Lowassa Vs. Membe - Tanzania's own "Thrilla in Manila"?

Lowassa Vs. Membe - Tanzania's own "Thrilla in Manila"?

Hakika Lowassa anatisha! Maana hamlali kila kukicha ni Lowassa!

Kwa umakini ukitafakari sana utaona Lowassa ndo anafaa ndo maana amekua kama mti wenye matunda mema mAana ndio unaotupiwa mawe.
 
haijawahi kwenye historia ya ccm, mtu anaetaka kuwa rais na mwenyekiti wa ccm
'akamponda waziwazi na kumdhalilisha mwenyekiti aliekuwepo madarakani'
bado mshtuko na athari zake hatujaziona bado..
the game this time is so different.........we have the unknowns unknowns so far.....
........mwenyekiti hakupondwa, alikumbushwa alichokuwa amekisahau, ndio maana ilifikia wakati alitikisa kichwa kukubaliana na yale aliyokuwa akikumbushwa na Lowassa, mfumo ndani ya ccm ni hatari kuliko ama Lowassa au Membe.... tukitambua hilo tutaweza kufanya maamuzi yenye maana.
 
What amazes me, is the arrogance. How in the God's earth do you think you can muscle your way through the top without listening to your employer? means(us).
What kind of employee are you going to be, if you give us all the red flags that you are not going to listen what your employer wants you to do?
If possible I would've loved Tanzania to stay without a president for a little while so we can study the actual definition of a president. Just wishful thinking.
 
........mwenyekiti hakupondwa, alikumbushwa alichokuwa amekisahau, ndio maana ilifikia wakati alitikisa kichwa kukubaliana na yale aliyokuwa akikumbushwa na Lowassa, mfumo ndani ya ccm ni hatari kuliko ama Lowassa au Membe.... tukitambua hilo tutaweza kufanya maamuzi yenye maana.

Hivi zile sherehe za kufurahia ushindi sasa zimehamia wapi? Nina harambee ya ujenzi wa kisima nyumbani kwangu na sasa naandaa hotuba ya kumsifia fisadi halafu nitamualika apige siasa za utakaso. Nahitaji milioni 45.
 
Kijiweni tulifikia conclusion kuwa hypothetically, ni bora JK aongezewe miaka 5 mingine (kutokana na katiba mpya atakayotengeneza) kuliko kwa mtu kama Membe kuwa rais. Tatizo tu ni kuwa hamna kati ya haya mawili yatakayowezekana. The hypothesis is bound to fail. Andazi haliwezi kuwa nanasi. CCM wasipouana kabla ya 2015, nguvu ya EL sioni wa kuidhibiti. Jamaa hutumia kila mbinu kupata anachokitaka, na ndio ameshaanza kampeni! Kazi kweli kweli, enjoying the show!
 
Wana JF,

Mimi nilishachoka na haya mazingaombwe! Ukweli ni kuwa kawaida ya kupokwzana vijiti bado ipo! JK alipo pewa URAIS na kundi lake la manyang'au walikubaliana atakayefuata kwenye list; wote twamjua; manywele.

Manywele ni makini sana, pamoja na kujua yeye ndo atakayefuata hakulala, akatengeneza insurance pilicy yake kwa kupanga safu kwenye maeneo muhimu yote!!! Ndo maana hata kuvua gamba imeshindikana; kila ukigusa manywele ametanda!!

JK ni mnafiki sana na ni mtu mwenye visasi sana; kwa sababu anazozijua yeye anataka kwenda nje ya makubaliano, ametengeneza kundi jipya kwa ajili ya 2015!!! KWa kuwa Manywele ni smart ameshtukia na yuko kamili kivita. Ukikumbuka maneno yake ya Singida akichangia harambee "...naamini nitashinda vita hii." JK ni mbishi na haambiliki na kama ataendelea na plan yake kufumbia macho makubaliano yao, CCM itameguka.
 
kwa nini unalinganisha kifo na usingizi?kwani wewe humjui Rais
 
kuna rafiki yangu mmoja alimuuliza membe siku moja, tatizo lake yeye na lowassa na sita na nchimbi? membe akajibu ' mbona nawapenda sana, ila anachukizwa na watu wengi kumpenda lowassa zaidi ya kikwete na akaapa kufanya juu chini lowassa achukiwe'.

membe alisema anajiandaa kwa kampeni za 2012 ili watu wengi zaidi wamkubali..

my take; sioni influence yoyote ya membe. hakubaliki kichama wala kiuongozi
 
tatizo lao ni wapo kwenye kinyang'anyiro kikaaali kati yao miaka michache ijayo,kaa mkao wa kula.
 
joka la mdimu huchukia wachuma ndimu ingawa lenyewe halili ndimu
 
Wote wezi na waroho wa madaraka hawawezi kukaa pamoja .
 
Ni nini hasa kilichowagombanisha hawa wanamtandao?
Mnyisanzu, kwanza hakuna ugomvi wowote kati ya watu hawa bali wanatofauti tuu katika comon interest ya urais wa 2015.

Kuna viongozi ambao ni born leader na made leader. Membe ni made leader na Lowassa ni born leader. Made leader anammaind born leader!

Kwa vile Ben alikuwa foreign na akawa rais, then JK alikuwa foreign akawa rais, Membe anaamini sasa ni zamu yake maana yeye ndiye yuko foreign!.

Lowassa was born to lead kutukomboa Watanzania!. Uwezo wa Membe mnaujua?. Ni afadhali ya JK mara mia!. Kama JK ndio ametufikisha hapa!, Membe si ndio atatuteketeza kabisa!. Hapa mtu ni EL tuu!.
 
Back
Top Bottom