Kuna gazeti mmoja nchini, limejikita vema kuchora mchoro walipotoka wavamizi wa Kibanda, Jinsi Kibanda alivyoenda Nyumbani, njia aliyopita, na njia walikopita watesaji wake. anajua vema sakata hili. Ni Mhariri wa Gazeti hili ndiye alitaja kuwa Ludovick asipokamatwa ushahidi muhimu kuhusu kuteswa kwa Kibanda usingepatikana. Ni mhariri huyu aliyetoa taarifa kuwa Ludovick ni shahidi muhimu ndiye wa kwanza kutuarifu kuhusu Ludovick kukamatwa akiwa Iringa, hata wana JF wa Iringa hawakuarifu kama alivyofanya yeye. Kama kweli tupo serious na uchunguzi wa jambo hili, huyo aliyechora mchoro huu ni shahidi muhimu sana. Kibanda bado hajahojiwa kutoa maelezo ya walipotokea wavamizi wake, kwanza katika maelezo Kibanda bado hataji Lwakatare wala Ludovick. Kinachosikika katika video kinataja Mwandishi wa habari wa mwananchi, gazeti hili limeendelea kushikilia waliohusika na Kibanda ni Lwakatare na Ludovick, tofauti kabisa na jinsi polisi walivyopeleka shitaka Mahakamani. Mahakamani inasomwa ugaidi na kupanga kujeruhi mwandishi.Hili gazeti lina siri nzito angalia picha
yawezekana