Lukuvi akwepa mdahalo na Lissu

Lukuvi akwepa mdahalo na Lissu

labda angeenda na Anna Makinda o Ndugai 7b walixhazoea uxhnd wa mezan
 
Huyo mwenyekiti wao Fast Jet tu hathubutu, hata akiandaliwa maswali kabla na Lissu asipewe hayo maswali atamtoa. Nadhani mnakumbuka maswali ya kutayarishiwa aliyoulizwa mwaka 2010 na Ephraim Kibonde, hapo ilikuwa baada ya wananchi kuwazomea sana CCM kwa kuogopa midahalo na Katibu wao mkuu wa wakati huo Mzee Makamba aliandika waraka wa kuwazuia wagombea wote wa CCM kwa nafasi zote wasishiriki midahalo iliyoandaliwa na mtaalamu Tido wa TBC1 baada ya kupata aibu vipindi vilipoanza tu, ikadhihirika uwezo mdogo wa wana CCM katika hoja za pao kwa papo zinazowagusa wananchi.
 
Hapa mi nadhani kaogopa mambo mawili...aidha kaogopa kwa sababu hana points(hoja) au kaogopa maana anajua anakutana na kichaa Lissu anything can happen..ugali mtamu bwana nani anapenda maumivu...!
 
Lukuvi tangu azaliwe hajawahi hata siku moja kuwa kwenye mdahalo wowote na mtu yeyote zaidi ya kupewa dakika 45 na ITV tuongee asubuhi na star TV,na Kipindi chaa TBC na Bungeni ambako huwa anadictate lakini mdahalo hauwezi kuna siku Chiku Abwao alimtoa kamasi bungeni anayejiita motto wa kike na kwamba LUkuvi hamuwezi itakuwa Lissu amefanya vizuri kukimbia manake angeenda choo bila kupenda
 
Waziri Lukuvi amekataa kushiriki katika mdaharo ulioandaliwa na asasi moja juu ya kilichojiri Bungeni kuhusiana na mchakato wa Katiba mpya.Mdaharo huo ambao ulipangwa kufanyika Jumapili kuanzia saa Saba mchana hadi saa Kumi na mbili jioni ungewashirikisha Waziri Lukuvi na Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bwana Tundu Antipasi Lissu.Katika maelezo yake ya kwanini hatashiriki kwenye mdaharo huo Waziri Lukuvi alidai kuwa hana taarifa kutoka ofisini kwake juu ya mwaliko huo kwasababu alikuwa ziarani mikoani kwa shughuli za kikazi na kwamba anapanga kuelekea Mkoani Iringa leo kama mwendelezo wa ziara zake za Mikoani za kikazi.

I think mleta mada unachuki binafsi na huyu waziri,alichokisema ni kwamba hana taarifa na pia sio ameogopa au kukimbia,ila anachokisema wapange muda au siku nyingine atakayo kuwa na nanafasi ili aweze kuwepo,hapo kwa leo sijaona kosa la lukuvi,wazungu wanasema give credits when......................
 
Lukuvi ni kilaza wa ajabu sijawahi kuona. hata ungemshikilia bunduki kwa nyuma asingeweza kwenda kwenye mdahalo huo kamwe!!!! Lukuvi hajui chochote kuhusu taratibu za bunge na pale bungeni anachofanyaga ni kuongea mambo aliyomezeshwa na mtu back anyemfahamu yeye. ndio maana kama mlishawahi kufuatilia vizuri kama ikiibuka issue mpya bungeni huwezi kumsikia Lukuvi akichangia na akiongea basi anaongea upuuzi mtupu ambao hata std seven akisikiliza atamcheka!!!!! Lukuvi anaongeaga yale mambo ambayo yalishatokea tayari na majibu kutengenezwa then yeye anaambiwa kaseme hivi!!!!! Lukuvi amepewa hiyo nafasi aliyonayo simply kwa sababu ana uthubutu wa kuongea issues hata zile za aibu ambazo mtu mwingine yeyote mwenye akili hawezi kuziongea. watu wa aina ya Lukuvi ni kama Wasira na Mwigulu Nchemba na Nape Nnauye na ndio maana unaweza kuona mwenyekiti wa ccm amewapa nguvu kubwa sana watu hawa katika kipindi hiki kigumu kwa CCM kwa sababu hawanaga aibu kuongea chochote hata kama ni cha kuwadhalilisha namna gani wao na familia zao. Kikwete ni psychologist mzuri sana maana aligundua kwamba watu ambao anaweza kuwatumia jinsi anavyotaka ili kufanikisha mambo yake bila kipingamizi chochote ni hawa maana wao ni watu rahisi sana kuwapeleka namna anavyotaka na hawaogopi kudhalilika!!!!!hawa ndio team ya ushindi ya mwenyekiti wa CCM.
 
Hahah hii siyo habari habari ingekuwa kama angeshiriki huo mdahalo
 
Hata ningelikuwa mimi ningelala mbele, yaani nipambanishwe na lissu, lissu ni level nyingine ile!
 
Haya ndio mambo yale yale ya kuiga kila kitu na kukosa ubunifu, hawa wametoka wapi na midahalo wakati hawakuwahi kuwanayo? Tangu yule dada wa watu na kipindi chake cha Tanzania tunayoitaka wamemchakachua badala ya kubuni nao ya kwao, acha Lukuvi awakimbie ni yale yale watanzania bwana, ukianzisha kioski hapa, kila mtu nae anataka hicho hicho, ni vizuri hivi vipindi navyo visajiliwe na kuwekwa patent loooo. Kwa hiyo wanataka kusema kila mtu anaweza aka host show na ikawa nzuri,
 
Mkuu midahalo ya wenzetu inakuwa so organized na inakuwa imeandaliwa na taasisi ambayo haifungamani na upande wowote, usifananishe midahalo hii na huu upup wa kitanzania ambao kwanza watu wanakaa na kutafuta namna ya kumkaanga mwingine na mnaletewa mtu kama R.K kuongoza mdahalo unategemea nini? mfano mzuri ni huu ambao LUKUVI ameukataa, tayari ilishafamika kuwa miongoni mwa wataohusika moja kwa moja ni mkuu wa SAUT, yule CDM 100% au mtu kama LWAITAMA au KAKOBE wahudhurie mdahalo what do you expect? Tanzania hatuna taasisi za kuandaa midahalo, inabidi kwanza tulione hilo badala ya kukimbilia kuwa mashabiki tu.

Mkuu unataka kusema aekimbia mdahalo kwasababu ya waandaaji wako affiliated na CDM au wewe unamsemea? na ikiwa ni hivyo alishindwa nini kuwa muungwana akasema hata shiriki kwasababu unayotuaminisha wewe.

Wewe inaonekana CCM huijui unakumbuka Mdahalo uliandaliwa na TBC wakati wa uchaguzi mwaka 2010? taasisi ya CCM TBC mbona walikacha hawakushiriki au kwakakuwa TBC ni ya CDM?

Tunachozungumzia hapa ni utashi na uwezo wa viongozi wa CCM kwenye midahalo, viongozi wengi ndani ya ccm ni wababaishaji hawajiamini na hawana uwezo wa kuchanaganua mambo kwenye midahalo wamezoea hotuba za kuandakiwa na idra na zile za kukariri tu.
 
Kwa kiongozi wa serikali kawaida tu hakuna la kushangaza mkuu, mtumishi wa siku nyingi sana yule, huwezi kumlinganisha na kiongozi tu wa chama cha siasa ambao nao wana nyumba za aina hiyo.

lazima tujue kapata wapi hizo mali zisizoendana na kipato chake,atakuwa mwizi na fisadi tu,nchi inaongozwa na majizi itaendeleaje? acha kujifanya hamunazo na kumtetea mwizi au na wewe ni jizi ndo maana unakuja na siasa nyepesi za kutetea uharamia?
 
Hata walioandaa huo mdahalo hawakutumia akili. Lukuvi hawezi kukaa meza moja na Lissu. Atasema nini cha maana?
 
Serikali ilishashtukia midahalo inayoandaliwa na kwa udhamini wa WAPINZANI, halafu hata hivyo kama wana hoja si wangepingana naye bungeni kama siyo ushahidi tosha kuwa wanatumia media vibaya.

bunge la makanjanja wa ccm acha maneno wewe.hoja ngap znazuiliwa kwa wing wa mazombi
 
[ Hakuna serikali yoyote duniani
inayoandaliwa midahalo na
media zenye mwelekeo wa
Upinzani, hata mimi
ningeshangaa kuona Serikali
inaingia mkenge kiasi hicho. ]

DA!! TUNA SAFARI NDEFU BADO
 
Nani akubali kwenda kudhalilika?, hata ningekuwa mimi nisingekubali.
Lakini hata hivyo, ni sera ya chama chetu kuepuka mahojiano na midahalo, maana watu wetu ni watupu vichwani na hawana hoja za kuongea kwenye midahalo.
 
mibunge ya ccm inajifanyaga mijanja ikiwa bungeni kazi ndiyoooooooooo,lakini ukija nje mimburula acha,lisu peke yake sawa na mibunge ya magamba 100
 
Hakuna serikali yoyote duniani inayoandaliwa midahalo na media zenye mwelekeo wa Upinzani, hata mimi ningeshangaa kuona Serikali inaingia mkenge kiasi hicho.
Acha uwongo dogo!!,
Mwaka 2010 wakati wa kampeni za uchaguzi TBC waliandaa midahalo CCM wakakimbia, unataka kutuambia kwamba TBC nayo ni media yenye mwelekeo wa upinzani?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom