Lowassa Vs. Membe - Tanzania's own "Thrilla in Manila"?

Mwandosya hafai kuwa rais hata kidogo. Si unakumbuka kipindi kile DAWASCO wanawakatia maji mawaziri wasiotaka kulipa bill za maji akasema waachwe. Pia akiwa waziri wa mawasiliano na uchukuzi inaemekana pia naye ameshiriki kuihujumu TTCL. Kwa wanaomfahamu vizuri wanasema pia ni mkabila sana. Naomba kuwasilisha.

Mwandosya amerudi juzi tu toka matibabu mnaanza na siasa zenu za kijinga kuhusu Urais!! Muacheni apumzike mtu wa watu kila kukicha mnamuota!!
 
In a presidential contenst, no body can ride on the luck of the incumbent. Not even Membe for he knows that when you assosicate with the incumbency, you carry with you, all what is perceived to be evil. Belieiving that the power of incumbency is all what takes one to win the nomination or even the presidency is as absurd as to think that splashing out ill gotten money is enough to endear one to the voters who very well know how devilish the candidate is. If Membe were to stand, he is man enough to articulate what he intends to stand for and the incumbent will only be an icing in the cake.

Membe is as bad as Lowassa if not worse only that he has not bee outed!!
 
"Mvua za mwanzo ni za kupandia" Baba wa Taifa. Sie watu wa vijijini tuko bze na kilimo wa Dar na urais 2015. Jamaa yangu wa Kigoma anasema mvua zinanyesha sana na huenda mavuno yakawa mazuri mwaka huu.Dar wabunge 2 tu wa majimbo upinzani, Kigoma CCM 3 tu kati ya wabunge 8.
 
Mashauri hoja zako zidi ya Mwakyembe na Mwandosya ziko very shallow!
Ushauri wangu kwa CCM big tribes kama Wanyakyusa,Wahaya,Chaga,Wasukuma,Wanyamwezi wapewe nafasi zingine ila sio URAISI
Maana uwingi wao na usomi wao utashangaa baraza zima la mawaziri wanatoka kumoja na iyo italipeleka taifa kwenye ukabila.
Ona ata historia Mzanaki then Mwinyi sijui mzaramo then Chinga then ****** si unaona vikabila vidogovidogo
Sikatai wapo waliotuangusha

Hili suala limepitwa na wakati; mikoa mingi sana ime catch up kielimu; in the next 15 years wazee hawa wakiondoka hali itakuwa tofauti kabisa, especially kwa Kagera na Mbeya;Msimamo wa Nyerere juu ya hili ulitokana na ukweli kwamba maeneo ya Mbeya, Uchagani, Bukoba, ndiko wakoloni walijenga mashule mengi kwani huko walikuwa more settled kutokana na Hali ya Hewa among other things; kwa sasa mikoa mingi sana ina catch up kielimu; Nina uhakia Sensa ijayo mwakani itatuacha midomo wazi iwapo tutagundua kwamba mkoa kama Ruvuma una wananchi wengi zaidi wanaojua kusoma na kuandika kwa mfano kuliko Mbeya;
 
Natamani sana kupewa ushahidi kwamba lowasa ana mali nyingi sana na anaccount nje na ni mwizi wa mali ya umma.

Tamaa yangu inatokana na sababu nyingi, na nyingine ni za kihistoria ila sababu kubwa ni kwamba sitaki kuingia kwenye dhambi ya kuhukumu bila ushahidi.

Wakati kambona anarejea nchini baada ya mfumo wa vyama vingi kufika nchini, mchungaji mtikila na wakina Fundikira. RIP. walituaminisha kuwa Kambona atatuletea ushahidi wa account za Mwl Nyerere alizokuwa nazo huko ulaya na watahakikisha pesa hizo zinarudishwa nchini. Waandishi walimwandama sana Mwl ajibu hizo hoja. Mwl akawaambia muulizeni aliyesema mpaka awape ushahidi na Mwl hakujibu ama kwa kukanusha au kukubali. Leo kila mmoja anaujua ukweli.

Wakati wa kumpata mgombea wa CCm 2005, Wanamtandao walituaminisha kuwa Dk Salim A Salim, ndiye aliyemuua Karume na Wazanzibar wakaamua kumpa Jk kura zao, wakasahau kabisa swala la zamu ya bara na visiwani, kwa sababu waliaminishwa vyema kwamba Dr ni Muuaji wa Kiongozi pendwa kwao. Omarilyas unalijua hili vizuri. Leo hii Kila mmoja anaujua ukweli.

RAISI AJAYE ATAAMULIWA NA WATANZANIA KUTOKANA NA UZURI WA SERA NA UWEZO WA KUSIMAMIA SERA ZA CHAMA CHAKE, NA KAMWE HAWEZI KUAMULIWA KWA PROPAGANDA ZA UFISADI, WIZI, UMALAYA NA MENGINEYO YASIYOKUWA NA USHAHIDI.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.

Kujua Lowassa ni mwizi au si mwizi hakuhitaji ushahidi wa account za nje wala degree au CPA. A person just a mere public servant, since his Bachelor (1975) and MA, hana historia yoyote ya kufanya kazi either internatinal organisation au kampuni yoyote kubwa. Just a mere civil servant wa nchi maskini kama Tanzania, leo hii unaona mara ananunua nyumba London, mara katoa mchango wa kujenga kanisa million 50. Anazitoa wapi hizo fedha?. Tunawasomi wangapi na civil servant wangapi wenye elimu tena wengine wametumikia taifa kwa muda mrefu kuliko yeye hawana uwezo huo. Kuitumikia Tanzania tu kwa level ya Ukurugenzi (AICC) pamoja na nyazifa za uwaziri kwa kipindi fulani ndio uwe tajiri hivyo?. Mambo mengine hayahitaji elimu ya degree kujua mtu ni mwizi au si mwizi, kwa mtu ambaye katumikia serikali na ubunge tu. Utetezi huu mnaoutoa nenda vijijini huko mkawadanganye watu mliozoea kuwaaminisha kila kitu na wenyewe wanaswallow tu kilivyo. Naona mnafanya kazi kubeba maji kwenye gunia kuja kumsafisha Lowassa hapa JF. Kwa tathmini ndogo tu hapa watu wengi ni waelewa, wengine ni watumishi wa serikali na private wa muda mrefu, wanajua ipi nyeusi na ipi nyeupe. Bora mkajikite huko vijijini mlikozoea kudanganya watu na wao wakawaamini

 
Taratibu Mbopo, kwa hiyo hutaki master of thieves kuwa rais ila unataka thief mdogo Membe kuwa rais??

Go west go east...EL yuko juu sana ya Membe. hili la wizi unaona mwenyewe linapungua nguvu mpaka watu wanawashindanisha

Mbopo sehemu ya wezi ni jela akiwa nje na hana kesi siyo mwizi, unless you have defined way of human system ya kuhukumu watu zaidi ya mahakama.

wasioweza kuwapeleka membe na EL jela ndiyo wabaya zaidi!

FYI Membe ana wakati mgumu sana tena baada ya kupokea fedha za Gaddafi za kusilimisha EAST AFRICA.

Subiri uone madudu yake,

sorry do not fall in love with politician they will disappoint in a second!

I cannot wait for that comedy to start playing.

Membe does not depend on JK or anybody else to ascend to power. We have said and we say it again: LOWASSA WILL NEVER BE THE PRESIDENT OF TANZANIA! No amount of money will buy the presidency. Kwa mtu asiye na akili kama wewe ndiye unayefikiri kwamba Gadaffi angeweza kumtumia Membe kwa lengo lako fake unalolizungumzia. Ilikuwa na rahisi kwenda west africa kuwasilimisha hao unaodai walikuwa wasilimishwe. Kinachofurahisha ni kwamba mnaunga unga kashfa na zote hazina mashiko. Ni vizuri mkafanya juhudi za dhati za kujaribu kumsafisha mfu wenu badala ya kuhangaika kurusha tope kwa wengine, hazitalipa. Labda mfanye yale ya Mwakyembe!
 
Kujua Lowassa ni mwizi au si mwizi hakuhitaji ushahidi wa account za nje wala degree au CPA. A person just a mere public servant, since his Bachelor (1975) and MA, hana historia yoyote ya kufanya kazi either internatinal organisation au kampuni yoyote kubwa. Just a mere civil servant wa nchi maskini kama Tanzania, leo hii unaona mara ananunua nyumba London, mara katoa mchango wa kujenga kanisa million 50. Anazitoa wapi hizo fedha?. Tunawasomi wangapi na civil servant wangapi wenye elimu tena wengine wametumikia taifa kwa muda mrefu kuliko yeye hawana uwezo huo. Kuitumikia Tanzania tu kwa level ya Ukurugenzi (AICC) pamoja na nyazifa za uwaziri kwa kipindi fulani ndio uwe tajiri hivyo?. Mambo mengine hayahitaji elimu ya degree kujua mtu ni mwizi au si mwizi, kwa mtu ambaye katumikia serikali na ubunge tu. Utetezi huu mnaoutoa nenda vijijini huko mkawadanganye watu mliozoea kuwaaminisha kila kitu na wenyewe wanaswallow tu kilivyo. Naona mnafanya kazi kubeba maji kwenye gunia kuja kumsafisha Lowassa hapa JF. Kwa tathmini ndogo tu hapa watu wengi ni waelewa, wengine ni watumishi wa serikali na private wa muda mrefu, wanajua ipi nyeusi na ipi nyeupe. Bora mkajikite huko vijijini mlikozoea kudanganya watu na wao wakawaamini


Hii attempt ya hawa jamaa kutakasa kinyesi itawafikisha wapi? Maskini watu hawa, wanapoteza muda kipuuzi kabisa. Kwani makanisa yamekwisha? Nendeni kwenye harambee Mtwara.
 
Mkuu kwa nini Membe aliwatambua Wahuni wa Misri? Kwa Nini Membe aliwatambua wahuni wa Tunisia? Huoni kuna kitu hapo Personal Baina ya Membe na Marehemu Gadafi? Au Wahuni wa Libwa (NTC) ni Wahuni Zaidi kuliko Wahuni wa Misri na Tunisia

Mkweree na Membe wamepita pita sana Libya enzi za Gadafi na mara nyingi aliwapa mabunda ya dola toka tentini kwake hivyo dhamira huwa inawasuta; hawaamini kuwa yalimfika yaliyomfika hivyo kuwachukia NTC!!!
 
These are not on my expectation list neither the national security lis; so do not bother concentrate on their matters. They are playing the opening match towards presidential race 2015 where we will have very new faces. That do not agree, time will tell.
 
Membe alisema Bungeni kuwa NTC hawawezi kupinduwa nchi kwa Pick UP, lakini NTC walipoweza hakusema kitu zaidi ya kukataa bendera ipandishwe, so mtu kama yeye hafai kuwa President coz HANA MAONO
 
Mubarak hayuko Madarakani Wahuni wa Misri waliandamana Wakapambana pale Cairo na sasa Misri haiko under Mubarak iko chini ya Viongozi wa Wahuni wa Misri kama Ilivyo Libya Chini ya Viongozi wa Wahuni wa Libya

Swali langu ni kwamba je Wahuni wa Libya ( kama anavyowaita mbopo) walikuwa ni Wahuni zaidi ya Wahuni ya Wahuni wa Misri na Tunisia?

..Hivi unajua kuwa uongozi wa Misri haukuchukuliwa na viongozi wa waandamanaji?? No research, No right to talk...
 
Ndani ya CCM hakuna mtu ambaye anaweza kusimama na kuhesabiwa. Wote waliomo mle ni matapeli tu, hakuna wapambanaji wala ushuzi dot com. Sitta ni msaliti...yeye anauma na kupulizia kwa ajili yake binafsi na familia yake. Membe, very cozy to JK and his Co....yeye na JK ni wale wale. Mwakyembe ndo hafai kabisa, yeye na Sitta ni walewale tu. Kapewa sumu sasa inammaliza wakati ana siri kubwa kuhusu Richmond. Lowassa ni tajiri mchafu ambaye bado hajaridhika na mali aliyonayo. Anataka kufanya yeye atakacho bila kuangalia kuwa sasa ni wakakti wa watanzania kuneemeka kutokana na rasilimali zao. Magufuli naye yuko kwa ajili ya nafsi yake tu, hana hulka ya kuwajibika na alishindwa kuonyeshwa uwajibikaji pale JK na Pinda walipomdhalilisha mbele ya kadamnasi. Nchimbi naye ni bomu lilie, anafikiri kuchukuwa hiyo PhD ya ukweli ataweza kulamba dume kwenye politics za Bongo.

Huu ni wakati wa watanzania kuachana na CCM maana system yote ya chama iko corrupted kuanzia balozi wa shina hadi kwa JK.
 
CCM haina mtu anayefaa kuwa Rais.
Sio Membe, Lowassa, Magufuli, Mwakyembe wala Asha Migiro.
System ya CCM ime collapse, imeshindwa kutatua kero za Mtanzania, imeshindwa kusimamia rasilimali zetu kwa ajili ya manufaa yetu na vizazi vyetu vijavyo.
Now its a time to say NO for CCM.

I see a point in your comment, but let say if they get another last last chance Magufuri can do it much better. However it's much better for Tanzanians to try other alternative,cause indeed the ruling party seems to have riched its climax in leading this nation. These are just my opinion ndugu.
 
I cannot wait for that comedy to start playing.

Membe does not depend on JK or anybody else to ascend to power. We have said and we say it again: LOWASSA WILL NEVER BE THE PRESIDENT OF TANZANIA! No amount of money will buy the presidency. Kwa mtu asiye na akili kama wewe ndiye unayefikiri kwamba Gadaffi angeweza kumtumia Membe kwa lengo lako fake unalolizungumzia. Ilikuwa na rahisi kwenda west africa kuwasilimisha hao unaodai walikuwa wasilimishwe. Kinachofurahisha ni kwamba mnaunga unga kashfa na zote hazina mashiko. Ni vizuri mkafanya juhudi za dhati za kujaribu kumsafisha mfu wenu badala ya kuhangaika kurusha tope kwa wengine, hazitalipa. Labda mfanye yale ya Mwakyembe!

Biashara ya kununua urais ilianza tangu uchaguzi wa 2005, hata Rais tuliye naye leo hii Ikulu aliupata urais huo kwa kuununua. Mzee Butiku ameliongelea sana hili la matumizi ya fedha nyingi sana kwenye Mkutano Mkuu wa CCM wa 2005 pale Chimaga, Dodoma. Kwa hiyo hiyo kauli yako ninaona ina mushkeli kidogo kwa kuwa yalishakuwa mazowea ndani ya vikao vya CCM kutumia fedha ili kuweza kupitisha agenda ya mhusika hata kama imepinda. No wonder hata Jairo alichangisha hela za "kufanikisha kupitisha bajeti" huku Ngeleja na Malima wakipewa milion nne kila mmoja ili kutoa "takrima" kwa wabunge ili waweze kupitisha bajeti ya wizara.

Swala la kununua kura limekuwa ni sehemu ya mfumo wa CCM, kama mgombea hana fedha basi hata kura hawezi kupata. Kama Lowassa alikuwa mchafu ilikuwaje wabunge wa CCM wakampitisha awe Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama na Mambo ya Nje ya Bunge? Serukamba [Peter] anajulikana kuwa ni mtetezi wa Lowasa, ilikuwaje akapenya na kuukwaa uenyekiti? Makamba Jr. [inasemekana yuko kambi ya Lowassa] ilikuwaje akaukwaa uenyekiti? Mama Shelukindo alimshukuru Lowassa kwa kumsaidia kumpigia kampeni na kuandaa lunch or dinner ili wabunge wampe kura. Hayo yote yalishaandikwa kwenye vyombo vya habari.

Kukuonyesha kwamba fedha inaweza kununua kura hata nafasi ya Spika nayo ni mwendo huo huo. Kura za Sitta kwenye u-Spika wa 2005 zilinunuliwa, waliomsaidia kuzinunua ndio hao hao waliokuja kumwangusha 2010, na ndio waliosaidia kununua u-Spika wa Mama Makinda. Ndani ya CCM kura zinauzwa na wajumbe wana bei pia.

Juzi UVCCM walijaa Dodoma mpaka wakasababisha taharuki, baada ya JK kuambiwa je alifanya nini? Nape alitoa taarifa kwa Mwenyekiti ili labda JK ajue nini kinaendelea hapo Dodoma, ingekuwa ni zama za uadilifu viongozi wa UVCCM wote waliokuwa Dodoma wangeitwa na kujieleza na baada ya hapo kibano kingefuata.

JK ni dhaifu kwa kuwa alingizwa Ikulu kwa kununua urais kwa kutumia fedha chafu. Kwa hiyo hana "moral authority" ya kuzuwia mwingine asiingie Ikulu kwa kununua nomination ya Chama.

Kama kauli yako ina uhakika, basi naomba uniambie je kuna mkakati gani wa kichama wa kuhakikisha kwamba biashara ya kuuza na kununua kura inakomeshwa within CCM? Ni nani ana jeuri hiyo iwapo yeye mwenyewe alifika hapo kwa njia hiyo?
 
Lowasa yupo juu na ni kiongozi makini. nampongeza alivyojiuzulu u waziri mkuu kwa makosa ya walio chini yake na juu yake, hiyo inaonesha dhana ya uwajibikaji. Membe samahani nikisema hana ubavu kabisa wa kupambana na EL. asanteni
 
Lowasa yupo juu na ni kiongozi makini. nampongeza alivyojiuzulu u waziri mkuu kwa makosa ya walio chini yake na juu yake, hiyo inaonesha dhana ya uwajibikaji. Membe samahani nikisema hana ubavu kabisa wa kupambana na EL. asanteni
 
haijawahi kwenye historia ya ccm, mtu anaetaka kuwa rais na mwenyekiti wa ccm
'akamponda waziwazi na kumdhalilisha mwenyekiti aliekuwepo madarakani'
bado mshtuko na athari zake hatujaziona bado..
the game this time is so different.........we have the unknowns unknowns so far.....

Mkuu The Boss,

Ni kweli kabisa haijawahi kutokea. CCM unayoiongelea wewe ni ya zama zile sio hii ya sasa yenye Rais na Mwenyekiti "dhaifu" asiye na msimamo. Ukiona Lowassa anafanya hivyo ujue kwamba anajiamini na anamjua vizuri sana Mwenyekiti wake. Yaliyotoke NEC juzi kwenye ni mwendelezo, Bungeni alishasema serikali imekuwa inashindwa kufanya maamuzi magumu na mazito kwa kuogopa lawama.

Yanayotokea sasa hivi ni kielelezo cha mapungufu ya Rais wetu na Mwenyekiti wa Chama. Ndiyo maana Tundu Lissu jana aliandika kwenye wall yake ya facebook kwamba "Eti huyu ndiyo Rais wa Nchi, 'ni kweli mna hoja lakini nisipo-saini huu mswaada wenzangu CCM watanielewa?'". Hizo ni dalili za Rais hafanyi maamuzi kwa kuangalia hoja bali anafanya maamuzi kwa kuangalia ni nani amesema/toa hoja husika.

Matokeo yake tuna Rais mwoga ambaye hana msimamo ila anaogopa kivuli cha wababe wake. No wonder hata akina Lowassa wanampelekesha puta na amebaki kuwatumia akina Nape Nnauye na akina Msekwa kwamba semeni hiki au waambieni hiki, halafu yeye akikutana nao hasemi kitu. Mwezi April magazeti yalimnukuu Lowassa akimwambia Msekwa kwamba Rais alipokutana na Lowassa Unguja hakuambiwa chochote na wala hayo ambayo Msekwa alikuwa akiyasema hakuambiwa, na akawa anashangaa. Same Rais akienda ukimbi wa Diamond anasema "anachosema Nape ni msimamo wa chama"! Kama ni msimamo wa chama kwanini usisimame mbele ya NEC na KK then useme jamani watuhumiwa ni hawa, tunaomba wajitetee na baada ya hapo tutawachukulia hatua stahiki.

Once you have so many unknowns, it may be very difficult to solve equation, na hapa ndipo tulipo. The game is on na hakuna anayejua what is next!
 
Back
Top Bottom