Ludovick Joseph akamatwa na Polisi...

Ludovick Joseph akamatwa na Polisi...

Mi siamini kama huyu dogo alihusika kuandaa video hii. Maana sipati mankiki kuwa muandaaji akubali jina lake, na sauti yake halisi vibaki recognisable kwenye dili chafu kama hii, tena mtu mwenyewe graduate!!!
Angekuwa amehusika lazima angefanya editing kuhakikisha identities zake hazibaki kwenye hiyo video

Otherwise ametumiwa na makachero, ili kwa kutambuliwa kwake aende 'akiri' uongo mahakamani kuwa kweli Lwakatare alikuwa namuagiza kufanya uovu, ili aitie CDM hatiani...

So far, hiyo ndio plan yenyewe, baadae ludo ataachiwa.
 
Kwanini wasikimbie ikiwa uwongo wao umekuwa ukibainishwa kadri wanavyoutengeneza.
Hii movie ya bukoba boy maccm yaliamini kwamba yataitumia kuimaliza Chadema lakini contrary na matarajio yao ime back fire vibaya na hawana pa kuficha sura zao.
Wajipange tu walete sinema nyingine kwakuwa hii tumeshaimaliza kilichobaki ni behind the scene!
Mkuu kula Like.
 
Hapo juu Invicible ametuambia Manyerere alitumika sana 2005, hata leo anatumika, kaanzisha tuhuma dhidi ya Ludovic ndani ya siku moja Ludo kakamatwa mh! JF imepiga kelele dhidi ya shehe Ilunga(tisho la kweli) hajakamatwa...Bashe akitoa maelezo anatuhumu vyombo vya usalama kuhusika...Mjengwa (ccm) naye ananawa mikono haraka akimsukumia kijana wake ktk ugaidi..hii ni cinema imeandikwa kuangamiza cdm..
 
Kwa vyovyote vile mwisho wa movie hili POLICCM, CCM na UWT watakuwa namajeraha makubwa sana ya kutibu.
 
polisi duniani kote hawapendwi kama wanafanya kazi zao vizuri. ukiona wanasifiwa na watu kama wewe ujue hapo mambo yanaweza kuharibika muda wowote. ndiyo maana hata Dr Slaa hawezi kusifia jeshi la polisi wala Idara ya Usalama wa Taifa kwani vyombo hivyo vimekuwa ni kikwazo kwake kutekeleza mipango yake ya kifedhuli
Atongwele, naona unafanya kazi ya ziada bila kujua maudhui ya mjadala huu. Tumia vizuri ubongo wako. Nia ya thread ni kujaribu kutafuta ukweli wa sakata la ndugu yetu Kibanda. Na hili linawezekana tu kwa kulijadili kwa kina kutoka kwa wachangiaji na si vibaya kufanya hivyo. Unapoanza kupinga kila mchango wa mtu as if you know the truth, inaleta wasiwasi juu ya ufahamu wako wa malengo ya JF. Tunajadili issues siyo ushabiki.
 
Hapo juu Invicible ametuambia Manyerere alitumika sana 2005, hata leo anatumika, kaanzisha tuhuma dhidi ya Ludovic ndani ya siku moja Ludo kakamatwa mh! JF imepiga kelele dhidi ya shehe Ilunga(tisho la kweli) hajakamatwa...Bashe akitoa maelezo anatuhumu vyombo vya usalama kuhusika...Mjengwa (ccm) naye ananawa mikono haraka akimsukumia kijana wake ktk ugaidi..hii ni cinema imeandikwa kuangamiza cdm..

Ilunga tishio la kweli, Lwakatare tishio la uongo ha ha haaa kupenda bwana kunamambo
 
Ludovick, mbali na kuwa na ukaribu na Lwakatare, pia ni mtu wa karibu na Mjengwa, akimsaidia katika shughuli mbalimbali hususani katika blog yake.

Kuna taarifa ambazo hazijathibitishwa kwamba Ludovick ni mtu wa idara ya usalama wa taifa na watu ambao wako naye karibu wanasema hawajui anafanya kazi gani zaidi.

Alipoulizwa ni kazi gani ambayo Ludovick anafanya, Mjengwa alisema hajui.

Ila katika maelezo yake aliyoandika kupitia kwenye mtandao wa Jamii Forum, Mjengwa anasema anamfahamu Ludovick tangu akiwa Chuo Kikuu (DUCE) na kwamba ni mmoja wa Watanzania wengi waliomfahamu kupitia kazi zake magazetini.

Haijaeleweka mara moja uhusiano wake na Lwakatare ni wa aina gani na katika kazi gani.


source.....mtanzani jumapili
 
jibu unalo unataka kujua nn zaidi ya hilo,mpigie cm m mjengwa
 
Ukisoma tu comment aliyotoa Shonza siku ile clip ya Lwakatare imetoka kuhusu Ludovick na kisha soma comment fupi sana ya saanane.

Unaweza kupata idea juu ya nini kinaendeshwa na hawa vijana ndani ya vyama vya siasa.

Inaelekea kuna genge kubwa.

Tatizo wengi wana njaa kali. Hawafanyi kazi hivyo rahisi sana kutumiwa na wanasiasa kwenye mambo machafu.

Sasa ndio naelewa kwanini Zitto alikuwa anakwepa kuonana na saanane. Zitto ana taarifa za kundi hilo.

Akina Shonza kuhamia Ccm kumefanya siri za kundi hilo kuwa nje na usalama wa taifa kuzipata.
 
TAARIFA RASMI KUTOKA Mtandao Wa Kijamii Wa MJENGWABLOG




Ndugu zangu,
Kutokana na kuwepo kwa taarifa rasmi za kipolisi zenye kumtuhumu Ludovic Joseph kuhusika na matukio ya kigaidi.
Uongozi wa Mtandao wa Kijamii wa Mjengwablog unasitisha rasmi, kuanzia leo Jumapili, Machi, 17,2013, kuwa na Ludovick Joseph kama msaidizi wa Mtandao wa Kijamii wa Mjengwablog na website ya Kwanza Jamii.
Maggid Mjengwa,
Mmiliki wa Mjengwablog /Kwanzajamii
 
sijuhi ndiye ninayemfahamu make kipindi namalza chuo alikuwa 1yr,nilimfahamu kutokana na itikadi zake ..pole sana L.
 
kwenye clip ya video ya lwakatare:

15:59 ...sauti inasika ikisema ‘’ unamuweka kwenye dilemma hajui adui ni nani yaani anakuja hapa anakukuta wewe ‘’LUDOVICK’’ ndiye unamfatilia’’...huyu Ludovick ni nani?( some dots needs to be collected and connected here ) yawezekana ni mmoja wa vijana waliokuwa wanajirekodi na hili ni jina lake halisi na wametajana pasi kujua au ni code name?..

17:10 kijana anayepewa maelekezo (‘’Ludovick) anauliza ‘’ kwa hiyo kama kila kitu kitaenda well inakwenda mpaka lini?’’ lakini katika kujibu clip inayomuonyesha lwakatarea akijibu swali hilo akisema ‘’ Bahati mbaya umekuja na majibu yasiyojitosheleza’’ ....katika majibu haya kuna mkanganyiko mkubwa maana hakuna uhusiano wa swali lililoulizwa na jibu lililotolewa....tangu dakika ya 15 ya clip hii maelezo ya sauti zinazosikika hayana mpangilio wa manaa... mengi yalilenga kufuatisha ishara na vitendo vya lwakatare alivyokuwa akiongea na ukitizama kwa makini hakuna uhusiano kati ya maneno yenyewe na mdomo wa lwakatare.............


Viziwi ni mabingwa wa kusoma midomo ya watu kwanini wasionyeshwe clip wakatuambia kile Lwakatare anachoongelea?
 
Ndio Matatizo ya Vijana kuishi maisha ya Ki-Day Waka.Graduate unaagizwa kupeleka Invoice na vitabu vya List Mungu wangu ngoja nikaa kimya nisije kula Ban.Si mwalimu huyu kwa asiende kutufundishia wanetu mashuleni sirikali inasema walimu hawatoshi kumbe wapo mjini wanatumika like Mtela na wenzie.

mkuu kujitambua ni jambo muhimu sana kwa vijana wetu wengi wanafikiria maisha ni rahisi sana na matokeo yake wanaingia kwenye kashehe kama hizi
 
Mjengwa naona anachokifanya nika ma kufificha kivuli cha mwili wake huyu anajua kila kitu huwezi kaa na mtu kwa muda wa zaidi ya mwaka usijue anafanya nini hata kidogo
 
Huyu kijana!!!!!!!!!!!! inatia shaka kuamini kama anaweza fanya mambo haya maana ni mtu ambaye hata huwezi kumdhania...I know him since we were at DUCE it is an implicated story!!! Let the Police force ensure justice is met.Pole Ludovick
mkuu hapa naona kunamchezo mchafu sana na pengine huwa naamini Mungu tu ndiye atusaidie na uhuni unaofanywa na jeshi letu la polisi wakishirikiana na usalama wa taifa ili kukamilisha malengo yao ya kuitetea ccm
 
Mi siamini kama huyu dogo alihusika kuandaa video hii. Maana sipati mankiki kuwa muandaaji akubali jina lake, na sauti yake halisi vibaki recognisable kwenye dili chafu kama hii, tena mtu mwenyewe graduate!!!
Angekuwa amehusika lazima angefanya editing kuhakikisha identities zake hazibaki kwenye hiyo video

Otherwise ametumiwa na makachero, ili kwa kutambuliwa kwake aende 'akiri' uongo mahakamani kuwa kweli Lwakatare alikuwa namuagiza kufanya uovu, ili aitie CDM hatiani...

hapa mkuu maswali ni mengi zaidi maana ilikuwaje mtu aliyerecond aache jinalake kwenye clip, inavyoonekana kuna kitu ambacho kiko nyuma yake. Lakini Mungu wetu ni mkuu hakika atafunua kilichojificha sio muda mrefu
 
Back
Top Bottom