Waziri Lukuvi amekataa kushiriki katika mdaharo ulioandaliwa na asasi moja juu ya kilichojiri Bungeni kuhusiana na mchakato wa Katiba mpya.
Mdahalo huo ambao ulipangwa kufanyika Jumapili kuanzia saa Saba mchana hadi saa Kumi na mbili jioni ungewashirikisha Waziri Lukuvi na Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bwana Tundu Antipasi Lissu.
Katika maelezo yake ya kwanini hatashiriki kwenye mdaharo huo Waziri Lukuvi alidai kuwa hana taarifa kutoka ofisini kwake juu ya mwaliko huo kwasababu alikuwa ziarani mikoani kwa shughuli za kikazi na kwamba anapanga kuelekea Mkoani Iringa leo kama mwendelezo wa ziara zake za Mikoani za kikazi.
-----------------
Mdahalo huo ambao ulipangwa kufanyika Jumapili kuanzia saa Saba mchana hadi saa Kumi na mbili jioni ungewashirikisha Waziri Lukuvi na Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bwana Tundu Antipasi Lissu.
Katika maelezo yake ya kwanini hatashiriki kwenye mdaharo huo Waziri Lukuvi alidai kuwa hana taarifa kutoka ofisini kwake juu ya mwaliko huo kwasababu alikuwa ziarani mikoani kwa shughuli za kikazi na kwamba anapanga kuelekea Mkoani Iringa leo kama mwendelezo wa ziara zake za Mikoani za kikazi.
-----------------
Katika hali inayosikitisha kabisa mnadhimu mkuu wa serikali bungeni, waziri nchi ofisi ya rais anayeshughulikia Bunge na sera, Mheshimiwa Willium Lukuvi(Mbunge wa Ismani-CCM) ameamua kwa makusudi kabisa kumkwepa na kumkimbia mnadhimu mkuu wa kambi ya Upinzani Bungeni Tundu Lissu(Mbunge wa Singida kusini-CHADEMA) katika mdahalo uliofanyika leo katika ukumbi wa Mlimani city uliokuwa unahusu mwenendo wa bunge katika mswaada wa kuandikwa kwa katiba mpya.
Willium alikataa katakata kuhudhuria licha ya waandaaji kumwalika kwa msisitizo zaidi ya mara mbili.
Tukio hili linatoa ishara mbaya kwa serikali na CCM kuwa inaogopa kupambana na wapinzani hadharani kwa hoja zenye nguvu na mvuto.
Kwa sasa umekuwa ni mtindo wa kawaida kwa viongozi wa CCM kukimbia midahalo na makongamano huru na muhimu ya kisiasa yanayohusisha wapinzani pia.
SOURCE:Nukuu katika Vyombo vya habari vya leo(Redio, magazeti, Runinga na Mitandao)