi wa sheria aliyebobea,bila dikteta ndugai kumkingia kifua hawezi hawezi mdahalo na yoyote,infact hakuna ccm yoyote hata jk anayeweza kuhudhuria.
 
Mkuu midahalo ya wenzetu inakuwa so organized na inakuwa imeandaliwa na taasisi ambayo haifungamani na upande wowote, usifananishe midahalo hii na huu upup wa kitanzania ambao kwanza watu wanakaa na kutafuta namna ya kumkaanga mwingine na mnaletewa mtu kama R.K kuongoza mdahalo unategemea nini? mfano mzuri ni huu ambao LUKUVI ameukataa, tayari ilishafamika kuwa miongoni mwa wataohusika moja kwa moja ni mkuu wa SAUT, yule CDM 100% au mtu kama LWAITAMA au KAKOBE wahudhurie mdahalo what do you expect? Tanzania hatuna taasisi za kuandaa midahalo, inabidi kwanza tulione hilo badala ya kukimbilia kuwa mashabiki tu.

Mkuu kubali kuwa magamba wanakwepa midahalo sababu hawana hoja. Kumbuka TBCCM ni taasisi ya serikali waliandaa midahalo uchaguzi 2010 walivyoona dsm na arusha wagombea wao wameshindwa kujibu hoja wakapiga marufuku gamba lolote kuhudhulia midahalo na wakampiga chini Tido. Kwa hiyo hoja hapa ni magamba yanakwepa midahalo inayotoa haki sawa ya wazungumzaji popote pale!
 
maccm bana wanamuogopa LISU kwa sababu akili ya TUNDU LISU ni sawa na Maccm 100
 
mkuu TECH WIZ hata kama ni mimi nikiitwa kwenye mdahalo halafu nikajua sina hoja, na mtu nitakayefanya naye mdahalo yuko vizuri kweli kweli; lazma niingie mitini. Simlaumu sana lukuvi maana sasa angefanyaje! na wakati akijaribu kuyapima maji; anaona wazi hawezi kuyavuka?
Acha kuropoka wewe. Yaani Lisu yuko vizuri kuliko Lukuvi? Mbona mnapenda kufananisha vitu ambavyo havipaswi kufananishwa. Lukuvi ni waziri tena mwenye mamlaka ya bunge. Anajua mambo mengi na ana vielelezo kuliko hawa waropokaji. Mbona siku ile alipotoa vielelezo bungeni wabunge wa chadema akiwemo Lisu hawakukanusha na badala yake wakaleta fujo ambazo zimewavunjia heshima?
 
Serikali ilishashtukia midahalo inayoandaliwa na kwa udhamini wa WAPINZANI, halafu hata hivyo kama wana hoja si wangepingana naye bungeni kama siyo ushahidi tosha kuwa wanatumia media vibaya.
Buku saba fc naona leo umeibuka unataka kuwaoiga bao hata wenzako,kodi ya pango imeisha nini kwa sababu haya mapovu mfululizo kuna kitu nyuma ya pazia.
 
Hao waandaaji wasingetenda haki sana kwa kumpambanisha Lukuvi na Lissu, jamani hakika hawaendani, Lukuvi mimi najua tu ni cheo kikubwa tu lakini ukweli hana kitu, zile ni natural confidence za kabila lake na kwa vile yuko chama kama CCM anaonekana mtu makini kweli hasa kwa serikali ya Kikwete, ukiongezea na hasira zake za asili plus ushushu uhakika wa kula ndani ya chama na serikali hii bado anao.

Kwa ccm watu makini hawana chao, ukimkuta mtu ulikuwa unamfahamu ni makini ndani ya mfumo wa ccm ya sasa anachofanya kwanza ni kuficha uelewa wake kwanza na kujifanya mbumbumbu ili aweze kuendana na mfumo na baada ya hapo maisha husonga mbele, yaani anakubali kuwa mnafiki kwanza. Mifano ipo mingi kwa wafatiliaji wa mambo mnajua, mfano mdogo sana mnaweza kumbuka lile kundi la ccm la wapinga ufisadi tangu enzi la Richmond, sio kwamba hawapo , lakini wametulia kimya ili kuendana na mfumo wao.

Tanzania yetu ina hali mbaya sana chini ya ccm ya sasa kuliko labda wakati mwingine wowote kwenye uhai wa nchi hii. Lukuvi anajijua alivyo, binafsi nampongeza kwa kutokubali huo mdaharo, ila tu asisingizie kutokuwa na taarifa, mara ziara nk, yeye aseme wazi hana uwezo wa kusimama na mtu makini kama Tundu Lissu kwenye mjadala wa kitaifa na kikanuni kama huo.
 
bora hata ameamua kuachana na mdahalo huo, kwa sababu ukiangalia washirki wengine wa mdahalo huo utagundua kuwa ni wa kupangwa kwa makusudi ili kuishambulia serikali, safi sana, nani ambaye hajui kilichonyuma ya pazia kwa kuwashirkisha watu kama yule mkuu wa SAUT? ambao hamjui nitafuteni kwenye private niwamegee.

wewe weka hapa, Dr. Charles Kitima ni padri wa kanisa katoliki mwenyeji wa Singida, anaikosoa sana serikali na pia anamkosoa Lissu kwa kasi ndogo ya maendeleo jimboni mwake! Unaficha nini sasa? JF where we dare talk openly
 
Waziri Lukuvi amekataa kushiriki katika mdaharo ulioandaliwa na asasi moja juu ya kilichojiri Bungeni kuhusiana na mchakato wa Katiba mpya.Mdaharo huo ambao ulipangwa kufanyika Jumapili kuanzia saa Saba mchana hadi saa Kumi na mbili jioni ungewashirikisha Waziri Lukuvi na Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bwana Tundu Antipasi Lissu.Katika maelezo yake ya kwanini hatashiriki kwenye mdaharo huo Waziri Lukuvi alidai kuwa hana taarifa kutoka ofisini kwake juu ya mwaliko huo kwasababu alikuwa ziarani mikoani kwa shughuli za kikazi na kwamba anapanga kuelekea Mkoani Iringa leo kama mwendelezo wa ziara zake za Mikoani za kikazi.

HA!HA!HA!HA! Kuna jamaa humu ndani alitabiri kwamba jamaa angetoa nje tu, nadhani huyo kamanda anaweza kuanza kutugawia kikombe cha BABU
Chezea vihiyo weye!
Aende Lukosi na Hamy D,
Hivyo ndo ilivyokuwa kwenye nchi ya wagagagigikoko na mfalme uyiuyi, Ameunda safari kama ile ya Bulicheka.....

Hapo sasa, Huko Waryoba kapasua Jipu huku safari ya Bulicheka, hiyo ndo busara na hekima ya kiti cha spika, Hawajachelewa wamwite Ndugai tushuhudie mtu anapata Pressure,
 
Anasubir aitwe kwenye kile kipindi chao cha kiboya cha dk 45.ambacho anajiuliza maswali na kujijibu mwenyewe.niliahidi kunya hadharani kama angeshiriki huo mdaharo
 
Waziri Lukuvi amekataa kushiriki katika mdaharo ulioandaliwa na asasi moja juu ya kilichojiri Bungeni kuhusiana na mchakato wa Katiba mpya.Mdaharo huo ambao ulipangwa kufanyika Jumapili kuanzia saa Saba mchana hadi saa Kumi na mbili jioni ungewashirikisha Waziri Lukuvi na Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bwana Tundu Antipasi Lissu.Katika maelezo yake ya kwanini hatashiriki kwenye mdaharo huo Waziri Lukuvi alidai kuwa hana taarifa kutoka ofisini kwake juu ya mwaliko huo kwasababu alikuwa ziarani mikoani kwa shughuli za kikazi na kwamba anapanga kuelekea Mkoani Iringa leo kama mwendelezo wa ziara zake za Mikoani za kikazi.

Bw Lukuvi amekataa ama amekatazwa na CCM?
 
Huyo mtu mzima kaogopa kuvuliwa nguo hadharani haki ya mama!
 
Viatu vya Lissu havimtoshi Lukuvi kwa namna yoyote, mnawonea bure kumweka na Lissu atapata aibu ya karne!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom